Wednesday, July 24, 2013

HATIMAE KITUKUU CHA MALKIA ELIZABETH CHAPEWA JINA....!!!


Prince William akiwa na familia yake saa24 baada ya mtoto George Alexander Louis kuzaliwa.

Prince William akiwa na familia yake saa24 baada ya mtoto George Alexander Louis kuzaliwa.
Prince William alipokuwa amezaliwa akiwa amebebwa na baba yake Prince Charles na mama yake Princess Diana mwaka 1982.

Prince William alipokuwa amezaliwa akiwa amebebwa na baba yake Prince Charles na mama yake Princess Diana mwaka 1982.

RAIS KIKWETE AWASILI BUKOBA, AKUTANA NA TAIFA STARS MWANZA, AWATAKIA USHINDI DHIDI YA UGANDA








 Jakaya Mrisho Kikwete akifungua jengo la Kagera Coperative Union leo Julai 24, 2013
mjini Bukoba.


 Picha ya Pamoja

MBONA MAJANGAAAAA: ALIKIBA NAE ATIWA MBARONI NJE YA NCHI... KISA ........!!!


Meneja wake Guru akiongea na mama yake Ally Kiba nyumbani kwao Kariakoo amesema bwana mdogo alikuwa uwanja wa ndege wa Amsterdam akisubiri ndege za American Airlines ili aelekee jijini Oklahoma City USA akiwa na mwanamama maarufu mwenye mvuto hapa bongo ndipo alipokamatwa.

Haijajulikana sababu za kukamatwa kwake na mpaka leo familia wapo kimya hawajafunguka na wanailinda habari isivuje japo baadhi ya wadau washazinasa. Haijajulikana sababu za kukamatwa ila mpaka kesho media zitatuambia sababu. Sina hakika kama kisa cha kukamatwa bwana Singleboy ni kitu cha Sembe au laaaaa!!! TUSUBIRI


HII NDIO PARTY TWO YA BIFU LA IRENE UWOYA NA LUCY KOMBA...!!!


NYOTA wa filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krrish’ ametoa kali ya mwaka baada ya kudai kwamba amemshika ugoni msanii mwenzake, Lucy Komba mara baada ya kuziona picha za msanii huyo akiwa na mumewe, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ wakiigiza filamu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutokea nchini Swaziland, Uwoya amepinga vikali utetezi unaosemwa kwamba Lucy na Kataut walikuwa wakishuti filamu na anaamini kuwa msanii huyo ameamua kumzunguka na kutaka kuibomoa ndoa yake. “Lazima kuna kitu kinaendelea kwani katika dunia hii sijawahi kuona filamu inayochezwa na watu wawili tu mwanzo mpaka mwisho, ninachotaka kusema ni kwamba Lucy ana mpango wa kuiharibu ndoa yangu,” alisema Uwoya kwa hasira. 

Uwoya amehoji usiri wa filamu hiyo na kila alipokuwa akimpigia simu mumewe alikuwa akimjibu kwamba yuko Rwanda kumbe alikuwa Bongo akiigiza filamu na Lucy. “Kwanza Lucy ashukuru niko mbali, laiti ningekuwa karibu angenieleza vizuri kwa sababu hata yeye angeweza kunipigia simu na kunifahamisha ushiriki wa mume wangu kwenye filamu hiyo kwa kuwa namba zangu anazo, ilikuwaje hakufanya hivyo?” alihoji.

 Kuonesha kwamba amechukizwa na kitendo hicho, Uwoya alisema kwamba akitua Bongo atamtafuta Lucy ili aweze kumshughulikia vizuri na ikiwezekana amuoneshe hiyo filamu waliyoigiza watu wawili tu. “Nitatua Bongo siku si nyingi na cha kwanza ni kumtafuta Lucy, anieleze vizuri kuhusu filamu hiyo waliyocheza na mume wangu,” alisema Uwoya. Filamu hiyo ambayo imekuwa maumivu makubwa kwa Uwoya, imechezwa na Lucy na Ndikumana tu mwanzo hadi mwisho na imepewa jina la Kwa Nini Nisikuoe

STARS YAMALIZA KAMBI YAKE JIJINI MWANZA KUONDOKA KESHO KUELEKEA UGANDA, KASEJA BADO CHAGUO BORA.

Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen (kulia) akizungumza  na wandishi wa habari (hawako pichani) ikiwa ni siku moja kabla ya kuondoka jijini Mwanza mara baada ya kumaliza kambi, kushoto ni Afisa habari wa TFF Michael Wambura. 
NA ALBERT G. SENGO: MWANZA
Ni takribani majuma mawili sasa Taifa Stars imekuwa jijini Mwanza ikiweka Kambi kuelekea kipute cha marudiano na 'The Cranes', katika mchezo unaotarajiwa kuchezwa jumamosi hii ya tarehe 27 mwezi wa 7mwaka 2013 mjini Kampala.

Sasa kambi imefikia tamati, yamesalia masaa kadhaa ambapo kesho mchana majira ya saa 7 na dakika 25, wawakilishi hao wa taifa la Tanzania, Taifa Stars wataondoka kwa ndege ya Shirika la Precission Air kuelekea nchini Uganda kuisaka tiketi ya CHAN. 

Msikilize hapo chini

.

KWA UFUPI: Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen amezungumzia mapengo yaliyopo kwenye kikosi chake kuanzia kutokuwepo kwa Kapombe kwenye idara ya ulinzi na sasa Mwinyi Kazimoto katika idara ya kiungo, bila shaka kikosi kitakuwa na utofauti ambao anaona ni sehemu ya marekebisho na anamaboresho.

WASHINDI WA TIGO ‘MILIKI BIASHARA YAKO’ WAKABIDHIWA BAJAJI ZAO


 
 Meneja Chapa wa Tigo, Bw. William Mpinga (kulia) akimkabidhi ufunguo wa Bajaji mshindi wa pili wa promosheni ya ‘Miliki Biashara Yako’, Bw. Riziki Lucas Kisemo (36) mfanyakazi wa viwandani, mkazi wa Makabe, Dar es Salaam. Tigo tayari imelipia leseni ya barabani (Road license) na bima kwa ajili ya Bajaji hizo. Anachotakiwa mteja sasa, ni kuanza biashara yake bila shida mara moja.


 
Meneja Chapa wa Tigo, Bw. William Mpinga (kulia) akimkabidhi ufunguo wa Bajaji mshindi wa kwanza wa promosheni ya ‘Miliki Biashara Yako’, Bw. Mohamed Ramadhani Mnjori (39) muuza nguo za mitumba, mkazi wa Ilala – Dar es Salaam kwenye halfla ya makabidhiano iliyofanyika eneo la Soko Kuu la Kariakoo, Dar es Salaam.

SHILOLE MATATANI WIZI SIMU ZA DIAMOND...!!!


 
Stori:Shakoor Jongo na Musa Mateja
STAA wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ..........

ameingia matatani akidaiwa kuingia mitini na simu tatu za mkononi alizoaminiwa nchini Afrika ya Kusini alikokwenda kufanya shoo.


Mfano wa aina ya simu anazo daiwa kuiba Shilole
Msanii huyo alikumbwa na kasheshe hilo Julai 19, 2013 nyumbani kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sinza Mori, Dar. Siku hiyo Diamond alikuwa akifuturisha na aliwaalika watu mbalimbali wakiwemo mastaa lakini nusura futuru iingie doa kufuatia zogo hilo.

MAGAZETI YA LEO JULAI 24, 2013

Tuesday, July 23, 2013

MASELA WAUWANA KWA MARUNGU KISA DEMU WA KISUMKUMA...!!!


Mnamo tarehe 21/07/2012 majira ya saa 23:30hrs huko kijiji cha Nkwangu wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, Seni s/o Sandu, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu aliuawa kwa kupigwa fimbo kichwani na Tolo s/o Seko, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu.

Chanzo ni ugomvi wa kumgombania msichana aitwaye Holo d/o Kulwa, miaka 16, Msukuma mkulima na mkazi wa Nkwangu.


Mtuhumiwa amekamatwa na taratibu za kumfikisha mahakamani zinaandaliwa.


Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishna msaidizi wa polisi diwani athumani anatoa wito kwa jamii kutojichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na kudhibiti hasira zao kwa kuyatatua matatizo ya kimapenzi kwa njia ya mazungumzo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.


Signed by, [Diwani Athumani – ACP] kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya. 


Source: Watemi

MAGAZETI YA LEO JULY 23, 2013


DSC 0061 f2b62
DSC 0062 6a196

KIKWETE AWATAKA UMOJA WA MATAIFA KURUHUSU SILAA KATIKA OPERATIONI ZAO



Rais Kikwete akitoa heshima za mwisho kwa marehemu askari waliouwawa huko Darfur wakitekeleza majukumu ya umoja wa mataifa ya kulinda amani.


Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete ameutaka Umoja wa Mataifa (UN), kuruhusu kutumika kwa mtutu katika operesheni za kulinda amani zinazoendelea.
Alitoa kauli hiyo jana baada ya kutoa heshima zake kwa wapiganaji saba wa Tanzania waliokuwa Darfur, Sudan katika operesheni ya kulinda amani ya UN na Afrika (Unamid) ambao waliuawa na kundi linalodaiwa la wanamgambo wa Janjaweed wanaoungwa mkono na Serikali ya Sudan inayoongozwa na Rais Omar al-Bashir.
Wapiganaji waliouawa ni Oswald Chaula kutoka 42KJ Chabruma, Songea, Peter Werema (44KJ Mbeya), Fortunatus Msofe (36KJ Msangani, Pwani), Rodney Ndunguru (92KJ Ngerengere), Mohamed Juma (94KJ Mwenge), Mohamed Chukilizo (41KJ Nachingwea) na Shaibu Othman (MMJ- Upanga).
“Lazima nikiri kuwa taarifa hiyo ya vifo vya vijana wetu ilinihuzunisha, kunisikitisha na kunikasirisha. Kwa nini watu wa Darfur wawaue wanajeshi wetu ambao wamekwenda kule kuwasaidia wapate utulivu ili kunusuru maisha yao, kuwaondolea wasiwasi na kuwawezesha wafanye shughuli zenye tija kuendesha maisha yao?
“Moja kwa moja sikusita kuamini kuwa waliofanya hivyo ni watu wahalifu. Tangu uhuru ni sera ya nchi yetu kutetea wanyonge dhidi ya ukoloni, ubaguzi, uonevu, dhuluma na watu wote walioko katika mazingira hatarishi Afrika na duniani. UN ifanyie marekebisho sheria ili majeshi yanayolinda amani yawe na nguvu za kujihami ili kuzuia maafa yanayoweza kujitokeza.”

GODBLESS LEMA AFYATUA KOMBORA LINGINE....!!!




CHAMA cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza kuanza kutoa mafunzo ya kujihami kwa vijana wao maarufu kama Red brigedi kuanzia Agosti mosi, mwaka huu.

Akitangaza tarehe hiyo jana wakati wa mkutano wa chama hicho uliofanyika Mbalizi wilaya ya Mbeya Vijijini, kiongozi wa ulinzi wa chama hicho kanda ya Nyanda za juu kusini Lucas Mwampiki, alisema kuwa ameamua kuweka wazi adhima hiyo ili serikali isiendelee kusumbuka kuwa inao uwezo wa kuwazuia.

‘’Polisi msisumbuke kutafuta kuwa tutaanza lini, ni hivi, tutaanza tarehe 1, mwezi wa nane mwaka huu’’ alisema Mwampiki ambaye pia ni diwani wa kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.

TAIFA STARS KUIFUATA UGANDA 'THE CRANES' JUMATANO, KUKIPIGA JUMAMOSI

 
 
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka Mwanza keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.
Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen kesho (Julai 23 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi chake. Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye hoteli ya La Kairo jijini Mwanza.

HAWA NDIO ASKARI WALIOKUFA DARFUR WAKILINDA AMANI - MUNGU ZILAZE ROHO ZAO PEMA PEPONI AMINA


 MT 97024 PTE Fortunatus Wilbard Msofe- 36 KJ

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...