Thursday, July 04, 2013
MGAMBO WAMUUA MKULIMA KWA KUMPIGA FIMBO YA KICHWA MBEYA...!!!
Watu wawili ambao ni askari mgambo, wamekimbilia kusikojulikana bado,
wanatafutwa na polisi baada ya kumpiga kwa fimbo kichwani na kumwua mkulima
aliyetambulika kwa jina la Gigwa Malegi (55, Msukuma) na mkazi wa kijiji cha
Iyonyo.
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Barakael Masaki inasema kuwa mauaji hayo yalitokea tarehe Mosi Julai, 2013 majira ya saa moja jioni katika kijiji cha Totowe wilayani Chunya, Mbeya.
Taarifa hiyo imewataja watuhumiwa kuwa ni Focus Fabian na Charles (jina la pili halijafahamika bado).
Imeelezwa kuwa chanzo cha kupigwa na kuuawa marehemu kinatokana na kukutwa akilisha mifugo (ng'ombe) kaitka eneo oevu kandoni mwa ziwa Rukwa.
Kamanda Masaki ametoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi badala yake amewasihi watatue matatizo yao kwa mazungumzo na kwa kufuata sheria.
Ametoa wito kwa watuhumiwa kujisalimisha mikononi mwa askari mara moja ama yeyote mwenye taarifa za watuhumiwa, azitoe mara moja katika mamlaka husika ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Barakael Masaki inasema kuwa mauaji hayo yalitokea tarehe Mosi Julai, 2013 majira ya saa moja jioni katika kijiji cha Totowe wilayani Chunya, Mbeya.
Taarifa hiyo imewataja watuhumiwa kuwa ni Focus Fabian na Charles (jina la pili halijafahamika bado).
Imeelezwa kuwa chanzo cha kupigwa na kuuawa marehemu kinatokana na kukutwa akilisha mifugo (ng'ombe) kaitka eneo oevu kandoni mwa ziwa Rukwa.
Kamanda Masaki ametoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi badala yake amewasihi watatue matatizo yao kwa mazungumzo na kwa kufuata sheria.
Ametoa wito kwa watuhumiwa kujisalimisha mikononi mwa askari mara moja ama yeyote mwenye taarifa za watuhumiwa, azitoe mara moja katika mamlaka husika ili hatua za kisheria zichukuliwe.
RAIS WA MISRI ATIMULIWA NA JESHI LA NCHI HIYO
jeshi nchini Misri limemuondoa madarakani Rais aliyechaguliwa kwa njia ya kidemokrasia nchini humo Mohamed Morsi na imemteuwa kiongozi wa muda wa nchi baada ya maandamano makubwa yanayoipinga serikali.
Akihutubia kwa njia ya televisheni jumatano jioni, mkuu wa jeshi, Abdul Fatah Khalil Al-Sisi alisema katiba ya Misri imesitishwa kwa muda na mkuu wa mahakama ya katiba ameteuliwa kuwa kiongozi wa muda nchini humo.
Sisi alitangaza kwamba jeshi linaangalia watu wa Misri kufuatana na maandamano makubwa ya upinzani yakidai kuwa Rais Mohamed Morsi ajiuzulu.
Kufuatia hotuba ya kwenye televisheni Bwana Morsi alitoa taarifa kupitia akaunti yake ya Twitter, akiita hatua ya jeshi ni “mapinduzi kamili”. Aliwasihi wa-misri wote kukataa hatua ya jeshi lakini pia aliwataka kuwa na amani.
Kiongozi mpya wa muda nchini Misri, Adli Mansour ana umri wa miaka 68 ni mkuu wa sheria katika mahakama ya juu ya katiba. Ataapishwa alhamisi.
Kama sehemu ya mwongozo mpya unaoungwa mkono na jeshi kwa nchi, sisi aliutaka uchaguzi wa urais na wabunge, jopo kutathmini katiba na kamati ya mashauriano kitaifa. Alisema mwongozo ulikubaliwa na makundi kadhaa ya kisiasa.
Wednesday, July 03, 2013
MJUKUU WA MANDELA AFIKISHWA MAHAKAMANI....!!!
Jamaa za familia ya aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela,
wamewasilisha kesi ya uhalifu dhidi ya mjukuu wa Mandela,Mandla Mandela.
Msemaji
wa polisi, Mzukisi Fatyela aliambia BBC kuwa maafisa wa usalama
watachunguza tuhuma dhidi ya Mandla za kufukua makaburi kinyume na
sheria
Mwendesha mashtaka wa umma, kisha ataamua ikiwa amshtaki Mandla au la.
Inahusisha
maiti za watoto watatu wa Mandela ambao inaaminika walifukuliwa na
Mandla kutoka makaburi ya familia miaka miwili iliyopita.
Katika
kesi nyingine, jamaa kumi na sita wa familia ya Mandela, wanataka
kurejesha miili hiyo katika kijiji cha Qunu, ambako Mandela, ambaye
anaumwa sana hospitalini anataka kuzikwa akifa.
Kesi hiyo
inayosikilizwa katika mahakama kuu ya Mthatha, katika mkoa wa Mashariki
iliakhirishwa hapo jana kuanza kusikilizwa leo.
Wiki
jana, mahakama ilitoa amri ya muda kwa maiti za watatu hao kuhamishwa
kutoka nyumbani kwa Mandla katika kijiji cha Mvezo hadi Qunu, umbali wa
kilomiya 22.
Lakini Mandla Mandela, ambaye alitawazwa kama kiongozi wa kijamii na babu yake, sasa anapinga vikali amri hiyo.
SIFA ZA GARI YA OBAMA INAWEZA KWENDA 97KM TU KWA SAA AT MAXIMUM ..... YA JK IPO JUU KWA SPEED
Walioona msafara wa obama wataona namna msafara ulipita kwa speed ya kawaida sana tofauti na ile speed tuliyozoea anapopita JK, our president normally huwa ana cruise at an average of 120kmh.
Ile speed ikanifanya nitafute habari zaidi, niliyoyaona yamenishangaza, kumbeMaximum speed ya limo ya obama ni 60mph tu, sawasawa na kilimita kama 97 kwa saa. hii gari haina ujanja wa kwenda hata 100km kwa saa, hata boda boda inaweza kwenda speed kuliko hii gari
- ina uzito unaokadiria kukaribia tani 9
- matumizi ya mafuta ni 8mpg, kwa
lugha ingine inahitahi lita 35.31 ili kutembea kilomita 100, hii ni sawa
na lita 1 kwa kila kilomita 2.8
- vioo vyote havifunguki isipokua pale kwa dereva kwa mbele. gari iko 100% sealed
- Vioo vya dirishani vina thickness ya inchi 5 wakati milango ni nchi 8.
- kutokana na unene wa madirisha
na milango, obama hawezi kusikia chochote kinachoendelea nnje, spika
zimewekwa ili kunasa sauti za nje
- gari ina night vision kamera zinazomuwezesha dereva kuendesha usiku bila hata kuwasha taa
OBAMA AAHIDI KUJA TENA NA KUPITA MITAANI ILI WATU WAMUONE...!!!
Kana kwamba
alisikia kilio cha wakazi wa Dar es Salaam waliokuwa na shauku ya
kumwona lakini ikashindikana, Rais Barack Obama wa Marekani amewaomba
radhi kwa hali hiyo.
Akizungumza
juzi wakati wa dhifa iliyoandaliwa kwa ajili yake na ujumbe wake na
Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Dar es Salaam, Obama alisema
akirudi nchini siku zijazo, atapita mitaani akiwa katika gari la wazi.
"Niliona
wananchi walivyojitokeza kwa wingi kutupokea barabarani, nilifarijika
sana lakini hawakuweza kutuona vizuri kwani tulikuwa ndani ya gari
maalumu-The Beast.
"Miaka ya
sitini Rais John Kennedy alipokuja hapa, alipita na gari la wazi
mitaani wananchi wakamwona, naomba radhi nikija tena nitaonekana,"
alisema Obama.
Watu wengi
waliozungumza na vyombo vya habari walionesha dhahiri kiu ya kutaka
kumwona Rais huyo wa kwanza mweusi wa Marekani, lakini wakaishia kuona
gari lake ambalo hata hivyo, lilipita kwa kasi barabarani kwenda Ikulu
na kurudi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
WATUHUMIWA WA MAUAJI YA DAUD MWANGOSI WAACHIWA HURU NA MAHAKAMA...!!!
Kiongozi huyo pamoja na wenzake walikuwa wakikabiliwa na makosa matatu likiwemo la kufanya mkutano bila kibali pamoja na kuharibu mali ambazo ni kofia za pikipiki (helmenti) 2 za polisi katika tukio lililosababisha kuuawa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Channel Ten Daudi Mangosi katika kijiji cha Nyololo wailayani Mufindi.
Kutokana na tuhuma hizo Chadema iliweka pingamizi za kutaka kesi hiyo ifutwe kwa kuwa ilifunguliwa kinyume cha sheria.
Wakili wa Chadema Lugaziya akisaidiana na mwanasheria wa Chadema Luka Sinkala Mwenda waliweka pingamizi kuwa aliyetoa amri ya kusitisha mkutano na kusababisha kifo cha mwandishi wa habari huyo ni kamanda wa Polisi Michael Kamuhanda ambapo aliingilia kazi ya OCD wa Mufindi kwa kuwa hakupaswa kutoa amri hiyo, kwamba wakati amri ya kusitisha mkutano ilitolewa wakati hakukukuwa na vurugu na polisi walipiga mabomu wakati watu wanatawanyika.
Pingamizi zingine ni kwamba aliyetoa amri ya kutawanya mkutano hakuwa na cheo chochote.Wakati Chadema ikizuiliwa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Bububu Zanzibar walikuwa na mkutano wa kampeni za uchaguzi..
STOKE CITY YAKAMILISHA DILI YA KUMSAJILI MARC MUNIESA KUTOKA BARCELONA
Marc Muniesa, Beki wa timu ya Barcelona aliyesaini mkataba wa kuichezea Stoke City Msimu ujao
Aliyekuwa
beki wa Timu ya Barcelona ya Uhispania Marc Muniesa kijana wa Miaka 29
amekamilisha Usajili wake wa kuicheza timu yake mpya ya Stoke City ya
Uingereza.
Marc
Muniesa alikuwa ni moja wa memba wa kikosi cha Hispania chini ya Miaka
21 kilichoshinda Katika ligi ya Ubingwa wa ulaya chini ya Miaka 21.
Marc
Muniesa, alisema " anafurahi kujiunga na timu ya Stoke City na
atajitahidi kadri ya uwezo wake katika kuhakikisha timu yake hiyo mpya
ya Stoke anailetea Ushindi"
Aliongezea
kwa kusema Hakuwa na uamuzi mgumu katika kuamua kujiunga na timu hiyo
ya Uingereza ya Stoke City na nimekuja uingereza jana kwaajili ya
kukutana na watu wa klabu hii ya Stoke City na kuangalia Uwanja wa
Mazoezi na kuona unavutia
MACHANGUDOA WALALAMIKIA UJUO WA OBAMA WASEMA AFADHALI UJIO WA BUSH:
Rais Barack Obama wa Marekani
Polisi wa Kimarekani waliokuwa mwiba mkali kwa ulinzi wa Obama
Machangudoa wakiwinda wazungu maeneo ya Oysterbay Karibu na Ubalozi wa Merikani
Machangudoa wakiwa kazini
Na Livingstone Mkoi
Katika hali ilisiyokuwa ya kawaida wakina dada maarufu wanaojihusisha na biashara ya kuuza miili yao
maarufu kwa majina ya machangudoa wameulalamikia ujio wa Rais Barack
Obama kwa kile kilichodaiwa haukuwa na faida yoyote kwa kukosa dili za
pesa.
Wakiongea
Xdeejayz kwenye baadhi ya sehemu wanazopatikana wakina dada hao walisema
kuwa” Tumesikitishwa sana na ujio wa Obama kwani tulikuwa tumejipanga
kupiga hela ndefu sana lakini patutu kwani watu wake tuliokuwa
tumewategemea kuwanasa walikuwa busy na usalama pia kukaa kipindi kifupi
kumechangia sisi kukosa mapato" Walisema wakina dada hao waliokutwa
maeneo ya Coco Beack
Tuesday, July 02, 2013
ANGALIA RAIS OBAMA AKIONYESHA UWEZO WAKE WA KUPIGA DANADANA....!!!
Rais Kikwete akimwangalia Obama wakati akipiga mpira danadana.
OBAMA akionyesha uwezo wa kumiliki mpira kwa kupiga kichwa bila kutua chini wakati alipotembelea mit
ambo ya kuvua umeme Ubungo jijini Dar es salaam muda mfupi kabla ya kuondoka nchini.
Hapa akipiga danadana huku akishuhudiwa na Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI AMALIZA ZIARA YAKE YA SIKU MBILI HAPA NCHINI
Rais
Barack Obama wa Marekani ameondoka nchini mchana huu kurudi nchini
Marekani,baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili hapa nchini
iliyoanza jana.Rais Obama na mwenyezi wake Rais Jakaka Kikwete,leo
walifanya ziara ya kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Symbion
iliopo Ubungo jijini Dar es Salaam na kuzindua rasmi mradi huo.
iliopo Ubungo jijini Dar es Salaam na kuzindua rasmi mradi huo.
MAREKANI KUFUNGUA UKURASA MPYA KATIKA UWEKEZAJI NCHINI.
Rais
wa Marekani Barack Obama akiwahutubia wafanyabiashara leo(jana) jijini
Dar es salaam juu ya mpango wa Nchi yake wa kufungua milango ya
ushirikiano na uwekezaji kwa Nchi za Afrika Mashariki katika sekta
mbalimbali na hivyo kuongeza kiwango cha bidhaa ya Afrika Mashariki
zinazoingia nchini Marekani.
Rais
wa Marekani Barack Obama akiwa katika mkutano jana (leo) jijini Dar es
salaam wa kujadiliana na watendaji wakuu(CEO) wa Makampuni mbalimbali
yaliyowekeza Afrika juu ya kuimarisha fursa za ushirikiano kati ya
Marekani na Afrika katika uwekezaji kwenye sekta mbalimbali za
maendeleo.
(Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaa)
………………………………………………
Na Eleuteri Mangi—MAELEZO—Dar es salaam
Serikali
ya Marekani imeahidi kufungua ukurasa mpya kwa Nchi za Afrika Mashariki
kwa kuongeza uwekezaji katika sekta mbalimbali ili kuinua uchumi wan
chi hizo.
Kauli
hiyo imetolewa leo mjini Dar es salaam na Rais Barack Obama kwenye
hotuba yake kwa wafanyabiashara wakati wa ziara yake ya siku mbili
nchini Tanzania.
Alisema
kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza kiwango cha bidhaa kutoka Nchi za
afrika Mashariki kuingia nchini Marekani na hivyo kuimarisha ushirikiano
wa kibiashara na kiuchumi kwa manufaa ya pande zote.
“Sasa
ni wakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwekeza nchini Marekani ili
kuongeza mauzo yake nchini Marekani hadi ifike asilimia 40,” alisema
Rais Obama.
NANDO WA TANZANIA APENDEKEZWA KUTOKA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER...KURA YAKO INAHITAJIKA
Mchezo unazidi kuwa mgumu kadri siku zinavyozidi kwenda sababu idadi ya wanaopaswa kuendelea na mchezo ndivyo inavyohitajika kuwa ndogo mpaka siku ya 91 atakapobaki mtu mmoja wa kukabidhiwa $300,000 kama zawadi ya BBA The Chase.
Nominations za wiki hii zimewagusa baadhi ya washiriki ambao hawajawahi kabisa kupendekezwa kutoka, na wengine ambao wameshawahi kupendekezwa mara moja na zaidi lakini waliokolewa na kura za watazamaji.
Baada ya kupona kutoka wiki iliyopita na kuwa HOH , cheo kilichompa nafasi ya kujiokoa katika nomination zilizopita Nando wa Tanzania ameungana na washiriki wengine 6 katika orodha ya majina yaliyotajwa na Biggie kuingia katika kikaango cha eviction ya wiki hii.
Washiriki ambao wameingia kwa mara ya kwanza katika nominations za wiki hii ni pamoja na aliyekuwa kipenzi cha Huddah mjengoni, Angelo wa Afrika Kusini ambaye amewekwa na HOH wa wiki hii Elikem aliyejiokoa na nafasi yake kumuwekea yeye.
Fatima wa Malawi, Bimp wa Ethiopia pamoja na Cleo wa Zambia ndio washiriki wengine ambao wameingia dangerzone kwa mara ya kwanza toka mchezo umeanza.
Washiriki ambao waliwahi kupendekezwa na kuokolewa na kura za watazamaji na wameingia tena wiki hii ni pamoja na Pokello wa Zimbabwe, Hakeem wa Zimbabwe pamoja na Nando wa Tanzania.
Wiki hii Ghana na Nigeria ndio zimekalia viti vya utawala wa nyumba, Ruby ikiongozwa na Elikem na Melvin akiiongoza Diamond.
Kura yako inahitajika kumwokoa Nando ili aendelee kubaki na kuiwakilisha Tanzania katika msimu wa 8 wa BBA The Chase unaoendelea Afrika Kusini.
MAHAKAMA YAWATIA MBARONI WAPENZI WAWILI WALIOAMUA KUTALII WAKIWA UCHI....!!!
Njemba moja, Stephen Gough aliyewahi kuwa mwanajeshi amekamatwa na polisi katika Jiji la Portsmouth, Uingereza baada ya kukutwa na mpenzi wake wakidunda kutalii mitaani wakiwa uchi wa nyama.
Mwanamke Melodine Roberts aliyefuatana naye aliachiwa na polisi kwa kuwa mara baada ya kuonywa kuacha tabia hiyo, aliacha lakini mpenzi wake huyo aligoma na hii ni mara ya 14 akifanya hivyo licha ya kufungwa jela huko nyuma.
Baada ya kugoma polisi walimfunga pingu na wakampeleka mahakamani moja kwa moja ambapo Mwendesha Mashitaka, Simon Jones alisema Gough alikuwa amekiuka sheria na aliwahi kufungwa miaka sita na moja ya makosa yaliyosababisha afungwe ni kutemba uchi wa mnyama hadharani.
Baada ya maelezo hayo, jaji aliyekuwa akisikiliza shauri hilo, Sarah Munro alisema kuwa kwenda jela kwa mtu huyo ndiyo ilikuwa njia pekee kwake kwa kuwa hilo ni kosa kubwa katika jamii ya Waingereza na ni ukiukwaji wa taratibu za umma wa sehemu hiyo.
POLISI WALA KICHAPO KIKALI KUTOKA KWA POLISI WENZAO BAADA YA KUKAIDI AMRI...!!!
MAAFISA watatu wa polisi wa utawala (AP)
walijeruhiwa kwenye mapigano yaliyozuka kati yao na wenzao wa Uganda
kwenye kisiwa kinachozozaniwa cha Migingo.
Mzozo huo wa
mwishoni mwa wiki ulianza pale maafisa wa Uganda waliokuwa na sare rasmi
walipoenda katika ufuo wa karibu wa Nyandiwa kurekebisha mashua yao.
Lakini wakazi wa
Nyandiwa waliwazuia kutia nanga wakisema kwa vile walikuwa na sare na
bunduki, walihofia wangeliwahangaisha kwa kuwapokonya samaki wao.
Mmoja wa
wavuvi wa eneo hilo Bw Oloo Okello, alisema maafisa hao wa Uganda
walirejea Migindo wakuwa na hasira bila ya kurekebisha boti lao.
“Waliporejea walisema
kwamba polisi wa Utawala wa Kenya wa kitengo cha kushika doria mpakani,
Rural Border Patrol Unit (RBPU), walio kisiwani Ugingo hawatakiwi kutia
guu Migingo.
TANZANIA YAUMBULIWA....GAZETI MAARUFU LA MAREKANI LAANIKA UKATILI UNAOTENDEKA NCHINI
Tanzania imekosolewa na gazeti maarufu la
Marekani wakati Rais Obama akipokewa kwa nderemo na
vifijo.
Gazeti hilo maarufu nchini Marekani la The New York Times, limechapisha habari za kuonesha matukio ya ukatili yanayofanyika Tanzania.
Habari hiyo iliyochapishwa katika toleo lake ya Juni 30, imeleza tukio la kuteswa na kuumiza kwa kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Stephen Ulimboka.
Mwandishi wa habari hiyo amejaribu kunukuu kauli ya Dk. Ulimboka akieleza jinsi alivyotekwa na kuteswa kinyama kisha kutupwa kwenye Msitu wa Mabwepande.
Mwandishi huyo amesema kuwa Tanzania inaheshimika nje ya nchi kama kisiwa cha amani ndani ya ukanda wenye machafuko wa Afrika Mashariki.
Kwamba kutokana na sifa hizo, Tanzania imejizolea sifa na ufadhili wa fedha kutoka kwa mataifa mbalimbali yaliyoendelea, ikiwamo Marekani, ambayo mwaka jana
iliipatia zaidi ya dola milioni 480.
Alisema kuwa wakati Rais Obama akiwasili Tanzania makundi ya kutetea haki za binadamu na chama kikuu cha upinzani wanasema matukio ya vitisho na ukandamizaji wa wapinzani wa kisiasa yanashika kasi. “Kuna woga, si amani”.
Gazeti hilo maarufu nchini Marekani la The New York Times, limechapisha habari za kuonesha matukio ya ukatili yanayofanyika Tanzania.
Habari hiyo iliyochapishwa katika toleo lake ya Juni 30, imeleza tukio la kuteswa na kuumiza kwa kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Stephen Ulimboka.
Mwandishi wa habari hiyo amejaribu kunukuu kauli ya Dk. Ulimboka akieleza jinsi alivyotekwa na kuteswa kinyama kisha kutupwa kwenye Msitu wa Mabwepande.
Mwandishi huyo amesema kuwa Tanzania inaheshimika nje ya nchi kama kisiwa cha amani ndani ya ukanda wenye machafuko wa Afrika Mashariki.
Kwamba kutokana na sifa hizo, Tanzania imejizolea sifa na ufadhili wa fedha kutoka kwa mataifa mbalimbali yaliyoendelea, ikiwamo Marekani, ambayo mwaka jana
iliipatia zaidi ya dola milioni 480.
Alisema kuwa wakati Rais Obama akiwasili Tanzania makundi ya kutetea haki za binadamu na chama kikuu cha upinzani wanasema matukio ya vitisho na ukandamizaji wa wapinzani wa kisiasa yanashika kasi. “Kuna woga, si amani”.
JINSI CIA NA FBI WALIVYOMLINDA RAIS OBAMA KWA ULINZI MKALI AJABU
Helikopta ya Polisi ikiwa katika doria ya hapa na pale, hata hivyo eneo lote la uwanja wa Ndege ulidhibitiwa na Wamarekani wenyewe ikiwemo na kazi ya kuongoza ndege.
Ulinzi kila
kona
Ulinzi
ulimarishwa.
Bendera ya
Tanzania ikiwekwa katika gari lililombeba Rais wa Marekani, Barack
Obama.
Gari
alilopanda Rais Obama
(Picha na Habari Mseto Blog)
KIKAPTURA KIFUPI CHA MTOTO WA KIKE WA RAIS OBAMA CHAZUA GUMZO KUBWA
amevaa kikaptura kifupi (short shorts, al maarufu kama daisy dukes.) Mapaparazzi walimpiga picha binti huyo akiwa mitaani na raha zake na kuuliza mitandaoni kama ni sahihi kwa binti wa miaka 12, kuvaa kaptura fupi hivyo. Kama kawaida za mitandaoni, kilichozuka ni ubishi mkali kati ya wanaoona si sahihi, hasa kwa binti ya rais, na wale wanaoona ni poa tu. Wewe upo kwenye camp ipi? Unaweza ruhusu binti yako avae kaptura kama hii?
Monday, July 01, 2013
HUU NDIO UJUMBE MZITO TOKA KWA ZITTO KABWE KWENDA KWA OBAMA
Obama: Tunataka Uwazi wa Mikataba. Omba radhi Kwa mauaji ya Lumumba
Hatimaye Barack Obama, Rais wa Marekani anatembelea tena bara la Afrika. Hii itakuwa ni mara ya pili Obama kutembelea Bara hili alikotoka baba yake baada ya ziara yake ya kwanza mwaka 2009. Mwaka huo alitembelea Ghana na Misri ilhali mwaka huu anatembelea Senegali, Afrika Kusini na Tanzania. Ziara hiyo itakayoanza tarehe 26 mwezi Juni, itamfikisha Tanzania tarehe 1 Julai na kuondoka siku ya pili yake.
Uchaguzi wa Obama kuwa Rais wa Marekani ulipokolewa kwa shangwe Afrika nzima. Wakati Waziri wa mambo ya nje wa Nigeria alilia kwa furaha, nchi ya Kenya ilitangaza siku ya mapumziko na Rais wa zamani wa Afrika Kusini ndugu Nelson ‘Madiba’ Mandela alisema ‘ushindi wa Obama unawafanya Waafrika wathubutu kuota ndoto (Jarida la The Economist). Hapa Tanzania kulikuwa kuna shamra shamra za kila namna na magazeti yaliweka vichwa vya habari kana kwamba ni Rais wa Tanzania aliyechaguliwa.
Waafrika walikuwa na matumaini makubwa sana na bwana Obama. Yamefikiwa?
Ni vema ifahamike kuwa Barack Obama ni Rais wa Marekani na siku zote atalinda maslahi ya Marekani tu. Kuwa na matumaini makubwa kwamba labda yeye angeliweza kuiweka Afrika mbele sana ilikuwa ni kujifurahisha tu nafsi. Maslahi ya Marekani ni ya kipaumbele kuliko kitu kingine chochote kwa Rais Obama. Kwa wengi Obama amekuwa kama amewavunja moyo.
Hatimaye Barack Obama, Rais wa Marekani anatembelea tena bara la Afrika. Hii itakuwa ni mara ya pili Obama kutembelea Bara hili alikotoka baba yake baada ya ziara yake ya kwanza mwaka 2009. Mwaka huo alitembelea Ghana na Misri ilhali mwaka huu anatembelea Senegali, Afrika Kusini na Tanzania. Ziara hiyo itakayoanza tarehe 26 mwezi Juni, itamfikisha Tanzania tarehe 1 Julai na kuondoka siku ya pili yake.
Uchaguzi wa Obama kuwa Rais wa Marekani ulipokolewa kwa shangwe Afrika nzima. Wakati Waziri wa mambo ya nje wa Nigeria alilia kwa furaha, nchi ya Kenya ilitangaza siku ya mapumziko na Rais wa zamani wa Afrika Kusini ndugu Nelson ‘Madiba’ Mandela alisema ‘ushindi wa Obama unawafanya Waafrika wathubutu kuota ndoto (Jarida la The Economist). Hapa Tanzania kulikuwa kuna shamra shamra za kila namna na magazeti yaliweka vichwa vya habari kana kwamba ni Rais wa Tanzania aliyechaguliwa.
Waafrika walikuwa na matumaini makubwa sana na bwana Obama. Yamefikiwa?
Ni vema ifahamike kuwa Barack Obama ni Rais wa Marekani na siku zote atalinda maslahi ya Marekani tu. Kuwa na matumaini makubwa kwamba labda yeye angeliweza kuiweka Afrika mbele sana ilikuwa ni kujifurahisha tu nafsi. Maslahi ya Marekani ni ya kipaumbele kuliko kitu kingine chochote kwa Rais Obama. Kwa wengi Obama amekuwa kama amewavunja moyo.
WATANZANIA 60 WAKAMATWA ZIARA YA OBAMA....!!!
Watanzania
60 wamekamatwa Afrika Kusini kutokana na maandalizi yaliofanyika nchini
humo ya kumpokea Rais Barack Obama wa Marekani.
Rais Obama amewasili Afrika Kusini juzi kwa ziara ya siku tatu akitokea Senegal.
Watu hao wamekamatwa baada ya kudaiwa kuishi kinyume cha sheria Afrika Kusini. Baada ya Watanzania hao kutiwa mbaroni na vyombo vya usalama wamehifadhiwa hapa nchini kusubiri hatua za kisheria zaidi.
Ofisa mmoja wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, Sadiki Msele amesema Watanzania hao walirejeshwa nchini jana na kwamba hivi sasa wanasubiri sheria kuchukua mkondo wake.
“Safisha safisha kama iliofanyika jijini Dar es Salaam, pia imefanyika Afrika Kusini na kuwaathiri wafanyabiashara na watu wengine,” amesema ofisa huyo.
Hivi sasa Rais Obama yupo Afrika Kusini akiwa ameongoza na mkewe Michelle Obama na watoto wao wawili; Malia na Sasha.
Leo Rais Obama na ujumbe wake anatarajiwa kutua Tanzania kwa ziara ya siku mbili na Jumanne ataondoka kurejea Marekani.
Rais Obama amewasili Afrika Kusini juzi kwa ziara ya siku tatu akitokea Senegal.
Watu hao wamekamatwa baada ya kudaiwa kuishi kinyume cha sheria Afrika Kusini. Baada ya Watanzania hao kutiwa mbaroni na vyombo vya usalama wamehifadhiwa hapa nchini kusubiri hatua za kisheria zaidi.
Ofisa mmoja wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, Sadiki Msele amesema Watanzania hao walirejeshwa nchini jana na kwamba hivi sasa wanasubiri sheria kuchukua mkondo wake.
“Safisha safisha kama iliofanyika jijini Dar es Salaam, pia imefanyika Afrika Kusini na kuwaathiri wafanyabiashara na watu wengine,” amesema ofisa huyo.
Hivi sasa Rais Obama yupo Afrika Kusini akiwa ameongoza na mkewe Michelle Obama na watoto wao wawili; Malia na Sasha.
Leo Rais Obama na ujumbe wake anatarajiwa kutua Tanzania kwa ziara ya siku mbili na Jumanne ataondoka kurejea Marekani.
WAPENZI WADONDOKA NA KUFA WAKATI WAKIFANYA MAPENZI DIRISHANI...!!!
Wapenzi wameanguka na kufa baada ya dirisha walipokuwa wakifanyia mapenzi kufunguka ghafla nchini China.
Wawili
hao wanasemekana kudondoka kutoka kwenye dirisha la jengo moja la
makazi kwenye jiji la Wuhan nchini humo pale dirisha hilo walilokuwa
wameegemea kufunguka.
Mashuhuda
walivieleza vyombo vya habari vya China kwamba wapenzi hao
walikumbatiana wakati wakianguka kwenye njia ya waenda kwa miguu nje.
Kwa
mujibu wa The Sun, chanzo kimoja cha habari kilisema: "Huku wawili hao
wakiwa wameshikamana vilivyo, walianguka nje ya jengo hilo."
Picha za kuogofya zimefichuliwa kwenye tovuti za nchini humo zikionesha wapenzi hao wakiwa wamefunikwa kwa mashuka na polisi.
Damu ilitapakaa kwenye njia ya waenda kwa miguu karibu na wapelelezi wanaonekana wakichunguza eneo la tukio.
Miili
ya wapenzi hao ilipigwa picha karibu na baiskeli ambayo ilikuwa
imelazwa chini, lakini hakukuwa na ripoti zozote kwamba yeyote chini
alikuwa amejeruhiwa katika ajali hiyo.
Ripoti zinasema kwamba madirisha hayo kwenye jengo hilo la makazi yalikuwa hayana ubora unaotakiwa.
Inafikiriwa
kwamba mwanaume huyo na mwanamke wanawezekana walikuwa wakijaribu
kujipooza kando ya dirisha hilo ndipo tukio hilo likatokea.
Haikufahamika ni umbali gani kutoka juu wawili hao walikuwa wakati wakianguka.
Wuhan ni jiji maarufu zaidi lililopo katikati ya China.
Ukiwa na historia ya miaka 3,500 ni moja kati ya miji mikongwe na iliyostaarabika katika China.
HUYU NDIYE MWANAMKE ALIYEMKATA UUME MUMEWE AFUNGWA MAISHA GEREZANI...!!!
Mwanamke mmoja wa California ambaye alituhumiwa kukata uume wa mumewe kabla ya kuutupa kwenye mashine ya kusagia taka amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani.
Catherine
Kieu, mwenye miaka 50, alipatikana na hatia ya mashitaka ya kutesa na
kosa la kuharibu viungo vya mwili katika shambulio la Julai 11, 2011 na
kuhukumiwa kifungo cha maisha jela, lakini anaweza kufikiriwa kupewa
msamaha baada ya kutumikia miaka saba.
Alitiwa hatiani Aprili kwa kila kosa moja la kutesa na kuharibu viungo vya mwili.
Muathirika, anayefahamika kama Glen wakati wote wa kesi, alikuwa mahakamani kwa ajili ya hukumu ya jana.
"Natumaini
hii itakuwa mara ya mwisho kabisa ninayoweza kumwona," alisema Glen.
"Najihisi nafuu kiasi fulani, na ilikuwa siku ya huzuni kubwa kwangu."
Muathirika huyo alikimbizwa hospitali, lakini upasuaji kurejesha uume wake haukufanikiwa.
Wakati
wa kesi hiyo, muathirika huyo mwenye umri wa miaka 60 alitoa ushahidi
kwamba uume wake hauwezi tena kuunganishwa mahali pake na kwamba anahisi
kama ameuawa.
Kieu
alikuwa na wivu na hasira kuhusu mipango ya mumewe kumpa talaka sababu
alimwona rafiki yake wa zamani wa kike, upande wa mashitaka ulisema.
Subscribe to:
Posts (Atom)