Tuesday, July 02, 2013

MAREKANI KUFUNGUA UKURASA MPYA KATIKA UWEKEZAJI NCHINI.

3
Rais wa Marekani Barack Obama akiwahutubia wafanyabiashara leo(jana) jijini Dar es salaam juu ya mpango wa Nchi yake wa kufungua milango ya ushirikiano na uwekezaji kwa Nchi za Afrika Mashariki katika sekta mbalimbali na hivyo kuongeza kiwango cha bidhaa ya Afrika Mashariki zinazoingia nchini Marekani.
4
Rais wa Marekani Barack Obama akiwa katika mkutano jana (leo) jijini Dar es salaam wa kujadiliana na watendaji wakuu(CEO) wa Makampuni mbalimbali yaliyowekeza Afrika juu ya kuimarisha fursa za ushirikiano kati ya Marekani na Afrika katika uwekezaji kwenye sekta mbalimbali za maendeleo.
(Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaa)
………………………………………………
 
Na Eleuteri Mangi—MAELEZO—Dar es salaam
Serikali ya Marekani imeahidi kufungua ukurasa mpya kwa Nchi za Afrika Mashariki kwa kuongeza uwekezaji katika sekta mbalimbali ili kuinua uchumi wan chi hizo.
Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dar es salaam na Rais Barack Obama kwenye hotuba yake kwa wafanyabiashara wakati wa ziara yake ya siku mbili nchini Tanzania.
Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza kiwango cha bidhaa kutoka Nchi za afrika Mashariki kuingia nchini Marekani na hivyo kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na kiuchumi kwa manufaa ya pande zote.
 “Sasa ni wakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwekeza nchini Marekani  ili kuongeza mauzo yake nchini Marekani hadi ifike asilimia 40,” alisema Rais Obama.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...