Monday, July 01, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 1, 2013


DSC 0234 1d864 
DSC 0233 b4230

HUU NDIO UJUMBE MZITO TOKA KWA ZITTO KABWE KWENDA KWA OBAMA

Obama: Tunataka Uwazi wa Mikataba. Omba radhi Kwa mauaji ya Lumumba

    Hatimaye Barack Obama, Rais wa Marekani anatembelea tena bara la Afrika. Hii itakuwa ni mara ya pili Obama kutembelea Bara hili alikotoka baba yake baada ya ziara yake ya kwanza mwaka 2009. Mwaka huo alitembelea Ghana na Misri ilhali mwaka huu anatembelea Senegali, Afrika Kusini na Tanzania. Ziara hiyo itakayoanza tarehe 26 mwezi Juni, itamfikisha Tanzania tarehe 1 Julai na kuondoka siku ya pili yake.

    Uchaguzi wa Obama kuwa Rais wa Marekani ulipokolewa kwa shangwe Afrika nzima. Wakati Waziri wa mambo ya nje wa Nigeria alilia kwa furaha, nchi ya Kenya ilitangaza siku ya mapumziko na Rais wa zamani wa Afrika Kusini ndugu Nelson ‘Madiba’ Mandela alisema ‘ushindi wa Obama unawafanya Waafrika wathubutu kuota ndoto (Jarida la The Economist). Hapa Tanzania kulikuwa kuna shamra shamra za kila namna na magazeti yaliweka vichwa vya habari kana kwamba ni Rais wa Tanzania aliyechaguliwa.

    Waafrika walikuwa na matumaini makubwa sana na bwana Obama. Yamefikiwa?
    Ni vema ifahamike kuwa Barack Obama ni Rais wa Marekani na siku zote atalinda maslahi ya Marekani tu. Kuwa na matumaini makubwa kwamba labda yeye angeliweza kuiweka Afrika mbele sana ilikuwa ni kujifurahisha tu nafsi. Maslahi ya Marekani ni ya kipaumbele kuliko kitu kingine chochote kwa Rais Obama. Kwa wengi Obama amekuwa kama amewavunja moyo.

WATANZANIA 60 WAKAMATWA ZIARA YA OBAMA....!!!

Watanzania 60 wamekamatwa Afrika Kusini kutokana na maandalizi yaliofanyika nchini humo ya kumpokea Rais Barack Obama wa Marekani.

Rais Obama amewasili Afrika Kusini juzi kwa ziara ya siku tatu akitokea Senegal.

Watu hao wamekamatwa baada ya kudaiwa kuishi kinyume cha sheria Afrika Kusini. Baada ya Watanzania hao kutiwa mbaroni na vyombo vya usalama wamehifadhiwa hapa nchini kusubiri  hatua za kisheria zaidi.

Ofisa mmoja wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, Sadiki Msele amesema Watanzania hao walirejeshwa nchini jana na kwamba hivi sasa wanasubiri sheria kuchukua mkondo wake.

“Safisha safisha kama iliofanyika jijini Dar es Salaam, pia imefanyika Afrika Kusini na kuwaathiri wafanyabiashara na watu wengine,” amesema ofisa huyo.

Hivi sasa Rais Obama yupo Afrika Kusini akiwa ameongoza na mkewe Michelle Obama na watoto wao wawili; Malia na Sasha.

Leo Rais Obama na ujumbe wake anatarajiwa kutua Tanzania kwa ziara ya siku mbili na Jumanne ataondoka kurejea Marekani.

ANGALIA MITAA MBALIMBALI YA BONGO ILIVYOPAMBWA KWA MAANDALIZI YA UJIO WA OBAMA

 
 
 
 
Barabara ya Baharini mchana wa leo, ikiwa shwari huku ikiwa imepambwa na mabango yenye picha za Rais wa Marekani, Barack Obama na Bendera za Nchi hiyo na Tanzania. KARIBU OBAMA
 
credit: sufiani mafoto

WAPENZI WADONDOKA NA KUFA WAKATI WAKIFANYA MAPENZI DIRISHANI...!!!

 
Wapenzi wameanguka na kufa baada ya dirisha walipokuwa wakifanyia mapenzi kufunguka ghafla nchini China.

Wawili hao wanasemekana kudondoka kutoka kwenye dirisha la jengo moja la makazi kwenye jiji la Wuhan nchini humo pale dirisha hilo walilokuwa wameegemea kufunguka.

Mashuhuda walivieleza vyombo vya habari vya China kwamba wapenzi hao walikumbatiana wakati wakianguka kwenye njia ya waenda kwa miguu nje.
Kwa mujibu wa The Sun, chanzo kimoja cha habari kilisema: "Huku wawili hao wakiwa wameshikamana vilivyo, walianguka nje ya jengo hilo."
Picha za kuogofya zimefichuliwa kwenye tovuti za nchini humo zikionesha wapenzi hao wakiwa wamefunikwa kwa mashuka na polisi.
Damu ilitapakaa kwenye njia ya waenda kwa miguu karibu na wapelelezi wanaonekana wakichunguza eneo la tukio.
Miili ya wapenzi hao ilipigwa picha karibu na baiskeli ambayo ilikuwa imelazwa chini, lakini hakukuwa na ripoti zozote kwamba yeyote chini alikuwa amejeruhiwa katika ajali hiyo.
Ripoti zinasema kwamba madirisha hayo kwenye jengo hilo la makazi yalikuwa hayana ubora unaotakiwa.
Inafikiriwa kwamba mwanaume huyo na mwanamke wanawezekana walikuwa wakijaribu kujipooza kando ya dirisha hilo ndipo tukio hilo likatokea.
Haikufahamika ni umbali gani kutoka juu wawili hao walikuwa wakati wakianguka.
Wuhan ni jiji maarufu zaidi lililopo katikati ya China.
Ukiwa na historia ya miaka 3,500 ni moja kati ya miji mikongwe na iliyostaarabika katika China.

HUYU NDIYE MWANAMKE ALIYEMKATA UUME MUMEWE AFUNGWA MAISHA GEREZANI...!!!

 

Mwanamke mmoja wa California ambaye alituhumiwa kukata uume wa mumewe kabla ya kuutupa kwenye mashine ya kusagia taka amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani.
Catherine Kieu, mwenye miaka 50, alipatikana na hatia ya mashitaka ya kutesa na kosa la kuharibu viungo vya mwili katika shambulio la Julai 11, 2011 na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela, lakini anaweza kufikiriwa kupewa msamaha baada ya kutumikia miaka saba.

Alitiwa hatiani Aprili kwa kila kosa moja la kutesa na kuharibu viungo vya mwili.
Muathirika, anayefahamika kama Glen wakati wote wa kesi, alikuwa mahakamani kwa ajili ya hukumu ya jana.
"Natumaini hii itakuwa mara ya mwisho kabisa ninayoweza kumwona," alisema Glen. "Najihisi nafuu kiasi fulani, na ilikuwa siku ya huzuni kubwa kwangu."
Muathirika huyo alikimbizwa hospitali, lakini upasuaji kurejesha uume wake haukufanikiwa.
Wakati wa kesi hiyo, muathirika huyo mwenye umri wa miaka 60 alitoa ushahidi kwamba uume wake hauwezi tena kuunganishwa mahali pake na kwamba anahisi kama ameuawa.
Kieu alikuwa na wivu na hasira kuhusu mipango ya  mumewe kumpa talaka sababu alimwona rafiki yake wa zamani wa kike, upande wa mashitaka ulisema.

Sunday, June 30, 2013

LOWASSA AMTAKA OBAMA ASIZUNGUMIE MAMBO YA USHOGA NA NDOA ZA JINSIA MOJA AKIWA TANZANIA



Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo yaNje na Ushirikiano wa Kimataifa, Edward Lowassa, amemtahadhalisha kujiepusha na kauli za kuunga mkono ushoga.
Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Alisema  jana kuwa ushoga na hai za ndoa kwa watu wa jinsia moja vinaweza `kuiharibu’ ziara yake hapa nchini.
Mapema wiki hii, Rais Obama alikaririwa akizungumzia masuala hayo yanayotajwa kuwa ni moja ya haki za msingi za binadamu, alipokuwa Senegal, lakini akapingwa.
“Watanzania hawatalikubali na wataendelea kushikilia uhuru na heshima walizojengewa tangu awali, kwamba ushoga na ndoa za jinsia moja havikubaliki,” alisema.
Akiwa Senegal, Rais Obama alitaka serikali za Afrika kutoa haki kwa mashoga kama inavyotoa kwa raia wengine.
"Ninachotegemea, I pray and hope (ninasali na kutegemea) kwamba kuhusu mashoga na ndoa za jinsia moja, Rais Obama hatarudia kauli aliyoitoa kule Senegal,” alisema.
Aliongeza, "ninasema hivi kwa sababu Tanzania hatuamini katika ushoga, na endapo utawalazimisha Watanzania, watakukatalia na kushikilia uhuru na heshima waliyojengewa toka awali."


JK AMGEUKA MWENYEKITI WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA JAJI JOSEPH WARIOBA

RAIS Jakaya Kikwete amemgeuka Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, kwa kuridhia azimio la Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutaka uwepo muundo wa serikali mbili.
Rais Kikwete ambaye juzi aliongoza kikao cha Kamati Kuu (CC), mjini Dodoma, aliridhia azimio hilo, huku akijua fika kuwa ndiye aliyemruhusu Jaji Warioba kuingiza kipengele hicho kwenye rasimu wakati alipoifikisha mbele yake kabla ya kuitoa hadharani.
Kutoka na hali hiyo, Kamati Kuu imewataka wanachama wao wote kupitia mabaraza ya CCM kuhakikisha wanakubaliana na msimamo wa chama wa kupinga muundo wa serikali tatu kama ilivyopendekezwa na tume ya Jaji Warioba.
Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho kutoka Zanzibar, waliliambia Tanzania Daima Jumapili kuwa Kamati Kuu
imepitisha azimio la kutaka mabaraza ya Katiba ya chama hicho yajadili na kuridhia msimamo wa kuwa na serikali mbili.
Kamati Kuu ya CCM imekuja na mapendekezo ya namna ya kurekebisha kasoro kubwa za Muungano ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikilalamikiwa na Wazanzibari.

BEYONCE ATINGA VAZI LA KANGA, ILIYOTENGENEZWA NA MTANZANIA



clip_image001[6] 
Christina (katikati)
Utajiskiaje kuona Beyonce akiwa amevaa vazi lililotengenezwa kwa kanga yenye maneno ya Kiswahili? ‘Wawili Ninyi Yawahusu….’ yanasomekana maandishi kwenye vazi alilolivaa mwanamuziki wa Marekani, 

 clip_image001
  Beyonce Knowles.
Vazi hili alilolivaa Beyonce kwenye moja ya show zake za tour ya Mrs Carter, limetengenezwa na mwanamitindo wa Tanzania aishie jijini London Uingereza, Christine Mhando mwenye brand ya Chichia London. Chichia London ndio brand iliyo maarufu sana nchini Uingereza kwa kutengeneza nguo za Kitanzania kwa kutumia Kanga na material mengine Kiafrika.
Hizi ni baadhi ya nguo alizotengeneza.
clip_image001[8]

LOWASSA AWATEKA WAENDESHA BODABODA ARUSHA...!!!

Wafanyabiashara maarufu jijini Arusha wakiongozwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Diwani wa Mererani, Mathias Manga, ndiyo waliyobuni wazo hilo la kuwaanzishia mfuko vijana wa bodaboda.
Katika harambee hiyo, sh milioni 84 zilipatikana huku Lowassa pamoja na marafiki zake wakichangia sh milioni 10 na pikipiki 1WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, amesema usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda ni sera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya kusaidia kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana.
Akizungumza katika haraambee na uzinduzi wa mfuko wa waendesha pikipiki maarufu mkoani Arusha, Lowassa alisema sera hiyo ni ya kuwakomboa vijana.

Alisema kuwa kitendo cha wafanyabishara wa Arusha kujipanga kusaidia bodaboda ni mfano kwa wafanyabishara wengine nchini.

“CCM ni chama kinachotetea wanyonge, na nyinyi ni wanyonge mnaohitaji kunyanyuliwa kimaisha, kitendo hiki cha wafanyabisharaa wa Arusha ni cha kuunga mkono sera ya CCM,” alisema.

Lowassa alisema tatizo la ajira ni bomu linalosubiri kulipuka na kwamba wasipowasaidia vijana kuondokana na tatizo hilo amani itatoweka.

“Ndiyo maana CCM katika ilani yake ya uchaguzi imeliweka hilo na pia kulisisitiza katika vikao vyake vya juu vya Mkutano Mkuu pamoja na Halmashauri Kuu,” alisema.

HUU NDIO WOSIA WA MZEE MANDELA NA MAHALI ANAPOPENDA KUZIKWA

Mzee Nelson Mandela ameandika wosia kwenye karatasi moja ya ukubwa wa A4 ambamo ameagiza azikwe katika milima iliyojitenga nyumbani kwa mababu zake huko Qunu, imebainika.

Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini, mwenye miaka 94, bado yuko mahututi lakini lakini hali yake inaimarika hospitalini mjini Pretoria ambako amekuwa huko kwa siku 21 zilizopita akitibiwa maambukizi kwenye mapafu.
Mnamo Januari 1996, wakati akiwa bado Rais, Mzee Mandela aliripotiwa kuandika wosia ambao aliagiza kufanyiwa maziko ya kawaida karibu na kijiji ambako alikulia kwenye rasi ya Mashariki.
Alisema kwamba wakati akifurahia kumbukumbu ya kulitumikia taifa hilo mjini Pretoria angetaka kuzikwa katika eneo la familia hiyo na kuwekewa jiwe la kawaida kama alama ya lilipo kaburi lake.
Gazeti la South African Mail na Guardian yaliripoti yakimnukuu rafiki wa siku nyingi wa familia akisema: "Hakuwahi kukifanya kifo kuwa jambo kubwa la kufikiriwa, lakini hakuwahi kutaka chochote cha ufahari".
Licha ya ukweli kwamba mauzo ya kitabu cha Mandela cha Long Walk To Freedom, na michoro yenye jina lake, kumpatia mamilioni ya pesa kwa hadhi wosia wake uliripotiwa kutosha kwenye karatasi moja ya ukubwa wa A4.

OBAMA ATOA SABABU YA KUTOFANYA ZIARA KENYA...!!!


Rais Barack Obama.
Wakati Rais wa Marekani, Barack Obama amesema asingeweza kufanya ziara Kenya kutokana na Rais wake, Uhuru Kenyatta na Naibu wake, William Rutto kukabiliwa na mashitaka katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC), pia amehadharisha Afrika kuhakikisha kuwa kampuni za kigeni zinaajiri wafanyakazi wazalendo ili wawekeze nchini mwao.



Alitoa kauli hizo mbili kwa nyakati tofauti, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na baadaye alipozungumza na viongozi vijana wa Afrika akiwa katika ziara yake nchini Afrika Kusini.
Akizungumza jioni jana na vijana katika eneo la Soweto jijini Johannesburg, Obama alisema ataangalia uwezekano wa kwenda Kenya akiwa bado madarakani kwani bado ana miaka mitatu na  miezi saba ya uongozi wake.

Saturday, June 29, 2013

MJUE MWIGIZAJI WA FILAMU YA YESU "BRIAN DEACON" AMBAYE BAADHI YA WATU HUDHANI KWAMBA NI YESU.

 
Brian Deacon akiigiza kama Yesu ndani ya filamu ya JESUS.
  Gospel kitaa imeamua basi kuwaletea historia ya mtu ambaye ameigiza filamu ya Yesu inayofahamika kwa jina la ''JESUS'' ambayo iliigizwa mnamo mwaka 1979 huko nchini Israel, GK imeamua kufanya hivi baada ya kuona ni kwa jinsi gani filamu hiyo imekuwa ikigusa maisha ya watu wengi kiasi kwamba baadhi ya watu wanasahau kwamba mtu aliyemo kwenye filamu hiyo ni mwigizaji tu na siyo Yesu.hata yeye amekiri kwamba wakati wa uigizaji alikuwa akisuluhisha mambo yaliyokuwa yakijitokeza yeye na waigizaji wenzake baada ya wao kusahau kwamba yeye si Yesu bali anaigiza tu. KARIBU.
Brian Deacon ndani ya filamu ya ''JESUS''
Brian Deacon ndio jina lake mwigizaji huyo ambaye ni mwingereza aliyezaliwa mnamo tarehe 13/02/1949 huko Oxford nchini Uingereza akiwa ni mtoto wa pili katika familia yao baba yake akiwa fundi makenika na mama yake akiwa ni nesi ndoa yake ya kwanza na Rula Lenska ilivunjika ambapo alizaa na mkewe huyo binti yao aitwaye Lara Deacon,ndoa yake ya pili alioana na mwanamama Natalie Bloch mnamo mwaka 1998 mpaka sasa wapo kwenye ndoa hiyo.
Aliigiza filamu ya Yesu ambayo pia ilimfanya aokoke mara baada ya kuitazama akiwa na miaka 30,baada ya kupita kwenye mchujo mkali wa waigizaji zaidi ya elfu moja ambao walifanyiwa mahojiano huku 260 wakijaribishwa kuigiza(screen test)kuona kwamba wanafaa akiwa ni mwingereza pekee kati ya waigizaji Waisrael walioingia kwenye usaili huo akiwa chini ya kampuni iitwayo New shakespears ambako alikuwa akifanya sanaa za majukwaani na uigizaji.

HII NDIO SABABU YA KAJALA KUNYOA BONGE LA UPARA...!!!

Mwigizaji aliyerudi uraiani hivi karibuni Kajala Masanja amefanya mabadiliko makubwa ya mtindo wake wa nywele baada ya kunyoa kipara “kikavu” kichwani mwake.
 Exclusive: Kajala aamua kunyoa kipara; kisa na mkasa? Soma hapa.
Katika picha alizozitoa mwigizaji huyo kupitia kwenye mtandao jana, mwigizaji huyo ameonekana akiwa na kipara tofauti na alivyozoeleka na nywele nyingi siku za nyuma.

Bongomovies.com tuliamua kumtafuta mwanadada huyu ili kujua “kunani”?? na staili hiyo na tulimpigia simu na maongezi yalikuwa kama ifuatavyo:
Bongomovies.com: Mambo kajala, mzima?
Kajala: Mzima, kwema?

Bongomovies.com: Kwema kabisa, vipi tena na kipara kichwani?
Kajala: Aha,..Siunajua tena mishe mishe, nipo na shoot movie yangu mpya ndo mana imenibidi ninyo kipara maana inanilazimu kuonekana hivyo ndani na Filamu hiyo.
Bongomovies.com: Okay, na itaitwaje?
Kajala: Itaitwa Heart attack

Bongomovies.com: Umewashirikisha nani na nani humo ndani?
Kajala: Atakuwepo Hemedi na mastaa wengine Kibao, kifupi ni bonge la movie yani.
Bongomovies.com: Basi tunaisubiri kwa hamu sana
Kajala: Pamoja sana.

MKE AMFUMANIA MUMEWE AKIWA NA KIMADA GESTI HUKO SINZA, MUME AMKIMBIA MKEWE AKIWA UCHI WA MNYAMA

Tukio hilo lililowashangaza wengi lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika gesti moja iliyopo Sinza jijini Dar. Awali Flaviana na bwana wake huyo walichukua chumba baada ya kushindwa kurudi nyumbani kutokana na kuzidiwa na kilevi.
Ilikuwaje fumanizi likatokea?
Ilielezwa kuwa wakati wawili hao wakiingia kwenye chumba cha gesti hiyo, Flaviana alikuwa bwii hivyo ‘kuzima’ kwenye kochi na kushindwa kufanya chochote.
“Wakati Aron akiwa chumbani pale, alifika shosti wa Flaviana aitwaye Dina na kwa kuwa Flaviana alikuwa hajitambui, wawili hao walianza kupeana malavidavi.

“Flaviana akiwa amelala alikuwa kama vile anasikia watu wakishughulika lakini alishindwa kufanya chochote kutokana na kuzidiwa na pombe.
“Wale wakaendelea kubanjuka. Ilipofika saa 12 asubuhi Flaviana akapata nguvu na kuamka kwenda kujisaidia, aliporudi akabaini shosti wake amemsaliti na ndipo alipoanzisha timbwili,” alidai mtoa habari wetu.

Flaviana apigia simu mapaparazi
Wakati timbwili hilo likiendelea chumbani hapo, Flaviana alipata mwanya wa kuwapigia simu mapaparazi ambapo ndani ya muda mfupi walifika na kumshuhudia Dina akiwa ndani ya Bajaj huku akivaa nguo kabla ya kumuamuru dereva kuondoka kwa spidi.
Naye mwanaume ambaye alikuwa ndani ya chumba cha gesti hiyo, aliposikia waandishi wamefika, alitokea mlango wa nyuma akiwa amevaa ‘boksa’ na tisheti, akaacha suruali yake chumbani hapo.
Akizungumza na Risasi Jumamosi huku akiwaonesha mapaparazi kitanda kilichokuwa vululuvululu, kilichotumika katika usaliti huo pamoja kondom, Flaviana alisema: “Nimeumia sana, yaani nimesalitiwa nikiwa humuhumu chumbani, Aron kanidhalilisha sana na huyo Dina naye kumbe siyo mtu, nitahakikisha namsaka nimshikishe adabu.”

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...