Saturday, June 29, 2013

HII NDIO SABABU YA KAJALA KUNYOA BONGE LA UPARA...!!!

Mwigizaji aliyerudi uraiani hivi karibuni Kajala Masanja amefanya mabadiliko makubwa ya mtindo wake wa nywele baada ya kunyoa kipara “kikavu” kichwani mwake.
 Exclusive: Kajala aamua kunyoa kipara; kisa na mkasa? Soma hapa.
Katika picha alizozitoa mwigizaji huyo kupitia kwenye mtandao jana, mwigizaji huyo ameonekana akiwa na kipara tofauti na alivyozoeleka na nywele nyingi siku za nyuma.

Bongomovies.com tuliamua kumtafuta mwanadada huyu ili kujua “kunani”?? na staili hiyo na tulimpigia simu na maongezi yalikuwa kama ifuatavyo:
Bongomovies.com: Mambo kajala, mzima?
Kajala: Mzima, kwema?

Bongomovies.com: Kwema kabisa, vipi tena na kipara kichwani?
Kajala: Aha,..Siunajua tena mishe mishe, nipo na shoot movie yangu mpya ndo mana imenibidi ninyo kipara maana inanilazimu kuonekana hivyo ndani na Filamu hiyo.
Bongomovies.com: Okay, na itaitwaje?
Kajala: Itaitwa Heart attack

Bongomovies.com: Umewashirikisha nani na nani humo ndani?
Kajala: Atakuwepo Hemedi na mastaa wengine Kibao, kifupi ni bonge la movie yani.
Bongomovies.com: Basi tunaisubiri kwa hamu sana
Kajala: Pamoja sana.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...