Tuesday, June 25, 2013

ANGALIA MUME WA JOYCE KIRIA NA VIJANA WENGINE WACHADEMA WAKIWA NA PINGU, KESI YA UGAIDI IGUNGA


Bw.Henry Kilewo akiwa na watuhumiwa wenzake wa mashtaka ya Ugaidi yanayowakabili wakati walipofikishwa Mahakama ya Hakimu mkazi mkoani Tabora kwa mara ya kwanza 

  
Wanachama wengine wa Chadema ambao wanahusishwa katika mashataka hayo ya Kigaidi ambapo imedaiwa kuwa watuhumiwa walifanya makosa hayo ya Ugaidi na kumjeruhi Bw.Mussa Tesha ambaye ni mwanachama wa CCM wakati wa kampeni za uchaguzi wa Ubunge wa jimbo la Igunga mnamo tarehe 9/9/2011 katika msitu wa Hanihani huko wilayani Igunga.


Kamanda Henry Kileo akiwa ndani ya gari pamoja na watuhumiwa wenzake wanne wakisubiri kupelekwa Gereza la Mahabusu hadi watakapoletwa tena Mahakamani hapo mnamo tarehe 8/7/2013.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 25, 2013

.
.

VIONGOZI WATANO WA CHADEMA WASHITAKIWA KWA UGAIDI .... MAJINA YA VIONGOZI HAO HAYA HAPA



Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Dar es Salaam na vijana wengine leo wameshtakiwa kwa Ugaidi katika mahakama ya Hakimu mkazi Tabora mjini.

Mbali ya Kileo, vijana wengine wa Chadema, ni Evodius Justinian wa Buboka, Oscar Kaijage wa Shinyanga, Seif Magesa Kabuta wa Mwanza, Rajab Daniel Kihawa wa Dodoma, leo wamesomewa shitaka la Ugaidi kwa kumteka na kumwagia tindikali Musa Tesha katika kampeni za Uchaguzi mdogo wa Igunga uliofanyika mwaka 2011.

Watuhumiwa hao walisomewa mashtaka mawili wote, la kwanza ni la kufanya ugaidi, na la pilini kumwagia tindikali Musa Tesha.

Kesi hiyo ilikuwa ilisikilizwa mbele ya hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, ya Tabora Mjini,Joktani Rushwera, huku upande wa serikali ukiwakilishwa na Wakili Juma Massanja na Ildefons Mukandara Baada ya kusomewa shitaka hilo, Upande wa utetezi wa ukiongozwa na wakili Prof Abdalah Safari, ukiwajumlisha Peter Kibatala na Gasper Mwalyela ulitoa hoja kuiomba mahakama hiyo ifutilie mbali mashtaka hayo kwa sababu, kwanza mashtaka hayakuwa na uhai kwa kuwa yamefunguliwa bila ridhaa ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini.

WABUNGE NA MASHOGA WATETA..... HOFU YA KUWA NA RAIS SHOGA TANZANIA YATANDA....!!!


WABUNGE wanachama wa Chama cha Kupambana na Ukimwi (TAPAC), wiki iliyopita walikutana na kujadiliana mambo mbalimbali na mashoga katika mkutano wa mwaka wa chama hicho uliofanyika kwa muda wa siku tatu mjini  Dodoma. Katika mkutano huo, baadhi ya wabunge walionyesha wasiwasi wa taifa kupata rais shoga katika miaka ijayo kutokana na ongezeko la mashoga hapa nchini.

Mbali na wasiwasi ulioonyeshwa na wabunge, mashoga waliokuwa wakihudhuria mkutano huo, walilalamikia vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa na wanajamii wenzao na kudai watambulike na wapatiwe huduma za msingi za kibinadamu.


Akizungumza katika mkutano huo uliomalizika jana, Mbunge wa Nkasi, Ally Kessy (CCM), alitahadharisha uwezekano wa nchi kupata rais shoga katika miaka ijayo, iwapo hatua za makusudi za kudhibiti hali hiyo hazitachukuliwa.


“Tabia ya kuwapeleka watoto kwenye shule za mabweni wangali wadogo wa umri wa miaka hadi miwili, itatuletea matatizo baadaye.

“Katika shule nyingi za bweni vitendo vichafu vinafanyika, vikiwamo vya ushoga. Katika vyuo vikuu hivi sasa kuna mashoga wasiopungua 40,000. Hii ni hatari, tusipojihadhari tutakuwa na rais shoga katika miaka ijayo,” alisema Kessy huku akishangiliwa na wabunge.

Mbunge huyo alitaka elimu dhidi ya ushoga na athari zake ienezwe nchini kupitia vyombo vya habari na nyumba za ibada.

MWANAMKE AOLEWA NA WANAUME WAWILI NA KUISHI NAO...!!!

MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani Katavi, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, ziliifikia Globu ya Jamii na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Monday, June 24, 2013

MSHTAKIWA WA EPA ASIMULIA JINSI WAJANJA WALIVYOMZIDI ‘KETE’ KWENYE AKAUNTI YAKE

Godfrey Mosha 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Principal Ltd, Godfrey Mosha amesimulia jinsi Benki ya Akiba Commercial (DCB), tawi la Kariakoo, ilivyoidhinisha malipo ya fedha kwa mtu mwingine kutoka akaunti yake ndani bila yeye kujua.
Mosha ni mmoja wa washtakiwa katika kesi ya  wizi wa fedha kwenye  Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Pamoja na wenzake, Bahati  Mahenge, Manase Makale, Davis Kamungu na Eda Makale, wanakabiliwa na kesi ya wizi wa Sh1.86 bilioni za EPA, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuipitia Kampuni ya Changanyikeni Residential Complex.
Katika kesi hiyo dhidi ya DCB, inayosikilizwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Warialwande Lema, Mosha anaidai benki hiyo Sh46.8 milioni, zilizolipwa kwa mtu asiyemfahamu kwa kutumia hundi nne tofauti na tarehe tofautitofauti.
Katika ushahidi wake Ijumaa  iliyopita, akiongozwa na Wakili wake, Michael Ngalo, Mosha alidai  alibaini uhamisho huo wa fedha  kutoka  akaunti yake namba 0400438671, Novemba 15, 2011 alipochukua taarifa ya benki.

SOGGY DOGGY NAE ATANGAZA KUGOMBEA UBUNGE 2015

 
Nguli wa muziki wa kizazi kipya Soggy Doggy Anter aka Anselm Tryphone Ngaiza leo ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, MWAKA 2015.
Msanii huyo ametiririka katika ukurasa wake wa facebook, na hapa nanukuu "Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.
 
Nilipoongea na Msanii huyu aliniambia ameamua kufanya ivi ili kuwasaidia na kuwaletea maendeleo wana-segerea na watanzania kiujumla.
Pia aliniambia ameamua kugombea kupitia CHADEMA, kwasababu ndo chama kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwasasa.
Nikamuuliza je amemfuata rafiki yake Joseph Mbilinyi aka "SUGU" katika chama icho, akasema hapana, hawajawahi kupewa ushawishi wowote wa kisiasa na Nguli huyo wa muziki wa Hip Hop.
Wana-Segerea kazi kwenu kijana ameamua na amedhamiria.

SIKU 17 KABURINI... FAMILIA YASHANGAA RIPOTI KIFO CHA NGWEA.


ZIKIWA zimekatika siku 17 tangu aliyekuwa mkali wa Hip Hipo Bongo, Albert Kenneth Mangweha ‘Ngwea’ alale kaburini, familia imeshangaa kupelekewa vitu vingine bila ripoti ya kifo chake.

Kwa mujibu wa mtu wa ndani wa familia hiyo, Millard Ayo wa Clouds FM ndiye aliyepewa majukumu ya kushughulikia kila kitu baada ya kifo tata cha Ngwea kilichotokea Johannesburg, Afrika Kusini Mei 28, mwaka huu.
 
Chanzo hicho kilieleza kuwa mara baada ya mwili wa marehemu Ngwea kuletwa Bongo, familia ilitarajia kukabidhiwa kila kitu ikiwemo ripoti ya nini kilimuua Ngwea.
 
“Hakuna swali tunaloulizwa kama ripoti ya kifo cha Albert (Ngwea). Kila mtu anataka kujua nini hasa kilitokea hadi akafa kwa sababu maneno ni mengi sana.
“Ripoti ndiyo ingeweza kumaliza maneno na kuwafunga watu midomo,” kilisema chanzo chetu mjini hapa.

Kiliendelea kunyetisha kuwa mwili ulipofika ilibidi familia ‘idili’ na maziko kwanza ambapo Millard aliahidi kuipeleka baada ya msiba.

“Kweli Millard alikuja tena juzikati, alichokabidhi ni cheti cha kifo (death certificate) na hati ya kusafiria ya marehemu Ngwea,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Familia nzima ilishangaa kwani ilikuwa ni tofauti na tulichotarajia lakini tulipomuuliza kuhusu ripoti ya kifo cha Ngwea, alikabidhi barua iliyoelezea kuwa chanzo cha kifo bado kinachunguzwa huko Afrika Kusini ambapo wanafanya critical investigation (uchunguzi wa kina) na tutajulishwa mara tu uchunguzi huo utakapokamilika.”

Baada ya kudakishwa habari hizo, Ijumaa Wikienda lilizungumza na mama wa marehemu Ngwea, Denisia Mangweha ambaye alikiri kupokea vitu hivyo na kwamba ni kweli familia ilijiandaa kupokea ripoti ya kifo lakini haikuwa hivyo.
Credit: GLP

SUMAYE AMPONDA LOWASSA KANISANI...!!!

WAZIRI Mkuu mstaafu Frederick Sumaye amesema anashangazwa na baadhi ya viongozi wa dini kutoa sifa nzuri kwa watu wanaochanga fedha na si kuzingatia uadilifu na wema walionao.



Kiongozi huyo alitoa kauli hiyo jana katika sherehe za kutimiza miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), zilizofanyika katika Chuo Kikuu cha Makumira mkoani Arusha.


Sumaye alihoji kuwa inakuwaje wema wa baadhi ya watu unajitokeza zaidi wakati nchi ikielekea kwenye uchaguzi unaotegemewa kufanyika mwaka 2015.


Sherehe hizo za kutimiza miaka 50 zilifanyika katika Chuo Kikuu cha Makumira na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa KKKT kutoka sehemu mbalimbali duniani pamoja na maaskofu wote wa dayosisi 20 zilizopo nchini.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 2, 2013 YA HABARI,UDAKU NA MICHEZO

DSC 0030 53cf9
DSC 0033 4b8a4

BAADA YAKUPIGWA MAKOPO DODOMA, HICHI NDICHO ALICHOKIONGEA OMMY DIMPOZ

 
 

MH. SUGU AMUOMBA RADHI WAZIRI MKUU

Mhe Sugu
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda
BAADA ya kauli yake iliyoibua mjadala mkubwa nchini dhidi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda kufuatia majibu yake aliyoyatoa wiki iliyopita Bungeni kwa kutaka Polisi kuendelea kuwapiga raia, Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe Joseph Mbilinyi 'Sugu', aomba radhi.
Sugu amemuomba radhi mhe Pinda na watanzania kwa ujumla kwa lugha aliyotumia katika kuonyesha hisia zake juu ya kauli aliyoitoa mhe Pinda bungeni.

Kupitia akaunti yake ya Facebook, Mbunge huyo machachari amenukuliwa akiwaomba radhi Watanzania waliokerwa na kauli yake iliyodai kwamba Tanzania haijawahi kuwapata Waziri Mkuu kama Mhe. Pinda kwa kusema;
"Ndugu watanzania, naombeni radhi kwa tusi nililolitoa kwa mhe Pinda, kwani nilikua nimeghafirika, halikuwa kusudio langu kumtukana mmoja wa viongozi wa nchi."

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA BARNABA (BI MARIAMUARUBETH)

Mama Diamond

Siku ya leo jumapili ndio ilikuwa siku husika kabisa katika kutoa heshima za mwisho kwa Bi Mariamu 
Arubeth aliezaliwa 4/12/1967 na kufariki tarehe 22/6/2013.


Zifuatazo ni picha za Mazishi Ya Mama mzazi wa Barnaba kuanzia nyumbani hadi makaburini....

Sunday, June 23, 2013

The Finest : FA apata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee.

Mwanamuziki Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee, baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake kuna jina la Jay Dee.
 
Tofauti na ilivyozooeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee ‘Anaconda’, hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.

Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kurudia wimbo huo na alipofika katika kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi huo ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.

Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.
Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa kama 250 tu.
Saa nne kamili mwanamuziki Hamis Mwinjuma, Mwana FA alikanyaga ‘red carpet’ akiwa na mbunifu wa mavazi Sheria Ngowi, na baada ya kuchukuliwa picha kadhaa alianza kuelekea nje ya ukumbi sehemu waliyosimama watu wakipata chakula na vinywaji, watu walizidi kufurika lakini kila aliyeingia alikuwa alwatan kidogo.

Waliendelea kuwasili mastaa na shoo inaanza Mashabiki wanaanza kuingia ukumbini saa tano kamili baada ya kupata vyakula na vinywaji nje, huku muziki wa taratibu ukipigwa na bendi ya muziki wa dansi ya Njenje. Mashabiki wanaendelea kubadilishana mawazo mpaka inapotimu saa tano na robo usiku, ambapo Mwana FA anapanda jukwaani.

Anaanza kazi kwa shoo ya aina yake baada ya kuimba hip hop live akiwa na bendi ya muziki wa dansi, kwenye shoo hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
FA alipanda jukwaani na wimbo wa Binamu akisindikizwa na wanamuziki Mandojo na Domokaya waliovalia suruali nyeusi na mashati meupe huku wakiwa wamevalia mikanda aina ya ‘suspender’, baadaye aliimba wimbo Unanijua Unaniskia na Bado Niponipo Kwanza ambao uliwapendeza mashabiki.

Alisimamisha shoo kwa muda na msanii Bernald Paul maarufu kama Benpol alipanda jukwaani na kuimba nyimbo zake tatu kwa kuziunganisha ukiwamo wa Maneno, Pete na Nikikupata na baadaye aliimba na Mwana FA wimbo wa Asubuhi aliomshirikisha Q Chief.
FA alipanda jukwaani na wanamuziki kadhaa katika vipindi tofauti akiwamo Linah Sanga ‘Linah’, Maua, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’.
Baadhi ya nyimbo alizoimba ni pamoja na Kama Zamani, Alikufa kwa Ngoma, Habari Ndio Hiyo, Leo, Mabinti, Unanitega, Yalaiti na nyingine nyingi.

HII NDIO HALI YA MSANII BARNABAS TANGU KUPOKEA TAARIFA ZA MSIBA WA MAMA YAKE



Kiukweli inasikitisha sana tangu asubuhi hajatia kitu chochote tumboni analia ananyamaza,akipewa chakula hakitaki.mungu mjalie ndugu yetu mpe nguvu aweze kumzika mama yake kwa aman na upendo.







R.i.P mamaa BARNABAS, Maziko ni leo saa 10 katika makaburi ya mburahati,kuanzia asubuhi saa 5 tutakuwa na misa maalum kwa ajili ya marehemu mama barnabas.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...