Monday, June 24, 2013

SOGGY DOGGY NAE ATANGAZA KUGOMBEA UBUNGE 2015

 
Nguli wa muziki wa kizazi kipya Soggy Doggy Anter aka Anselm Tryphone Ngaiza leo ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, MWAKA 2015.
Msanii huyo ametiririka katika ukurasa wake wa facebook, na hapa nanukuu "Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.
 
Nilipoongea na Msanii huyu aliniambia ameamua kufanya ivi ili kuwasaidia na kuwaletea maendeleo wana-segerea na watanzania kiujumla.
Pia aliniambia ameamua kugombea kupitia CHADEMA, kwasababu ndo chama kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwasasa.
Nikamuuliza je amemfuata rafiki yake Joseph Mbilinyi aka "SUGU" katika chama icho, akasema hapana, hawajawahi kupewa ushawishi wowote wa kisiasa na Nguli huyo wa muziki wa Hip Hop.
Wana-Segerea kazi kwenu kijana ameamua na amedhamiria.

SIKU 17 KABURINI... FAMILIA YASHANGAA RIPOTI KIFO CHA NGWEA.


ZIKIWA zimekatika siku 17 tangu aliyekuwa mkali wa Hip Hipo Bongo, Albert Kenneth Mangweha ‘Ngwea’ alale kaburini, familia imeshangaa kupelekewa vitu vingine bila ripoti ya kifo chake.

Kwa mujibu wa mtu wa ndani wa familia hiyo, Millard Ayo wa Clouds FM ndiye aliyepewa majukumu ya kushughulikia kila kitu baada ya kifo tata cha Ngwea kilichotokea Johannesburg, Afrika Kusini Mei 28, mwaka huu.
 
Chanzo hicho kilieleza kuwa mara baada ya mwili wa marehemu Ngwea kuletwa Bongo, familia ilitarajia kukabidhiwa kila kitu ikiwemo ripoti ya nini kilimuua Ngwea.
 
“Hakuna swali tunaloulizwa kama ripoti ya kifo cha Albert (Ngwea). Kila mtu anataka kujua nini hasa kilitokea hadi akafa kwa sababu maneno ni mengi sana.
“Ripoti ndiyo ingeweza kumaliza maneno na kuwafunga watu midomo,” kilisema chanzo chetu mjini hapa.

Kiliendelea kunyetisha kuwa mwili ulipofika ilibidi familia ‘idili’ na maziko kwanza ambapo Millard aliahidi kuipeleka baada ya msiba.

“Kweli Millard alikuja tena juzikati, alichokabidhi ni cheti cha kifo (death certificate) na hati ya kusafiria ya marehemu Ngwea,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Familia nzima ilishangaa kwani ilikuwa ni tofauti na tulichotarajia lakini tulipomuuliza kuhusu ripoti ya kifo cha Ngwea, alikabidhi barua iliyoelezea kuwa chanzo cha kifo bado kinachunguzwa huko Afrika Kusini ambapo wanafanya critical investigation (uchunguzi wa kina) na tutajulishwa mara tu uchunguzi huo utakapokamilika.”

Baada ya kudakishwa habari hizo, Ijumaa Wikienda lilizungumza na mama wa marehemu Ngwea, Denisia Mangweha ambaye alikiri kupokea vitu hivyo na kwamba ni kweli familia ilijiandaa kupokea ripoti ya kifo lakini haikuwa hivyo.
Credit: GLP

SUMAYE AMPONDA LOWASSA KANISANI...!!!

WAZIRI Mkuu mstaafu Frederick Sumaye amesema anashangazwa na baadhi ya viongozi wa dini kutoa sifa nzuri kwa watu wanaochanga fedha na si kuzingatia uadilifu na wema walionao.



Kiongozi huyo alitoa kauli hiyo jana katika sherehe za kutimiza miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), zilizofanyika katika Chuo Kikuu cha Makumira mkoani Arusha.


Sumaye alihoji kuwa inakuwaje wema wa baadhi ya watu unajitokeza zaidi wakati nchi ikielekea kwenye uchaguzi unaotegemewa kufanyika mwaka 2015.


Sherehe hizo za kutimiza miaka 50 zilifanyika katika Chuo Kikuu cha Makumira na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa KKKT kutoka sehemu mbalimbali duniani pamoja na maaskofu wote wa dayosisi 20 zilizopo nchini.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 2, 2013 YA HABARI,UDAKU NA MICHEZO

DSC 0030 53cf9
DSC 0033 4b8a4

BAADA YAKUPIGWA MAKOPO DODOMA, HICHI NDICHO ALICHOKIONGEA OMMY DIMPOZ

 
 

MH. SUGU AMUOMBA RADHI WAZIRI MKUU

Mhe Sugu
Waziri Mkuu, Mhe. Pinda
BAADA ya kauli yake iliyoibua mjadala mkubwa nchini dhidi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda kufuatia majibu yake aliyoyatoa wiki iliyopita Bungeni kwa kutaka Polisi kuendelea kuwapiga raia, Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe Joseph Mbilinyi 'Sugu', aomba radhi.
Sugu amemuomba radhi mhe Pinda na watanzania kwa ujumla kwa lugha aliyotumia katika kuonyesha hisia zake juu ya kauli aliyoitoa mhe Pinda bungeni.

Kupitia akaunti yake ya Facebook, Mbunge huyo machachari amenukuliwa akiwaomba radhi Watanzania waliokerwa na kauli yake iliyodai kwamba Tanzania haijawahi kuwapata Waziri Mkuu kama Mhe. Pinda kwa kusema;
"Ndugu watanzania, naombeni radhi kwa tusi nililolitoa kwa mhe Pinda, kwani nilikua nimeghafirika, halikuwa kusudio langu kumtukana mmoja wa viongozi wa nchi."

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA BARNABA (BI MARIAMUARUBETH)

Mama Diamond

Siku ya leo jumapili ndio ilikuwa siku husika kabisa katika kutoa heshima za mwisho kwa Bi Mariamu 
Arubeth aliezaliwa 4/12/1967 na kufariki tarehe 22/6/2013.


Zifuatazo ni picha za Mazishi Ya Mama mzazi wa Barnaba kuanzia nyumbani hadi makaburini....

Sunday, June 23, 2013

The Finest : FA apata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee.

Mwanamuziki Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee, baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake kuna jina la Jay Dee.
 
Tofauti na ilivyozooeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee ‘Anaconda’, hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.

Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kurudia wimbo huo na alipofika katika kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi huo ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.

Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.
Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa kama 250 tu.
Saa nne kamili mwanamuziki Hamis Mwinjuma, Mwana FA alikanyaga ‘red carpet’ akiwa na mbunifu wa mavazi Sheria Ngowi, na baada ya kuchukuliwa picha kadhaa alianza kuelekea nje ya ukumbi sehemu waliyosimama watu wakipata chakula na vinywaji, watu walizidi kufurika lakini kila aliyeingia alikuwa alwatan kidogo.

Waliendelea kuwasili mastaa na shoo inaanza Mashabiki wanaanza kuingia ukumbini saa tano kamili baada ya kupata vyakula na vinywaji nje, huku muziki wa taratibu ukipigwa na bendi ya muziki wa dansi ya Njenje. Mashabiki wanaendelea kubadilishana mawazo mpaka inapotimu saa tano na robo usiku, ambapo Mwana FA anapanda jukwaani.

Anaanza kazi kwa shoo ya aina yake baada ya kuimba hip hop live akiwa na bendi ya muziki wa dansi, kwenye shoo hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
FA alipanda jukwaani na wimbo wa Binamu akisindikizwa na wanamuziki Mandojo na Domokaya waliovalia suruali nyeusi na mashati meupe huku wakiwa wamevalia mikanda aina ya ‘suspender’, baadaye aliimba wimbo Unanijua Unaniskia na Bado Niponipo Kwanza ambao uliwapendeza mashabiki.

Alisimamisha shoo kwa muda na msanii Bernald Paul maarufu kama Benpol alipanda jukwaani na kuimba nyimbo zake tatu kwa kuziunganisha ukiwamo wa Maneno, Pete na Nikikupata na baadaye aliimba na Mwana FA wimbo wa Asubuhi aliomshirikisha Q Chief.
FA alipanda jukwaani na wanamuziki kadhaa katika vipindi tofauti akiwamo Linah Sanga ‘Linah’, Maua, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’.
Baadhi ya nyimbo alizoimba ni pamoja na Kama Zamani, Alikufa kwa Ngoma, Habari Ndio Hiyo, Leo, Mabinti, Unanitega, Yalaiti na nyingine nyingi.

HII NDIO HALI YA MSANII BARNABAS TANGU KUPOKEA TAARIFA ZA MSIBA WA MAMA YAKE



Kiukweli inasikitisha sana tangu asubuhi hajatia kitu chochote tumboni analia ananyamaza,akipewa chakula hakitaki.mungu mjalie ndugu yetu mpe nguvu aweze kumzika mama yake kwa aman na upendo.







R.i.P mamaa BARNABAS, Maziko ni leo saa 10 katika makaburi ya mburahati,kuanzia asubuhi saa 5 tutakuwa na misa maalum kwa ajili ya marehemu mama barnabas.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 23, 2013

DSC 0019 578e1

DSC 0022 d20cc
DSC 0023 43257

ASKOFU AITAKA SERIKALI KUWABANA WASIOTAKA NCHI ITAWALIKE.

RAIS Jakaya Kiwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali na dini wakati alipohudhuria sherehe za miaka 25 ya Askofu wa jimbo kuu la Morogoro Telesphol Mkude wa pili kulia kwa rais katika viwanja vya shule ya ST Peter mkoani Morogoro jana.


SIKU chache baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutaka Serikali iachwe ifanye kazi yake katika kudhibiti vurugu zinazoibuka kila kukicha, Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, Mhashamu Telesphor Mkude naye ameitaka Serikali kuwadhibiti wote wasiotaka nchi itawalike.Askofu huyo amesema kuonya pekee hakusaidii, bali inawajibu wa kuwachukulia hatua kali ili kukomesha vitendo vinavyotishia amani nchini.Askofu Mkude aliyasema hayo jana wakati wa maadhimisho ya Jubilei ya miaka 25 ya uaskofu wake kwenye viwanja vya Seminari ya Mtakatifu Petro mjini hapa ambapo Rais Jakaya Kikwete alikuwa miongoni mwa wageni mashuhuri waliohudhuria.

RIHANNA AMPIGA SHABIKI WAKE NA KIPAZA SAUTA BAADA YA SHABAKI HUYO KUMKERA...!!!


MWIMBAJI nyota wa muziki wa R&B, Robyn Rihanna Fenty, anayefahamika zaidi kwa jina  la Rihanna, amenaswa na kamera akimpiga shabiki ‘mic’ usoni alipokuwa akifanya shoo huko Birmingham, Uingereza Jumatatu iliyopita.

Rihanna alifanya tukio hilo la kushtua alipojichanganya kwenye umati wa mashabiki, huku akiimba kwenye shoo hiyo ambayo ni sehemu ya ziara yake ya dunia inayojulikana kama ‘Diamond World Tour’ akiitangaza albamu yake ya saba ya ‘Unapologetic’ iliyotoka mwaka jana.

Ilidaiwa kuwa Rihanna mwenye umri wa miaka 25 alishindwa kudhibiti hasira zake baada ya shabiki huyo asiyefahamika kumng’ang’ania mkono wake.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo aliandika kwenye ukurusa wake wa Twitter: "Rihanna amempiga mtu mmoja na mic yake katika ajali haha oops."

Na Rihanna alijibu akisema kuwa alikusudia kumpiga shabiki huyo kwa sababu alikuwa akimzuia.

TAMASHA LA KILI MUSIC AWARDS NDANI YA UWANJA WA JAMHURI DODOMA.....OMMY DIMPOZ APIGWA CHUPA NA MASHABIKI JUKWAANI..!!

Ommy dimpoz arushiwa chupa na mawe jukwaaani dodoma na kushindwa kufanya show ya kilimanjaro muzik award dodoma. Wadau wa dom wasema kamwe msanii yoyote atakaye mdisi msanii wa dodoma awatamkubari kufanya show dom na watamshusha jukwaani kama walivyo fanya leo

 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,Linex akiwasalimia mashabiki na wapenzi wa Muziki waliofurika kwa wingi ndani ya Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma leo,ambapo usiku huu kulikuwa na bonge moja la Show ya Kilimanjaro Tanzania Music Tour 2013.




 Msanii Ben Pol akighani moja ya nyimbo zake.

 

POLISI 7 WAFUNGWA JELA MIAKA 5 KWA KOSA LA MAUAJI HUKO KIGOMA

 

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora imewahukumu kifungo cha miaka mitano jela askari saba wa Jeshi la Polisi mkoani Kigoma ambao walikuwa wakishtakiwa kwa mauaji.

Akitoa hukumu yake katika kikao cha Mahakama Kuu kilichokuwa kikifanyika mkoani Kigoma Jaji wa mahakama hiyo, Sam Mpaya Rumanyika alisema kuwa baada ya kupitia ushahidi mbalimbali Mahakama hiyo imewatia hatiani askari hao kwa kosa la kuua bila kukusudia.
Katika kesi hiyo namba 35 ya mwaka 2012 washitakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo na kusomewa shitaka la kumuua Festo Stephano, mkulima wa kijiji cha Rungwe Mpya Wilaya ya Kasulu mkoani hapa katika tukio lililotokea Agosti 6, mwaka 2011.

Askari hao waliohukumiwa ni pamoja na Baraka Hongdi, Koplo Mawazo, Koplo Swahib, D/C Charles, D/C Shamsi, D/C Jerry na D/C Amrani ambao kwa pamoja walikana shitaka lao katika kesi hiyo namba 35 ya mwaka 2012.
Akitoa utetezi kabla ya hukumu hiyo wakili wa washitakiwa, Method Kabuguzi aliiomba Mahakama kuwafutia shitaka washitakiwa hao na kuwaachia huru kwani wote bado vijana na wameoa hivi karibuni.
Sambamba na hilo Kabuguzi alisema kuwa askari hao walikumbwa na mkasa huo wakati wakitekeleza jukumu lao la ulinzi wa taifa ambapo walimkamata mtuhumiwa wa kutumia silaha na ndipo kifo kikatokea wakati wakitekeleza majukumu yao.

Source: http://www.wavuti.com

AMANDA APIMA NGOMA, PRESHA YAPANDA YASHUKA

Stori:Gladness Mallya
MSANII wa filamu za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ hivi karibuni alijikuta akipandwa na kushukwa na presha  mara baada ya kwenda hospitali kupimwa Ugonjwa wa Ukimwi.Kikizungumza na Exclusive chanzo makini ambacho kilishuhudia tukio zima katika Hospitali ya Dokta Mvungi, Kinondoni, jijini Dar kilisema baada ya Amanda kupewa majibu ya vipimo na daktari, alianza kuhaha huku na kule kama mtu aliyechanganyikiwa, kisha presha ikampanda baadaye ikashuka.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Amanda na kumuuliza juu ya tukio hilo ambapo bila hiyana alitiririka:
“Ile ilikuwa ni mara ya tatu kupima ngoma yaani wakati nikisubiri majibu, presha ilipanda ghafla mpaka daktari akawa na wakati mgumu wa kunipa majibu.



“Nilienda kuchukua majibu na sikutaka kuyaangalia, nilimpelekea daktari ambaye aliniambia niko safi yaani sikuamini nilitoka nikiwa naongea peke yangu, nilikuwa sijiamini si unajua tena ujana ni maji ya moto sasa presha ,” alisema Amanda.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...