Friday, June 21, 2013

AUNTY LULU..... "MAZISHI YANGU WATAJAA MASHOGA NA WATOTO TU"

MSANII wa filamu Bongo, Lulu Mathias ‘Aunty Lulu’ amefunguka kuwa siku akifa anaamini mbali na watu wengine mazishi yake yatatawaliwa na mashoga pamoja na watoto
 
 

Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Aunty Lulu alisema kutokana na ukweli kwamba wengi wanaompenda na ambao wamemzoea ni watoto waliokuwa wakimsikiliza kwenye Kipindi cha Watoto Shoo kupitia Radio One na ITV na mashoga ambao awali alikuwa kama mama yao, hao ndiyo watakaojaa kwenye mazishi yake.
Alisema sababu kubwa ya msiba wake kujaa mashoga wengi ni kwa kuwa kabla hajabadili mfumo wa maisha anayoishi sasa, alikuwa akiwalea hivyo siku ya mazishi lazima wakumbuke fadhila.
“Unajua kufa ni kama kulala, naamini siku ya mazishi yangu watakaokuwa wengi ni watoto pamoja na mashoga ambao zamani nilikuwa mama yao, wengine ni waandishi na wasanii mbalimbali wa filamu na muziki,”alisema Aunty Lulu.

WEMA SEPETU NA KAJALA MASANJA WAGEUKA "PAKA NA CHUI "....ZILE MILIONI 13 ZALETA BALAA ZITO

Utabiri wa wengi kuwa ushosti wa waigizaji masistaduu wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Kajala Masanja kutumbukia nyongo unadaiwa kutimia na sasa wametibuana, 

Habari za ndani kutoka kwa mtu wa karibu (jina linahifadhiwa), mwanzoni baada ya Wema kumlipia Kajala faini ya Sh. milioni 13 na kumnusuru kutokwenda Segerea a.k.a Segedansi, wawili hao walikuwa marafiki kama pete na kidole.

“Walishinda wote, walilala wote, walikwenda klabu wote yaani Kajala alikuwa anamnyenyekea ‘madam’ Wema kwa kumuepusha na kifungo cha miaka 7 jela,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Kuna wakati hapa katikati Kajala alikuwa kama katibu muhtasi wa madam, si unajua lazima atumikie fedha za watu?


“Kabla hajaenda Mwanza kwa ajili ya mapumziko kwa bibi zake, nilimsikia Kajala akilalama kuwa madam aliamka siku moja akawa amemchunia, unaambiwa hata salamu ikawa hakuna. “Hapo ndipo maneno ya pembeni yakaanza kwa sababu mbali na Kajala, Wema pia ana wapambe wengine na mbali na Wema, Kajala naye ana kampani. Kwa hiyo sosi ya manenomaneno ni hizo kampani zao.

 “Ipo siku kabisa Wema alimlalamikia Kajala hadharani kuwa amekuwa akimsema vibaya kwa watu.
 “Yale maneno yalimuuma sana Kajala, ikabidi arudi nyumbani kwao lakini akawa anaogopa kumwambia mama yake kuwa ametibuana na Wema hadi alipotimkia Mwanza.

“Lakini kabla ya hii ishu ya kulaumiana, kipindi cha nyuma kidogo Kajala alipata dili la kwenda kurekodi filamu nchini China na mastaa wengine lakini ikadaiwa kuwa Wema alichomoa hivyo mwigizaji huyo hakwenda pamoja na kwamba alishapewa baraka zote na baba yake.

MABONDIA WANNE WA TANZANIA WAFUNGWA JELA MIAKA 15 BAADA YA KUNASWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI MAURITIUS


Mabondia wanne wa Tanzania wafungwa miaka 15 jela nchini Mauritius kwa makosa ya kuingiza dawa za kulevya aina ya heroin.
Mabondia hao ni Case Ramadhani Fills, Nathanael Elia Charles, Ally Rajabu Msengwa na Petro Charles Mtagwa.
Wakati kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa, wote walikiri makosa ya kuingiza mihadarati hiyo nchini Mauritius wakati walipokwenda kushiriki mashindano ya ndondi barani Afrika mwaka 2008.
Wakiwa mbele ya Jaji, waliiambia mahakama kuwa walilazimika kuingia katika biashara hiyo haramu kutokana na hali zao za maisha kuwa maskini.
 "Tunaomba radhi kwa taifa la Mauritius", waliiambia mahakama.
 
"Tu watu maskini na tunategemewa na familia, watoto na wazee wetu wanaotugemea. "Kwa dawa hizi tungepata kiasi cha Pauni £4,000". walisema

Jaji Benjamin Marie Joseph alisema katika kutoa adhabu hiyo yote hayo ameyafikiria, kwani walitoa ushirikiano mzuri wakati wote wa uchunguzi wa kesi hiyo, kulikowezesha hata wafanyabiashara hiyo, raia wa Mauritius kukamatwa.

Wamekuwa mahabusu kwa siku 1,722, sawa na miaka miatano, hivyo watatumikia miaka kumi iliyobakia jela. Pia watatakiwa kulipa faini ya pauni £1,600 na gharama nyingine za uendeshaji wa kesi hiyo.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa BBC nchini Mauritius Yasine Mohabuth in Mauritius, Jaji aliwashutumu kwa kuukosea umma wa Mauritius kwa kuingiza dawa hizo za kulevya aina ya heroin.

Mabondia hao waliwasili Mauritius tarehe 10 Juni 2008 na kuweza kupita uwanja wa ndege bila kunaswa hadi walipokamatwa katika hoteli waliyofikia ya Quatre Bornes.

Kwa pamoja walimeza gram 4639.04 za heroin zikiwa katika vifuko 358 vijulikavyo kama pipi.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 21, 2013


.
.
.
.

Thursday, June 20, 2013

MAMA LANGA.... "NINGEKUWEPO TANZANIA MWANANGU ASINGEKUFA HARAKA"


MAMA wa marehemu Langa Kileo, Vanessa Kimei amefungua kinywa chake na kusema kifo ni mipango ya Mungu lakini kama angekuwepo nyumbani kwake Mikocheni, Dar, mwanaye asingekufa haraka kiasi hicho.Akizungumza na Amani hivi karibuni, Mama Langa alisema wakati mwanaye alipoanza kuugua hadi kupatwa na umauti Juni 13, mwaka huu, yeye alikuwa safarini nchini Marekani kumuona mwanaye mwingine aliyekuwa amejifungua.
“Wakati mwanangu ameanza kuumwa sikuwepo, nilikuwa safarini Marekani nilikoenda kumuona mwanangu wa kike aliyekuwa amejifungua, kwa mila za kwetu ni lazima mama kwenda kumuogesha mtoto lakini ningekuwepo mwanangu asingeondoka jamani,’’ alisema mama Langa.
Akifafanua kauli yake, mama huyo alibainisha kuwa kipindi alipokuwa akiishi na mwanaye kabla hajasafiri, mara nyingi alikuwa akimhudumia alipokuwa akiumwa hivyo hata katika ugonjwa uliosababisha mauti yake basi angeweza kumtibu yeye mwenyewe.
Alisema kuwa wakati mwingine alikuwa akimuwekea hadi dripu za dawa akiwa pale nyumbani na kunusuru maisha ya mwanaye lakini ghafla kifo kimetokea wakati yeye hayupo.


“Nilikuwa namuwekea dripu za dawa mwanangu hapahapa nyumbani, alikuwa anaugua kwa muda na kisha anarudi katika hali ya kawaida,” alisema kwa uchungu mama Langa.
Hata hivyo baadhi ya waombolezaji waliokuwepo msibani walimsihi mama huyo kukubaliana na mipango ya Mungu kwamba kila mwanadamu lazima atakufa, hali iliyompa faraja na kumfanya anyamaze.
Marehemu Langa aliyefariki baada ya kusumbuliwa na kile kilichoelezwa kuwa ni ugonjwa wa malaria kali na homa ya uti wa mgongo, alizikwa Jumatatu iliyopita katika Makaburi ya Kinondoni, Dar.

MWANDISHI WA HABARI WA CHANNEL TEN AFARIKI DUNIA




Na Steven Kanyeph.
Mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha chanel Ten CHARLES HILILA amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospital ya Mkoa wa Shinyanga.

Marehemu Charles Hilila alilazwa katika hospital ya mkoa tarehe kumi mwezi june mwaka huu akisumbuliwa na maradhi ya TB ya mifupa ambapo tarehe kumi na sita mwezi huu alihamishiwa chumba cha wagonjwa mahututi mpaka mauti yalipomchukua .


Kwa mujibu wa mke wa marehemu amesema kuwa mazishi yatafanyika katika kijiji cha Jomu Tinde mahali alipozaliwa marehemu yakitanguliwa na misa takatifu ya mazishi itakayofanyika katika kanisa kuu la mama mwenye huruma la Ngokolo mjini Shinyanga.

Marehemu Hilila ameacha mjane mmoja na watoto watatu, wakike mmoja na wakiume wawili.

Marehemu Hilila enzi za uhai wake alifanya kazi katika kituo cha televisheni cha chanel Ten lakini aliwahi kufanya kazi katika kituo cha matangazo cha radio Faraja. Mungu alaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amina.

MSIKILIZE MBUNGE ALLY KEISSY WA NKASI ANAYEWAVUNJA MBAVU WABUNGE

Stori ya kwanza ni ya Mbunge wa Nkasi Ally Keissy June 18 2013 bwana alivunja rekodi ya kuwa mbunge aliechekesha watu wengi wakiwemo wabunge bungeni, sio tu kwa sababu ya kutoa vichekesho lakini pia ni kwa namna alivyokua akieleza mambo pamoja na kuikosoa Serikali.
.
Mbunge wa Nkasi Ally Mohamed Keissy.


Anakwambia ‘Twende Kigoma, Mwanza, Tabora, Mpanda, Shinyanga tuwaulize watu mnataka reli au viwanja vya ndege… mtashangaa wenyewe, vipaumbele gani mnapeleka viwanja vya ndege? mtu gani wa Tabora anapanda ndege kama sio Mbunge, DC na Mkuu wa mkoa… ? ni Treni…… hawataki viwanja vya ndege, viwanja vya ndege baadae…. 

kwanza ndege zenyewe zikwapi? mna ndege nyie???? mabilioni ya hela mnajenga viwanja vya ndege… ndege hatuna, wapanda ndege ni nyie wenyewe Wabunge na Mawaziri… jamani tutulie tuweke vipaumbele ambavyo vinaweza kusaidia Wananchi na uchumi wa nchi,  mtapakia mizigo, madebe mawese kwenye ndege? migebuka kwenye ndege? acheni mambo ya kurukiakurukia ndege zenyewe hamna”

WABUNGE WA CHADEMA WASIMULIA MATESO WALIYOYAPATA RUMANDE...!!!

Wabunge wanne wa Chadema, ambao waliachiwa na polisi kwa dhamana wamesimulia mateso waliyoyapata wakiwa rumande baada ya kukamatwa juzi. Vigogo hao; Mbunge wa Mpanda Mjini Said Amour Arfi, Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti maalumu), walikamatwa juzi baada ya wao na wafuasi wa chama hicho kutawanywa kwa mabomu ya machozi na polisi kwenye Viwanja vya Soweto, Arusha.Wabunge hao waliachiwa baada ya kujidhamini wenyewe huku watu wengine 65 waliokamatwa pamoja nao wakiachiwa baada ya kudhaminiwa.
 Wote wanatakiwa kuripoti kwenye kituo hicho Julai 22, mwaka huu na wataelezwa hatma ya suala hilo.Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja alisema jeshi lake linaendelea kuwasaka Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha, Godbless Lema na kuwaonya kuwa wanatakiwa kujisalimisha mara moja.Chagonja alisema Mbowe na Lema wanatafutwa kwa kosa la kufanya kusanyiko lisilo halali katika viwanja hivyo vya Soweto walipokuwa wakitaka kuomboleza vifo vya watu watatu; Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally waliofariki dunia baada ya kuumizwa kutokana na mlipuko wa bomu, Jumamosi iliyopita.
Pia aliwaamuru Mbowe na Lema kuwasilisha mara moja ushahidi wa kuwahusisha polisi na shambulio la bomu na kama hawana imani na Polisi, basi wawasilishe ushahidi wao kwa Rais Jakaya Kikwete.

MAGAZETI YALEO ALHAMISI JUNI 20, 2013


.
.

Wednesday, June 19, 2013

LUNDENGA AMTIMUA MREMBO JUKWAANI BAADA YA KUTINGA NA KIVAZI CHA NUSU UCHI...!!!


MWENYEKITI wa Kamati ya Mashindano ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga Jumamosi iliyopita alimtimua mshiriki wa shindano la Redd’s Miss Morogoro 2013, Saphina Chumba (20) jukwaani wakati shindano hilo lilipokuwa likiendelea.
Tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita katika Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Nashera mjini hapa wakati mrembo huyo alipokuwa akiwania kuvaa taji la mkoa huo.

Kisa cha mrembo huyo aliyevalia namba 5 kutimuliwa ni kukiuka maadili na kanuni za mashindano hayo kwa kuvaa nusu utupu mbele ya mgeni rasmi ambaye alikuwa Mbunge wa Kilosa, Mustapha Mkulo na mbele ya Kamati nzima ya Miss Tanzania.
Baada ya kuona jinsi alivyovaa, Lundenga na kamati yake walikubaliana kumtimua mshiriki huyo kwa kumwita Jaji Mkuu wa shindano, Alex Niktasi na kumtaka amuondoe haraka.
Mbali na Chumba, pia jaji alimtimu mrembo mwingine aliyevalia namba 8, Neema Joel (20) kutokana na kushiriki shindano  hilo mara mbili mwaka huu, inadaiwa mara ya kwanza alishiriki mkoani Arusha.
Lundenga alipohojiwa na waandishi wa habari alisema kamati yake inataka kuendeleza nidhamu tangu ngazi ya chini, hivyo hawawezi kuruhusu utovu wa nidhamu.

CCM YAOMBWA IRUHUSU WATU KUJITANGAZA URAIS.

VUGUVUGU la Uchaguzi Mkuu wa 2015 linazidi kupamba moto ambapo juzi aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, ameomba CCM itoe ruhusa mapema kwa wanaowania urais kuanza kutangaza nia lakini bila kukampeni.

Sumaye ambaye alipata kugombea urais mwaka 2005, alionya kuwa kama CCM haitaruhusu wagombea kutangaza nia leo, yanayofanyika chini chini ni mabaya zaidi.

Akizungumza katika kipindi cha dakika 45 juzi, Sumaye mbali na kuitaka CCM kuruhusu wanachama wake kuan

za kutangaza nia ya kugombea mapema, pia alielezea athari za muundo wa Serikali tatu uliopendekezwa na Rasimu ya Katiba mpya na mfumo mpya wa kusoma Bajeti ya Serikali bungeni.


Urais 2015

MDADA ACHEZEA KICHAPO KWA KUFANYA UKAHABA JIRANI NA MSIKITI...!!!

 Richard Bukos na Issa Mnally

KHAAA! Operesheni Fichua Maovu ‘OFM’ iliyo chini ya Global Publishes, ipo mzigoni na hivi karibuni imenasa tukio la aina yake ambapo mke wa mtu amechezea kichapo ‘hevi’ akidaiwa kufanya ukahaba jirani na msikiti, Risasi Mchanganyiko lina kisa kamili.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu majira ya usiku jirani na msikiti huo uliopo nyuma ya Corner Bar, Kijitonyama jijini Dar ambapo mwanamke huyo na wenzake walikamatwa na baadhi ya vijana waumini wa Kiislamu waliokerwa na kitendo cha wao kutoa huduma haramu ya ngono maeneo hayo.


WENZAKE WATOKA NDUKI
Baada ya wenzake kufanikiwa kutoka nduki mithili ya mwanariadha Usai Bolt wa Jamaika, mwanamke huyo alishuhudiwa akila bakora kisha akapelekwa katika Kituo cha Polisi Kijitonyama, Dar akaunganishwa na wengine waliokamatwa usiku huo.
Ilielezwa kuwa wanawake hao wamekuwa wakiuza miili kwa wanaume karibu na msikiti huo na pembezoni mwa baa hiyo.
Ilisemekana kuwa kumekuwa na kawaida ya wanawake hao kusimama maeneo ya nyumba hiyo ya ibada na kufanya biashara hiyo huku wakichafua mazingira kwa kutupa ovyo kondomu na kujisaidia maeneo hayo. 


NGUO YA NDANI YAMVUKA
Wakati mwanamke huyo akicharazwa bakora, nguo ya ndani ilimvuka huku akipiga kelele kuwa hatarudia kufanya hivyo na kama akirudia basi akatwe kichwa.

BAADA YA KUZUSHIWA KIFO, HIKI NDICHO ALICHOSEMA MSANII SAIDA KAROLI

 
Baada ya taarifa kuzushwa kuwa Mwanamuziki wa asili, Saida Karoli amefariki katika ajali ya meli habari za uhakika ni kuwa Saida Karoli wala hayuko mahala popote jirani na Ziwa Victoria. 
Baada ya kuweko Dar es Salaam wiki iliyopita, Saida na kundi lake walikodishwa na kuelekea Makongorosi Chunya mahala aliko mpaka asubuhi hii.
Saida Karoli anasema "sina mpango wowote wa kufa hivi karibuni".
MUNGU AMUONGEZEE SIKU NYINGI ZENYE FARAJA KATIKA MAISHA YAKE

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 19, 2013

.
.

HOFU YATANDA MKOANI SHINYANGA JUU YA MAUAJI YA WATOTO

( Picha na maktaba )

Na Steve Kanyeph
Wakazi wa manispaa ya Shinyanga wamegubikwa na hali ya hofu na wasiwasi kufuatia matukio ya mara kwa mara ya kuuawa kwa watoto wa kike wanaofanyiwa ukatili na unyanyasaji na kisha kuuawa ama kutelekezwa wakiwa hawajitambui.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi hao walisema vitendo vya unyanyasaji kwa watoto wa kike wenye umri wa kuanzia miaka tisa hadi kumi na nne katika manispaa ya Shinyanga kwa zaidi za miezi minne sasa vimekithiri hali ambayo inatishia amani kwa wakazi hao.

Akizungumza na Jambo Tz jana mkazi wa eneo la Ngokolo katika Manispaa ya Shinyanga bi Dafrossa Pius ambaye ni mjasiliamali, siku moja baada za tukio la kuuawa kikatili kwa binti mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kumi na mbili hadi kumi na tatu, kisha mwili wake kufungwa kama mzigo kwenye boksi na kutupwa kwenye ghuba la takataka katika eneo hilo la ngokolo mitumbani,alisema ni ukatili usiovumilika hata kidogo “ukatili kama huu kwa watoto wa kike wasio na hatia haupaswi kuvumiliwa wala kufumbiwa macho``

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...