Saturday, March 09, 2013

MBUNGE WA CHADEMA KORTINI


MBUNGE wa Ukerewe, Salvatory Machemli (CHADEMA) amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashitaka ya uchochezi. 
Machemli (39) amesomewa mashitaka hayo jana mbele ya 
hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya, Rouben Luhasha akidaiwa kutenda kosa hilo mwaka mmoja na nusu uliopita. 

MAKAMPUNI YA SIMU YAUNGANA KUTOA HUDUMA YA MAWASILIANO KWA WOTE


Wawakilishi mbalimbali wa makampuni ya simu wakitiliana saini ya makubaliano ya kuendesha Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote kulia ni Mkuu wa kitengo cha uhimalishaji mitandao wa Voda Com Eng,Nguvu Kamando anaefuata ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania TTCL Bw, Kamugisha Kazaura na wengine wanaoshudia makubaliano hayo nyuma kushoto ni Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Tekinolojia Profesa Makame Mbawara 


WAWAKILISHI WA MITANDAO

RAIS DK SHEIN AHUDHURIA MAULIDI YA MTUME, TEMEKE JIJINI DAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ALhaj Dk.Ali
Mohamed Shein,akisalimiana na Sheikh Alhad Mussa Salum,alipowasili
katika msikiti Masjid majmuatil Islamia,wa Temeke mwisho kuhudhuria
katika maulid ya Mtume Muhamad SAW.
Sheikh,Dk.Usama Mohammed Esmail,kutoka nchini Misri akitoa mawaidha wakati wa Maulid ya Mtume Muhammad SAW,yaliyofanyika jana katika Msikiti Masjid Majmuatil Islamia,wa Temeke mwisho,yaliyohudhuriwa na Viongozi wa Dini mbali mbali,na mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein.
Sheikh Alhad Mussa Salum,wa Mkoa wa Dar es
Salaam,akiwatambulisha wageni mbali mbali waliohudhuria katika Maulid
ya Mtume S.A.W. yaliyohudhuriwa na maelfu ya waumini wa Jiji la Dar
es Salaam,katika Msikiti Masjid Majmuatil Islamia,wa Temeke mwisho.
Sheikh Alhad Mussa Salum,wa Mkoa wa Dar es
Salaam,akiwatambulisha wageni mbali mbali waliohudhuria katika Maulid
ya Mtume S.A.W. yaliyohudhuriwa na maelfu ya waumini wa Jiji la Dar
es Salaam,katika Msikiti Masjid Majmuatil Islamia,wa Temeke mwisho.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akiwaongoza Viongozi mbali
mbali wa Dini na Serikali katika Maulid ya Mtume Muhammad S.A.W
yaliyofanyika jana katika Msikiti Masjid Majmuatil Islamia,wa Temeke
mwisho.
Wanamadrasatul Az-har ya Koma Kisiwani Dar es Salaam,wakisoma Qaswida Ya swalatu Alan Nabii,katika Maulid ya Kumswalia Mtume Muhammad SAW,yaliyofanyika jana katika Msikiti Masjid Majmuatil Islamia,wa Temeke mwisho.
Baadhi ya waumini wa Dini ya Kiislamu wa Jijini Dar es Salaam,waliohudhuria katika Maulid ya Kumswalia Mtume Muhammad SAW,yaliyofanyika jana katika Kumswalia Mtume Muhammad
SAW,yaliyofanyika jana katika Msikiti Masjid Majmuatil Islamia,wa
Temeke mwisho.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.

MKE WA MTU ATUPIA PICHA YA NUSU UCHI FACEBOOK KWA MADAI KUWA MUMEWE HAYUKO FACEBOOK, HIVYO HAWEZI KUONA


Picha Hii ni Imepostiwa kwenye facebook na Mke wa mtu sasa hapo we can't tell if ni yeye ama la...ila kwa kifupi nimemuuliza why ameweka na haoni itamsababishia matatizo na mumewe akanijibu kwa kifupi kuwa mumewe hayupo Facebook so hawezi kujua ..

WATU WATATU WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUMTUSI SPIKA WA BUNGE



Watu watatu wamefikishwa mahakamani katika mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma na Mkoa mpya wa Simiyu kwa tuhuma za kutumia lugha za matusi na uchochezi dhidi ya Spika wa Bunge la Jamhuri yak Muungano wa Tanzania.

UHURU KENYATTA AIBUKA MSHINDI WA KITI CHA URAIS NCHINI KENYA


Mchuano  ulikuwa  mkali  kweli  kweli, lakini  hatimaye  Uhuru Kenyatta ameibuka  mshindi wa  kinyang'anyiri  hicho  kwa  asilimia  50.3  ya  kura  zote  zilizopigwa  huku  Raila Odinga  akijipatia  asilimia 43.28  ya  kura zote

UN's Navi Pillay condemns Tanzania attacks on albinos

Salum Khalfani Bar'wani - November 2010  
Salum Khalfani Bar'wani became the first Tanzanian with albinism to be elected an MP in 2010
.
 
The UN human rights chief has condemned a recent spate of "horrific attacks" on people with albinism in Tanzania, including the murder of a young boy. The government should act to stop the "vicious killings" and discrimination they faced, said Navi Pillay. 

The mutilation and murder of people with albinism is often linked to witchcraft, the UN says. Only five people have been convicted in Tanzania since 2000 for killing people with albinism, it adds. Some 72 people have been killed in that time.

In 2009, President Jakaya Kiwete said the murders had brought shame to Tanzania and launched a national campaign to end the persecution of people with albinism.
 
'Arm hacked off'
In 2010, Salum Khalfani Bar'wani became the first person with albinism to be elected as an MP in Tanzania.
 
 
Navi Pillay UN human rights chief

In a statement, Ms Pillay said four attacks on Tanzanians with albinism had been documented in just 16 days between the end of January and mid-February. They included:
  • the murder of a seven-year-old boy, Lugolola Bunzari, on 31 January at Kanunge village in the Tabora region. His attackers slashed his forehead, right arm and left shoulder, and chopped off his left arm just above the elbow. The boy's grandfather, aged 95, was also killed in the attack as he tried to protect his grandson;
  • a seven-month-old baby, Makunga Baraka, narrowly escaped death on 5 February after armed men attacked his home in the Simiyu region. Villagers chased the attackers away and surrounded the house to protect him. The baby and his mother were taken to the police station the following morning and given temporary sanctuary;
  • a 39-year-old woman Maria Chambanenge was attacked on 11 February by five armed men, allegedly including her husband, in Mkowe village in the Rukwa region. They hacked off her left arm while she was sleeping with two of her four children. The five suspects were subsequently arrested and the victim's arm recovered - their trial is reportedly under way
  • a 10-year-old boy, Mwigulu Matonange, was attacked on his way home from school and his left arm chopped off above the elbow by two unidentified men in Msia village in Rukwa. Three men have been arrested in connection with the attack.
"These crimes are abhorrent. People with albinism have the right to start living, like anyone else, without fear of being killed or dismembered," Ms Pillay said. Tanzania's authorities needed to step up efforts to bring the attackers to justice, she added.

Public awareness campaigns should also be launched to end the stigma associated with albinism, Ms Pillay said. "I am deeply alarmed by the general discrimination and social exclusion many people with albinism suffer, as a result of their skin colour, not just in Tanzania but in other countries as well," she said. Some witchdoctors say that magic charms are more powerful if they contain body parts from people with albinism - this has led to a lucrative criminal trade in these body parts.

Balozi Tuvako Manongi akisaini kitabu cha maombolezo ya Hugo Chavez

 Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi, jana  Ijumaa aliungana na  Mabalozi wengine katika kutia saini kitabu cha Maombolezo  kufuatia kifo cha Rais wa Venezuela,  Hugo Chaves, aliyefariki siku  ya jumanne wiki hii kwa ugonjwa wa  kansa. Kitabu hicho  kilifunguliwa katika Ubalozi wa Kudumu wa  Venezuela katika Umoja wa Mataifa.

RAIS KIKWETE NA ABDULRAHAMAN KINAN WAMJULIA HALI MHARIRI MTENDAJI WA HABARI CORPORATION ABSALOM KIBANDA AFRIKA KUSINI


 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation Absalom Kibanda aliyelazwa katika hospitali ya Mill Park iliyopo mji wa Johannesburg, Afrika ya Kusini leo jioni. Kulia ni Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

Bwana Kibanda alipelekwa Afrika ya kusini kwa matibabu zaidi baada ya kujeruhiwa vibaya na watu wasiojulikana juzi usiku.Rais Kikwete yupo Afrika ya Kusini kuhudhuria Mkutano wa Viongozi wa Vyama vilivyokuwa mstari wa Mbele katika mapambano dhidi ya Ukoloni na ubaguzi wa Rangi.Mkutano huo umeandaliwa na Chama cha African National Congress(ANC).

Friday, March 08, 2013

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU MWANZA AUMBULIWA NA PICHA ZA UCHI-BBM


DENTI wa chuo kimoja kilichopo jijini Mwanza (jina tunalihifadhi) aliyefahamika kwa jina la Fatma Omar amejikuta akiumbuka kwenye mtandao wa BBM baada ya picha zake chafu alizokuwa ‘akimfoadia’ mpenzi wake kuvuja.

Picha hizo zikiwemo zinazomuonesha mwanadada huyo mwenye asili ya Kiarabu akiwa amevaa nguo ya ndani tu zinapatikana mtandaoni na inadaiwa kuwa mwenyewe amejikuta akiugua ghafla baada ya kubaini ameaibika.

Baada ya Ijumaa kuzinasa picha hizo na kubahatika kupata namba zake, mwandishi wetu alimpigia simu Fatma ili kujua kilicho nyuma ya pazia ya picha hizo ambapo alifunguka:

SAKATA LA JACK PATRICK KUJIUZA LACHUKUASURA MPYA BAADA YA SERIKALI KUVUNJA UKIMYA


BAADA ya hivi karibuni msanii wa filamu, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ kunaswa akipelekwa kuuzwa kwa mwanaume, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla anadaiwa kuicharukia skendo hiyo ambapo juzikati alimvaa Rais wa Shirikisho la Filamu (TAFF), Simon Mwakifwamba na kumuuliza juu ya tukio hilo la aibu. 

Chanzo cha habari kutoka ndani ya shirikisho hilo kilitonya kuwa, Mhe. Makalla alimvaa Mwakifwamba kwenye mkutano na wasanii uliofanyika ndani ya Hoteli ya Kibadamu, Ubungo jijini Dar.

TUME YA UCHUNGUZI WA KUSHUKA UFAULU KIDATO CHA NNE 2012 YAWAOMBA WATANZANIA KUTOA USHIRIKIANO.

Mkiti wa Tume 1 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya kuchunguza kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 Prof. Sifuni Mchome (katikati)akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu kuanza kwa zoezi la ukusanyaji wa maoni kutoka wadau mbalimbali. Wengine ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene (kushoto) na Bi.Tunu Temu mjumbe wa Sekretarieti ya Tume hiyo.
…………………………………………………………………              
Na. Aron Msigwa -MAELEZO, Dar es salaam.
 Tume ya Taifa iliyoundwa na Mh. Waziri mkuu Mizengo Pinda kuchunguza kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 imewaomba watanzania kuipa ushirikiano kwa kutoa maoni yao ili iweze kukamilisha majukumu iliyopewa kwa muda na ufanisi mkubwa.
 Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa Tume hiyo Prof.Sifuni Mchome ameeleza kuwa tume hiyo ilianza kazi mara baada ya kuzinduliwa na Waziri mkuu tarehe 2 mwezi Machi mwaka huu na kufafanua kuwa jukumu lililopo sasa ni kuanza kazi ya kukusanya maoni kutoka kwa watanzania ili kubaini sababu za matokeo mabaya ya mtihani huo.
 Amesema kuwa tume hiyo pamoja na mambo mengine imepewa jukumu la kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua ili kukabiliana na tatizo la mwenendo wa kushuka kwa kiwango cha elimu nchini huku mapendekezo hayo  yakizingatia kipindi cha muda mfupi , kati na kipindi cha muda mrefu.
 Prof. Sifuni ameeleza kuwa tume hiyo inafanya kazi kwa kuzingatia hadidu mbalimbali  za rejea zikiwemo kubainisha sababu za matokeo mabaya ya kidato cha nne 2012, sababu za kushuka kwa kiwango cha ufaulu, nafasi ya Halmashauri katika kusimamia elimu ya sekondari katika halmashauri zake. 
  Rejea nyingine ni pamoja na pamoja na kuanisha sababu nyingine zinazoweza kuwa zimechangia hali ya matokeo hayo pamoja na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua mara moja kwa wanafunzi 240,903 waliofeli mitihani yao kwa kupata daraja sifuri.
 Amefafanua kuwa tume katika kutekeleza majukumu yake itapitia mitaala na mihutasari ya Elimu ya Msingi na Sekondari, kutathimini kiwango na mazingira ya ufundishaji na ufunzaji, kuangalia mfumo wa upimaji na tathmini ya mitihani pia usimamizi na uendeshaji.
 Pia pamoja na mambo mengine tume itatathmini mchango wa jamii na wazazi/ walezi katika maendeleo ya wanafunzi, hali ya upatikanaji wa chakula cha mchana, upungufu wa majengo ya shule,madarasa, maabara na maktaba.
Vilelevile tume hiyo itafuatilia mwamko wa wazazi katika kufuatilia mkazo wa eliimu kwa watoto na suala la mmomonyoko wa maadili unaotokana na ukuaji wa utandawazi hususan teknolojia ya Habari na Mawasiliano na kutathmini athari ya mfumo wa ufundishaji wa  mikondo miwili iliyopo katika shule za Zanzibar.
 Aidha mwenyekiti wa Tume hiyo amebainisha kuwa tume itaanza rasmi kukutana na wadau mbalimbali kwa lengo la kupata maoni kuanzia tarehe 11 mwezi huu kwa kuanza na mkoa wa Dar es salaam, Zanzbar na maeneo mengine nchini kwa kukutana na viongozi wa ngazi mbalimbali za Wizara, Mikoa, Wilaya, Halmashauri, Kata, Shule, Taasisi mbalimbali za kijamii na wananchi kwa ujumla na pia kuwasilisha maoni kwenye tume kupitia Mwenyekiti wa Tume, Tume K4-2012, S.L.P 5909 Dar es salaam au kupitia simu 0737206038, Barua pepe: maoni@tumek4.go.tz au kwa kutembelea Tovuti ya tume ya www.tumek4.go.tz.

DIAMOND ATINGA KWENYE MAULIDI AKIWA KAVAA KANZU HERENI NA CHENI .JIONEE MWENYEWE

MWANAMUZIKI Nasibu Abdul ‘Diamond’ hivi karibuni aliwachefua waumini wenzake wa dini ya Kiislam baada ya kutinga kwenye Maulidi akiwa amevaa hereni na cheni.

Tukio hilo lilijiri maeneo ya Tandale, Dar ambapo mama yake aliyemtambulisha kwa jina la Aunt Shani aliandaa maulidi kwa ajili ya kumshukuru Mwenyezi Mungu.
Akiwa mmoja wa waalikwa, Diamond alinaswa akiomba dua sambamba na rafiki yake aitwaye Remeo Jones ‘RJ’ huku akiwa amevaa kanzu safi na balaghashia lakini akaharibu kwa kuvaa hereni na cheni.
Kitendo hicho kiliwachefua Waislam ambapo baadhi walifikia hatua ya kumchana laivu kuwa, alichokifanya kilikuwa kinyume na Uislam.

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI: SALMA KIKWETE, DIAMOND, NANCY SUMARI NA WENGINE KIBAO WAFUNGUKA

Leo ni miaka 99 tangu kuanzishwa kwa siku ya wanawake duniani iliyoadhimishwa kwa mara ya kwanza March 8, 1914 ambapo mwanzoni ilikuwa ikijulikana kama ‘Siku ya wanawake wafanyao kazi duniani’. 

Ni siku ya kuwapa heshima wanawake, kuwapongeza na kuwaonesha upendo katika jitihada zao kiuchumi, kiasiasa na kijamii.

Katika nchi zingine siku hii imefunika ile ladha ya kuchanganyika na siasa na kuwa siku ya wanaume kuelezea upendo wao wanawake kama ilivyo Mother’s Day na Valentine’s Day. Soma jinsi watu mbalimbali mashuhuri nchini (na kwingineko) wanavyoizungumzia siku hii.
Mama Salma Kikwete
602888_515306958500762_1804884203_n
Leo ni siku ya wanawake Duniani.,ni siku ya kujitazama kama Taifa juu ya hali ya wazazi hawa na walezi wa Taifa hili. Ni siku ya kujipima na kutathimini namna gani, wanawake wamewezeshwa kujitambua na kushirikishwa katika mipango ya maendeleo ya jamii yetu. Tunapofikiri kama Taifa ni namna gani tunaweza kujikomboa katika Umasikini tulionao ni lazima mipango hiyo iende sambamba na mipango na mikakati ya ukombozi kwa wanawake wa Taifa hili. 
Nancy Sumari 529850_10151364540678380_2140979918_n
Even when we are a mess, we still put on vests with ‘S’ on our chests, Oh yes, we are Super Women, and today is our day…Happy Womens day!!

Diamond
dia1
HAPPY WOMEN’S DAY……. I LOVE MY MAMA MORE THAN ANYTHING IN THIS WORLD….SHE HAS BEEN THROUGH ALOT WITH ME…… MUCH LOVE TO ALL WOMEN’S IN THIS WORLD…..!!

Tamko Kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM):Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kuvamiwa, kupigwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) na Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006 Ndugu Absalom Kibanda

Katibu wa CCM itikadi na Uenezi Nape Nnauye
--

Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kuvamiwa, kupigwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) na Mhariri Mtendaji wa New Habari 2006 Ndugu Absalom Kibanda usiku wa kuamkia Jumatano Machi 6, 2013.
Chama Cha Mapinduzi kinalaani kwa nguvu zote kilichotokea kwa Absalom Kibanda, kwani ni unyama usiokubalika hata kidogo, unafaa kulaaniwa na Watanzania wote.
CCM tunaitaka Serikali kuhakikisha inawapata waliofanya unyama huo na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria ili sheria ifuate mkondo wake, na kukomesha matukio ya namna hiyo.
Aidha, Chama Cha Mapinduzi kinatoa pole kwa Uongozi wa Jukwaa la Wahariri, Afisa Mtendaji Mkuu wa New Habari 2006, familia ya Ndugu Kibanda, wanahabari na wadau wote wa habari nchini, na tunamwombea kwa Mwenyezi Mungu apone haraka na kurejea katika kazi zake za Ujenzi wa Taifa.

Imetolewa na:
Nape M. Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UEENEZI
08/03/2013

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...