Katika
gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna
habari yenye kichwa chenye maneno
‘ SIRI YA KUUAWA ZITTO YAFICHUKA’ na
vichwa vidogo ‘yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini’ dk. Slaa
atajwa kumtuma Saanane kummaliza’. Habari hii imeniletea usumbufu mkubwa
kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wangu, wamejazwa na
wasiwasi mkubwa sana kwamba ninaweza kuuwawa. Napenda kusema yafuatayo:
Moja,
sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa Ben Saanane
na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu
kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa Hoteli ya Lunch Time ambayo sio
tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi. Haijawahi kutokea mimi
kufanya kikao cha pamoja na Ben Saanane, Juliana Shonza na Mtela
Mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika na hivyo naomba
mwandishi ahakikishe kuwa vyanzo vyake vya habari vimempa habari sahihi.















Mwakilishi
wa Wabunge waliomaliza mafunzo maalumu ya muda mfupi ya Jeshi la
Kujenga Taifa(JKT)katika kambi ya RUVU Ester Bulaya akikabidhi risala
kwa niaba ya wenzake kwa Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
leo mchana.
Wabunge
waliomaliza mafunzo ya muda mfupi ya Jeshi la kujenga Taifa wakipita
kwa ukakamavu mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mris
Wabunge
waliomaliza mafunzo ya muda mfupi ya Jeshi la kujenga Taifa wakipita
kwa ukakamavu mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho kikwete
wakati wa gwaride maalumu la kumaliza mafunzo hayo huko kambi ya RUVU
leo.
Wabunge
walihudhuria mafunzo ya muda mfupi Ruvu JKT wakionesha walijifunza kwa 





