Saturday, February 23, 2013

Mafao ya viongozi wastaafu yashtua


WAKATI Watanzania kwa mamilioni wakiendelea kukosa huduma mbalimbali muhimu ikiwamo afya na njaa kutawala katika maeneo mengi nchini, imebainika kuwa viongozi wastaafu wanarundikiwa mafao.
Ukubwa wa mafao hayo na posho kwa marais, makamu wa rais na mawaziri wakuu wastaafu unatajwa kuwa huenda ndiyo chanzo cha uongozi kupiganiwa kwa udi na uvumba na kwa gharama yoyote, kutokana na kuwa vyeo hivyo huwanufaisha katika maisha yao yote na baada ya wao kufariki wategemezi wao huendelea kunufaika.
Sheria ya Mafao ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1999, ambayo ilirekebishwa mwaka 2005, inaeleza kuwa Rais Mstaafu anapomaliza kipindi chake cha uongozi, hupata mafao ya mkupuo.
Ingawa kiwango cha mshahara wa Rais wa Tanzania ni siri, sheria hiyo inaeleza kuwa mafao yao hukokotolewa kwa kuzingatia mshahara wa juu aliowahi kupata miezi aliyofanya kazi.
Kiwango cha mafao hayo hukokotolewa kwa kutumia kanuni za kiwango cha asilimia itakayopangwa na mamlaka husika.
Mbali ya mafao yake ya kazi, Rais Mstaafu hulipwa posho ya kila mwezi kiasi cha asilimia 80 ya mshahara wa rais aliyeko madarakani. Kiasi hicho ni sawa na Sh80 kwa kila Sh100 anayopata Rais aliye madarakani.
Licha ya posho hiyo, Rais hupewa ulinzi, msaidizi, katibu muhtasi, mhudumu wa ofisi, mpishi, dobi, mtumishi wa ndani, mtunza bustani, madereva wawili na gharama za mazishi atakapofariki.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...