Saturday, September 27, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 27, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KESI YA MUBARAK YAAHIRISHWA MISRI

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak akiwa mahakani
Uamuzi wa kesi inayomkabili rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak kuhusu mashtaka ya ufisadi na mauaji ya waandamanaji wakati wa mapinduzi ya mwaka 2011 umeahirishwa.
Jaji alisema kuwa hatua hiyo imechukuliwa kutokana na sahabu ya kuwepo kwa ushahidi ambao bado mahakama haijausikiliza.
Wakati wa kesi ya leo kanda moja ya video ilionyesha mrundiko wa stakabadhi za ushahidi.
Bwana Mubarak alipatikana na hatia mnamo mwaka 2012 na kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani lakini baadaye hukumu hiyo ikabatilishwa.
Mahakama hiyo imesema kuwa itatoa hukumu yake mwezi Novemba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANAMKE APIGWA MAWE HADI KUFA SOMALIA


Wapiganaji wa Alshabaab
Mwanamke mmoja ameuawa kwa kupigwa mawe nchini Somalia na kundi la wanamgambo wa Al Shabaab.
Ripoti zinasema kuwa takriban watu 200 akiwemo gavana wa eneo hilo walishuhudia watu wakimpiga mawe mwanamke huyo kwenye mji wa Barowe.
Mwanamke huyo wa umri wa miaka 30 alikuwa ameshutumiwa kwa kufanya mapenzi nje ya ndoa.
Wadadisi wanasema kuwa mauaji hayo ini ishara ya ushawishi wa kundi la Al shabaab hata baada ya kushambuliwa na serikali ya Somalia pamoja na vikosi vya muungano wa Afrika.
Mji wa Barowe ambao uko umbali wa kiomita 200 kutoka mji mkuu Mogadishu umekuwa ngome ya Al Shabaab. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

LOUIS VAN GAAL AKIRI WACHEZAJI MAN UNITED HAWAELEWI MBINU ZAKE

1411724782154_wps_5_FILE_PHOTO_Louis_van_Gaal
Louis van Gaal alishuhudia vijana wake wakipokea  kutoka kwa Leicester wikiendi iliyopita
LOUIS van Gaal  amekiri kuwa wachezaji wa Manchester United wana matatizo ya kuelewa mbinu zake mpya.
Mholanzi huyu aliitisha kikao kilichodumu kwa saa moja baada ya kufungwa na 5-3 na Leicester jumapili iliyopita.
Mshambuliaji wa United, Robin van Persie alisema kulikuwa na mgongano wa mawazo katika kikao hicho, lakini anahisi yote ilikuwa ni kwa faida ya kikosi.
The defeat prompted the Dutchman to accept that some of his players have not adapted to his methods
Mholanzi huyu amekiri kuwa Kipigo kilitokana na ukweli kwamba baadhi ya wachezaji wameshindwa kuelewa mbinu zake
Ikiwakosa wachezaji 10 kutokana na majeruhi na kutumikia adhabu, leo United inatarajiwa kuwa na muonekano mpya dhidi ya West Ham, Ingawa Van Gaal amekiri baadhi ya wachezaji hawajaendana na mbinu zake.
“Tulizungumaza mambo mengi na wanatakiwa kufanyia kazi” Alisema Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RATIBA EPL LEO: LIVERPOOL v EVERTON, CHELSEA v ASTON VILLA, ARSENAL v TOTTENHAM, HULL CITY v MAN CITY, MAN UNITED v WEST HAM…!!!

article-2771118-21B0F6B100000578-503_964x386  Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
StandingsENGLAND: Premier League  
04:45   Liverpool - Everton      
07:00   Chelsea - Aston Villa      
07:00   Crystal Palace - Leicester      
07:00   Hull City - Manchester City      
07:00   Manchester United - West Ham      
07:00   Southampton - QPR      
07:00   Sunderland - Swansea      
09:30   Arsenal - Tottenham  

Friday, September 26, 2014

BAWACHA YAPANGA KUMUONA RAIS KIKWETE KWA MAANDAMANO...!!!


Mwenyekiti wa Baraza la wanawake Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), Halima Mdee akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu mandamano ya kupinga kuendelea kwa vikao vya Bunge la katiba. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Bara, Hawa Mwaifunga.

Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) limetangaza maandamano kwenda Ikulu kumuomba Rais Jakaya Kikwete asikubali kutia saini Rasimu ya Katiba inayopendekezwa iwapo itapitishwa na Bunge.

Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee alisema jana kwamba maandamano hayo yatafanyika mwishoni mwa wiki ijayo, baada ya maandalizi yatakayofanyika kwa siku saba kuanzia jana kukamilika.

Mdee ambaye pia ni mbunge wa Kawe, alisema baraza hilo limeamua kuitisha maandamano hayo ili kuwakilisha kilio cha wanawake ambao ndiyo waathirika wa kwanza pale nchi inapokuwa katika mfumo usio wa haki.

Alivitaka vyombo vya dola hasa polisi kujitokeza kuwasindikiza na kuandamana nao kwa kuwa nao ni miongoni mwa Watanzania ambao wataathiriwa na uamuzi usiolenga kujenga umoja wa kitaifa.

Hata hivyo, Polisi imetahadharisha kuwa itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria wanachama wa Chadema watakaojiingiza katika maandamano yaliyopigwa marufuku nchini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA WATISHIWA MAISHA


Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, wakiwa katika vikao vya Bunge hilo Dodoma jana. Picha ya Maktaba

Siku tatu kabla ya Bunge la Katiba kuanza kupigia kura Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, watu wasiojulikana wameanza kusambaza vitisho vya kuwatia hofu wajumbe wa Bunge hilo.

Watu hao wamesambaza vipeperushi katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma usiku wa kuamkia jana, wakiwataka wajumbe kutoingia bungeni vinginevyo yatakayowapata watajuta, huku wajumbe kutoka Zanzibar wakitishiwa kwa ujumbe wa simu kupitia mtandao wa WhatsApp.

Tayari, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd ametoa kauli kuhusu vitisho hivyo akisema Serikali itachukua kila hatua kuhakikisha wajumbe kutoka visiwani humo ambao wamekuwa wakipokea vitisho wanakuwa salama.

Mbali na kusambazwa kwa karatasi hizo, maandishi mekundu yamechorwa katika kuta za jengo la Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma yakisomeka, “No Katiba. No ufisadi.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZAIDI YA RAIA 3, 000 WA ULAYA NI WAFUASI WA I.S


Inakisiwa kuwa zaidi ya raia 3000 kutoka Ulaya ni wafuasi wa Islamic State
Idadi ya raiya kutoka Uropa wanaojiunga na kundi la wapiganaji wa Kiislamu nchini Syria na Iraqi imeongezeka hadi zaidi ya 3,000 kulingana na mkuu wa kitengo cha kupambana na ugaidi bara la ulaya.
Gilles de Kerchove ameonya kuwa mashambulizi ya hewa yanayofanywa na nchi za Magharibi yataongezea hatari ya mashambulizi ya kulipiza kisasi katika bara la Ulaya.
Vikosi vikiongozwa na Marekani vimetekeleza mashambulizi ya hewa mia mbili dhidi ya wanamgambo wa Islamic state wa Iraqi tangu Agosti na Jumatatu iliyopita wakaanza kulenga wale walioko Syria.
Bunge la Uingereza litapiga kura kwa mashambulizi ya hewa dhidi ya Iraqi siku ya Ijumaa.
Kundi la IS wameteka sehemu kubwa za Syria na Iraqi katika miezi ya hivi karibuni.
CIA inakisia kuwa kundi la IS linaweza kuwa na wapiganaji mpaka 31,000 huko Iraq na Syria, mara tatu zaidi ya wale waliohofiwa.
Mashambulizi haya yaliotekelezwa siku ya Alhamisi na ndege za Marekani, Saudi na UAE zilikuwa zinalenga mitambo 12 ya kusafisha mafuta nchini Syria .
Msemaji wa Pentagon Rear Admiral John Kirby alisema kuwa kusudi la mashambulizi haya ya hewa halikuwa kuwaua wanamgambo hao lakini ilikuwa kuharibu maeneo ambayo yalikuwa yakiletea kundi hilo fedha kupitia soko nyeusi.
Baadaye, siku ya Ijumaa, wabunge wa Uiungereza wataulizwa kuunga mkono mashabulizi dhidi ya wanamgambo wa IS Iraqi lakini sio Syria. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TALIBAN YATEKA MJI WA GHAZNI AFGHANISTAN


Afisa wa usalama akishika doria katika mji wa Ghazni
Maafisa huko mashariki mwa Afghanistan wanasema kuwa wapiganaji wa Taliban wamechukua udhibiti wa baadhi ya Wilaya katika jimbo la Ghazni.
Watu zaidi ya 70 wanahofiwa kufariki katika Wilaya ya Ajrestan katika mapambano hayo ya kuteka vijiji vyao hapo jana jioni.
Ripoti zinasema Kuna makabiliano makali ya risasi huku walinda usalama wakifanya kila wawezalo kujaribu kutwaa tena wilaya hizo zilizotekwa.
Ghazni ni mji muhimu umnaochukuliwa kama mlango unaounganisha mji mkuu Kabul na eneo la kusini mashariki mwa nchi hiyo.
Wadadisi wa hali ya usalama nchini humo wanasema kuwa kutekwa kwa mji huo ni ilani kwa miji iliyoko karibu na
Ghazni huenda pia zikatekwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...