Saturday, October 26, 2013

MAALIM SEIF ATANGAZA KUWANIA URAIS 2015

Seif20hamad201 2f850MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SMZ), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema atagombea urais hadi nguvu zitakapomuishia katika maisha yake.
Mbali na hilo amesema kuwa ataendelea kutetea nafasi yake ya ukatibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), katika uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaoanza Novemba Mosi mwaka huu.
Kauli hiyo aliitoa mjini hapa jana, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo alielezea miaka mitatu ya utendaji wa SMZ katika awamu ya saba ya uongozi wa Serikali hiyo.
"Nitastaafu pale nitakapoishiwa nguvu, wengine wanaona Maalim ni kizingiti, aondoke, nasema siondoki ng'o. Nitaendelea kuwatumikia Wazanzibari na ndiyo ahadi yangu kwao, nasema nikiwa mzima nitagombea urais na ukatibu mkuu wa chama changu.
"Mchakato wa uchaguzi CUF tayari umeanza na utafanyika katika matawi yote Novemba mwaka huu, na uchaguzi mkuu utafanyika mwakani pamoja na mkutano mkuu kati ya Mei na Juni mwakani na Inshaallah nitagombea tena," alisema Maalim Seif.
Akizungumzia mafanikio yaliyofikiwa na Serikali hiyo ya pamoja inayoundwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja na Chama cha Wananchi (CUF), alisema katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali hiyo, moja ya mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kupandisha bei ya karafuu.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 26, 2013

DSC 0370 ef46f
DSC 0371 4a462

SIRI NZITO ZA OPERESHENI KIMBUNGA ZAFICHUKA


Naibu Kamishna wa Polisi nchini na msimamizi wa operesheni kimbunga, Kamanda Simon Sirro akieleza jambo hivi karibuni. Picha ya maktaba 
*******

Hivi karibuni Serikali ilianzisha operesheni maalumu iliyopewa jina la ‘Operesheni Kimbunga’ kwa lengo la kuwaondoa nchini watu wote ambao hawana uraia au haki ya kisheria kuishi nchini.
Baadhi ya mambo mazito yaliyoibuliwa na operesheni hiyo ni kubainika kwa wahamiaji haramu ambao huja nchini kwa lengo la kufanya ujangili. Aidha wengine huja maalumu kwa lengo la kufanya ujambazi.
Kama hiyo haitoshi imebainika kwamba wapo ambao wanakuja nchini kwa ajili ya kuuza silaha mbalimbali zikiwemo bastola na bunduki za aina mbalimbali zikiwamo Smg kutoka Burundi nan chi zingine. Wapo pia ambao huingia nchini kwa lengo la kulisha mifugo yao, na uthibitisho wa hili ni kwamba wapo ng’ombe kadhaa na mifugo mingine ambayo imekamatwan nchini ikiletwa kwa ajili ya kulishwa.

CHADEMA ARUSHA WAVURUGANA .... MWENYEKITI WA CHADEMA ARUSHA, SAMSON MWIGAMBA ASIMAMISHWA UONGOZI


Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Ndugu Samson Mwigamba amesimamishwa nafasi ya uongozi hiyo mara moja kuanzia leo na Baraza la Uongozi la Kanda ya Kaskazini, huku taratibu zingine za kinidhamu zikiendelea kwa kufuata katiba, kanuni, maadili, miongozo na taratibu za chama.

Kikao hicho kimechukua hatua hizo mara moja baada ya Ndugu Mwigamba kukiri kwa maandishi kuwa ameandika kwa kutumia jina bandia na kutuma kwenye mitandao ya kijamii, kutoa tuhuma za uongo na kupotosha umma dhidi ya chama na viongozi, kinyume na katiba, kanuni, maadili, miongozo na taratibu za chama.

Hatua hiyo ya kukiri na kusimamishwa uongozi, ilifuatia baada ya Ndugu Mwigamba kutuhumiwa kusambaza katika mitandao tuhuma za uongo, upotoshaji na uchonganishi, ambapo kikao kilimwagiza kusalimisha kompyuta yake ili wataalam wa masuala ya IT wa CHADEMA, Kanda ya Kaskazini, waweze kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo.

Thursday, October 24, 2013

MAMA KANUMBA "HUYU MCHUNGAJI KAIRUKI ANANITAFUTA KWA KUDAI KANUMBA YUPO HAI"

Baada ya hivi karibuni kuibuka tena kwa yule nabii na Mchungaji George Kaiuruki na kudai kuwa Marehemue Steven Kanumba bado yu hai, FROLA Mtegoa - mama mzazi wa aliyekuwa mwigizaji nyota filamu wa Bongo marehemu Steven Kanumba amesikitishwa na tabia ya mtu anayejiita Nabii George Kairuki kwa kutumia jina na kifo cha marehemu mwanaye kama njia ya kujitengenezea fedha na umaarufu, mama Kanumba anasema kuwa awali Kairuki alitumia msiba wa mwanaye katika kuongelea vitu ambavyo hata familia haivijui isipo kuwa yeye pekee yake.

Mama Kanumba anadai kuwa hivi karibuni Kairuki alijitokeza kwa kudai kuwa Kanumba hajafa na amemtumia fedha katika simu yake, na kusema kuwa karibu atamrudisha duniani na kuendelea na maisha yake jambo ambalo mama wa marehemu anapingana nalo kwa kusema kuwa yeye kwa imani yake anaamini kuwa mwanaye amefariki na hakuna miujiza mingine.

“Huyu mtu anayeitwa Nabii George Kairuki sijui anatafuta nini katika familia yangu, Kanumba alikuwa ni kipenzi cha watu na sisi sote tumeshuhudia hilo kama kweli yeye ana uwezo wa kumfufua amfufue watu wote watafurahi kipenzi chao kurudi kama anavyosema yeye, mimi simjui hata sura zaidi ya kumuona katika picha,”anasema mama Kanumba

Mama Kanumba anasema kuwa iwapo Kairuki ataendelea na tabia hiyo itabidi afanye utaratibu wa kumfungulia mashitaka na hata ikibidi kumfungulia mashitaka na kumfunga endapo ataendelea na tabia ya kutumia sana jina la Kanumba katika kujitafutia fedha na kutangaza maneno ya ajabu ajabu.

VATICAN YAMSIMAMISHA ASKOFU KWA KUPENDA RAHA


Page_12_0_47c17.jpg
Kumekuwa na kelele za waumini nchini Ujerumani wakishinikiza askofu huyo afukuzwe kwa kukiuka taratibu.
Vatican City. Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani (Vatican) yamemsimamisha kazi Askofu wa Jimbo la Limburg, Ujerumani Franz-Peter Tebartz-van Elst anayekabiliwa na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha kwa shughuli za kifahari.
Vatican ilieleza jana kuwa uamuzi huo umechukuliwa baada ya kuridhika kuwa Askofu van Elst amekiuka maadili yaliyowekwa na Papa Francis kwa viongozi walioko chini yake akiwataka waishi maisha ya uchaji, umaskini.
Hadi sasa, kumekuwa na kelele nyingi miongoni mwa waumini nchini Ujerumani wakitaka askofu huyo afukuzwe kazi.
Miongoni mwa matumizi yake makubwa ni ujenzi wa makazi yake binafsi yaliyogharimu Euro 2.9 milioni (Dola 3.9 milioni), ukumbi wa chakula wenye mita za mraba 63 ambao ni pamoja na mesi na bafu yenye thamani ya Euro 15,000.

M23 WAIVURUGA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

m3 8b114
KUNDI la waasi wa M23, linalopambana na Jeshi la Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), limetajwa kuwa chanzo cha kuisambaratisha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Kauli hiyo imetolewa juzi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, katika mahojiano yake na kituo cha redio cha Clouds.


Membe amesema kinachosababisha Tanzania itengwe na baadhi ya nchi wanachama wa jumuiya ya EAC, ni hatua yake ya kupeleka majeshi katika mji wa Goma ulio Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kwa ajili ya kupambana na waasi wanaoipinga Serikali ya Rais Joseph Kabila.
Amesema hatua hiyo ya Tanzania ilizikera baadhi ya nchi wanachama wa EAC, zenye maslahi ya moja kwa moja na kundi hilo na kusisitiza kuwa hata kama itatengwa, kamwe haitaondoa vikosi vyake DRC na badala yake vitaendelea kupambana.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS OKTOBA 24, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.

.
.

AJALI MBAYA YATOKEA IRINGA JANA




k_fe241.jpg
Daladala aina ya Coster yenye namba za usajiri T.960 AQY inayofanya safari zake za Kibwabwa mjini Iringa mara baada ya kugongana na gari aina ya Isuzu Tipa, lenye namba SM 3363 katika Mlima wa Ipogolo eneo la Kisima cha Bibi.
l_dd9a2.jpg
m_74746.jpg
Taxi ambayo nayo ilisababishiwa ajari ikiwa katika eneo la tukio, huku askari polisi wakilinda usalama wa mali za abiria na baadhi ya vitu katika eneo la tukio.

n_7bc78.jpg
Wananchi wa mji wa Iringa wakitazama ajari hiyo katika mlima wa Ipogolo (Kisima cha Bibi).

MSAFARA WA RAIS KIKWETE WAKUMBWA NA BALAA LA MOTO MKALI

Moto mkubwa ukiteketeza msitu wa Sao Hill Mufindi



 Msafara  wa rais Jakaya  Kikwete ukiwa  umesimama kwa muda eneo la  msitu wa  taifa  wa Sao Hill Mufindi  katika barabara kuu ya Iringa- Mbeya  kufuatia  moto mkubwa kuwaka katika msitu huo jana mchana.


 Askari polisi akimamisha  msafara  wa rais Kikwete kutokana na moto  mkubwa  kutanda  eneo hilo la Changalawe katika  msitu wa Taifa  wa Sao Hill umbali wa mita  mbili kuelekea  barabara  ya Ikulu ndogo mjini Mafinga


 Askari  wa FFU  wakishuka katika gari lao kwenda  kuangalia  usalama  wa rais Kikwete na  kulia gari la kwanza ni naibu waziri wa ujenzi gari la pili la la tatu ni magari ya Ikulu yakiwa  yamesimama


 hapa  askari  wakishuka  kuingia katika moshi mzito  kuangalia  usalama  wa rais katika eneo hilo ambalo moshi mzito  ulitanda barabarani

ZIARA YA WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA CHENGDU - CHINA

IMG_0119
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakipata maelezo kuhusu kiwanda cha kutengeneza maligafi za viwanda vya plastiki cha Hongda Chlor alkali Chemical Base cha Chengdu nchini China akiwa katika ziara ya kikazi Oktoba 22, 2013,. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Abdallah Kigoda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) IMG_0427
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akizungumza na viongozi wa kampuni ya Dalian International ya China kwenye hoteli ya Shangri-la, Chengdu akiwa ktika ziara nchini China. Oktoba 22, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
IMG_0496
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akikagua eneo la Mradi wa umwagiliaji la Dujiangyan lililopo Chengdu nchini China akiwa kaika ziara nchini humo Oktoba 22,2013.(Picha naOfisi yaWairi Mkuu)
 IMG_0573
Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda akitia saini kitabu cha wageni baada ya kutembelea mradi wa umwagiliaji wa Dujiangyan uliopo Chengdu nchini China akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo   Oktoba 22, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Monday, October 21, 2013

TUME YA WARIOBA YAOMBA MUDA ZAIDI

warioba_1_bc902.jpg
Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeomba kuongezewa muda wa mwezi mmoja kutokana na ugumu wa kazi ya uchambuzi wa maoni yaliyotolewa na wananchi na asasi mbalimbali.
Tume hiyo inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba ilitakiwa kufanya kazi kwa miezi 18 kwa mujibu wa Sura ya 83 ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Maana yake ni kuwa Tume hiyo iliyoanza kazi Mei 1, mwaka jana ilitakiwa kukamilisha kazi yake Novemba 1, mwaka huu.
Ikiwa maombi hayo ya Tume yatakubaliwa ina maana watatakiwa kukabidhi ripoti yake Desemba 1, mwaka huu.
Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Augustine Ramadhan aliliambia gazeti hili kwa simu jana kuwa wamepeleka serikalini maombi ya kuongezewa muda wa kufanya kazi.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 21, 2013

DSC 0057 aae29
DSC 0058 6a210

Sunday, October 20, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 20, 2013

.

.

KENYATTA ARUHUSIWA KUTOHUDHURIA BAADHI YA VIKAO VYA KESI


017113680_35400_1b04e.jpg
Mahakama ya ICC jana Ijumaa(18.10.2013)ilimruhusu kwa kiasi fulani Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kutohudhuria baadhi ya vikao vya kesi dhidi yake, ili kumpa muda wa kushughulikia majukumu ya kisiasa.
Kenyatta , ambaye alichaguliwa kuwa rais mwezi Machi mwaka huu, amekuwa akidai kwa muda mrefu sasa kuwa kesi hiyo mjini The Hague itazuwia uwezo wake wa kuiongoza nchi.
"Mahakama hiyo kimsingi inamuondolea Uhuru Kenyatta ulazima wa kuwapo wakati wote katika kesi dhidi yake inayoanza Novemba 12, imesema mahakama hiyo ya ICC katika taarifa, lakini ikasisitiza kuwa ni lazima afike kwa ajili ya ufunguzi wa kesi hiyo.
Majaji wamesema kuwa ruhusa ya Kenyatta inatolewa kwa misingi kwamba anaweze kutimiza majukumu aliyonayo kama rais wa Kenya, na sio kwasababu ya kutoa hadhi kwa kazi yake kama rais.
Atakuwapo wakati wa kutoa ushahidi
Mahakama hiyo iliyoko nchini Uholanzi pia inasisitiza kuwa Kenyatta anapaswa kuwapo wakati pande zote zitakapokuwa zinatoa taarifa zao za mwisho katika kesi hiyo, wakati wahanga wanatoa ushahidi wao na pia,iwapo kutakuwa na haja wakati wa kikao cha kutoa hukumu.

MSHAHARA WA RAIS KAA LA MOTO


jk 17ab9
Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe kutaja hadharani mishahara ya Rais Kikwete na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, serikali imekataa kuizungumzia mishahara hiyo.
Msimamo wa Serikali kutotaja mishahara ya viongozi wakuu unatofautiana na utamaduni wa nchi nyingine kama Marekani, Afrika Kusini, Ufaransa na Kenya ambazo mishahara ya wakuu wake huwekwa wazi kwa umma.
Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema akiwa wilayani Igunga Mkoani Tabora, alisema Rais Kikwete anapokea zaidi ya Sh30 milioni kwa mwezi (sawa na Sh360 milioni kwa mwaka) ikiwa ni marupuru na mshahara kwa mwezi bila kodi, huku Pinda akipokea Sh 26 milioni kwa mwezi.
Akizungumza na Mwananchi kwa simu jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani alisema kiongozi yeyote haruhusiwi kutaja mshahara wa mtu mwingine kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria ya utumishi wa umma.
"Kuutaja mshahara wa mtu mwingine ni kinyume cha sheria na kosa, siyo utaratibu. Kwani wewe upo tayari watu waujue mshahara wako?" alihoji.

MATOKEO YA LIGI KUU YA UINGEREZA

2816039_orig_51785.jpg
Source: bongostaz

Friday, October 18, 2013

PAPII KOCHA, BABU SEYA...... NAFASI YA MWISHO, WANAHITAJI SALA NA DUA ZETU

 

Na Mwandishi Wetu

KITENDO cha Mahakama ya Rufaa kukubali kusikiliza marejeo ya hukumu ya kifungo cha maisha jela katika kesi iliyokuwa ikimkabili mwanamuziki Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ kimetafsiriwa kuwa ni kama wamepata nafasi ya mwisho ya kuweza kujinasua.


WARAKA WA PAPII KOCHA
Mahakama hiyo ilikubali ombi hilo hivi karibuni na kueleza kuwa marejeo hayo yanatarajiwa kusikilizwa Oktoba 30, mwaka huu ikiwa ni miezi kadhaa baada ya Papii Kocha kutuma waraka wa kuomba msamaha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu ndiye aliyekubali kuufikisha kwa JK hivyo kuna madai kuwa huenda waraka huo ndiyo umezaa matunda.
 
WARAKA UMEZAA MATUNDA?
“Unajua ule waraka ulikuwa na maneno ya kuumiza sana. Inawezekana kabisa kuwa ulimfikia JK akaagiza suala hilo liangaliwe upya. Haina maana kuwa JK anaingilia sheria. Nadhani wanasheria wana vipengele vingi ambavyo vinaruhusu marejeo ya rufaa hiyo. Kilichopo hapa ni namna ya kuzitafsiri sheria kisha kuona kama rufaa hiyo inaweza kusikilizwa.

SAKATA LA UFOO SARO LACHUKUA SURA MPYA UPANDE WA WAKWE...!!!



UTATA wa risasi umegubika tukio la kifo cha mzazi mwenzake na mwandishi wa habari wa ITV, Ufoo Saro, marehemu Anthery Mushi, aliyejiua kwa kujipiga risasi. Utata huo umeibuka baada ya ndugu wa marehemu Mushi kushangazwa na kuhoji mazingira ya kifo cha ndugu yao anayedaiwa kujipiga risasi mbili kidevuni na kupoteza maisha papo hapo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Msemaji wa familia hiyo ambaye pia ni kaka wa marehemu, Isaya Mushi alisema familia imebaki kizani juu ya kifo cha ndugu yao na kwamba anayejua siri nzito juu ya kifo hicho ni mzazi mwenzake, Ufoo.

Isaya, alisema mazingira ya kifo cha Mushi ni ya kutatanisha kwani baada ya mwili wake kufanyiwa uchunguzi na madaktari, zilitolewa risasi mbili kichwani, huku wakihoji risasi ya pili.

Kwa mujibu wa wataalamu waliobobea katika silaha, ni vigumu mtu kujiua kwa risasi mbili katika eneo la kichwa kwa maelezo kuwa risasi moja inatosha kumaliza uhai wa mtu katika eneo hilo.

“Sisi kama familia bado tukio hili linatupa utata, hivyo tunaomba Jeshi la Polisi litumie busara katika kufanya uchunguzi wa kina kwani, Mushi haiwezekani akajipiga risasi kidevuni ikanasa kwenye ubongo, halafu akajipiga tena kidevuni upande wa kushoto… imetushangaza na hatuelewi tukio hili,” alisema Mushi.


Alisema wanafahamu fika maisha aliyoishi kijana wao kwani alikuwa ni mtaratibu, hivyo maamuzi aliyoyachukua yalikuwa magumu.

“Kijana wetu enzi za uhai wake alikuwa ni mtaratibu, hivyo maamuzi aliyoyachukua yalikuwa ni magumu mno na mwenye siri hiyo ni mzazi mwenzake Ufoo, tuna imani ataeleza,” alisema Mushi.

ASKARI JKT WATEMBEZA KICHAPO KWA RAIA


Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Erick Komba
*******
Vurugu kubwa zilizopelekea mapambano makali kati ya wakazi wa kijiji cha Maramba wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga na askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi cha Maramba  na kusababisha watu 15  wakazi wa kijiji kujeruhiwa vibaya baada ya kupewa kipigo kutoka kwa askari hao.

Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Erick Komba,  alithibitisha  kutokea kwa vurugu hizo ambazo zilianza baada ya kumalizika kwa mechi ya soka kati ya timu ya JKT Maramba na Maramba City inayoundwa na wakazi wa kijiji hicho.

Komba alisema viongozi wa JKT kikosi cha Maramba wapo katika harakati za kutafuta chanzo cha vurugu hizo na kwamba hakuna  athari iliyotokea wala wananchi kujeruhiwa katika mapambano hayo.

MUME AMKATA MKEWE MKONO KISA WIVU WA MAPENZI


Majeruhi Leah Clement (24), akiuguza jeraha lake wodini katika Hospitali Teule ya Wilaya Geita kwa madai ya kukatwa mkono wake wa kushoto na mumewe.(PICHA:RENATUS MASUGULIKO)
Mwanamke mkazi wa kijiji cha Nyamikoma Kata ya Bugarama Wilaya ya Geita, Leah Clement (24), anadaiwa kukatwa mkono wake wa kushoto na mumewe kutokana na wivu wa mapenzi.
Hivi sasa mwanamke huyo amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita akiendelea kupatiwa matibabu.
Aidha, mtuhumiwa wa ukatili huo, anadaiwa ametoroka na kwenda kujichimbia kwa `sangoma' kwa imani kwamba hatakamatwa.

Tukio hilo lilitokea Oktoba 9, mwaka huu saa 1:30  usiku katika kijiji cha Chifufu kata ya Bugarama wilayani Geita.

Imeelezwa kwamba mtuhumiwa huyo alikwenda jikoni kwa mkewe na kukuta akisonga ugali kisha akamvamia na kumshambulia kwa panga lengo likiwa ni kumkata shingo yake.

RIPOTI YA MO IBRAHIM: RWANDA, TANZANIA ZINA UTAWALA BORA ZAIDI EAC

Kagame Kikwete2
Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete (kushoto)  na Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, nchi zao zimetajwa kuwa na utawala bora katika jumuiya ya Afrika mashariki
……………………………………………………………………………………………………………………………
Mahmoud Ahmad Arusha
Tasisi ya Mo Ibrahim juu ya Utawala Bora Afrika, imebaini nchi za Rwanda na Tanzania kuwa nchi zenye utawala bora zaidi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kati ya nchi 52 za kiafrika.
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa Jumatatu na taasisis ya Mo Ibrahim imesema Rwanda imepata wastani wa asilimia 57.8 ikiwa ni zaidi ya wastani wa kiafrika wa asilimia 51.6.
Hii inamaanisha kwamba nchi hiyo imeboresha utawala bora kwa zaidi ya asilimia 10.9 tangu mwaka 2000, ikiwa nafasi ya kwanza kwa nchi za Afrika mashariki ikifuatiwa na Tanzania iliyoshika nafasi ya 17 barani Afrika kwa kupata asilimia 56.9 huku Uganda ikiwa ya tatu ECA kwa kuwa ya 18 kwa kupata asilimia 56. Kenya imekuwa ya 21 na kushika nafasi ya nne kwa kupata asilimia 53.6 huku Burundi iliyopata asilimia 43.8 ikishika nafasi tano kwa EAC.

MWANAFUNZI AUNGUZWA MAKALIO KISA KAPOTEZA MBUZI

Untitled 22
Mwanafunzi wa darasa la nne shule ya msingi Bukokwa,  Wilaya ya Sengerema  mkoani Mwanza Cristina John (13)  aliyeunguzwa na jiko la mkaa na dada yake Paulina John baada ya kupoteza Mbuzi aliyekuwa malishoni.
Untitled 33
Paulina John  aliyefanya unyama wa kumuunguza mdogo wake Cristina John bila huruma na hajachukuliwa hatua zozote za kisheria huku vyombo vya dola vipo na vinafanya kazi.(picha na Daniel Makaka, Sengerema).
Na. Daniel Makaka, Sengerema.
Mwanafunzi mmoja  aitwaye Cristina John  mwenye umri wa miaka 13, ambaye anasoma darasa la nne 4,  katika shule ya msingi Bukokwa iliyopo kata ya Nyakarilo wilayani Sengerema ameunguzwa  jiko lilokuwa na mkaa wa moto na dada yake.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bwn. Timoth John  wakati akiongea na redio Sengerema hivi karibuni amesema kuwa, mtoto huyo ameunguzwa  na  jiko hilo lililokuwa na mkaa wa moto katika makalio yake ikiwemo sehemu zingine za mwili wake, kwakile kilichoelezwa kuwa  alipoteza mbuzi wakati akiwa amewapeleka malishoni.
 
Amefahamika kuwa tukio hilo limebainika baada ya  mtoto huyo kuomba msaada wa kupelekwa hospitalini kupatiwa matibabu, kutokana na  maumivu yaliyosababishwa na majeraha aliyoyapata.
 
Imeelezwa kuwa baada ya kutoa taarifa kwa wananchi wasamalia wema walimchukua na kumpeleka  katika zahanati ya kijiji hicho, na kupatiwa matibabu na baadaye taarifa hizo walizifikisha kwa Afisa mtendaji wa kijiji hicho, huku wakilaani kitendo hicho  kuwa ni cha kinyama na mhusika anapaswa kufikishwa katika vyombo vya dola.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 18, 2013



DSC 0012 f3426
DSC 0013 769e6

WAKIMBIZI WA SIRYA WATESEKA MISRI

AleppoCivilians_31072012_de2da.jpg
Shirika la kimataifa Amnesty International,linasema kuwa maafisa nchini Misri wanawazuilia mamia ya wakimbizi wa Syria katika mazingira mabaya sana.
Wakimbizi hao wanatoroka vita vinavyoendelea Syria.
Katika ripoti yake mpya, shirika hilo linasema kuwa idadi kubwa ya watoto wanazuiliwa wengi wakiwa hawana wazazi.
Kwa mujibu wa shirika hilo, baadhi ya wakimbizi wamezuiliwa katika vituo vya polisi ambako hali ni duni wengi wakiwa hawapati chakula wala matibabu kwa walio wagonjwa.
Linasema kuwa mjini Alexandria , mapacha wawili wenye mwaka mmoja walipatikana miongoni mwa wale waliozuiliwa.
Maafisa wa utawala bado hawajajibu tuhuma za shirika hilo.
Misri imekuwa ikikumbwa na vurugu za kisiasa tangu kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa Rais Hosni Mubarak mwaka 2011.

Thursday, October 17, 2013

REFA ALIYEPIGWA NA YANGA MWAKA JANA KUCHEZESHA PAMBANO LA WATANI JUMAPILI TAIFA

01_d16d6.jpg
Na Princess Asia, Dar es Salaam
REFA aliyewahi kupigwa na wachezaji wa Yanga SC Machi mwaka jana timu hiyo ikifungwa 3-1 na Azam FC katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Israel Nkongo Mujuni ndiye atakayepuliza filimbi katika mchezo wa timu hiyo dhidi ya watani wa jadi, Jumapili.
Nkongo alipigwa na wachezaji wa Yanga baada ya kumtoa kwa kadi nyekundu beki Nadir Haroub 'Cannavaro' akiwa tayari amempa kadi nyekundu kiungo Haruna Niyonzima pia.
Stefano Mwasyika aliyehamia Ruvu Shooting alimtupia ngumi ya 'kibondia' Nkongo na Nadir Haroub 'Canavaro' alionekana kuhusika katika vurugu hizo wote wakafungiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF). Mashabiki wa Yanga SC walifanya vurugu kubwa na kuvunja viti Uwanja wa Taifa siku hiyo.

Yamepita hayo na Nkongo amepewa tena mechi ya Yanga. Marefa wote wanne walioteuliwa kuchezesha mechi hiyo ya watani wa jadi, Simba na Yanga mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wanatambuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA)
Mbali na Nkongo atakayepuliza filimbi, wengine ni Hamisi Chang'walu atakayeshika kibendera upande wa jukwaa kuu na Ferdinand Chacha atakayeshika kibendera upande wa pili, wakati mezani atakaa Orden Mbaga.

MUSEVENI ATAKA WAPINZANI WAMUOMBE RADHI

col-kizza-besigye_3dbc4.jpgyuweri_71085.jpg

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amewataka viongozi wawili waandamizi wa upinzani nchini Uganda kuacha mapambao ya kisiasa wasiyoweza kushinda na badala yake wajiunge na chama tawala cha National Resistance Movement-NRM.
 Bwana Museveni alimshutumu mpinzani wake Kizza Besigye na meya wa Kampala, Erias Lukwago kwa kupinga program za maendeleo za serikali na kutangaza uongo. Alitaka aombwe msamaha na wapinzani hao wawili.
Lakini wote Besigye na Lukwago walipuuza wito wa Museveni wakiuita mchezo wa kisiasa wa kutaka kupata uungaji mkono wa chama tawala katika mji mkuu ambako wapiga kura mara nyingi hawakiungi mkono chama tawala.
Rais Museveni na chama chake tawala cha NRM wamekuwa madarakani tangu mwaka 1986. Lakini Lukwago anasema matamshi ya karibuni ya Museveni ni matokeo ya kile anachosema kinaonekana ni mgawanyiko katika chama tawala.
Lukwago alisema maafisa wa utawala mara kwa mara wanakataa kufanya kazi na wapinzani kuhusu wasi wasi wa umma shutuma ambazo wawakilishi wa chama tawala wanazikanusha hazina ukweli. Wanaushutumu upinzani kwa kuzorotesha juhudi za serikali za kuendeleza sheria na kanuni na kuhakikisha amani na uthabiti nchini humo. Kitu ambacho Lukwago hakubaliani nacho. Chanzo: voaswahili

Wednesday, October 16, 2013

WAZIRI MKUU MH. MIZENGO PINDA AWASILI CHINA NA KUPOKEA TAARIFA, ASIKITISHWA NA USAFIRISHAJI WA DAWA ZA KULEVYA



IMG_0072
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
*Asikitishwa na idadi kubwa ya wasafirishaji wa dawa za kulevya

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewasili Beijing, China saa 10 leo jioni (Jumatano, Oktoba 16, 2013) na kuanza vikao ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi yake ya siku tisa kwa mwaliko wa Serikali ya nchi hiyo.
Mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Beijing, Waziri Mkuu alielekea kwenye nyumba ya wageni ya Serikali ya Diaoyatui ambako alipokea taarifa fupi kuhusu hali ya kisiasa na kiuchumi nchini China.
Akiwasilisha taarifa hiyo mbele ya Waziri Mkuu, Balozi wa Tanzania nchini China, Luteni Jenerali (Mst.), Abdulrahman Shimbo alisema sehemu kubwa ya utekelezaji wa miradi kati ya Tanzania na China iko chini ya mwamvuli wa FOCAC (Forum on Africa China Cooperation) ambayo inagawanyika katika maeneo sita.
 Alyataja maeneo hayo kuwa ni misaada (grants), mikopo ya masharti nafuu (preferential loans), mikopo ya kibiashara (preferential buyers credit), uwekezaji, ushirikiano maalum na ushirkianao wa kihistoria.

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN ASISITIZA AMANI BARAZA LA IDD ZANZIBAR

DSC_0112
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein wapili kushoto akiomba Dua pamoja na viongozi wengine wa Kitaifa katika Swala ya Idi –El-Hjji ilioswaliwa Kitaifa huko katika kitongoji cha Marumbi Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja.kulia kwake ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar Khamis Haji Khamis na kushoto yake ni Katibu mtendaji wa Wakfu na Mali ya Amana Sheikh Abdalla Twalib,Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanizbar Maalim Seif Sharif Hamadi na wamwisho ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmod Mussa Wadi. DSC_0230
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akitoa hotuba katika baraza la Idi -El-Hajji lililofanyika huko Tunguu Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja DSC_0206
Baadhi ya Viongozi na Wananchi waliohudhuria katika Baraza la Idi-El-Hajji lililofanyika huko Tunguu Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja
PICHA ZOTE NA YUSSUF SIMAI ALI-HABARI MAELEZO ZANZIBAR

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...