Thursday, October 17, 2013

MUSEVENI ATAKA WAPINZANI WAMUOMBE RADHI

col-kizza-besigye_3dbc4.jpgyuweri_71085.jpg

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amewataka viongozi wawili waandamizi wa upinzani nchini Uganda kuacha mapambao ya kisiasa wasiyoweza kushinda na badala yake wajiunge na chama tawala cha National Resistance Movement-NRM.
 Bwana Museveni alimshutumu mpinzani wake Kizza Besigye na meya wa Kampala, Erias Lukwago kwa kupinga program za maendeleo za serikali na kutangaza uongo. Alitaka aombwe msamaha na wapinzani hao wawili.
Lakini wote Besigye na Lukwago walipuuza wito wa Museveni wakiuita mchezo wa kisiasa wa kutaka kupata uungaji mkono wa chama tawala katika mji mkuu ambako wapiga kura mara nyingi hawakiungi mkono chama tawala.
Rais Museveni na chama chake tawala cha NRM wamekuwa madarakani tangu mwaka 1986. Lakini Lukwago anasema matamshi ya karibuni ya Museveni ni matokeo ya kile anachosema kinaonekana ni mgawanyiko katika chama tawala.
Lukwago alisema maafisa wa utawala mara kwa mara wanakataa kufanya kazi na wapinzani kuhusu wasi wasi wa umma shutuma ambazo wawakilishi wa chama tawala wanazikanusha hazina ukweli. Wanaushutumu upinzani kwa kuzorotesha juhudi za serikali za kuendeleza sheria na kanuni na kuhakikisha amani na uthabiti nchini humo. Kitu ambacho Lukwago hakubaliani nacho. Chanzo: voaswahili

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...