Saturday, January 07, 2017

KLABU YA MBOWE YAZAMISHWA RASMI

nhc 
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limeanza kubomoa jengo la iliyokuwa Klabu Bilicanas na ofisi za Free Media inayomiliki gazeti la Tanzania Daima zinazomilikiwa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe, lililopo makutano ya barabara ya Mkwepu na Indira Gandhi lenye kitalu namba 725-726/24 na hati namba C. T No. 186018/15 and C. T No. 186018/10. 

Ubomoaji huo ulioanza jana unafanyika wakati Mbowe ameingia katika mgogoro na NHC baada ya kampuni ya udalali ya Poster and General Traders kumtolea vyombo nje mwanzoni mwa Septemba, mwaka jana kwa kudaiwa Sh bilioni 1.2 ambayo ni deni la pango ya miaka 20.

Gazeti hili lilishuhudia ubomoaji huo ukiwa katika hatua za awali na baadhi ya vijana walionekana wakianza kuondoa vioo na vigae vilivyoezekwa katika jengo hilo wakiwa chini ya usimamizi wa walinzi.

Hata hivyo, walipoulizwa watu waliokuwa wakisimamia katika eneo hilo walidai kuwa ubomoaji huo ni wa kawaida na ulipangwa kufanyika muda mrefu na endapo waandishi watahitaji maelezo wawasiliane na uogozi wa NHC.

NANA AKUFO ADDO AAPISHWA RASMI KUWA RAIS WA GHANA

Nana Akufo-Addo akila kiapo wakati akiapishwa 
 
Viongozi kadha wa Afrika leo wamekusanyika katika mji mkuu wa Ghana, Accra, kuhudhuria sherehe za kutawazwa rais mpya, Nana Akufo Addo.

Maelfu ya wageni walialikwa kwenye sherehe katika Medani ya Uhuru mjini Accra. Bwana Akufo Addo, aliyewahi kuwa wakili wa haki za kibinaadamu, alimshinda Rais John Dramani Mahama, katika uchaguzi wa mwezi uliopita.
Madaraka yanakabidhiwa kwa kiongozi mwengine kwa salama, jambo linaloonekana kuwa mfano mwema wa demokrasi Afrika ambako katika baadhi ya nchi, viongozi hawataki kun'gatuka.

Baada ya kuapishwa kwa rais, sasa viongozi waliohudhuria sherehe hiyo, watajadili namna ya kuhakikisha kuwa Rais wa Gambia, Yahya Jammeh, anaondoka madarakani. Kiongozi huyo amekataa kustaafu ingawa alishindwa katika uchaguzi wa Mwezi Disemba.

Tuesday, January 03, 2017

MKULIMA MWINGINE AJERUHIWA KWA SIME KILOSA

524332cd04985aff0de9f1e645398d62

MTU mmoja mkazi wa Kijiji cha Mamoyo, Kata ya Mabwerebwere, Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, Omary Sululu (52), amenusurika kifo baada ya kukatwakatwa na sime kichwani na watu wanaodaiwa kuwa ni wafugaji.

Taarifa zilizopatikana kijijini hapo, zinasema Sululu alijeruhiwa na wafugaji hao wakati alipokuwa akizuia mifugo isile mazao katika shamba lake.

Tukio hilo limetokea siku chache baada ya Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Joshua Lugaso, kutoa tamko la  kulaani matukio ya kikatili yanayofanywa  na  wafugaji dhidi ya wakulima wilayani Kilosa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii akiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa, Sululu alisema alijeruhiwa Januari mosi, saa za mchana wakati alipokuwa katika shamba lake la mahindi na migomba. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

ANGALIA PICHA ZA BABU MWENYE MIAKA 77 MWENYE NGUVU ZA AJABU AKIVUTA GARI KWA SHINGO....!!!

meet-the-77-years-old-strongest-man-in-akwa-ibom-photos-2
 
Babu wa miaka 77 kutoka mji wa Akwa Ibom, nchini Nigeria ambaye ana uwezo wa kuvuta gari kwa kutumia shingo yake.

Babu huyo amefahamika kwa jina la Sampson, ila yeye anataka afahamike kwa jina la African Superman, ana uwezo pia wa kuweka mkono wake juu na wanaume 10 wakabembea bila kuushusha mkono wake chini.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 03, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

04dafa6a-93c3-49cf-be2f-ccff44ac58ae

PLUIJM AKARIBIA KUPEWA MIKOBA YA UKOCHA AZAM FC

Mabingwa watetezi wa Kombe la Kagame, Azam FC wamebakiza hatua chache kukamilisha mpango wa kumkabidhi timu hiyo aliyekuwa kocha wa zamani wa Yanga, Hans Pluijm.

Habari za kuaminika kutoka vyanzo makini ndani ya Azam zilithibitisha kuwa tayari Azam imekuwa na mazungumzo ya kina na kocha huyo Mdachi ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa ufundi Yanga.
Awali, Azam ilipanga kumpa timu hiyo kocha wa Majimaji, Kally Ongala ambaye amewahi kuitumikia klabu hiyo kama kocha msadizi, lakini wakabadilisha mawazo kutokana na kocha huyo kuwa na uzoefu mdogo na michezo ya kimataifa.

Mwenyekiti wa Azam, Nassoro Idrissa ‘Father’ amesema Pluijm ni kocha wa kiwango cha juu na amethibitisha hilo nchini kwa kuipa Yanga mataji manne tofauti, hivyo watafurahi kama atafanya nao kazi. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Sunday, January 01, 2017

Saturday, December 31, 2016

SERIKALI NA UPINZANI WAAFIKIA MWAFAKA DRC

Wapatanishi wanaojaribu kutatua mzozo wa kisiasa huko Jamhuri ya Kidemocrasi ya Congo wamesema serikali ya nchi hiyo na vilevile washirika kutoka makundi ya upinzani sasa wameafikia mwafaka.

Maaskofu kutoka kanisa katoliki waliokuwa wakiendesha kikao hicho cha majadiliano wanasema makubaliano ni kwamba rais Joseph Kabila anaweza kusalia madarakani kwa mda wa mwaka mmoja, lakini ni sharti uchaguzi ufanyike ndani ya kipindi cha miezi 12.

Sharti jingeni ni kuwa rais Kabila asiwanie tena kiti cha urais katika uchaguzi huo.
Mwafaka huo unatarajiwa kutiwa saini hii leo. 

Mda wa utawala wa rais Kabila umemalizika mwezi huu lakini kutong'atuka kwake kumesababisha maandamano yaliyokumbwa na ghasia ambapo watu zaidi ya 40 wamefariki.

TRUMP AMONGEZA PUTIN KWA KUTOLIPIZA KISASI

 
Rais mteule wa Marekani Donald Trump amempongeza mwenzake wa Urusi Vladmir Putin kwa kutowafukuza wanadiplomasia wa Marekani ,licha ya Marekani kufanya hivyo kujibu madai ya kuingilia uchaguzi wa Marekani.

Bwana Trump alituma ujumbe katika mtandao wa Twitter: Hatua nzuri ya kusubiri, nilijua kwamba yeye ni mwerevu sana!.

Moscow imekana madai yoyote ya kuingilia uchaguzi wa Marekani kupitia udukuzi.
Lakini katika hatua moja ya mwisho ya uongozi wa rais Obama ,Marekani iliagiza kuondoka kwa wanadiplomasia 35 wa Urusi kufikia siku ya Jumapili mchana. Lakini Putin alikataa kulipiza kisasi.

Mvutano huo unafuatia madai kwamba Urusi ilidukua kampeni ya chama cha Democrat na mgombea wake Hillary Clinton na kutoa habari kupitia mtandao wa Wikileaks ili kumsaidia Bwana Trump kushinda uchaguzi .

Mashirika kadhaa ya Marekani ikiwemo lile la FBI na CIA yamesema hayo yalitendeka ,lakini Trump amekuwa akipuuzilia mbali madai hayo akisema ni ya ''ujinga''. Hatahivyo amesema kuwa atakutana na maafisa wa ujasusi nchini Marekani ili kuelezewa hali halisi. Serikali ya Obama ilitangaza kisasi hicho siku ya Alhamisi.

Sunday, December 25, 2016

JAMBO TZ INAWATAKIA KHERI YA CHRISTMAS WATU WOTE DUNIANI

 
Jambo Tz inawatakia heri ya Christmas🎄 wakristu na watu wote duniani. Tusherehekee kwa amani na utulivu.
Like page yetu ya facebook/jambotz

Thursday, December 22, 2016

UWEZO WA WANAWAKE KUPATA MIMBA WASHUKA TANZANIA

Viwango vya wanawake kuweza kupata mimba nchini Tanzania vimepungua hadi 5.2 kwa kila mwanamke nchini Tanzania mwaka 2015/2016 kutoka 6.2 kwa kila mwanamke miaka ya 1991/92, kulingana na utafiti wa afya nchini humo

Kulingana na gazeti la The Citizen la nchini Tanzania, utafiti huo uliofanywa na kutolewa na Afisi ya kitaifa ya Takwimu nchini humo NBS wiki iliopita unaonyesha kushuka kwa viwango vya uwezo wa kushika mimba miongoni mwa wanawake .

Kwa mfano mwaka 1996 ripoti hiyo inaonyesha watoto 5.8, mwaka 2004/05} ni watoto 5.7 mwaka 2010 ni watoto 5.4.

WAJUMBE WAIDHINISHA USHINDI WA TRUMP

Wajumbe wa jopo la wateule wanaoamua ushindi wa rais wa Marekani, wamemwidhinisha Donald Trump kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Novemba 8, mwaka huu.

Hatua hiyo imezima juhudi za dakika za mwisho za kutaka kumzuia Trump kuingia ikulu ya White House Januari 20.

Baada ya ushindi huo, Trump ameahidi ‘kufanya kazi kuunganisha nchi yake na kuwa rais wa Wamarekani wote’.

RAIS WA GAMBIA ASEMA HANG'ATUKI MADARAKANI NG'OO............!!!

Rais wa Gambia Yahya Jammeh ameonya kuwa atakataa jaribio lolote la viongozi wa kieneo kumlazimisha kuondoka madarakani licha ya kushindwa katika uchaguzi na mfanyibiashara Adama Barrow.

Akihutubia wanachama wa muungano wa Bar Afrika nchini humo Bw Jammeh alisema: ''Waje wajaribu kuniondoa.wanasubiri nini? mimi ni mtu mpenda amani lakini haimaanishi kwamba sitalitetea taifa langu, kwa ujasiri na uzalendo na kuibuka mshindi''.

Amesema kuwa alikataa wito wa muungano wa viongozi wa mataifa ya Magharibi ECOWAS akiwemo rais Muhammadu Buhari wa Nigeria na Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia kuondoka nchini Gambia.

Saturday, December 10, 2016

RAIS DR. MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA DANGOTE IKULU DAR ES SALAAM

Rais Magufuli alivyokutana na Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao cha pamoja na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote mara baada ya kumaliza kwa kikao chao Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kumaliza kikao chake na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mtwara Alhaji Aliko Dangote akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Desemba 2016, amekutana na kufanya mazungumzo na Mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo  Mtwara, Alhaji Aliko Dangote.

Katika mazungumzo hayo, Rais Magufuli amemhakikishia mfanyabiashara huyo kuwa serikali ya Tanzania itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wote nchini katika kutimiza lengo lake la kuwa na Tanzania ya Viwanda. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...