Wednesday, January 07, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 07, 2015

.
.
.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ZIARA YA MH. RIDHWANI KIKWETE JIMBONI KWAKE CHALINZE


 Ridhiwani akihutubia wananchi katika Kitongoji cha Chalinze Mzee wakati wa ziara ya kuwashukuru wananchi na kusikiliza kero zao pamoja na kuwashuru kwa kumchagua, pia alisema atatumia unasheria wake kuwasaidia baadhi ya wakazi wa jimbo hilo wanaonyimwa haki zao za msingi ikiwemo kuporwa ardhi.
 Mkazi wa Chalinze, Bibi akitoa malalamiko yake mbele ya Mbunge Ridhiwani Kikwete ya kudhulumiwa shamba lake na watu wasiojulikana.
 Mkazi wa Chalinze Methodius Kaijage, akiuliza swali kuhusu alama za x zilizowekwa kwenye nyumba zao kwa ajili ya upanuzi wa barabara ambazo alidai ni takribani miaka kumi imepita bila kupewa fidia hivyo kusababisha kukosa maendeleo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UTATA WAJITOKEZA KIFO CHA MESHACK YEBEI

William Ruto 

hali tata imezidi kujitokeza juu ya kifo cha Meshack Yebei, anayetajwa kuwa shahidi katika kesi inayomkabili Naibu Rais wa Kenya William Ruto.
Shahidi huyo alitarajiwa kutoa ushahidi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu-ICC dhidi ya naibu Rais wa Kenya.
Lakini mwishoni mwa wiki mwili wa Yebei ambao ulionekana kuunguzwa kiasi ,ulikutwa umetupwa kando ya mto huko Eldoret Magharibi mwa nchi hiyo.
Familia ya Yebei wanashuku kwamba chanzo cha mauaji hayo ilikuwa ni kumzuia ndugu yao asiweze kutoa ushahidi wake katika mahakama ya ICC huko The Hague. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SHELL YAKUBALI KULIPA FIDIA NIGERIA

Kampuni ya Shell nchini Nigeria 
 
Kampuni kubwa ya mafuta ya Shell imekubali kulipa dola milioni 80 kama fidia.
Kampuni hiyo ya Uholanzi imewapa fidia wakazi wa jamii ya Bodo katika eneo la Niger Delta walioathiriwa na uvujaji wa mafuta.
Mawakili wa wavuvi 15,600 wa Nigeria wamesema wateja wao watapokea dola za Kimarekani 3,300 kila mmoja kutokana na hasara iliyosababishwa na uvujaji wa mafuta hayo.
"Kiasi kilichobaki cha dola milioni 30 zitatumika kwa ajili ya shughuli za jamii ya Bodo ambayo iliathirika vibaya kutokana na matukio mawili ya kuvuja mafuta mwaka 2008 na 2009".
Mawakili hao wamesema mafuta hayo yaliharibu maelfu ya hekta za mikoko kusini mwa Nigeria.
Fidia hiyo imesemekana kuwa kuwa kubwa kuwahi kuliko zote zilizowahi kulipwa nchini Nigeria, na hivyo kumaliza mvutano wa kisheria uliodumu kwa miaka mitatu. Wanaharakati wanasema kampuni ya Shell ililazimika kukiri kosa hilo mapema zaidi.
Matukio yote mawili ya kuvuja kwa mafuta yametokea katika bomba hilo hilo la Trans Niger Pipeline, linaloendeshwa na kampuni ya Shell, ambalo linachukua mafuta kutoka visima vyake(Shell) kwenda kituo cha mwisho cha kusafirisha mafuta hayo nje kilichopo pwani ya Bonny. Bomba hilo linasafirisha mapipa 180,000 ya mafuta kwa siku. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KASEJA, YANGA GIZA NENE

kaseja
IPO misemo mingi ambayo huashiria kutokea kwa jambo liwe nzuri au baya, moja ya misemo hiyo ni ule usemao dalili ya mvua ni mawingu.
Msemo huu unaweza ukawa na na maana kubwa hivi sasa kwa golikipa wa timu ya Dar es salaam Young African, Juma Kaseja ambaye hivi sasa inaonekana hana mawasiliano mazuri na uongozi wa timu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar  es salaam.
Mchezaji huyo mwenye heshima kubwa nchini mwishoni mwa mwaka uliopita aliachwa katika kikosi cha timu hiyo kilichoelekea visiwani Zanzibar kushiriki michuano ya mapinduzi, lakini isitoshe jina la Kaseja halijaonekana kwenye orodha ya wachezaji wa timu hiyo iliyotumwa shirikisho la soka barani Afrika CAF kwa ajili ya ushiriki wa kombe la shirikisho.
Matukio hayo yote yameibua maswali mengi kwa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo juu ya hatma ya mlinda mlango huyo, hatua iliyotufanya tumtafute afisa habari na mawasiliano wa klabu hiyo Jerry Muro kutaka kufahamu kinaga ubaga kinachoendelea kati ya Kaseja na Yanga..
Muro amesema Kaseja kutohusishwa katika kikosi kilichopo Zanzibar na kilichotumwa CAF ni kujitakia mwenyewe.
http://jambotz8.blogspot.com/
Jerry Muro.  
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SIMBA KUWASHA CHECHE ZANZIBAR LEO

SAM_4333
ROBO fainali ya kwanza ya kombe la Mapinduzi inapigwa leo majira ya saa 2:15 usiku uwanja wa Amaan Zanzibar baina ya Simba na Taifa ya Jang’ombe.
Mechi hii imetabiriwa kuwa tamu kutokana na kiwango kikubwa walichoonesha Simba katika mechi ya mwisho ya makundi dhidi ya JKU ambapo walishinda goli 1-0.
Siku hiyo Simba waliuanza mchezo kwa kasi katika vipindi vyote, wakicheza pasi za haraka haraka na kutumia njia ya pembeni kuipenya ngome ya JKU.
Kocha Goran Kopunovic alitumia muda mwingi kuwaelekeza wachezaji wake namna ya kucheza mpira ambapo alisisitiza kwa ishara akiwataka wachezaji wapigiane pasi na kushambulia kupitia mawinga na kukaba kwa uangalifu.
Kocha huyo ameonekana kupenda kucheza mpira wa kasi muda wote na amekuwa akiwapa wachezaji wake mazoezi magumu ya kuongeza nguvu na pumzi.
Robo fainali nyingine tatu zitapigwa kesho uwanja wa Amaan ambapo majira ya saa 9:00 alasiri, mabingwa watetezi, KCC ya Uganda watachuana na Polisi Zanzibar.
Azam fc watashuka dimbani katika robo fainali ya tatu majira ya saa 11:00 jioni kuonesha kazi na Mtibwa Sugar.
Hii itakuwa mechi kali kutokana na ubora wa timu zote hususani Mtibwa Sugar wanaoongoza katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara.
Robo fainali ya mwisho itawakutanisha Yanga na JKU majira ya saa 2:00 usiku. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

"KIWANGO CHA NGASSA KIMESHUKA, LAKINI NI MCHEZAJI MWENYE AKILI, LAZIMA ATARUDI KATIKA KIWANGO CHAKE" - PLUIJM

KOCHA mkuu wa Yanga SC, Mholanzi, Johannes Hans van der Pluijm anaamini Mrisho Ngassa atarudi katika kiwango chake cha zamani.
Pluijm alikiri wazi kuwa nyota huyo ameshuka kiwango kwa sasa  na ndio maana anaanzia benchi katika mechi mbalimbali, lakini anaonesha juhudi kubwa mazoezini kitendo kinachoonesha wazi ametambua alipo sasa.
“Kiwango cha Ngassa kimeshuka, lakini ni mchezaji mwenye akili, lazima atarudi katika kiwango chake”. Alisema Pluijm.
NGASSA-MRISHO
Kocha huyo anayependa soka la kushambulia aliongeza kuwa kwasasa kikosi chake kimesheheni nyota wa kiwango cha juu, hivyo inawalazimu wachezaji kufanya jitihada za kumshawishi.
Moja kati ya mechi kubwa ambayo Ngassa hakuanza chini ya Pluijm mwishoni mwa mwaka jana ni ile ya ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Azam fc iliyopigwa desemba 28 mwaka jana uwanja wa Taifa ambapo timu hizo zilitoka sare ya 2-2.
Katika mechi hiyo, Ngassa alichezeshwa dakika 7 tu kitendo kilishoashiria mchezaji huyo kipenzi kwa Wana Yanga si mchezaji tegemeo tena katika kikosi cha Yanga. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

DROO YA KUPANGA MECHI KOMBE LA FA YAFANYIKA

Mabingwa watetezi wa kombe la FA, wakishangilia ushindi mwaka uliopita. 
 

Droo ya kupanga mechi za raundi ya 4 ya Kombe la FA imefanyika.
Katika mpangilio huo, vigogo Manchester United imepangwa kucheza na timu ya daraja la chini ya Cambridge United.
Mabingwa Watetezi, Arsenal, watakuwa Ugenini kucheza na Brighton au Hove Albion ambayo ipo Daraja la chini ya Ligi Kuu England.
Chelsea itakipiga na Mill wall au Bradford City. Manchester City itapepetana na Middlesbrough
Southampton/Ipswich na Crystal Palace
Blackburn Rovers na Swansea City
Michezo ya raundi ya nne inatarajiwa kupigwa Januari 24 na 25.
NAKO kwenye kombe la mapinduzi
Baada ya kutojulikana kuwa nani atacheza na Simba katika mechi ya robo fainali ya Kombe la Mapinduzi, sasa kila kitu kiko wazi. Simba itaivaa Taifa Jang'ombe katika mechi ya michuano hiyo hatua ya robo fainali hii leo usiku.
Mechi hiyo itachezwa saa 2 usiku kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Siku inayofuata Alhamisi, mechi nyingine ya robo fainali itapigwa jioni, nayo ni kati ya Azam dhidi ya Mtibwa Sugar.
Mechi hiyo inaaminika kuwa moja ya zile ngumu na safi za michuano ya Mapinduzi.
Yanga sasa itacheza mechi yake ya robo fainali dhidi ya maafande wa JKU.
Mechi hiyo itapigwa Alhamisi kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Yanga inakutana na JKU baada ya kumaliza vinara wa kundi A wakiwa na pointi 9. Walipata pointi hizo baada ya kushinda mechi zote tatu katika makundi kwa kujikusanyia mabao tisa, wakiwa hawajafungwa hata moja.
Walikamilisha pointi hizo tisa baada ya kuifunga Shaba kwa bao 1-0 katika mechi tamu na ya kuvutia jana usiku.
Bao la mchezo huo lilifungwa na Mbrazil Andrey Coutinho. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MATOKEO YA MECHI ZA JANA KOMBE LA FA ENGLAND HAYA HAPA… EVERTON YATOKA SARE

2475D89E00000578-0-image-a-88_1420581200502
 Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
England – FA Cup January 6
FT Everton 1 – 1 West Ham United
FT Scunthorpe United 2 – 2 Chesterfield

Tuesday, January 06, 2015

PROFESA SOSPETER MUHONGO AFANYA ZIARA SIMIYU KUKAGUA MIRADI YA UMEME

 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akitoa maelekezo kwa mtaalamu kutoka kampuni ya Symbion iliyopewa kazi ya kujenga miundombinu ya  umeme katika kijiji cha Nyamikoma kilichopo wilayani Busega Bw.  Steve Thomson (kushoto)
 Meneja wa Tanesco- Kanda ya Ziwa Mhandisi Joyce Ngahyoma, akifafanua jambo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na  wananchi wa kijiji cha Nyamikoma wilayani Busega (hawapo pichani)
 Mkazi wa kata ya Ijitu  iliyopo wilayani Busega ambaye  jina lake  halikupatikana mara moja akitoa hoja yake mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ( wa pili kutoka kushoto  waliosimama mbele) mara Waziri alipofanya ziara katika kijiji hicho na kusikiliza kero za wananchi
Diwani wa Kata  ya  Ijitu iliyopo wilayani Busega Vumi Magoti  akielezea kero za umeme katika kata yake mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ( wa pili kutoka kushoto), viongozi na wananchi  (hawapo pichani).
 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipokelewa na baadhi ya watendaji kutoka  Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) Kanda ya Ziwa na Nishati na Madini mara baada ya kuwasili katika  Uwanja wa Ndege wa Mwanza. Profesa Muhongo anafanya ziara  katika mikoa ya Simiyu, Tabora na Shinyanga lengo likiwa ni kukagua miradi  ya umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Taneesco. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 06, 2015

.
.
.

Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

URUSI KURUHUSU ASKALI KUTOKA NJE

Meli za ulinzi za Urusi 
 
Urusi imeanza kuruhusu askari kutoka nje wenye utalaam ili kuingia katika jeshi lake.
Hata hivyo, wataalam wa Urusi wanasema hatua hiyo haina uhusiano wowote na mgogoro nchini Ukraine.
Rais Vladimir Putin ameidhinisha sheria inayowawezesha raia wa kigeni kufanyakazi angalau kwa miaka mitano katika jeshi la Urusi ili mradi wanajua kuzungumza Kirusi.
Wataalam hao wanatarajiwa zaidi watatoka katika jamhuri za Asia ambazo awali zilikuwa sehemu ya muungano wa nchi za Soviet.
Wageni wa kujitolea, wakiwemo Warusi wamekuwa wakipigana nchini Ukraine. Hata hivyo Urusi imekuwa ikikana kupeleka majeshi yake huko.
Serikali ya Ukraine na nchi za magharibi wanasema Urusi imetuma silaha nzito na askari wenye utaalam wa hali ya juu kuwasaidia watu wanaotaka kujitenga mashariki mwa Ukraine. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

YANGA KUENDELEZA DOZI KOMBE LA MAPINDUZI...?!

8 (1)
HATUA ya makundi ya kombe la Mapinduzi inatarajia kumalizika leo kwa mechi nne kupigwa viwanja viwili tofauti hapa visiwani Zanzibar.
Mapema majira ya saa 9:00 alasiri katika uwanja wa Amaan, Mabingwa watetezi wa kombe hilo, KCC ya Uganda watachuana vikali na mabingwa wa Zanzibar, KMKM katika mchezo wa mwisho wa kundi B.
Mabingwa watetezi wa Tanzania bara, Azam fc watahitimisha mechi ya kundi B kwa kuchuana na Mtende, uwanja wa Amaan.
Katika dimba la Mao Dze Tung, Taifa ya Jang’ombe itakuwa kibaruani kuhitimisha mechi ya kundi A dhidi ya Polisi.
Yanga wao watacheza mechi ya mwisho ya makundi kwa kukabiliana na Shaba majira ya saa 2:15 usiku.
Yanga wanaingia katika mechi hii wakiwa tayari wameshafuzu hatua ya robo fainali kwani mechi mbili za kwanza dhidi ya Taifa ya Jang’ombe na Polisi, zote walishinda mabao 4-0. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SIGARA YAMPONZA KIPA ARSENAL

244D419E00000578-0-image-a-5_1420499963467
Mzee wa fegi, Wojciech Szczesny 
GOLIKIPA wa Arsenal, Wojciech Szczesny ametozwa faini ya paundi laki mbili kwa kosa la kuvuta sigara bafuni baada ya mechi.
.
Bosi wa kipa huyo mwenye miaka 24, Arsene Wenger aligeuka ‘mbogo’ alipomkuta akipiga fegi baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Southampton siku ya mwaka mpya.
Szczesny alilazimika kuomba msamaha kwa tabia hiyo, lakini haijulikani kama ataondolewa katika kikosi cha wiki hii kitakachoikabili Stoke kwenye mechi ya ligi kuu England. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

STEVEN GERRARD AIBEBA LIVERPOOL FA

 Steven Gerrard, nahodha wa timu ya Liverpool akishangilia bao na wachezaji wenzake katika moja ya mechi alizoichezea timu hiyo 
 
Steven Gerrard ameonyesha ubora na uongozi na Liverpool itamkosa mchezaji wa aina hii wakati atakapohama Anfield.
Ni Gerrard aliyewainua mara mbili vitini mashabiki wa Liverpool ilipoizamisha AFC Wimbledon mabao 2-1 katika michezo inayoendelea ya Kombe la FA.
Gerrard, akicheza mchezo wake wa kwanza tangu atangaze kuihama Liverpool katika msimu ujao na kwenda kukipiga Marekani, alionyesha pengo atakaloliacha atakapoihama timu yake aliyokulia na kupata mafanikio makubwa.
Nahodha huyo wa Liverpool ambaye atasherehekea miaka 35 katika siku ya mwisho ya Kombe la FA, tarehe 30 mwezi Mei aliiongoza timu hiyo kupata mafanikio na amefanya hivyo mara nyingi wakati timu ilipojikuta katika matatizo.
Gerrard alianza kuichezea Liverpool mwaka 1998. Gerrard amefunga magoli 182 katika michezo 696 aliyoichezea timu ya Liverpool.
Na katika mchezo mwingine Tottenham walitoka sare na Burnley kwa kufungana goli 1-1. Burnley ndio waliokuwa wenyeji wa mchezo huo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...