Serikali
imesema imeyafungia mashindano ya Miss Tanzania baada ya waandaaji
kukiuka taratibu na kanuni huku pia yakitajwa kukithiri kwa rushwa ya
ngono na upendeleo.
Mashindano hayo yalifunguliwa mwaka 1994,
yamefungiwa kwa miaka miwili baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa
wananchi na washiriki.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Bazara la Sanaa Tanzania
(Basata), Godfrey Mngereza alisema jana kuwa Kamati ya Miss Tanzania
kupitia kampuni yake ya Lino Agency, imekiuka kanuni na taratibu
zinazoongoza mashindano hayo.
“Ni kweli kwamba tumeifungia Miss Tanzania kwa
miaka miwili, lakini haya si maazimio ya tathmini iliyofanyika mapema
mwezi huu, bali kulikuwa na vikao mbalimbali vilivyofanyika na si
kimoja, ni uamuzi mgumu ambao umekuja kutokana na sababu maalumu,”
alisema Mngereza.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.