Monday, December 22, 2014

"WATANZANIA KUNUFAIKA NA AJIRA QATAR" PINDA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema Watanzania watanufaika na kipato na maarifa ya teknolojia ya kisasa kutokana na ajira, ambazo watapata katika nchi ya Qatar baada ya mkataba kusainiwa hivi karibuni.

Alitoa kauli hiyo jana jijini Doha, Qatar wakati akizumgumza na waandishi wa habari ili kuwapa taarifa fupi juu ya mambo yaliyojiri kwenye mazungumzo yake na Waziri Mkuu wa Qatar, Sheikh Abdulla Nasser Al Thani.
Katika mazungumzo hayo ambayo yalifanyika ofisini kwa Sheikh Abdulla, Pinda alisema wamekubaliana kutoa ajira kwa Watanzania kwa sababu nchi hii inahitaji wafanyakazi wengi kwenye sekta mbalimbali na raia wake ni wachache.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 22, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WAHITIMU 344 WA DARASA LA SABA HAWJUI KUSOMA NA KUANDIKA...!!!


Wanafunzi 344 waliomaliza darasa la saba mwaka huu mkoani hapa wamebainika kuwa hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu. Ofisa elimu wa mkoa, Nestory Mloka alitoa taarifa hiyo juzi katika kikao cha elimu kilichoitishwa kwa ajili ya kuchambua matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuwapangia shule wahitimu waliofaulu.

Mloka alisema kati ya walihitimu hao ambao hawajui kusoma na kuandika, wavulana ni 163 na wasichana 181. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KIKWETE "HATUWEZI KUENDELEA KWA KUTEGEMEA RAMLI"

Sehemu ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliyoko Tengeru, Arusha

Sehemu ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliyoko Tengeru Arusha.

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa kamwe Tanzania, kama ilivyo nchi nyingine yoyote duniani, haiwezi kuendelea kwa kutegemea mazingaombwe ama ramli bila kuwekeza kwenye maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Aidha, ametaka Watanzania kuacha mwenendo wa kutumia ubishi wa kisiasa kutafuta majawabu ya changamoto za maendeleo akisisitiza kuwa majawabu ya maendeleo yatapatikana katika maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Amewataka Watanzania kuongeza kasi yao ya matumizi ya intaneti akisema kuwa mfumo huo wa habari na mawasiliano ni chimbuko kubwa la elimu ikiwemo elimu ya sayansi kuliko kutegemea kupata elimu hiyo katika magazeti.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MUME AMJERUHI MKEWE KWA SHOKA KISA WIVU WA MAPENZI

Muonekano wa Malaysia.

Mama mwenye watoto watatu anapata matibabu hospitalini nchini Malaysia baada ya mumewe kuvamia mikono yake na miguu nakumcharanga kwa shoka la kucharangia nyama,na baadaye mwanamume huyo kujinyonga .
Mama huyo anatajwa kama K Menaga,amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Kluang upande wa kusini mwa jimbo la Johor baada ya shambulio hilo hatari lililotokea mapema mwezi huu.
Ingawa taarifa kutoka hospitalini hapo zinaarifu kuwa mama huyo ameshatolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi baada ya hali yake kuendelea vyema,na amelazwa katika wodi ya wagonjwa wa kawaida.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

WAAMUZI 11 WA KITANZANIA KWENYE ORODHA YA FIFA

Nembo ya shirikisho hilo,iliyo nakshiwa vyema.
 
Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA limetoa orodha mpya ya waamuzi linaowatambua ,Kwenye orodha hiyo kuna jumla ya waamuzi 18 kutoka Tanzania,miongoni mwa waamuzi hao waamuzi 11 wapya na 7 wa zamani.
Waamuzi wapya wa kati kutoka Tanzania ni Mfaume Ali Nassor kutoka visiwani Zanzibar pamoja na Martin Saanya kutoka Morogoro, pia wamo waamuzi watatu wa kike ambao ni Florentina Zabron ,Jonesia Rukyaa pamoja na Sofia Ismail.
Kwa upande wa waamuzi wasaidizi wanaume ni Frank John Komba na Soud Idd Lila , kwa upande wa wanawake ni Kudura Omary Maurice,Hellen Joseph Mduma,Dalila Jafari Mtwana na Grace Mawala.
Waamuzi wa zamani wa Tanzania kwenye orodha ya FIFA ,kwa upande wa wanaume ni Israel Mujuni Nkongo na Waziri Sheha Waziri,kwa upande wa waamuzi wasaidizi ni Josephat Bulali,Fernand Chacha,John Longino Kanyenye ,Ali Kinduli na Samuel Hudson Mpenzu .
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

STERLING MWANASOKA BORA CHIPUKIZI

Raheem Sterling.
 
Mshambuliaji kinda wa Liverpool, Raheem Sterling amekabidhiwa Tuzo ya Mwanasoka bora chipukizi mwaka 2014 na Chama cha soka cha England FA.
Sterling alikabidhiwa tuzo hiyo kabla ya Mechi wa ligi kuu ya England kati ya Liverpool dhidi ya Arsenal wakiwa uwanja wa nyumbani Anfield, ambapo mechi hiyo imemalizika kwa sare ya goli 2-2.
FA imekuwa na utaratibu wa kutoa tuzo ya Mwanasoka bora wa mwaka kwa wachezaji chipukizi wanaofanya vizuri katika mchezo wa soka.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Sunday, December 21, 2014

BIBI AMUUA MJUKUU WAKE KWA KUMTUPA NJE YA BASI

 
Mmoja wa abiria waliokuwamo kwenye basi hilo, Ebenezer Hans alilieleza gazeti hili kwamba mama huyo akiwa miongoni mwa abiria, alikuwa na mtoto wake mwenye umri unaokadiriwa miaka 14 na wajukuu wawili, ambao alikuwa akisafiri pamoja nao. PICHA|MAKTABA  

Jeshi la Polisi mkoani Singida, linamshikilia Nawaridi Saidi (45), mkazi wa Dar es Salaam kwa tuhuma za kumtupa mjukuu wake Mayasa Meshack (6) kutoka ndani ya gari wakati akisafiri kwenda Kigoma akitokea Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 18, saa 2 usiku katika Kijiji cha Igugumo, wilayani Iramba ambapo mama huyo akiwa kwenye basi aina ya Scania, alifungua dirisha kutoka katika kiti alichokaa na kumtupa Mayasa wakati basi likiwa katika mwendo.

“Mama alikuwa anaenda mkoani Kigoma kwa ajili ya Sikukuu za Krisimasi na Mwaka Mpya, aliambatana na mtoto wake mwingine ambaye jina bado halijafahamika,” alisema Kamanda Sedoyeka. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

SERIKALI YAONYA DAFTARI LA WAPIGAKURA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Mh. Willium Lukuvi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) William Lukuvi, ameonesha kutoridhishwa na utaratibu mbovu unaotumika kuandikisha wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura, kutokana na kuwa na mianya inayoweza kuingiza wasio raia wa Tanzania.
Lukuvi aliyasema hayo jana, wakati alipotembelea kituo cha Bunju A kuangalia uandikishwaji wa wananchi kwa kutumia teknolojia mpya ya Biometric Voter Registration (BVR).
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MITAA 89 KURUDIA UCHAGUZI LEO DAR



Jumla ya mitaa 89 kutoka wilaya tatu za Mkoa wa Dar es Salaam, leo zinatarajiwa kufanya uchaguzi wa marudio wa Serikali za Mitaa kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi uliofanyika Desemba 14 mwaka huu.

Moja ya kasoro hizo ni kuchanganywa kwa majina ya wagombea wa uenyekiti na wajumbe.

Manispaa ya Temeke ina mitaa 10, Kinondoni 16 na Ilala 63 .

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni, Mhandisi Mussa Natty, ameingia kwenye mvutano mkubwa na Chama cha Wananchi (CUF), kuhusu uamuzi wake wa kutaka uchaguzi urudiwe katika Mtaa wa Mwinyimkuu huku ikidaiwa chama hicho kilishinda.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DESEMBA 21, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUSABABISHA KIFO CHA PUNDA...!!!

pua 
Mwanaume mmoja nchini Hispania amefunguliwa mashtaka ya kutesa wanyama baada ya kusababisha kifo cha punda aliyemuua wakati akimkalia kwa lengo la kupiga nae picha.
Sabu ya kifo cha punda aliejulikana kwa jila na Platero inasemekana ni uzito uliopitiliza wa mwanaume huyo na kusababisha kumpa maumivu makali mnyama huyo hadi alipopoteza maisha baada ya siku tatu.
dd
Picha hiyo iliwekwa katika mitandao ya kijamii ikimuonyesha mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 38 akitabasamu huku akipiga picha na mnyama huyo.
Baada ya siku mbili Punda huyo aliyekua akiugulia maumivu alishindwa kusimama na baada ya uchunguzi wa Polisi aligundulika kuvunjika baadhi ya viungo vyake kutokana na kubeba kitu kizito. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

POLISI WAWILI WAUAWA MAREKANI

Eneo la mauaji ya polisi wawili mjini New York nchini Marekani.
 
Maafisa wawili wa polisi mjini New York Marekani wameuawa kwa kupigwa risasi walipokuwa ndani ya gari lao eneo la Brooklyn.
Kamishna wa idara ya polisi mjini New York Bill Bratton amesema kuwa maafisa hao walilengwa na kuuawa kutokana na sare walizokuwa wamevaa.
Alisema kuwa awali mwanamume huyo alikuwa ameandika ujumbe wa kuwashutumu polisi kwenye mtandao wa kijamii baada ya kumfyatulia risasi na kumjeruhi vibaya mpenzi wake wa zamani .
Mauaji hayo ya polisi yanajiri wakati kunashuhudiwa ghadhabu kali kufuatia uamuzi wa hivi majuzi wa kutowafungulia mashtaka polisi wazungu waliohusika kwemye mauaji ya waamerika weusi.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PLUIJM ATOA SIKU SABA (7) KUIBADILI YANGA


Kocha Hans Van Der Pluijm akiwa na Boniface Mkwasa katika moja ya mechi za Yanga Uwanja wa Taifa.

BAADA ya kupewa mkataba wa mwaka moja na nusu kukinoa kikosi cha Yanga kocha Hans van der Pluijm ameomba siku saba kuibadili timu hiyo.

Pluijm alisema atahakikisha anatoa mbinu zake zote alizokuwa nazo za ukocha ili aweze kuipa mafanikio timu hiyo msimu huu ikiwemo kutwaa ubingwa wa Tanzania bara.
Pluijm aliyetua Yanga kwa mara ya pili akichukua nafasi ya Mbrazil Marcio Maximo alisema kwa kuanza atatumia siku saba kwa ajili ya kubadilisha mfumo na kasi ya wachezaji ili waweze kushinda mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya mabingwa watetezi Azam FC utakaopigwa Uwanja wa Taifa Desemba 28.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

U.S.A YAITAKA KOREA KASKAZINI KUILIPA SONY

Wakuu wa kampuni ya filamu ya Sony Pictures.Marekani imeitaka Korea Kazkazini kuilipa kampuni hiyo kwa hasara iliopata baada ya madai ya kuhusika na uhalifu wa mtandao dhidi yake.
 
Marekani imezitaka China na nchi zingine kuthibitisha kuwa Korea Kaskazini ilihusika na uhalifu wa mtandao dhidi ya kampuni ya Sony Pictures.
Marekani inasema kuwa Korea Kaskazini ni lazima ikiri kuwa ilihusika na iilipe Kampuni ya Sony kutokana na hasara ambayo imepata
Korea Kaskazini imeyataja madai hayo ya Marekani kuwa ya uongo.
Wataalamu wanasema kuwa kuna ushahidi wa kutosha kuwa Korea Kaskazini ilihusika.
Lakini mwandishi wa BBC nchini Korea Kusini anasema kuwa kampuni ya Sony Pictures nchini Marekani na wakuu wake nchini Japan watahitajika kuamua iwapo wataonyesha filamu ya uchesi yenye utata ya rais wa Korea Kazkazini Kim Jong-un. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...