Monday, November 17, 2014

MKAPA ATAKA WAZEE NCHINI WASIBEZWE


Rais Mstaafu Benjamin Mkapa  

Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa, amewataka viongozi na Watanzania kutobeza busara na hekima za wazee kwa kuwa bado wana mchango mkubwa kwa Taifa.

Kadhalika mkuu huyo wa zamani wa nchi, alisema kuwa, mzee kuota mvi kichwani haina maana ya kupungukiwa na hekima na maarifa kama wengi wanavyofikiria

Mkapa alitoa kauli hiyo juzi jioni wakati mahafari ya kwanza ya Shule ya Sekondari ya St Peter Claver iliyoko nje kidogo ya Mji wa Dodoma.

Alisema anashangazwa kuona maeneo mengi wazee wanapuuzwa na kudharauliwa kama vile hawana mchango wowote kwa maendeleo ya jamii. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PROF. MAGHEMBE ASEMA URAIS SIO MASHINDANO YA UREMBO

Waziri wa Maji, Prof Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari wa gazeti hili, walipomfanyia mahojiano maalumu ofisini kwake mjini Dodoma, hivi karibuni. 

Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe ameshangazwa na utitiri wa watu wanaotaka kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu 2015, akisema nafasi hiyo ya juu nchini haifanani na mashindano ya urembo ambayo mtu yeyote anaweza kujaribu.

Mbunge huyo wa Mwanga alisema watu hao wanaojitokeza kuwania urais hawaelezi wanataka kulifanyia nini Taifa na akashauri wasioweza kueleza hoja zao wasichaguliwe kushika nafasi hiyo.

“Urais unahitaji kuwa na sifa, dira na ajenda kwa Taifa,” alisema Profesa Maghembe wakati wa mahojiano maalumu na gazeti hili mjini hapa.

Kauli ya Profesa Maghembe imekuja wakati Taifa likijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, 2015, huku chama chake, CCM kikikabiliwa na kazi ngumu ya kumpata mrithi wa Rais Jakaya Kikwete ambaye anamaliza muda wake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SHY-ROSE, SPIKA ZZIWA KIKAANGONI TENA


Mbunge Shy-Rose Bhanji.
Bunge la Afrika Mashariki (Eala) limeitishwa tena, zamu hii jijini Nairobi, Kenya ambako litakutana kuanzia leo mchana, huku kukiwa na shinikizo kubwa kutoka kwa wabunge 32 linalotaka kung’olewa kwa Spika wa Bunge hilo, Dk Margaret Zziwa na kuwajibishwa kwa mbunge kutoka Tanzania, Shy-Rose Bhanji.
Bunge hilo linakutana baada ya kuahirishwa kwa muda usiojulikana kutokana na kukosekana kwa mwafaka baina ya wabunge kwa upande mmoja na baadhi ya wabunge na Spika Zziwa kwa upande mwingine lilipokutana Kigali, Rwanda hivi karibuni. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAZIRI AJIUZULU KUPISHA UCHUNGUZI

 
Miguel Macedo waziri wa mambo ya ndani wa Ureno aliyejiuzulu 
 
Waziri wa mambo ya ndani wa Ureno amejiuzulu kupisha uchunguzi kuhusu tuhuma za rushwa inayohusishwa na utoaji vibali vya mgawo wa makazi.
Miguel Macedo amesema hahusiki na kashfa hiyo lakini anajiuzulu kulinda heshima ya taasisi za serikali.
Polisi wamewakamata watu 11, akiwemo mkuu wa idara ya uhamiaji nchini humo, siku ya Alhamisi.
Ureno inatoa visa za daraja la kwanza kwa wageni wanaotaka kuwekeza nchini humo.
Mnufaika mkuu wa uharakishaji wa vibali ni raia wa China ambao wamekuwa wakiwekeza kiasi kikubwa nchini Ureno.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAFUA YA NDEGE YATHIBITISHWA UINGEREZA

Ndege wanaofugwa wanakabiliwa na milipuko ya mafua ya ndege

Mlipuko wa mafua ya ndege umethibitishwa katika shamba moja la kuzalishia bata mashariki mwa Yorkshire, nchini Uingereza, wamesema maafisa.
Wizara ya Mazingira, Chakula na Masuala ya Vijijini (Defra) imesema hatari kwa afya ya umma ni ndogo sana. Ndege wasiohitajika wanaondolewa kutoka eneo hilo na eneo la kuwatenga limeandaliwa.
Tatizo hilo bado halijathibitishwa, lakini aina ya kirusi cha H5N1 hakijaweza kubainishwa na maafisa wa Defra.
Kirusi hicho husambaa kati ya ndege na katika matukio ya nadra, kinaweza kuwaathiri binadamu.
Picha ikimwonyesha mchuzi akiuza bata wake katika mtaa mmoja mjini Shanghai,China
Eneo la kuwatenga ndege lililopo kuzunguka shamba hilo litazuia ndege na kinyesi cha ndege ndani au nje ya eneo hilo.Ndege wote pia watatengwa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Sunday, November 16, 2014

MTOTO ANAYEDAIWA KUGEUKA NYOKA AZUA KIZAA ZAA

Mtoto mchanga mwenye umri wa miezi minne amezua kizaazaa cha aina yake, baada ya kuwapo taarifa kwamba mara kadhaa umbo lake limekuwa likigeuka na kuwa nyoka na mwili wake ukiendelea kudhoofu kutokana na kukataa kunyonya maziwa ya mama yake.
Mtoto huyo (jina lake tunalihifadhi kwa sasa), wiki iliyopita alivuta umati wa wakazi wa Kijiji cha Nkome mkoani Geita ambao walifurika ndani na nje ya Kanisa la AICT Nkome, lililopo kijiji hapo, kushuhudia maombi ambayo alikuwa akifanyiwa ili kumkomboa katika kile kilichotafsiriwa kuwa ni mateso dhidi yake.
Ilikuwa saa 4.00 asubuhi Jumamosi, Novemba 8 mwaka huu wakati mtoto huyo alipofikishwa katika kanisa hilo na kuanza kufanyiwa maombi na sababu ya hatua hiyo ikielezwa kuwa ni kutokana na kuwa na umbo la nyoka na kwamba matendo yake yanaashiria kwamba mwenye asili ya nyoka ndani ya roho yake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MBOWE AILIPUA SERIKALI KUHUSU BANDARI BUBU NCHINI

 
Mwenyekiti wa Chacha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe. PICHA|MAKATBA  

Mwenyekiti wa Chacha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema kuwa uwepo wa bandari bubu zinazopitisha bidhaa kwa magendo kutoka nje ni miongoni mwa sababu zinazoua viwanda vya sukari hapa nchini.
Amesema kuwa viwanda vya miwa vinapokufa, wanaoumia siyo wenye viwanda bali wakulima wa miwa. Mbowe alisema hayo juzi alipohutubia mamia ya wafuasi wa chama hicho mjini Turiani , Mkoa wa Morogoro katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo.

Ziara hiyo ni ya Operesheni Delete CCM (ODC) yenye lengo la kuvihamasisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kuiondoa CCM madarakani kuanzia katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA AHIMIZA KUCHANGIA ELIMU

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. PICHA|MAKTABA 

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ametoa rai kwa Watanzania kujenga utamaduni wa kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu, badala ya kujikita kuchangia sherehe za harusi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Stephen Kwebwe aliyezungumza kwa niaba ya Pinda katika sherehe ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari Mwenyeheri Anuarite iliyopo Makoka, jijini Dar es Salaam.
“Urithi pekee kwa watoto wetu ni elimu, unaweza kumwachia mali, lakini itakwisha, ukimwachia elimu hakika huu ndiyo urithi pekee…: Watanzania wenzangu, tujitoe kuchangia sekta ya elimu kama ambavyo tunafanya katika sherehe,” alisema Kebwe akiongeza:
“Utamkuta mtu anachangia fedha nyingi katika harusi na kama tunavyojua harusi moja, ukianza na ‘send off’, ‘kitchen part’ na harusi yenyewe ni fedha nyingi, lakini mtu huyo huyo ukimwambia achangie masuala ya elimu, hutamwona.”
Naye Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Gaudence-Makoka wamiliki wa shule hiyo, Padre Evarist Tarimo, alisema kuwa malengo ya sherehe hiyo ni kuchangisha Sh250 milioni kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa bweni la wavulana ili kuondoa adha wanayoipata kwa sasa.
“Hivi sasa vyumba vya madarasa tunavitumia kama mabweni, hivyo wanasomea humo na kulala humo humo, jambo ambalo kitaaluma si zuri. Tunatarajia tutakapomaliza ujenzi huo tutawawezesha wanafunzi wetu kusoma na kulala katika mazingira mazuri na nina hakika juhudi za wadau zitaweza kukamilisha ujenzi huu,” alisema. Habari tulizozipata baadaye zilisema jumla ya Sh41.2 milioni zilikusanywa. Fedha taslimu ni Sh13.3 milioni. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 16, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
. 
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, November 15, 2014

BUTIKU AMKINGIA KIFUA WARIOBA

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Mwalimu Nyerere , Joseph Butiku 

Taasisi ya Mwalimu Nyerere imesema kuwa wanaotaka aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akae kimya kuhusu Katiba Inayopendekezwa hawana hoja.
Imesema kuwa wanaosema hivyo hasa wale wa chama tawala (CCM) wanatakiwa kujiuliza kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita wamefanya nini kuhusu Katiba, ikisisitiza kuwa itaendelea kufanya midahalo ya kuwaelimisha Watanzania kuhusu mchakato wa Katiba ili utakapofika wakati wa kura ya maoni waelewe kipi wanatakiwa kukifanya kwa mustakabali wa taifa.
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Joseph Butiku alisema hayo jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalumu na gazeti hili kuhusu kazi na majukumu ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere tangu ilipoanzishwa hadi sasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

G20 YAMUONYA PUTIN AONDOKE UKRAINE

Viongozi wa mataiifa ya magharibi wanaohudhuria mkutano wa mataifa tajiri, G-20 mjini Brisbane, Australia, wameionya Urusi ifuate makubaliano ya kusitisha mapigano Ukraine, ama sivyo itakabili vikwazo zaidi.
Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, alimwambia Rais Putin kuwa uhusiano baina ya Ulaya na Urusi utabadilika iwapo wanajeshi wa Urusi watabaki Ukraine.
Rais Obama alisema hatua za Urusi zinachusha.
Urusi inakanusha kuwa ina wanajeshi wake ndani ya Ukraine.
Msemaji wa Bwana Putin alitoa maanani ripoti kuwa kiongozi wa Urusi anapanga kuondoka mapema kwenye mkutano. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

EBOLA YAISHA DRC, YAONGEZEKA S-LEONE

Jamhuri ya Demokrasi ya Congo imejitangaza kuwa haina tena virusi vya ebola baada ya virusi kuambukiza watu kwa miezi mitatu na kuuwa wagonjwa karibu 50.
Virusi vya Ebola vilivyoathiri Congo ni tofauti na vile vya Afrika Magharibi.
Lakini Waziri wa Afya, Felix Kabange Numbi, amewasihi watu bado kuwa macho - kwamba kumalizika kwa ugonjwa, haimaanishi kuwa nchi haiko kabisa hatarini.
Na Daktari wa Sierra Leone ambaye ameambukizwa Ebola amepelekwa Marekani kwa matibabu.
Martin Salia, ambaye ana kibali cha makaazi Marekani na ambaye ameoa Mmarekani, atatibiwa wakati ametengwa kwenye kitengo maalumu katika jimbo la Nebraska.
Haijulikani iwapo Dr Salia, daktari wa upasuaji, aliuguza wagonjwa wa Ebola Sierra Leone.
Hospitali alikofanya kazi haina kituo cha kuuguza wagonjwa kama hao.
Dakta Salia atakuwa mgonjwa wa 10 wa Ebola kuuguzwa Marekani.
Hadi sasa watu zaidi ya 5,000 wamekufa kutokana na Ebola Afrika Magharibi.
Juma hili iliripotiwa kwamba wakati idadi ya maambukizi ya Ebola yanapungua Liberia na Guinea, bado yanaongezeka nchini Sierra Leone.
Na katika tukio jengine, Ufaransa imewashauri raia wake wasiende katika sehemu fulani za Mali baada ya watu watatu kufariki huko kwa sababu ya Ebola.
Raia wa Ufaransa walioko Mali wameambiwa wafuate ushauri wa serikali ya Mali. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 15, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

GUINEA IKWETA KUANDAA AFCON 2015


Guinea ya Ikweta inaandaa michuano ya AFCON mwakani

Shirikisho la soka la Afrika CAF limeichagua na kuipatia nafasi Guinea ya Ikweta kuandaa fainali za kombe la Afrika 2015 kuchukua nafasi ya Moroko iliyojitoa wiki iliyopita. Awali Rais wa CAF Issa Hayatou alikuwa na majadiliano yenye manufaa na Rais wa nchi hiyo tajiri ya mafuta Teodoro Obiang Nguema mjini Malabo kabla ya kufikia hatua ya kuikabidhi nchi yake dhamana hiyo.
Taarifa ya CAF imethibitisha leo ijumaa kuwa Guinea ya Ikweta mojawapo ya nchi ndogo barani Afrika imepewa jukumu hilo kubwa la kuokoa jahazi la michuano hiyo na itashiriki fainali hizo kama ilivyo kawaida ya mwenyeji. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...