Tuesday, November 11, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAFUNZI 47 WAUAWA SHULENI

Wapiganaji wa Boko Haram wamekuwa wakishambulia eneo hilo la Potiskum

Kumetokea shambulizi katika shule moja ya upili wakati wanafunzi wakiwa wamekusanyika shuleni humo mjini Potiskum Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Duru zinasema kuwa wanafunzi 47 wameuawa katika shambulizi hilo linalosemeklana kufanywa na mshambuliaji wa kujitoa mhanga ambaye alikuwa amevalia sare za shule.
Shambulizi lilitokea wakati wanafunzi wakiwa wamekusanyika wakati wa asubuhi. Mji wa Potiskum ambapo shule hiyo ipo, umekuwa kitovu cha mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanywa na Boko Haram.
Shule hiyo ni ya mafunzo ya sayansi. Mwalimu mmoja alinukuliwa akisema kuwa alisikia mlio mkubwa wa kutisha wakati bomu hilo lilipolipuka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

USALAMA MDOGO, BENI DRC

Kikosi cha UN, DRC kinashutumiwa kwa kutolinda usalama vya kutosha
Baada ya miezi kadhaa ya utulivu katika eneo la mashariki mwa DRC, ghasia zimerejea tena.
Zaidi ya watu 120 wakiwemo wanawake na watoto waliuawa kwa mapanga na mashoka mwezi uliopita katika eneo la mpakani na Uganda.
Inadhaniwa kuwa kundi la waasi kutoka nchini Uganda la ADF ndilo linalohusika na mashambulizi hayo.
Vikosi cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo MONUSCO kimekuwa kikilalamikiwa katika mji huo wa Beni kwa kushindwa kuzuia mauaji, licha mamia ya wanajeshi wake kuweka kambi katika eneo hilo.
Lakini hata hivyo wenyewe wanasema ni vigumu kuweza wakuwalinda raia wote, licha ya kuchukua hatua kadhaa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SOCIEDAD WAMUITA MOYES KUWA MENEJA

David Noyes
Kocha wa zamani wa timu ya Manchester United David Moyes ametajwa kuwa meneja mpya wa timu ya kutoka Hispania,Real Sociedad.
Kocha huyo mwenye miaka 51, hii ni kazi yake ya kwanza baada ya kutimuliwa kwenye kilabu cha Man U mwezi wa nne mwaka huu, .
Moyes anachukua nafasi ya Jagoba Arrasate ambaye pia ametimuliwa na Sociedad baada ya matokeo mabaya na kusababisha timu hiyo kuangukia nafasi ya 15 katika ligi kuu nchini humo, maarufu kama La Liga.
Mkataba wa Moyes na Real Sociedad ni mpaka june mwaka 2016 na kwama mara ya kwanza ataonekana katika mechi ya Deportivo November 22. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NANI MWENYEJI WA CAF 2015...???



Kombe la mataifa ya Africa

Hatma ya nani atakuwa mwenyeji wa kombe la mataifa ya Africa 2015 maarufu kama Africa Cup of Nations lazima ajulikane, kwani kamati ya shirikisho la vilabu vya soka barani Africa imekutana kujadili juu ya suala hili .
Morocco ndiye aliyekuwa anapewa nafasi kubwa kuwa mwenyeji wa michuano hiyo kuanzia tarehe 17 mwezi wa kwanza hadi mwezi wa pili tarehe 8, lakini kuna kila dalili Morocco inataka kuahirisha michuano hiyo kwa hofu dhidi ya ugonjwa hatari wa Ebola kuwa utaingia nchini humo.
Leo ndiyo leo, leo inapaswa kuwa siku ya kuamua kati ya Morocco na bodi ya shirikisho la mpira wa miguu barani Africa CAF, ile sintofahamu baina yao inatatuliwa.
Mwishoni mwa wiki iliyopita waziri wa michezo wa Morocco,alisimama na kuongea kwa kifupi yakwamba hawataweza kuwa mwenyeji wa michuano hiyo na badala yake wasikilizwe ombi lao la kuahirishwa kwa michuano hiyo mpaka mwaka wa 2016.
Wakati hayo yakijiri CAF wametoa msimamo wao ya kuwa tarehe ya kuanza kwa michuano hiyo haitabadilika,sasa swali linakuja je CAF wana nchi nyingine iliyotayari kupokea michuano hiyo na kuwa mwenyeji? Ilhali imebakia wiki kumi tu? Na kama inawezekana basi itakuwa ni kati ya nchi zilizokuwa wenyeji wa michuano hiyo miaka ya karibuni,ambayo CAF ina uhakika na miundo mbinu yake na uwanja ulio tayari ndani yake.
Mnamo mwaka 2013, mwenyeji wa michuano hiyo ilikuwa ni Africa Kusini ambayo tayari imekwishatoa msimamo wake kuwa wala wasiitie mawazoni kuwa wao ndo kimbilio la kunusuru michuano ya mwaka huu.
Nao CAF sasa wanatarajiwa kutoa tamko lao la mwisho juu ya suala hili, haraka iwezekanavyo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, November 10, 2014

UTATA TENA: MISS TANZANIA MPYA SI RAIA WA TANZANIA...??!

Baada ya taji la Miss Tanzania kuvishwa kwa mshindi wa pili, utata mwingine umeibuka baada ya mrithi huyo, Lilian Kamazima kudaiwa kuwa si raia.

Jana kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kulikuwa na taarifa zinazodai kuwa Lilian siyo raia wa Tanzania na kwamba anatokea Rwanda.

Akizungumzia tuhuma hizo, Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ndiyo waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania, Hashim ‘Uncle’ Lundenga alisema tuhuma hizo kuhusu Lilian siyo kweli. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MBOWE 'AMWAGA SUMU' NYUMBANI KWA SAMUEL SITTA...!!!


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiwasili kwenye Uwanja wa Extended mjini Urambo, Tabora alikohutubia mkutano wa hadhara juzi. 


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amefanya mkutano mkubwa Urambo Mashariki na kumshutumu Mbunge wa jimbo hilo, Samuel Sitta kwa kuchakachua maoni ya wananchi katika mchakato wa Katiba Mpya.

Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Extended mjini hapa takriban mita 100 kutoka nyumbani kwa Sitta aliyeongoza Bunge la Katiba, Mbowe alisema historia ya nchi hii itamhukumu mbunge huyo kwa maovu hayo.

Alisema kutokana na uovu huo wa Sitta ambaye amekuwa akiisifia Katiba Inayopendekezwa kuwa itakuwa nzuri Afrika Mashariki na Kati, vyama vya upinzani vitaendelea kuidai katiba ya wananchi hata kwa miaka 100 ijayo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

IKULU: "TUMEFEDHEHESHWA KWA KITENDO CHA JAJI WARIOBA KUSHAMBLIWA"


Balozi Ombeni Sefue


Serikali inapitia upya ulinzi wa viongozi wastaafu ili kuepuka fedheha iliyotokana na vurugu alizofanyiwa Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba hivi karibuni.

Mpango huo umeelezwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue mwishoni mwa wiki, akisema Serikali imekerwa na kufedheheshwa kutokana na tukio hilo lililotokea wakati wa mdahalo wa Katiba Inayopendekezwa katika Hoteli ya Blue Pearl, Dar es Salaam Novemba 2, mwaka huu.

“Kimsingi tutakachokifanya ni kupitia upya mpango wa ulinzi wa viongozi wote waliostaafu, japokuwa huwa tunafanya hivyo mara kwa mara, lakini kwa hili la Mzee Warioba tunaliangalia kwa umakini wake.

“Tumekerwa sana na tukio lile, halikutufurahisha hata kidogo kama Serikali kwa kuwa limemvunjia heshima Mzee Warioba, yule ni mzee wetu, anahitaji heshima, kwanza heshima yake na ulinzi.”

Kauli hiyo ya Sefue imekuja wakati mdahalo huo uliovunjika baada ya Mzee Warioba kushambuliwa, ukiwa umetangazwa kufanyika upya Jumapili Novemba 16, mwaka huu katika hoteli hiyohiyo.

Mjumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole alithibitisha jana kuandaliwa kwa mdahalo huo kuanzia saa 9.00 alasiri siku hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

'KURA YA MAONI MWANZO WA KUDAI KATIBA MPYA'


Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo - Bisimba akizungumza na waandishi wa Gazeti la Mwananchi katika mahojiano maalumu yaliyofanyika hivi karibuni Dar es Salaam.

Wakati Serikali ikihaha kuhakikisha inaandika historia mpya kwa kupitisha Katiba Inayopendekezwa Aprili 30, mwakani, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo – Bisimba amesema siku hiyo itakuwa mwanzo wa Watanzania kudai Katiba Mpya.

Dk Kijo – Bisimba, mmoja wa wanaharakati maarufu wa haki za binadamu nchini, amesema katika mazingira ambayo mchakato wa Katiba una dosari nyingi, ilikuwa ni busara kuusimamisha kwanza ili kujitathmini kabla ya kuendelea na Kura ya Maoni.

Mhitimu huyo wa shahada ya uzamivu ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Warwick, Uingereza, alisema hayo katika mahojiano maalumu na gazeti hili yaliyofanyika wiki iliyopita.

“Katiba hata ikiwa nzuri kiasi gani, kama haitokani na wananchi, haiwezi kukubalika,” alisema Dk Kijo – Bisimba akisisitiza hoja yake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MLIPUKO WATIKISA SHULE NIGERIA

Kumetokea shambulizi katika shule moja ya upili wakati watoto wakiwa wamekusanyika shuleni humo mjini Potiskum Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Hata hivyo hakuna taarifa kamili kuhusu idadi ya majeruhi kufikia sasa.
Mlipuko huo ulitokea katika shule ya mafunzo ya sayansi ya vijana mjini humo.
Kundi la wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram huenda ndilo limefanya shambulizi hilo, ila taarifa bado hazijathibitisha hilo.
Kundi hiulo limekuwa likishambulia shule katika harakati zake za miaka 5 likitaka kuunda dola ya kiisilamu. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

RAIS OBAMA AIZUNGUMZIA IRAQ

Rais wa Marekani Barack Obama
Rais Obama amesema awamu ya kwanza ilikuwa ni kwa ajili ya kuandaa serikali ya pamoja na yenye kuaminika nchini Iraq. Kitu ambacho amesema kimefanyika, na kuongeza kwamba muungano huo wa kijeshi unaopambana dhidi ya kundi hilo la wapiganaji unajiandaa kwa mashambulizi.
Tulichojua ni kwamba awamu ya kwanza iulikuwa ni kupata serikali ya umoja wa Kitaifa na ya uhakika Iraq. Na tumefanya hicho. ''..Na sasa tulichofanya ni zaidi ya kulimaliza nguvu kundi hilo la ISIL.
Kwa sasa tupo katika nafasi ya kuanza tena mashambulio kama ya awali. Mashambulizi ya anga yaliyofanywa yalifanikiwa katika kushusha uwezo wa kundi hilo la ISIL na kupunguza nguvu hatua waliyopiga.
Sasa tunachohitaji ni jeshi la ardhini, Jeshi la ardhini la Iraq, litakaloweza kuwarudisha nyuma..'' Nchini Iraq kwenyewe maafisa wanasema jeshi limekuwa likipiga hatua katika jihada za kuwaondoa wapiganaji hao wa kiislamu katika mji wa Baiji. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, November 08, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 08, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TAZAMA PICHA ZA BILIONEA ALHAJ ALIKO DANGOTE ALIPOTEMBELEA KIWANDA CHAKE MTWARA, NI KILE CHA KUZALISHA SARUJI

Gari iliyombeba mfanyabiashara maarufu barani Afrika, Mwenyekiti wa kundi la makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote, likipita mbele ya majengo yatakayokuwea kiwanda cha kuzalisha sarujit nje kidogo ya mji wa Mtwara, Nov 6, 2014. Ujenzi wa kiwanda hicho unatarajiwa kukamilika Juni 2015

mfuko wa kwanza wa sementi utaanza kufyatuliwa Juni 8, 2015.
Alhaj Dangote akiteta jambo na kaimu mkuu wa mkoa wa Mtwara, Ponsiano Nyami, baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea kiwanda hicho
Alhaj Dangote, (Kulia), akipokelewa na mwakilishi mkazi wa kampuni ya Dangote hapa nchini, Esther Baruti kwenye uwanja wa ndege wa Mtwara
Mainjinia wakimpatia maelezo ya maendeleoya ujenzi wa kiwanda hicho, mmiliki wake, Alhaj Aliko Dangote, (akiwa ndani ya gari) Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU 10 WAUAWA KATIKA MLIPUKO NIGERIA

Mlipuko katika eneo la bauchi nchini Nigeria
Ripoti kutoka kaskazini mwa Nigeria zinasema kuwa watu kadhaa wameuawa na mlipuko wa bomu karibu na mashine ya kutoa pesa ya ATM.
Walioshuhdia walisema kuwa ,mwanamume mmoja alikaribia watu waliokuwa wamepanga foleni kwenye mashine hiyo kwenye mji wa Azare ulio katika jimbo la Bauchi .
Walisema kuwa mwanamme huyo alikuwa amebeba bahasha ambayo baadaye ililipuka.
Siku ya Jumatano watu wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram walivamia kiwanda kimoja cha saruji ambapo walichukua baruti wanayotumia kwenye milipuko. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...