Thursday, August 14, 2014

SOMA HAPA UPATE ELIMU KUHUSU KUJIKINGA NA UGONJWA HATARI WA EBOLA

Hivi karibuni tumesikia Mlipuko wa Ugonjwa Hatari wa Ebola ambapo tayari umesharipotiwa kuua zaidi ya watu 1000 huko Guinea, Siera Lione, Liberia ...Na Juzi umeripotiwa Kuingia Nigeria......na Mpaka Sasa watu takribani 1750 wameripotiwa kuathirika na Ugonjwa huu.
SASA TUJIFUNZE KIDOGO

Ebola Ni Nini?

Ebola ni ugonjwa wa Mlipuko ambao virusi vyake hushambulia mfumo wa Damu wa Binadamu. Kwa Lugha ya Kisayansi Ebola huitwa haemorraghic fever, Ugonjwa huu hupelekea Muathirika kuvuja damu sehemu karibu sehemu yoyote ile ya mwili wake na hatimaye kusababisha kifo kutokana na muathirika huyo kupoteza damu nyingi. Na Kuvuja Damu huko kunaweza kuwa ni ndani ya Mwili au Nje ya Mwili.

Dalili za Ugonjwa Wa Ebola huanza kuonekana siku mbili hadi wiki tatu mara baada ya mtu kuambukizwa virusi hivyo na Kupelekea Homa, Muscle kuuma pamoja na Kichwa Kuuma huku dalili zingine zikiwa ni Kutapika, kuharisha kukifuatiwa sambasamba na Kupungua kwa ufanyaji kazi wa Ini na Figo katika Mwili wa Binadamu.

Virusi Vya Ebola vinaweza kupatikana kwa kugusa damu au majimaji kwenye mizoga ya Wanyama hususani Nyani na Popo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MABWENI YA SHULE YA SEKONDARI YA MIVUMONI ILIYOPO KWENYE MSIKITI WA MTAMBANI KINONDONI YATEKETEA KWA MOTO

 Moto Mkubwa ukiendelea kuwaka katika eneo la juu la Jengo la Shule ya Sekondari ya Kiislam ya Mivumoni (Mivumoni Islamic Seminary) iliyopo ndani ya Msikiti wa Mtambani,Kinondoni B Jijini Dar es Salaam leo.

 Moto mkubwa ukiendelea kuwaka kwenye eneo hilo.
 Ulinzi mkali wa Polisi ulitawala katika eneo la Msikiti huo wa Mtambani kuhakikisha Usalama unakuwepo kwenye eneo hilo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BIASHARA MPYA, KONDOM ZAAGIZWA KWA SIMU, ZINALETWA MAHALI ULIPO, SIKILIZA HII...!!!

Huenda uliwahi kupata huduma ya taxi au kuletewa chakula popote ulipo kwa kupiga tu simu, lakini je utanyanyua simu kwa kutaka huduma ya condom?
Kundi la wafamasia nchini Uganda wameibuka na ubunifu wa kipekee wa kupata huduma ya condomu kwa kupiga tu simu.
Huduma hiyo inaitwa DIAL A CONDOM...yaani unapiga simu tu na kuaguza Condom.
Na hutoa nambari za simu ambazo wateja huweza kupiga, kwa ahadi kuwa watapelekewa aina yoyote ya condom katika kipindi cha dakika 15 au chini ya hapo.
Muliro Telewa anaelezea zaidi kuhusu huduma hiyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

AFANDE SELE AFIWA NA MAMA TUNDA....!!!



Msanii kutoka Morogoro Selemani Mshindi maarufu kwa jina la Afande Sele kupitia ukurasa wa facebook ametoa taarifa ya kufiwa na mzazi mwenzake mama Tunda. Afande Sele ameandika;-

“Ndugu zangu!! Nimefiwa na mzazi mwenzangu (Asha) /mama wa wanangu (mama Tunda) ..ni pigo kubwa kwangu na wanangu. SISI NI WAJA WA MWENYEZI MUNGU NA HAKIKA KWAKE TUTAREJEA; MUNGU AMPUMZISHE PEMA." Jambo Tz tunatoa pole kwa Afande Sele na famila kwa ujumla kwa kuondokewa na kipenzi chao.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS AGOSTI 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HIZI NDIZO HATUA ZAIDI ZA KUZIA KUSAMBAA KWA EBOLA

Jitihada zaidi zafanywa kupambana na Ebola
Jitihada zinaendelea kuzuia kusambaa kwa maradhi ya Ebola, Afrika Magharibi.Tangu mwezi Machi kirusi hicho kimeua zaidi ya watu elfu moja, wengi wao kutoka Sierra Leone, Liberia na Guinea.
Nigeria nayo imetangaza kuwepo kwa mtu wa tatu aliyekuwa na ugonjwa huo. Wakati huohuo, Shirika la Afya Dunia limeielezea Kenya kuwa katika hatari kwani kuna uwezekano mkubwa wa kusambaa kwa virusi hivyo kutokana na kuwepo safari nyingi za ndege kutoka nchi hiyo kuelekea Afrika magharibi.

Huko nchini Nigeria ambako tayari Ebola imesababisha vifo vitatu, serikali imewataka watu wote kushirikiana na wataalamu wa afya hasa baada ya kuwapo kwa taarifa ya muuguzi aliyetoroka hosipitalini baada ya kuwekwa chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya kufuatia kuhofiwa kuwa ameathirika na Ebola. Muuguzi huyo ameelekea nyumbani kwake huko mashariki mwa Nigeria hali inayowatia hatarini watu wengi.

Hivi sasa kiasi kidogo cha dawa za majaribio kimefika nchini Liberia kuwatibu madaktari wawili. Maabara iliyotoa dawa hiyo huko marekani inasema imeishiwa kabisa dawa hizo.
Siku moja tu baada ya shirika la afya duniani kutoa ruhusa ya kutumiwa dawa hizo Canada nayo imetangaza kuwa itatuma dozi 1000 za chanjo kwenda afrika magharibi ambako wahudumu wa afya ndio watakaopewa dawa hiyo ingawa haijawahi kufanyiwa majaribio.

Huko Sierra Leone daktari bingwa mwingine amefariki kwa ugonjwa wa ebola. Modupeh Cole amekuwa akifanya kazi mjini Freetown na kifo chake kinakuja baada ya mtaalamu pekee wa virusi nchini humo kufariki wiki mbili tu zilizopita. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI KUTUMIA NJIA MBADALA IRAQ

Marekani kutumia njia mbadala kuokoa Wayazidi
Marekani sasa imesema inafikiria kutumia njia mbadala za kuwaokoa maelfu ya Wayazidi, wananchi wa Iraq waliokwama katika mlima kaskazini mwa Iraq wakikimbia kushambuliwa na wapiganaji wa dola ya
Kiislamu.
Ikulu ya Marekani imerudia kauli yake kuwa haitatumia majeshi ya ardhini kupambana na wapiganaji hao wa dola ya kiislam lakini ikasema inaweza kuwatumia katika kutoa msaada wa kibinadamu.
Msemaji wa Ikulu ya marekani Ben Rhodes amesema Serikali yake ilikuwa ikijadili wazo la Ufaransa, Australia na Canada nao kutoa msaada wa kibinadamu.
Kwa upande wa Uingereza Waziri Mkuu David Cameron amesema mipango thabiti ilikuwa ikiwekwa sawa kwa ajili jumuia ya kimataifa kuwaokoa Yazidi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, August 13, 2014

UKAWA WAANZA VITA UPYAAA...!!!



Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Freeman Mbowe  akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.  Wanaomfuatia ni wenyeviti wenza wa umoja huo James Mbatia (katikati) na Profesa Ibrahimu Lipumba.


Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umemtaka Rais Jakaya Kikwete kusitisha Bunge Maalumu la Katiba linaloendelea mjini Dodoma na iwapo hatafanya hivyo utaongoza maandamano nchi nzima.

Umoja huo pia umeeleza kuwa kuendelea kwa Bunge hilo ni sawa na kuvuruga mchakato wa kupata Katiba Mpya, kuiweka nchi rehani, kufuja fedha za walipakodi, kuwahadaa Watanzania kwa kupitisha Katiba isiyotokana na maoni yao, huku kanuni zikibadilishwa na kuingizwa mambo ya Tanganyika katika Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Kadhalika, umemtaka Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalumu wa matumizi ya fedha za Bunge hilo kwa maelezo kuwa zinatumika bila maelezo sahihi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


..
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RONALDO AIONGOZA MADRID KUICHAPA SEVILLE MABAO 2-0 NA KUTWAA UBINGWA WA SUPER CUP.

Capture
Cristiano Ronaldo amefunga mabao yote mawili yaliyoipa ushindi wa mabao 2-0 timu yake ya Real Madrid dhidi ya FC Seville kwenye mchezo wa UEFA Super Cup ulipigwa nyumbani kwa Gareth Bale Mjini Cardiff kwenye dimba la Millenium.
Nyota huyo wa zamani wa Manchester United alifunga mabao hayo mbele ya mashabiki 33,500 na kuipa Real ubingwa huo kwa mara nyingine tangu mwaka 2002.mchezo huo pia ulihudhuliwa na kocha wa zamani wa Man Utd Sir Alex Ferguson
Real Madrid kwenye mchezo huo iliwatumia nyota wake iliowasajili msimu huu kiungo mjerumani Toni Kroos pamoja na mshambuliaji raia wa Argentina James Rodriguez.
Nahodha wa timu hiyo Iker Casillas alikaa milingotini siku moja tu baada ya aliyekuwa mpinzani wake msimu uliopita Diego Lopez kujiunga na AC Milan ya Italia.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, August 12, 2014

MJUMBE WA BUNGE LA KATIBA APIGWA, ALAZWA...!!!




Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kutoka Kundi la 201, Thomas Mgoli akiwa amelazwa katika Hospital ya Mkoa wa Dodoma, jana.

Dodoma. Mjumbe wa Bunge la Katiba, kutoka Kundi la 201, Thomas Mgoli amelazwa katika Hospitali ya Dodoma baada ya kupigwa na watu aliodai kuwa ni wafuasi wa Chadema.

Mjumbe huyo alidai kuwa kati ya watu waliompiga yumo mtumishi wa Bunge na ameshamshtaki kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta huku akisema akimuona anaweza kumtambua.

Mgoli ambaye anatokea Chama cha Alliance Democratic Change (ADC), alisema kuwa alipokea kipigo kikubwa juzi katika maeneo ya Area A karibu na Shule ya Msingi Chamwino A.

Akiwa katika wodi ya daraja la kwanza hospitalini hapo, alieleza kuwa chanzo cha mapigano hayo ni mabishano waliyokuwa nayo na vijana wanne mmoja aliyemtaja kwa jina la Vampaya. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UCHAWI WASHIKA KASI, ALBINO WAANGAMIA


Vifaa vinavyodaiwa kuwa ni vya kishirikina

Jana tulichapisha habari za kusikitisha kutoka wilayani Urambo, mkoani Tabora kuhusu Pendo Sengerema, msichana wa miaka 15 mwenye ulemavu wa ngozi (albino), ambaye watu wenye imani za kishirikina wamemkata mkono wa kulia na kuondoka nao.

Huu ni uthibitisho kwamba Watanzania wenzetu wenye ulemavu wa ngozi wanaendelea kupoteza maisha au kupata vilema vya kudumu kutokana na sehemu ya jamii yetu kukumbwa na imani potofu za kishirikina kwamba viungo vya watu hao vinaleta utajiri mkubwa na wa haraka.

Hatuna maneno stahiki ya kuelezea tukio hilo, isipokuwa tu kusema kwamba linasikitisha na kufadhaisha.

Kama msichana mdogo hivyo anaweza kufanyiwa ukatili wa kiwango kikubwa kiasi cha kupoteza kiungo muhimu kama mkono, ambao ungekuwa tegemeo kubwa kwake katika kufanya shughuli za kumwezesha kujitegemea kimaisha, basi tukubaliane kwamba ushirikina umeigeuza jamii yetu kuwa sawa na jamii ya wanyamapori.

Ni imani hizo potofu ambazo zimeikumba jamii yetu tangu mwaka 2000 wakati nchi yetu ilipoanza kushuhudia mauaji ya kinyama dhidi ya ndugu zetu hao wenye ulemavu wa ngozi.

Miaka 14 imepita sasa na vitendo hivyo vinaendelea. Bahati mbaya Serikali imeshindwa kuonyesha dhamira ya kutokomeza uovu huo, bali imebakia kutoa machozi ya mamba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HIKI NDICHO KIOJA ALICHOZUA MTUHUMIWA MAHAKAMANI


Rwanda imekuwa ikiendedesha harakati za upatanishi na pia kuwakumbuka waliokufa katika mauaji hayo
Mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Emmanuel Mbarushimana amekataa uendeshwaji wa kesi yake na mahakama ya Kigali kwa kutoa pingamizi kwamba hana haki zilizo sawa na mwendesha mashitaka.
Mshukiwa huyo alikabidhiwa Rwanda na nchi ya Denmark mapema mwezi wa saba mwaka huu ili kujibu mashitaka ya kuhusika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.
Mushukiwa huyo Bwana Emmanuel Mbarushimana amesema kesi yake haiwezi kusikizwa hadi pale atakapopata haki zilizo sawa na mwendesha mashitaka. Hoja yake ilikuwa kwamba ni lazima na yeye aruhusiwe kukaa badala ya kusimama wakati kesi yake ikisikilizwa na wakati huo huo mwendesha mashitaka asimame badala ya kukaa kama ilivyozoeleka.
Aidha, amesema kuwa hajafurahia utaratibu unaotumiwa wa kuingia katika chumba cha mahakama ambapo mwendesha mashitaka na majaji wanaingia kwa kutumia mlango mmoja kinyume na mushitakiwa. 
Mwendesha mashitaka amemshitaki kwa kushiriki katika mauaji dhidi ya watutsi yaliyotokea katika maeneo mbali mbali katika mkoa wa zamani wa Butare kusini mwa Rwanda. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKUU WA POLISI LIBYA AUAWA


Kanali Muhammad Suwaysi aliteuliwa kama mkuu wa polisi mjini Tripoli mwaka 2012
Mkuu wa polisi katika mji mkuu wa Libya Tripoli, ameuawa na watu wasiojulikana.
Kanali Muhammad Suwaysi alipigwa risasi, alipokuwa anaondoka kwenye mkutano katika eneo la Tajoura , mtaa ulio mashariki mwa mji mkuu Tripoli.
Wenzake wawili walitekwa nyara kwa mujibu wa taarifa za wizara ya ndani.
Libya imekumbwa na vurugu zinazosemekana kusababishwa na wapiganaji wa kiisilamu, ambao walisababisha harakati za kumuondoa mamlakani Muammar Gaddafi mwaka 2011.
Maelfu ya watu wamelazimika kutoroka Tripoli. Zaidi ya miaka mitatu baada ya kuondolewa mamlakani kwa Gadaffi, jeshi la polisi nchini Libya linasemekana kuwa dhaifu,
ikilinganishwa na wapiganaji wanaodhibiti sehemu kubwa za nchi hiyo.

Wapiganaji wa kiisilamu ambao wamekuwa wakizua vurugu nchini Libya
Afisa huyo aliuawa wakati alipokuwa anatoka katika mkutano na maafisa wa mtaa wa Tajoura. Maafisa wengine wawili waliokuwa naye, walitii masharti ya washambuliaji na kuondoka kwenye gari lao huku wakitekwa nyara.
Mamia ya watu wamefariki katika miezi ya Julai na Agosti katika kile kinachoonekana kuwa kukithiri kwa vurugu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ANGALIA PICHA ZA MELI ALIYOKODI TAJIRI BILL GATES KWA TSHS BILLION 8 KWA WIKI...!!!

article-2719109-2057AB6700000578-788_634x422 Katika meli hiyo helikopta zinamchukua Gates kumpeleke nchi kavu kucheza golf na kumrudisha Ni tajiri namba moja duniani mwenye utajiri unaofikia dola bilioni 79.2 hivyo kutumia shilingi bilioni nane kwa wiki si kitu kinachoweza kumpunguzia chochote Bill Gates. Na ndio maana Bill Gates yupo mapumzikoni ambayo tunategemea kwa mtu tajiri zaidi duniani ayafanye. 
article-2719109-2057BE7A00000578-683_634x422 

Tajiri huyo amekodi meli binafsi maarufu yacht ambayo analipa dola milioni 5 (zaidi ya shilingi bilioni 8) kwa wiki.  Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...