Wednesday, June 18, 2014

MBASHA APANDISHWA KIZIMBANI KWA UBAKAJI

Mwimbaji wa nyimbo za Injili na mfanyabiashara, Emmanuel Mbasha. PICHA|MAKTABA 

Mwimbaji wa nyimbo za Injili na mfanyabiashara, Emmanuel Mbasha amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa mashtaka ya ubakaji. Mbasha ambaye pia ni mume mwa mwimbaji maarufu wa Injili nchini, Flora Mbasha alipandishwa kizimbani jana na kusomewa mashtaka mawili ya ubakaji.
Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda makosa hayo kwa nyakati tofauti kati ya Mei 23 na 25, mwaka huu, eneo la Tabata Kimanga, Ilala, Dar es Salaam.Wakili Katuga alidai kuwa katika tarehe hizo, mshtakiwa alimbaka mtoto (jina linahifadhiwa), mwenye umri wa miaka 17, kinyume cha sheria.
Hata hivyo, Wakili Katuga alisema upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika. Ingawa dhamana ya mshtakiwa huyo ilikuwa wazi, aliswekwa mahabusu, baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo yalikuwa kuwa na wadhamini wawili, mmoja akiwa ni mfanyakazi wa taasisi inayotambulika, ambao watasaini hati ya dhamana ya Sh5 milioni kila mmoja.
Hakimu Wilberforce Luhwago anayesikiliza kesi hiyo aliiahirisha hadi kesho itakapotajwa kwa ajili ya kuangalia iwapo mshtakiwa amekamilisha masharti ya dhamana. Mbasha alifikishwa mahakamani hapo asubuhi akiwa amevaa shati jekundu la mikono mirefu, suruali ya rangi ya udongo na kandambili nyekundu.
Mahakamani hapo alikuwa ameambatana na wanaume wawili. Wakati akisubiri kupelekwa mahabusu, saa 7:35, watu hao aliokuwa ameambatana nao walikwenda kumnunulia chakula na maji kabla ya kuongozwa na polisi kwenda kupanda basi la Magereza kuungana na mahabusu kuelekea Gereza la Keko saa 7:05. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAKUU WA POLISI WAFUTWA KAZI NCHINI KENYA

Inspekta wa polisi Kenya, David Kimaiyo
Idara ya polisi nchini Kenya imefanya mabadiliko ya dharura katika afisi kuu za Kaunti ya Lamu, kutokana na mashambulio yaliyosababisha vifo vya watu 60 wiki hii. Inspekta mkuu wa polisi nchini Kenya David Kimaiyo amechapisha katika mtandao wa jamii Twitter, maelezo ya wakuu wa polisi katika kaunti hiyo waliofutwa kazi mara moja, wakiwemo makamanda wa polisi.
Afisa mkuu wa kituo cha Polisi, OCS, pia amehamishwa kituo mara moja. Hatua hii tayari imepokewa kwa hisia tofauti huku wakenya wengi wakielezea kutoridhishwa na adhabu hiyo.
Miongoni mwa walioandika malalamiko yao kwa Bwana Kimaiyo, wamesema kuwa mabadiliko yalistahili kufanyika hadi ngazi ya juu zaidi, baadhi hata wakimtaka yeye mwenyewe kama Inspekta wa polisi kujiuzulu.
Tangu kutokea shambulio la Jumapili usiku katika kijiji cha Mpeketoni, karibu na kisiwa cha Lamu pwani ya Kenya, lawama zimeelekezwa kila upande, huku baadhi wakidai kuwa wanasiasa wamehusika na wengine wakilalamikia utepetevu wa polisi katika kutekeleza majukumu yao.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alihutubia taifa Jumanne akisisitiza kuwa ana imani kuwa mashambulio hayo yalichochewa kisiasa. Ametoa matamshi hayo licha ya taarifa kutoka kwa kundi la wapiganaji wa kiislamu wa AL shabaab waliodai kuwa wao ndio waliohusika.
Matamshi ya rais Kenyatta yame kejeliwa na wanasiasa wa upinzani nchini humo waliodai kuwa rais huyo hana ufahamu wa yale yanayoendelea nchini mwake.

Seneta kutoka chama kikuu cha upinzani, Moses Wetangula amesema matamshi ya rais sio ya kweli. '' Badala ya kuitisha usaidizi wa wenzetu wenye teknolojia bora, hata tutumie ndege zisizo na rubani kuwalipua huko waliko, tunakaa hapa Nairobi na kudai AL shabaab hawakuhusika.'' Wetangula aliambia bunge la Kenya. '' Huu ni mzaha,'' Aliongeza bwana Wetangula.
Lakini uchunguzi uliofanywa na BBC umeonesha kuwa huenda kuna uzito kwa madai ya rais Kenyatta. Wakaazi wengi wa Mpeketoni waliozungumza na BBC wametueleza kuwa, wanaamini shambulio la Jumapili usiku linatokana na mzozo wa ardhi kati ya jamii zinazoishi huko. Wakaazi hao wamesema kuwa Al shabaab wamedakia tu kujigamba kwa yaliotokea huko ila wao wanaamini kuwa ni jambo lililokuwa likitokota kwa muda mrefu.
polisi waimarisha usalama
Huku hayo yakiarifiwa, polisi wanasemekana kuimarisha doria katika eneo la Lamu na vitongoji vyake. Wanajeshi wachache wametumika kuimarisha usalama hasa katika kijiji cha Mpeketoni. Katika taarifa zilizotufikia ni kuwa Polisi wameimarisha usalama katika mkoa wa magharibi mwa Kenya kutokana na duru walizopokea kuwa huenda eneo hilo likalengwa kwa shambulio.
Al shabaab wamefanya mashambulio ya mara kwa mara katika sehemu mbali mbali nchini Kenya tangu majeshi ya Kenya yaingie nchini Somalia mwaka wa 2011, katika oparesheni ya kuwafagia kutoka nchini humo. Shambulio la punde zaidi linadaiwa kufanywa kama kulipiza kisasi ya kuuawa kwa masheikh 2 wa kiislamu katika mji wa Mombasa pwani ya Kenya hivi majuzi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DAKIKA 90 ZA MECHI ZA KOMBE LA DUNIA ZA JUNI 17

Kwenye mechi zilizochezwa usiku wa June 17 2014 matokeo yake ni Russia 1 (Kerzhakov 74′ ) – 1 Korea Republic goli lao lilifungwa na K Lee kwenye dakika ya 68.
Game nyingine ilikua ya Brazil vs Mexico iliyoisha kwa 0-0 huku ile ya nyingine ya mwanzo ikiwa ni Belgium 2 ( Fellaini 70′ + Mertens 80′) – 1 Algeria (Feghouli aliefunga kwa penati dakika ya 25 ) Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MASHABIKI WA SOKA WALIPULIWA

Mlipuko watokea Yobe watu wakitizama kombe la dunia
Shambulio limetokea katika jimbo la Yobe nchini Nigeria wakati watu wakitazama mechi za kombe la dunia. Jimbo hilo limewekwa katika hali ya hatari huku maafisa wa usalama wakijaribu kukabiliana na mashambulio yanayofanywa na wanamgambo wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Wakaazi wanasema walisikia sauti ya mlipuko mkubwa nje ya eneo la kutazama sinema mjini Damaturu ambapo mashabiki wa soka walikua wamejumuika kutazama mechi za kombe la dunia. Walioshuhudia wanasema mshambuliaji wa kujitolea mhanga aliyekuwa amebebwa kwa baiskeli alijilipua karibu na mgahawa katika jimbo la Yobe wakati mechi kati ya Brazil na Mexico ikiendelea.
Yobe imekumbwa na mashambulizi ya Boko Haram katika miaka iliyopita.
Duru kutoka hospitalini zinasema malori kadhaa yamewasafirisha majeruhi kupata matibabu na polisi wanasema maafisa wamepelekwa katika eneo hilo. Mfanyikazi mmoja wa hospitali ameaimbia BBC kuwa waliopelekwa hapo wana majeraha mabaya huku baadhi yao wakipoteza miguu na mikono.

Wiki iliyopita maafisa wa utawala katika jimbo la Adamawa ambalo liko katika eneo hilo la Kaskazini mwa Nigeria walipiga marufuku watu kujumuika katika maeneo ya umma kutazama mechi za kombe la dunia kutokana na hofu ya Usalama. Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya shambulio kutokea katika eneo la burudani na kusababisha mauaji ya watu kadhaa.

Majimbo ya Borno, Yobe na Adamawa yako katika hali ya tahadhari kuanzia mwezi Mwezi 2013 kufuatia mashambulizi ya kila mara ya wapiganaji wa kundi la kiislamu la Boko Haram. Takriban watu 2,000 wamepoteza maisha yao yangu visa vya uasi kuanza kutekelezwa mwaka wa 2009. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, June 17, 2014

CHENGE: "SERIKALI IMEKOSA UBUNIFU"


Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge. PICHA|MAKTABA 

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge amesema Serikali imekosa ubunifu na haitaki kupokea ushauri kuhusiana na vyanzo vipya vya mapato ya uchumi kwa mwaka 2013, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2014/15 pamoja na utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka 2013/14, Chenge alisema kuongeza ushuru katika bia, soda, juisi na vinywaji vikali, kumepitwa na wakati.

Wakati Chenge akieleza hayo, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imetaja vyanzo mbadala vya mapato vinavyofikia Sh6 trilioni. Katika taarifa yake, Chenge alisema mpaka mwisho wa mwaka wa fedha 2013/14, Bajeti ilikuwa pungufu kwa Sh2 trilioni, huku Bajeti ya mwaka 2014/15 ikiongezeka kwa asilimia 8.8 (trilioni 1.6), huku ikiwa na deni la Sh1.3 trilioni ambalo halikuingizwa katika Bajeti ya mwaka 2014/15.
“Hali hii inaweza kutafsiriwa kuwa Bajeti ya mwaka 2014/15 tayari ina pengo la Sh4.9 trilioni. Yaani Sh2 trilioni ambazo hazikupatikana mwaka wa fedha 2013/14 na Sh1.6 trilioni ambayo imeongezeka ikilinganishwa na bajeti ya mwaka jana na deni la Sh1.3 trilioni.
“Kuna umuhimu wa kuharakishwa kuletwa bungeni sheria ya bajeti itakayofanya kazi sambamba na sheria mpya ya ununuzi ili kudhibiti matumizi mabaya kwa nia ya kuweka nidhamu katika utekelezaji wa bajeti ya Serikali,” alisema Chenge. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MWANAMUZIKI APASULIWA HUKU AKIIMBA...!!!

Alama Kante afanyiwa upasuaji
Katika tukio la kwanza la aina yake mwanamziki mmoja nchini Ufarasa amefanyiwa upasuaji kuondoa uvimbe kooni huku akiimba. Madaktari wanasema hatua hiyo ilichukuliwa ili kuepuka kuharibu mishipa inayosaidia binadamu kutoa sauti.

Mwimbaji huyo Alama Kante, ambaye ni raia wa Guinea anayeishi Ufaransa alipewa dawa za kumfanya asihisi uchungu wakati upasuaji huo ukiendelea. Kante alikua na hofu kuhusu kupoteza sauti yake kutokana na upasuaji huo lakini daktari wake akapendekeza aimbe huku akipasuliwa ikiwa ni mara ya kwanza hatua kama hiyo kuwahi kuchukuliwa kote duniani.

Profesa Giles Dhonneur, aliyeongoza upasuaji huo katika hospitali ya Henri Mondor hospital, ameonyesha video ya mwanamziki huyo akiimba huku naye akiendelea na upasuaji. Ameelezea matuamani kuwa mambo yatakuwa sawa.
Amesema ni uchungu sana kufanya upasuaji kama huo bila kutumia dawa ya kumfanya mgonjwa asihisi uchungu lakini mbinu na dawa aliyotumia ilimuwezesha Kante kuhimili bila matatizo yoyote. 
Kante ambaye amepata nafuu amesema wakati upasuaji ukiendelea alihisi kama yuko Senegal na alipoamka na kuzungumza tena madkatari na wauguzi walifurahi sana kutimiza lengo lao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI KUTUMA MAJESHI IRAQ

majeshi ya marekani Iraq

Marekani imetangaza kuwa inatuma wanajeshi 275 nchini Iraq kusaidia kulinda maafisa na Ubalozi wake mjini Bagdad. Tangazo hilo limetolewa wakati maafisa wa Marekani na Iran wakifanya mazungumzo kuhusu hali nchini Iraq katika kongamano linalojadili maswala ya nyuklia mjini Viena.

Rais Obama ameandika barua kwa baraza la Congress kueleza mipango ya kutuma wanajeshi hao 275 mjini Baghdad. Anasema jukumu la kikosi hicho ambacho kitakabidhiwa silaha ni kulinda raia wa Marekani wanaoishi nchini Iraq na mali yao. Wanajeshi hao wataendelea kukaa nchini humo hadi hali ya usalama itakapoimarika.

Hatahivyo hakuna ishara yoyote ya hali kuimarika huku kundi la wapiganaji la ISIS likiendeleza harakati zake katika baadhi ya maeneo ya Iraq. Rais Obama ambaye anaonekana kutafakari kuhusu hatua ambazo Marekani inaweza kuchukua, anashauriwa na maafisa kutoka kitengo cha usalama wa kitaifa. Kwingineko maafisa wa Marekani wamethibitisha kuwa wamefanya mazungumzo mafupi na maafisa kutoka Iran kuhusu hali nchini Iraq.

Awali waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry alisema yuko tayari kushauriana na Iran ambayo wakati mmoja ilikua hasimu wa Marekani. Hatahivyo maafisa wa Marekani wametupilia mbali uwezekano wa ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Chanzo BBC

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HIVI NDIVYO RADIO COUNTRY FM ILIVYO ADHIMISHA SIKU YA MTOTO AFRIKA

Wafanyakazi wa radio country fm wakiwa katika picha ya pamoja walipotembelea kitu cha watoto wenye ulemavu wa viungo cha SAMBAMBA kilichopo Kitwiru
Kaimu meneja wa Radio Country fm Chiku Mbilinyi akimkabidhi diwani wa kati ya kitwiru zawadi kwa ajiri ya watoto wenye ulemavu
kaimu meneja wa radio country fm CHIKU akimkabidhi mratibu wa kituo hicho zawadi kwa ajiri ya watoto wenye ulemavu
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS KIKWETE ATETA NA WASANII DODOMA

D92A1853Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisistiza jambo wakati akizungumza na msanii wa kizazi kipya Nasib Abdul “Diamond” ikulu ndogo mjini Dodoma wakati chakula cha usiku alichowaandalia wasanii walioshiriki katika tamasha la Uzalendo na Uzinduzi wa Video ya wimbo maalum wa miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma jumamosi.Kulia ni mbunge wa Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete.D92A1860Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na msanii wa kizazi kipya Nasib Abdul “Diamond” ikulu ndogo mjini Dodoma wakati chakula cha usiku alichowaandalia wasanii walioshiriki katika tamasha la Uzalendo na Uzinduzi wa Video ya wimbo maalum wa miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma jumamosi.Kulia ni mbunge wa Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete.D92A1891Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza kwa makini mwanamuziki wa kizazi kipya Ommy Dimpoz wakati chakula cha usiku alichowaandalia wasanii walioshiriki katika tamasha la Uzalendo na Uzinduzi wa Video ya wimbo maalum wa miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma jumamosi iliyopita kulia ni Mh. Ridhiwani Kikwete Mbunge wa jimbo la Chalinze(picha na Freddy Maro). Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...