Monday, May 19, 2014

TAHADHARI USALAMA WAKO UKIWA KENYA

Kenya imekabiliwa na mashambulio kadhaa hivi karibuni
Tahadhari zaidi zimetolewa nchini Kenya za kutokea mashambulio katika baadhi ya maeneo ya umma na foleni za barabarani.
Mitandao ya kijamii ya twitter na face book imetumiwa kusambaza ujumbe miongoni mwa wananchi kutoa tahadhari hiyo.
Usalama umeimarishwa katika Ubalozi wa Marekani Kenya na ofisi za Umoja wa mataifa Nairobi, na hatua madhubuti zimechukuliwa kupunguza msongamano wa watu katika maeneo hayo.
Na huku hayo yakiarifiwa sekta ya utalii nchini humo imeendelea kupata hasara kubwa kutokana na kuondolewa kwa raia wa kigeni hasa Uingereza waliokuwa katika mji wa kitalii wa Mombasa kufuatia tishio la kulengwa katika shambulio.
Afisa Mkuu wa Shirika la kampuni linaloshughulikia utalii nchini, Kenya Tourism Federation, Agatha Juma anasema upungufu wa watalii nchini Kenya utasababisha ukosefu wa ajira, zaidi kwa raia wa Kenya wanaofanya katika hoteli mbali mbali nchini.
Kenya imeshuhudia mashambulio kadhaa katika siku za hivi karibuni katika maeneo mbali mbali nchini ukiwemo mji wa Mombasa na Nairobi, yaliosababisha vifo vya watu kadhaa na wengine wengi kujeruhiwa.Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

Sunday, May 18, 2014

MBWANA SAMATA NA THOMAS ULIMWENGU WAJIUNGA TAIFA STARS KIKABILI ZIMBABWE LEO

Samata 
Na Boniface Wambura, Dar es  salaam
Wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wametua Dar es Salaam jana (Mei 17 mwaka huu) mchana, na kujiunga moja kwa moja kwenye kambi ya Taifa Stars kwa ajili ya michuano ya Afrika dhidi ya Zimbabwe (Mighty Warriors).
Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza ya michuano hiyo itafanyika leo (Mei 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
Washambuliaji hao wa Taifa Stars wamewasili saa 7.25 mchana kwa ndege ya Ethiopian Airlines wakitokea Khartoum, Sudan ambapo juzi (Mei 16 mwaka huu) timu yao ya TP Mazembe ilicheza mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Hilal ya huko.
Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij amesema kikosi chake kipo tayari kwa ajili ya mechi hiyo, kwani kimepata mechi za kirafiki na mazoezi ya kutosha kwenye kambi iliyoanzia Tukuyu mkoani Mbeya ambapo kulikuwa na utulivu mkubwa.
Naye Kocha Msaidizi wa Zimbabwe, Kalisto Pasuwa amesema hawaifahamu vizuri Taifa Stars lakini wamekuja kwenye mechi hiyo itakayoanza saa 10 jioni kwa ajili ya kushinda, na kuwataka mashabiki wajitokeze kwa wingi kuona kiwango cha timu yake.
Milango kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Ghana wakiongozwa na Joseph Odartei Lamptey itakuwa wazi kuanzia saa 6 kamili mchana, na tiketi zitapatikana katika magari maalumu uwanjani hapo.
Viingilio katika mechi hiyo ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, kijani na bluu, sh. 10,000 kwa VIP C na B, na sh. 20,000 kwa VIP A. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 18, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAIA WA UCHINA WAJERUHIWA VIETNAM

Shirika rasmi la habari nchini Uchina Xhinua limesema kuwa serikali imewaondoa zaidi ya raia wake 3000 kutoka nchini Vietnam kufuatia ghasia dhidi raia wa Uchina nchini humo.
Wafanyikazi wawili wa Uchina wameuawa kufuatia ghasia hizo zilizosababishwa na hatua ya Uchina kupeleka meli yake ya kuchimba mafuta katika eneo linalozozaniwa kusini mwa bahari ya Uchina.
Mapema hii leo takriban raia 16 wa Uchina waliojeruhiwa vibaya waliondoshwa nchini humo kupitia usafiri wa ndege maalum.
Serikali mjini Beijing inaandaa safari nyingine za ndege huku naibu waziri wa maswala ya kigeni Liu Jianchao akizuru Vietnam kwa mazungunmzo na mamlaka.
Aidha waziri huyo amewatembelea baadhi ya raia wa Uchina waliojeruhiwa hospitalini.
Wanaharakati nchini Vietnam wameitisha maandamano zaidi dhidi ya raia wa Uchina hii leo licha ya mwito wa serikali wa kutaka kusitishwa kwa maandamano hayo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC Swahili

WATU 70 WAUAWA KATIKA VITA NCHINI LIBYA

Mwanamgambo nchini Libya
Maafisa nchini Libya wanasema kuwa idadi ya watu waliofariki katika vita mjini Benghazi imeongezeka na kufikia zaidi ya 70.
Jeshi limetangaza kwamba hakuna ndege itakayoruhusiwa kupaa juu ya mji huo huku spika wa bunge akisema kuwa mtu anayeongoza vita hivyo Khalifa Haftar anajaribu kufanya mapinduzi.
Bwana Haftar amesema kuwa ataendelea na kampeni yake ya kuwaondoa wale aliowataja kama magaidi nje ya mji wa Benghazi huku akiongezea kuwa anaungwa mkono na raia wengi wa mji huo ambao ni wa pili kwa ukubwa nchini Libya.
Hatahivyo familia nyingi zinahamia magharibi mwa mji huo kufuatia vita vikali kati ya vikosi vya Haftar na wanamgambo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC Swahili

ARSENA BINGWA KOMBE LA FA

BAO la dakika ya 109 la Aaron Ramsey limeipa Arsenal ubingwa wa Kombe la FA baada ya kuichapa Hull City 3-2 ikitoka nyuma kwa 2-0 Uwanja wa Wembley.
Ramsey alifunga bao hilo akimalizia kazi nzuri ya Olivier Giroud na kuondoa uwezekano wa mchezo huo kuhamia kwenye mikwaju ya penalti.
Arsenal waliuanza kichovu mchezo huo na kujikuta wanafungwa mabao mawili ndani ya dakika nane, Chester akianza kufunga la kwanza dakika ya nne na Davies akafunga la pili dakika ya nane.
article-2630209-1DF2D11300000578-658_964x520
Santi Cazorla aliifungia Arsenal bao la kwanza dakika ya 17 kwa shuti la mpira wa adhabu kabla ya Koscielny kufunga la pili dakika ya 72 na Ramsey la ushindi dakika ya 108.
Ushindi huo ni furaha kwa kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ambaye hajatawaa taji lolote kwa miaka tisa.
Mara ya mwisho Arsenal walitwaa taji mwaka 2005, ambalo lilikuwa Kombe hilo hilo la FA wakiendeleza mafanikio ya msimu wa 2003-2004 walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu na Ngao ya Jamii.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Fabianski, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Arteta, Ramsey, Cazorla/Wilshere dk105, Ozil/Rosicky dk105, Podolski/Sanogo dk61 na Giroud.
Hull: McGregor, Chester, Bruce/McShane dk67, Davies, Elmohamady, Livermore, Huddlestone, Meyler, Rosenior/Boyd dk103, Quinn/Aluko dk74 na Fryatt.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ATLETICO MABINGWA WA LA LIGA

atletico_187be.jpg
Atletico Madrid imenyakua kombe la ligi kuu ya Hispania La liga baada ya kutoka sare ya 1 – 1 dhidi ya Barcelona na hivyo kumaliza ligi ikiwa na pointi 90 huku Barcelona ikishika nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 87.
Real Madrid iliyoshinda mechi yake dhidi ya Espanyol kwa 3 - 1 ikishika nafasi ya tatu kwa kumaliza ligi ikiwa na pointi 87 lakini ikizidiwa na Barcelona kwa tofauti ya goli moja.
Barcelona wana tofauti ya magoli 67 wakati Real Madrid ikiwa na tofauti ya magoli 66.
Katika mechi hiyo ya Barcelona dhidi Atletico Madrid ambayo ilikuwa ni ya kuamua ni timu ipi itanyakua ubigwa wa La Liga msimu huu, Barcelona ndio waliokuwa wa kwanza kuutikisa wavu wa Atletico Madrid kwa goli lililofungwa na Alexis Sanchez katika ya 34 kipindi cha kwanza.
Baadae Atletico Madrid walikuja juu na kuanza kulishambulia goli la Barcelona ambapo Diego Godin katika dakika ya 49 kipindi cha pili aliIsawazishia timu yake kwa goli safi alilolipachikwa wavuni kwa njia ya kichwa na hivyo kufanya mechi hiyo imalizike kwa jumla ya goli 1 - 1 .
Atletico Madrid inakuwa mabingwa wa La Liga tangu baada ya kulikosa kombe hilo tangu mwaka 1996. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Saturday, May 17, 2014

MSANII NA MUONGOZAJI WA FILAMU 'ADAM KUAMBIANA' AMEFARIKI DUNIA GHAFLA ASUBUHI YA LEO...!!!

Adam Kuambiana enzi za uhai wake.
Mwili wa Marehemu Adam Kuambiana ukitolewa nje ya Hospitali  ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuhifadhiwa leo mchana huu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

HOMA YA DENGUE, MABASI 600 KUPULIZIWA DAWA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki

Serikali imeiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kuhakikisha mabasi yote 600 yanayofanya safari zake mikoani yanapulizia dawa ya kuondoa mazalia ya mbu wanaoeneza ugonjwa wa dengue.

Manispaa za Dar es Salaam zimetengewa Sh. milioni 218 kwa ajili ya kununua dawa na vifaa vya kupulizia mazalia ya mbu hao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki alisema kuwa tayari serikali imefanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa ili usienee kwa wengine. Alisema mabasi yatakayokaidi agizo hilo yatafungiwa safari zake lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha ugonjwa huo hausambai katika mikoa mingine.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki alisema kuwa tayari serikali imefanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa ili usienee kwa wengine.

Alisema mabasi yote yanatakiwa kuhakikisha yanapulizia dawa ili yanapoanza safari zake ili yasiondoke na mbu hao katika mikoa mengine. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

FILAMU YA JOTI SANDUKU LA BABU KUINGIA SOKONI HIVI KARIBUNI

Msanii Lucas Mhavile 'Joti'baada ya kukaa kimya kwa mda sasa ameibuka na filamu yake ya Joti Sanduku la Babu ambayo amecheza katika husika tofauti tofauti.
Filamu hiyo itakuwa ikisambazwa na Kampuni yaproin promotions ya jinini Dar es salaam akizungumzia filamu hiyo Joti alisema kuwa amekuja kivingini kwani kitu alichofanya katika filamu hiyo haijawai kutokea wala kufanywa na mtu yoyote yule katika tasinia hii ya filamu nchini hivyo wapenzi wangu wakae mkao wa kula tu kwani wakati wowote kuanzia sasa itakuwa inaingia sokoni kwani filamu hii si yakukosa mana unambiwa uzee mwisho chalinze mjini kila mtu honey hivyo wapenzi wa filamu nawaomba wanunue nakala alisi ya filamu hiyo pindi itakapotoka ambapo nimelezea mambo mbalimbali ya ujana usichana pamoja na uzee mbali na hivyo filamu hiyo imebeba mambo matatu muhimu kwanza ina burudisha pia ina elimisha na kupata ujumbe muhimu kabisa katika jamii inayotuzunguka' filamu hiyo ya kwanza tangu joti aweke kando mambo ya filamu na kujingiza katika mambo ya uchekeshaji kupitia luninga sasa ameludi tena katika filamu yake mwenyewe inayokwenda kwa jina la Joti sanduku la babu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

PROFESA LIPUMBA AWASHANGAA VIJANA WA IRINGA

Baadhi ya vijana waliohudhuria mkutano huo

Lipumba wa CUF akisisitiza jambo

Mchungaji Msigwa wa Chadema
Danda Juju wa NCCR-Mageuzi
 Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

ASKOFU DALLU KUSIMIKWA RASMI KESHO


dalu_1b119.jpg
Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Tanzania Askofu Mkuu Fransisko Montecillo Padilla, anataraji kuongoza Misa Takatifu ya kusimikwa kwake Askofu Mpya wa Jimbo Kuu la Songea, Mhashamu Damian Dennis Dallu (Pichani).

Tukio hilo litafanyika katika Kanisa la Mtakatifu Mathias Mulumba Kalemba la Jimbo Kuu la Songea hapo kesho. Leo hii baadhi ya waumini wamesafiri mpaka katika mpaka wa Mkoa wa Ruvuma na Njombe kwa ajili ya kumpokea Askofu Dallu anayeingia Jimboni Songea na leo Jumamosi atafanyiwa Ibada ya kukabidhiwa Kanisa.

Tukio hilo linalotaraji kuhudhuriwa na Viongozi wengi wa Madhehebu ya dini, litahudhuriwa pia na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Wiliam Mkapa. (PERAMIHO PUBLICATIONS)
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

WATU 10 WAUAWA KATIKA MILIPUKO NAIROBI

Haijulikani na nani aliyesababisha milipuko ingawa washukiwa tayari wamekamatwa
Milipuko miwili ilitikisa Soko kubwa la nguo la Gikomba mjini Nairobi na kuwaua watu 10 huku zaidi ya hamsini wakijeruhiwa..
Soko hilo linapakana na mtaa wa Easleigh ambako wasomali wengi wanaishi na kufanya kazi.
Shirika la serikali la kushughulikia majanga linasema kuwa angalau watu 10 wamefariki na wengine zaidi ya hamsini kujeruhiwa.
Mlipuko wa kwanza ulitokea katika gari la abiria wakati la pili likitokea ndani ya soko.
Soko la Gikomba ni maarufu kwa nguo za mitumba
Milipuko hiyo ilitokea siku moja baada ya Uingereza kutoa onyo kwa raia wake wanaoishi nchini humo kurejea makwao kwa hofu ya usalama na pia baada ya tahadhari kutolewa ya kutokea kwa mashambulizi ya kigaidi nchini humo.
Gikombaa ni soko kubwa la kuuza nguo ambalo linapakana na mtaa wa Eastleigh ambako wasomali wengi wanaishi na kufanya kazi.
Kenya imekuwa ikikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa wawu wenye uhusiano na kundi la wanamgambo la kiisilamu nchini Somalia la Al Shabaab. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC Swahili

USALAMA WA NIGERIA KUANGAZIWA UFARANSA

Kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakr Shekau
Rais wa Ufaransa Francois Hollande anaanda mkutano hii leo mjini Paris kuangazia hali ya usalama nchini Nigeria.
Mkutano huo utawaleta pamoja viongozi kutoka nchi za Nigeria,Benin,Cameroon,Chad na Niger ili kutafuta njia za kukabiliana na kundi la wanamgambo wa kiislamu wa Boko haram.

Wawakilishi wa Marekani muungano wa Ulaya na Uingereza wataangazia kazi iliofanywa na wataalam wa Uingereza, Ufaransa na Marekani waliotumwa nchini humo ili kuisaidia mamlaka ya Nigeria kuwanusuru zaidi ya wasichana 200 waliotekwanyara na kundi hilo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Chanzo: BBC Swahili

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...