Thursday, January 30, 2014

MKUU WA WILAYA AFUNGA KIWANDA CHA SUKARI

miwa e4424
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Antony Mtaka amekifungia kwa muda usiojulika shughuli za uzalishaji, Kiwanada cha Sukari cha Mtibwa mpaka kiwanda hicho kitakapolipa madeni ya wafanyakazi na wakulima wa miwa.
Akitoa msimamo wa Serikali ya wilaya hiyo juu ya kukifungia kiwanda hicho mbele ya wafanyakzi na wakulima hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi za mtendaji wa kata ya Mtibwa wilayani hapa, Mtaka alisema, wamechukua uamuzi huo baada ya mabishano ya muda mrefu baina ya pande mbili kutofikia muafaka.
Mkuu huyo wa wilaya katika mabishano hayo ya muda mrefu juu ya madai ya wakulima na wafanyakazi alisema wanakidai Kiwanda cha Mtibwa zaidi ya Sh1.9 bilioni ambazo ni za mauzo ya miwa na mishahara ya wafanyakazi.
Mtaka alisema shughuli nyingine kiwandani hapo zitaendelea kama huduma ya afya, ulinzi na idara ya fedha ili kuwezesha makundi hayo kupata mafao yao mwishoni mwa wiki hii kama ilivyoahidiwa na uongozi wa kiwanda hicho.
Meneja mkuu Hamad Juma alisema, kiwanda hicho kilikwama kulipa madeni hayo kutokana na uingizwaji mwingi wa sukari nchini uliosababisha wao kukosa soko ingawa waliahidi kuanza kulipa mwezi huu. Chanzo: mwananchi

MAN UNITED YAKATAA MABILIONI KWA JANUZAJ

JANU eb4eb
HATUTAKI, na tena hatutaki hata kusikia. Na ikiwezekana msirudi tena. Ndivyo ambavyo mapovu yamewatoka mdomoni watu wa Manchester United baada ya PSG kurudi mezani juzi Jumapili na ofa ya kumtaka kinda wao mahiri, Adnan Januzaj.
PSG wamekuwa wakitokwa udenda kwa kinda huyo mwenye asili ya Albania aliyezaliwa Ubelgiji miaka 18 iliyopita na hawajali kama aliingia mkataba mpya wa kuichezea Man United mwishoni mwa msimu uliopita.
Hata hivyo, kocha David Moyes amekataa ofa hiyo ya PSG inayodhaniwa kuanzia Pauni 25 milioni na kuendelea huku wakisisitiza kwamba hawana mpango hata wa kukaa chini na kuzungumza na matajiri hao wa mafuta kutoka Paris.
Man United imempatia mkataba mrefu wa miaka mitano Januzaj Oktoba mwaka jana baada ya kugundulika kuwa huenda mchezaji huyo angekuwa huru na kuondoka Mei mwaka huu mara baada ya msimu kumalizika.

RAIS KIKWETE AMPIGA KIJEMBE RAGE

rage1 1d2f4
RAIS Jakaya Kikwete amemshangaa Mwenyekiti wa Simba SC ya jijini Dar es Salaam, Ismail Aden Rage kwa kuitisha mkutano wenye ajenda moja kwa ajili ya wanachama wa klabu hiyo. Wiki iliyopita, Mwenyekiti wa Simba Rage, alitangaza kuwepo kwa mkutano wa klabu hiyo Machi 23 na kueleza wazi kuwa kutakuwa na ajenda moja ya kujadili mapungufu ya Katiba.
Akizungumza mbele ya umati wa watu waliohudhuria mazishi ya Mbunge wa Chalinze, Saidi Bwanamdogo mwishoni mwa wiki iliyopita, Rais Kikwete ambaye alifika katika eneo la makaburi, alimuuliza Mwenyekiti huyo wa Simba kuhusiana na maandalizi ya mkutano huo.
"Ndugu yangu Rage mimi Mwenyekiti mwenzio, lakini sijawahi kuona mkutano wenye ajenda moja ndio kwanza huo wa kwako, yaani wewe kiboko, pamoja na makelele yote lakini umeweza kutuliza hali ya mambo mpaka leo umedumu kuwa mwenyekiti," alisikika Rais Kikwete akisema huku mamia ya waombolezaji wakicheka.
Akizungumzia kauli hiyo ya Rais Kikwete, Rage alisema ili kuwa kiongozi imara ndani ya klabu za Simba na Yanga, inakupasa kuwa na roho ngumu, kwani bila ya kufanya hivyo wanachama watakuwa wakikuchezea kila kukicha.
"Mheshimiwa Rais kuwa kiongozi ndani ya klabu hizi mbili kunahitaji umakini sana, kwani bila ya kufanya hivyo wewe utakuwa ni kiongozi wa kupelekwa kila siku na hatimaye unamaliza muda hakuna ulichokifanya ndani ya uongozi wako," alisema Rage. Chanzo: mtanzania

IKULU YAVUNJA UKIMYA KUHUSU "MAWAZIRI MIZIGO" ...!!!


kawambwa_2846f.jpg
SHUKURU KAWAMBWA
Dar es Salaam. Ikulu imetaka kufungwa kwa mjadala wa kuhusu kurudishwa kwa mawaziri wanaodaiwa kuwa ni mizigo kwenye Baraza la Mawaziri na badala imetaka waachwe wafanye kazi.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema kuendeleza mjadala huo ni kupoteza muda, kwani Rais Jakaya Kikwete alishamaliza kazi yake.

Rweyemamu alisema Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuteua mawaziri ambao wana wajibu wa kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake, hivyo si sahihi wateule hao kuitwa 'mizigo' kwani yeye (Rais) ameona wanafaa.
"Rais anapoteua watu anaangalia wanaofaa kumsaidia na si vinginevyo. Kwani lengo lake ni kuona nchi ina 'move forward' (inasonga mbele) kimaendeleo," alisema Rweyemamu. Alisema watu wanapaswa kukumbuka kuwa mtu anapoteuliwa kwenye uwaziri kuna suala la uwajibikaji: "Anatakiwa kutekeleza uwajibikaji wa pamoja. Sasa kumshambulia mtu binafsi na kumwita mzigo siyo sahihi."

Rweyemamu alisema mjadala huo kwa sasa umepitwa na wakati na kuwataka wananchi na wachambuzi kuwaacha mawaziri hao kuchapa kazi.
"Ni vizuri wananchi wakawapa nafasi mawaziri hawa ya kufanya kazi na baadaye kuwapima na kuwachambua kutokana na utendaji wao," alisema.
Chimbuko la majadala
Mjadala kuhusu suala hilo unatokana na Rais Kikwete kuwarejesha katika Baraza la Mawaziri baadhi ya mawaziri ambao walidaiwa kuwa ni mizigo kutokana na udhaifu katika utendaji wao.

NEC "DAFTARI LA WAPIGA KURA LITABORESHWA"

 
Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva.PICHA|MAKTABA 
**********
Pamoja na kushindwa kutaja tarehe rasmi ya kuanza kuboresha daftari la kudumu la wapigakura, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) imesema daftari hilo litaboreshwa kabla ya kuanza kwa upigaji wa kura ya maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya. Upigaji wa kura hiyo utafanyika ndani ya siku 70 baada ya kumalizika kwa Bunge Maalumu la Katiba linalotarajiwa kuanza katikati ya mwezi ujao mjini Dodoma. Litafanyika kwa kati ya siku 70 na 90.

Nec imetoa ufafanuzi huo baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wananchi kwamba tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, daftari hilo halijawahi kuboreshwa, jambo ambalo litasababisha upigaji wa kura kwa ajili ya kupata Katiba Mpya kutawaliwa na vurugu. Malalamiko hayo yanatokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya watu waliotimiza umri wa kupiga kura lakini hawamo katika daftari hilo.
Pia waliopoteza vitambulisho vya kupigia kura na wenye kasoro mbalimbali zinazowafanya wapoteze sifa.

HAYA HAPA MATOKEO YA MECHI ZA LIGI KUU YA UINGEREZA, USIKU WA JUMATANO

MAGAZETI YA LEO JANUARI 30, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Tuesday, January 28, 2014

"MBWA MWITU" SASA TISHIO KWA WANANCHI WA TABATA DAR


Dar es Salaam. Wakazi wa Tabata na viunga vyake, sasa wanaishi kwa wasiwasi mkubwa kutokana na kuibuka kwa kundi la vijana, wanaojiita Mbwa Mwitu wakitumia silaha za jadi, kujeruhi watu na kupora mali nyakati za usiku.
Mmoja wa wananchi wa Tabata Matumbi alisema wiki mbili zilizopita, vijana hao walimuua mwanamume mmoja kwenye Daraja la Reli la Matumbi. Kwa mujibu wa mtoa habari huyo ambaye hata hivyo hakutaka jina lake litajwe, mtu huyo alichinjwa na kichwa chake kutenganishwa na kiwiliwili.
“Watu walipeleka kiwiliwili kituo cha polisi, maana kichwa hakikupatikana na haikufahamika kama alitambuliwa au vipi. Yaani sasa hivi ikifika saa tatu watu inabidi tubaki ndani,” alisema.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

M4C OPERESHENI PAMOJA DAIMA NDANI YA IRINGA


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia maelfu ya wakazi wa Manispaa ya Iringa, katika mkutano wa hadhara wa Operesehni M4C Pamoja Daima, uliofanyika kwenye Uwanja wa Mwembe Togwa jana.
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee akihutubia katika mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), uliofanyika kwenye Uwanja wa Mwembe Togwa mjini Iringa jana.
Maelefu ya wakazi wa Manispaa ya Iringa na vitongoji vyake wakiwa katika mkutano wa hadhara wa Operesheni ya M4C Pamoja Daima wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), uliofanyika kwenye Uwanja wa Mwembe Togwa jana. (PICHA NA CHADEMA)

 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

KINANA KUPIGA KAMBI Z’BAR KUIMARISHA CCM

kinana_98cb1.jpg
Na Mwinyi Sadallah, Mwananchi
Zanzibar. Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana amesema ameamua kuweka kambi Zanzibar, lengo likiwa ni kuimarisha chama hicho na kuhakikisha CCM inarejesha majimbo yake yaliyopotea tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1995.
Kinana aliweka msimamo huo kwenye mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa miaka 37 ya kuzaliwa CCM, uliofanyika uwanja wa Soka Kiembesamaki mjini hapa juzi.
Alisema kambi hiyo itaanza kabla ya Aprili mwaka huu, kwa kufanya ziara kuanzia ngazi ya wadi, jimbo, wilaya hadi mikoa kukagua hali ya kisiasa na kuweka mikakati mipya ya chama hicho kisiwani Zanzibar.
"Nitaanza ziara maalumu kabla ya sherehe za Muungano, mengi nitayazungumza wakati huo ukifika, lengo kubwa ni kuangalia uhai wa chama chetu na kuweka mikakati ya kisiasa kabla ya mwaka," alisema Kinana.
Alisema kazi kubwa ya CCM ni kutekekeza sera na ilani yake ya uchaguzi tofauti na vyama vya upinzani, ambavyo ni mahiri na hodari wa kusema bila ya kuonyesha vitendo.
Katibu Mkuu huyo aliviponda vya upinzani nchini na kwamba, CCM imewaachia kazi ya kusema, yenyewe imekijikita kuwatumia wananchi na kutekeleza majukumu yake ya kisera, mipango na mwongozo.
Kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, Kinana alisema watu waliobeza Mapinduzi hayo hivi sasa wamefedheheka kwa kushuhudia yakitimiza miaka 50 huku taifa likiwana hali ya amani, umoja na mshikamano.

 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MTWARA WASHUSHIWA BEI YA KUINGIZA UMEME HADI TSH. 27,000/=

mhongo 67365
Serikali imetangaza neema kwa vijiji vinavyopitiwa na bomba la gesi ambavyo vipo mkoani Mtwara na Lindi, sasa wataunganishiwa kwa Sh27,000. (HM)
Hatua hiyo ilitangazwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwenye uzinduzi mradi wa umeme wilayani Nanyumbu na Masasi.
Profesa Muhongo alisema gharama za kuunganisha umeme kwa sasa ni Sh177,000.
Alisema zaidi ya vijiji 50 vimepewa upendeleo huo ili kuwawezesha wananchi kuwa na maisha bora.
Lengo la Serikali ni kufikia asilimia 30 ya wasasatu waliounganishwa na umeme na kwamba, hivi sasa ni asilimia 23 pekee wanaopata umeme nchini wakati Mtwara ni asilimia nne.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

CHADEMA WAANZA KAMPENI ZA URAIS...!!!

Willibrod-Slaa 9cd30
Viongozi mbalimbali wa Chadema wameanza kupiga kampeni za urais mwaka 2015 kupitia Operesheni Pamoja Daima. (HM)
Akihutubia mamia ya wakazi wa Mkoa wa Njombe huku mvua kubwa ikinyesha jana, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa aliwatahadharisha vigogo wa Serikali wanaoiba fedha za umma kuwa, atawashtaki na kuwafilisi iwapo chama hicho kitashinda uchaguzi mwaka 2015.
Alisema chama hicho kikishinda dola, kitaboresha masilahi kwa watumishi waadilifu lakini mafisadi wanaotafuna fedha za Serikali watapata wakati mgumu.
"Tutakuwa wakali kwa walarushwa," alisema Dk Slaa.
Dk Slaa alisema watendaji walarushwa na wezi watashtakiwa ili mali walizowaibia Watanzania zirejeshwa Serikalini.
"Ninawapa miezi 15 kabla ya uchaguzi mkuu, vigogo hao kurudisha mali walizoiba vinginevyo watajuta kwa sababu tutawashtaki tutakapoingia madarakani." alisema.
Naye Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo alisema chama hicho kitatumia kila aina ya 'silaha' kilichonayo kuhakikisha majimbo yote ya Mkoa Kilimanjaro yananyakuliwa na chama hicho 2015.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

NYOKA MKUBWA AINA YA COBRA AILAZIMISHA NDEGE KUTUA BILA KUFIKA MWISHO WA SAFARI

NewsImages/6694982.jpgMoja ya ndege zinazo milikiwa na shirika na ndege la Misri.
NYOKA aina ya Cobra amesababisha kizaza kwenye ndege na kuilazimisha kukatisha safari yake na kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Hurghada nchini Misri, auliwa baada ya kumjeruhi abiria .
Nyoka huyo alizua mtafaruku huo baada ya kutoka katika mfuko alipokuwa amehifadhiwa na kumjeruhi abiria mmoja raia wa Jordan aliekuwa amekaa karibu na mfuko uliokuwa amehifadhiwa nyoka huyo.
Abiria walianza kumshambulia wakijaribu kumuua kwa kumpiga na viatu na hatimae kufanikiwa kumuua, abiria aliejeruhiwa alipatiwa huduma ya kwanza, na kuhamishiwa hospitalini kwa matibabu zaidi na kuwekwa chini ya uangalizi kwa masaa 24, hali iliopekea kukatisha safari yake.

Uchunguzi wa awali uliofanywa umebaini kwamba, mmoja wa abiria alimficha nyoka huyo kwenye mkoba na alifanikiwa kupita katika vizuizi na kuingia na nyoka huyo kwenye ndege.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya 
Jambo Tz

MWANAMKE ANASWA NA NGOZI YA CHUI...!!!

Mwanamke anaswa na ngozi za chui
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia Mwajuma Hamisi, mkazi wa Yombo Vituka kwa kosa la kukutwa na ngozi mbili za chui kinyume cha sheria, zenye thamani ya sh milioni 11.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema mwanamke huyo alinaswa Januari 18, mwaka huu katika eneo la Yombo Vituka, Wilaya ya Temeke.
Kova alisema mwanamke huyo alinaswa baada ya Ofisa Mhifadhi Wanyamapori mkazi wa Ukonga, kutoa taarifa kituoni hapo kwamba kuna mwananchi anauza ngozi za chui.
Alisema askari walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa na walipompekua chumbani kwake, walimkuta na nyara hizo za serikali.

Wakati huo huo, jeshi hilo limesema limemuua jambazi sugu la uhalifu wa kutumia silaha katika majibizano ya risasi na polisi.
Alisema awali polisi waliweka mtego ili kuyanasa majambazi hayo Januari 22 baada ya kufanya tukio la uporaji wa sh milioni 29 kwa mfanyabiashara wa Mtaa wa Kariakoo, anayejulikana kwa jina la  Shanys Abdalla, mkazi wa Mbezi.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 28.01.2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...