Thursday, December 12, 2013

BASI LA BURUDANI LAPATA AJALI LEO HII MKOANI TANGA, WATU 12 WAPOTEZA MAISHA NA WENGINE KUJERUHIWA




Basi la Burudani baada ya ajali leo Wilaya ya Handeni, Tanga.

Basi la Burudani leo limepata ajali kijiji cha Kwaluguru Kata ya Kwedizinga  wilayani Handeni, Imeripotiwa mpaka sasa watu zaidi ya 12 wamefariki na majeruhi zaidi ya 55. Watu 4 wamepelekwa MOI na KCMC. Tuwaombee majeruhi.

Hospitali ya wilaya ya Korogwe.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 12, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


.

Tuesday, December 10, 2013

'BABU SEYA, PAPII LAZIMA WATAACHIWA HURU TU'


Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na Johnson Nguza ‘Papii Kocha’.
NGUZA Mbangu, mtoto mkubwa wa mwanamuziki mahiri wa muziki wa dansi anayetumikia kifungo cha maisha jela, Nguza Viking maarufu kama Babu Seya, amesema mzazi wake pamoja na mdogo wake, Papii, ni lazima wataachiwa huru hivi karibuni.

Mbangu, ambaye pia hufahamika kisanii kama Mashine, ambaye hivi sasa ni mwinjilisti, alitoa kauli hiyo hivi karibuni alipozungumza na gazeti la Uwazi, akisema kuwa kutolewa jela kwa ndugu zake hao, kutawafanya Watanzania kumsujudia Mungu kupitia tukio hilo.

“Amini nakuambia, Mungu amenipa maono, Babu Seya na Papii wako huru, watatoka tu, kinachosubiriwa ni muda tu ambao hauko mbali, ni lazima watatoka kwa sababu hawana hatia,” alisema Mbangu, ambaye pia alihukumiwa kifungo cha maisha jela kama mzazi wake, lakini akaachiwa wakati walipokata rufaa kwa mara ya kwanza mahakamani.

JIONEE PICHA ZAIDI YA 200 ZA IBADA YA KUMUOMBEA MANDELA INAVYOENDELEA IKIWAMO NA MARAIS NA VIONGOZI WALIOWASILI

Sombre occasion: Members of Nelson Mandela's family take their seats amid heavy rain ahead of his memorial service at the FNB Stadium in Soweto, near Johannesburg

Respect: Nelson Mandela is shown on a giant screen inside the stadium as thousands of South Africans and global dignitaries file into the ground

NORA AFUNGUKA KUHUSU RAY ADAI ALIMTONGOZA. MSIKILIZE HAPA..!!!

Muigizaji wa kike aliyefanya vizuri kupitia kundi la Kaole Sanaa Group, Nuru Nassoro aka Nora amedai kuwa amekuwa akifanyiwa fitina na muigizaji mwenzake Vicent Kigosi aka Ray kwa kuwa aliwahi kumtaka kimapenzi akamkataa.
  
Nora amefunguka kupitia kipindi cha Filamonata cha 100.5 Times Fm na kudai kuwa Ray amekuwa akimbania hata kwenye baadhi ya makampuni ambayo anapeleka kazi zake.
 
Mpaka kwenye kampuni ambayo nimepeleka kazi nimeshawahi kusikia wanasema, wakaniahidi sana mpaka nikawakubalia walichokuwa wanataka wao. Lakini yeye (Ray) alitanguliza movies zake, akasema ana movie zake sijui kitu gani..” amelalamika Nora.
 
Ameeleza kuwa Ray amewahi kumbania kufanya kazi na marehemu Kanumba, na hata Mtitu sababu ikiwa ile ile kumkataa kimapenzi.

WINNIE MANDELA NA GRACA MACHEL WAKUTANA MSIBANI, MARAIS ZAIDI YA 90 KUHUDHURIA MAZISHI.... R.I.P MANDELA


Marais zaidi ya 90 wa nchi mbalimbali duniani akiwemo Barack Obama wa Marekani ni miongoni mwa maelfu ya waliojitokeza Johannesburg South Africa kwenye uwanja wa soka wa FNB leo kumuaga Mzee Mandela anaetarajiwa kuzikwa Jumapili ijayo December 15 2013.
madiba 9
Serikali ya Afrika Kusini imeimarisha ulinzi kwa kutumia vikosi vyake vya jeshi vyenye ulinzi wa hali ya juu ambapo sniper team ni miongoni mwa wanaohusika na ulinzi kwenye eneo lote la kiwanja anakoagiwa Mzee Mandela huku helicopter pamoja na ndege za kijeshi zikipita angani mara kwa mara.

ANGALIA PICHA ZA BIRTHDAY PARTY YA NICK MINAJ, BONGE LA KEKI...!!!


First lady wa label ya YMCMB Nicki Minaj amesherehekea birthday yake ya kutimiza miaka 31 na mafanikio ya kujivunia kwenye kazi yake ya muziki ambapo party ilifanyika huko L.A na Restaurant nzima ilibadilika rangi yake na kuwa ya pink maalum kwa ajili ya party ya Minaj ambayo ilihudhuriwa na Lil Twist, Safaree boyfriend wa Nicki Minaj na watu wengine.
nicki-minaj-birthday-5nicki-minaj-birthday-3

YAFAHAMU MAAJABU 10 YA MSIBA WA MANDELA...!!!

RAIS wa zamani wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela, mweusi wa kwanza kushika wadhifa huo katika taifa lenye uwezo mkubwa kiuchumi na kijeshi barani Afrika, alifariki dunia Alhamisi iliyopita akiwa nyumbani kwake jijini Johannesburg.
Kifo chake kimeushtua ulimwengu na kwa mara ya kwanza katika historia, dunia nzima imesimama nyuma ya jemedari huyo, kila mmoja akionesha masikitiko yake. Wakati dunia ikisubiri mazishi yake ambayo pia yatavunja rekodi ya mazishi yote yaliyowahi kufanywa tokea kuumbwa kwa uso wa dunia hapo Desemba 15 mwaka huu, Uwazi limebaini maajabu kumi yanayoambatana na msiba huo.

AIR FORCE ONE KUBEBA MARAIS WATANO WA MAREKANI
AIR Force One ni ndege inayombeba Rais wa Marekani aliye madarakani na kumpeleka popote duniani. Lakini katika hali ya kushangaza, Idara ya Usalama ya Marekani imetoa ruhusa kwa marais wastaafu wakiwa na wake zao, kuandamana na Rais Barak Obama kuhudhuria mazishi ya shujaa huyo wa dunia.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 10, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.


Monday, December 09, 2013

JE, UNAJUA KUWA WOGA, AIBU HUPUNGUZA KUJIAMINI KATIKA MAPENZI...??!

https://www.facebook.com/jambotz

KARIBU mpendwa wa blog yetu ya Jambo Tz inayopendwa na wengi na kuwashukuru wote wanaotumia muda wao kutupongeza wengine kutukosoa ili kuiboresha blog yetu.


Vilevile wapo walio na matatizo wanaoomba msaada ambao nashukuru umewasaidia wengi. Kama ilivyo ada, umekaa mkao wa kula kutaka kujua leo nimekuja na mpya gani. Nasema hakuna jipya chini ya jua kwa sababu kitu mapenzi kilikuwapo tangu enzi ya mababu na hata hao waliyakuta tokea enzi ya Adamu na Eva.
Tumepata malalamiko mengi kutoka kwa wasomaji wetu waliolalamika juu ya matatizo wanayokumbana nayo katika kula chakula cha roho, wengi wanalalamika kuwa hawali chakula kilichokamilika.
Kwa mfano mtu anauliza; Mbona mpenzi wangu si mtaalam wa mambo flani?, wengine hudiriki kusema tangu waanze mapenzi na waume zao au wake zao hawajafurahia mapenzi na kushangaa kusikia mapenzi yakikukolea hukufanya upandishe mashetani na kumaliza maneno yote mdomoni au kumfanya mwanaume atoe ahadi ambazo hana hata uwezo nazo kwa kusema atakununulia ndege wakati hata baiskeli hana.

Yote hayo ni mtu kuguswa pale panapomfanya ajione yupo dunia nyingine na kujiona juu hayupo wala chini hayupo. Wao hujiuliza kulikoni wenzao wafaidi wao wasifaidi kwani wamekosa nini.

Swadakta swali zuri sana, kumekuwa na utamaduni wa watu wengi kuona aibu kuuliza jambo walisilolijua hasa katika mapenzi hii imepelekea watu kuwa wavivu kujifunza kwa kuona aibu kuuliza kitu wasichokijua kwa kuogopa kuitwa washamba.
Nani alikuambia wote wamezaliwa wanajua, usichokijua uliza usisubiri aibu ikukute kwa mpenzio, kuuliza nje au kutoa nje udhaifu wako. Siku zote wasiojua huwa wajanja sana ili kuficha udhaifu wao lakini unauficha udhaifu wako wakati lazima uingie kwenye gemu.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU YA MIAKA 52 YA UHURU DESEMBA 09, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.

MARAIS KUINGIA KWA KADI MAZISHI YA MANDELA...!!!



Qunu, nyumbani kwa Mandela 
TISHIO la vitendo vya kigaidi vinavyotokea kwenye maeneo mbalimbali hapa duniani, vimeifanya Serikali ya Afrika Kusini, kutoa kadi kwa marais na viongozi watakaohudhuria mazishi ya baba wa taifa hilo, Nelson Mandela. Mandela aliyefariki Desemba 5, atazikwa Desemba 15 kijijini kwake Qunu, eneo alilolichagua kabla ya mauti yake. 
Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya kimataifa, usalama katika miji ya Afrika Kusini, unatarajiwa kuimarishwa zaidi kuliko hata ule unaotumika kwa marais wa Marekani wanapofanya ziara kwenye mataifa mbalimbali.  
Taarifa hizo zinabainisha kutokana na idadi kubwa ya watu kuhudhuria mazishi hayo, utawala wa nchi hiyo umebuni mbinu hiyo ya utoaji kadi kwa watu watakaokuwa eneo la maziko wakiamini itasaidia kuimarisha ulinzi.  
Mazishi hayo yanatarajiwa kuvunja rekodi ambapo yanalinganishwa na yale ya Papa John Paul II mwaka 2005, ambayo yalihudhuriwa na wafalme watano, malkia sita wa falme mbalimbali na marais wapatao 70 na mawaziri kadhaa, wakiwamo wafuasi wake zaidi ya milioni mbili.  
Ratiba ya kutoa heshma za mwisho yatangazwa Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa jana na Serikali ya Afrika Kusini, mwili wa Mandela utawekwa katika jengo la serikali kwa muda wa siku tatu, kutoa fursa kwa wananchi kutoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi waliyempenda. Meya wa jiji la Cape Town, Patricia de Lille, alisema ibada ya kumuaga Mandela itafanyika Jumanne kwenye uwanja wa mpira mjini Johannesburg.  
Jana maelfu ya raia wa Afrika kusini kutoka matabaka yote na rika zote walishiriki katika ibada ya pamoja ya dini mbalimbali, ambayo ilifanyika mjini Cape Town mahali ambako Mandela alitoa hotuba yake ya kwanza baada ya kuachiwa huru kutoka jela. 
Chanzo: TANZANIA DAIMA

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...