Wednesday, November 06, 2013

UJUMBE MZITO WA LULU KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameliomba Bunge kurekebisha sheria za Magereza katika vikao vyao vinavyoendelea mjini Dodoma.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam juzi, Lulu alisema kutokana na kukaa huko kwa mwaka mmoja, ameona mambo mengi ambayo yanatakiwa kufanyiwa marekebisho.
“Unaweza ukamkuta mfungwa ana miaka zaidi ya 20 lakini hajawahi kufikishwa mahakamani wala kuulizwa chochote kutokana na kitu ambacho kimempeleka hapo, kiukweli hata kama ana makosa haiwezekani kumkalisha miaka yote hiyo pasipo kusikilizwa,” alisema.
Alisema yeye amekaa huko kwa muda mfupi lakini amepata shida sana kuyazoea mazingira hayo, kwani huwezi kuishi kama nyumbani, hivyo ni vizuri ukiwekwa utaratibu mtu anasomewa kesi yake kwa muda gani.
Lulu alilazimika kukaa gerezani kwa muda huo kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa nguli wa filamu nchini, Steven Kanumba, aliyefariki dunia nyumbani kwake Sinza Vatican Aprili 7, mwaka jana

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 06, 2013

.
.
.

MAELEZO BINAFSI YA MH. ESTER BULAYA KUHUSU WAHARIFU WA DAWA ZA KULEVYA.....!!!


 bulaya
Haya ni maelezo binafsi ya Mheshimiwa Ester Amos Bulaya bungeni Dodoma November 4 2013 kuitaka serikali kufanya mabadiliko ya sheria ya dawa za kulevya na kuanzisha mahakama maalum ya kushughulikia wahalifu wa dawa za kulevya.
Kwa mujibu wa Kanuni ya 28(8) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la mwaka 2013, napenda kutoa maelezo binafsi ya juu ya tatizo sugu la uagizaji, uuzaji na usafirishaji wa dawa za kulevya linaloongezeka kwa kasi kubwa nchini, lengo likiwa ni kuitaka serikali ifanye mabadiliko/marekebisho ya sheria ya Dawa za kulevya na kuanzisha Mahakama Maalum kushughulikia wahalifu wanaojihusisha na usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya.
chinese
Mheshimiwa Spika,
Nimeona ni wakati muafaka kutoa maelezo haya, ili Bunge lako tukufu na Serikali ipate fursa ya kuona uzito wa tatizo hili kutokana na ukweli kwamba katika miaka ya karibuni tatizo la dawa za kulevya katika nchi yetu limeongezeka kwa kasi ya ajabu hali inayopelekea athari kubwa za kiuchumi, kijamii na kiafya. Na mbaya zaidi kundi kubwa linaloathirika ni kundi la vijana, ambao ndio nguvu kazi ya Taifa letu.

HILI NDILO JUMBA LA KIFAHARI LENYE UWANJA WA NDEGE HAPO HAPO NYUMBANI

article-2486741-1923386700000578-170_634x475Nyumba hii ipo huko Las Vegas Marekani na ina heka 40 na indoor car parking kubwa sana kuingiza magari zaidi ya kumi kwa wakati mmoja na upande wa mwingine ina zoo humohumo ndani, jet inayopark kwenye airport yako binafsi hapo mjengoni haina haja ya kwenda kwenye public airport na ukitaka kumiliki hii nyumba inabidi zikutoke $ 48 millioni.
article-2486741-1923389000000578-571_634x475
Vyumba vya kulala vipo vingi kiasi kwamba wakati mwingine inabidi kuwasiliana kwa simu chumba hadi chumba kwasababu ya umbali wa kufikia vyumba vingine pia kuna ofisi binafsi kiasi kwamba unaweza usiende sehemu yoyote kazi zako zote zikafanyika ndani ya hizi heka 40.
Upande wa michezo kuna uwanja wa kucheza golf, basketball, swimming pool kubwa likiunganishwa na water falls na pia kuna eneo kubwa sana la wazi na humo ndani kumewekwa nakshi na material ya gharama kuanzia dinning, jikoni hadi vyumbani.

article-2486741-1923388400000578-459_634x475

RAIS KIKWETE KULIHUTUBIA BUNGE KESHO....!!!

jk_d71ab.jpg
Rais Jakaya Kikwete, kesho anatarajiwa kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Habari zilizopatikana Mjini Dodoma jana na kuthibitishwa na uongozi wa Bunge pamoja na Ikulu, Dar es Salaam zinasema atahutubia mchana.
Kutokana na ujio huo, Serikali imewaelekeza Mawaziri na Manaibu Waziri kutotoka nje ya Dodoma hadi hapo Rais atakapokuwa amehutubia Bunge. 
Kadhalika safari zote za Kamati za Bunge ambazo zilikuwa katika mchakato wa kutekelezwa zimeahirishwa hadi baada ya kesho, ili kutoa fursa kwa wabunge wote kuwapo wakati wa hotuba hiyo.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema jana kuwa hata yeye amesikia taarifa kuwa Rais atazungumza bungeni lakini hajui atazungumza kitu gani... "Hata mimi nimesikia kuwa atazungumza lakini sijui atazungumza jambo gani kwa kuwa siyo miongoni mwa watu wanaomwandalia hotuba," alisema Balozi Sefue.
Kadhalika, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alithibitisha kuwa Rais Kikwete atalihutubia Bunge, Alhamisi... "Nathibitisha ni kweli, ila kwa taarifa nyingine watafuteni watendaji wa Bunge, kama Katibu wa Bunge nadhani wana taarifa zaidi."

M23 'WAMALIZA UASI' BAADA YA KIPIGO

130913125600_m23_congo_304x171_afp_nocredit_ab833.jpg
Waasi wa M23 katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametangaza kumaliza uasi wao ndani ya nchi hiyo muda mfupi baada ya kupigwa katika ngome yao ya mwisho na majeshi ya serikali ya Congo yakishirikiana na kikosi maalum cha Umoja wa Mataifa kilichopewa uwezo wa kupigana na waasi hao.
Katika taarifa walioitoa waasi hao wamesema badala ya kufanya uasi sasa wataendesha harakati zao kutumia njia ya kisiasa.
Muda mfupi uliopita Kiongozi wa waasi hao Bertrand Bisimwa ametangaza kuwaamuru mkuu wa wapiganaji wa M23 na makamanda wa vikosi vyote muhimu wa kundi hilo kuwaandaa wapiganaji wao kusalimisha silaha, kutawanyika kuondoka katika eneo la mapigano na kukubaliana na matakwa yatakayowekwa na serikali ya Congo
Awali Msemaji wa Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Lambert Mende aliambia BBC kuwa majeshi ya nchi yameishambulia ngome ya mwisho ya waasi na wamekimbia na wengine huenda wakawa wamejisalimisha.
Majeshi ya serikali ya Kongo yakishirikana na kikosi maalum cha Umoja wa Mataifa kilichopewa uwezo wa kupambana na waasi hao walianza mapambano dhidi ya M23 Octoba mwaka huu na kufanikiwa kuwaondoa katika eneo la Bunagana kwenye mpaka wa Uganda ambayo ni ngome yao muhimu.

Tuesday, November 05, 2013

NEY WA MITEGO AMPA KICHAPO BABA 'AKE...!KISA KUMUONEA MAMA' AKE...!

Nay wa Mitego ni moja kati ya wasanii wenye tungo zenye utata sana tangu anaanza kufanya muziki ambapo alikuwa akisikika kwenye baadhi ya ngoma akimchana hata baba yake mzazi kwa kushindwa kuwa responsible kwake. Hit maker wa ‘Muziki Gani’ ambae anakiri kuwa zamani alikuwa mkorofi sana na kwamba sasa hivi amebaki kuongea tu kwenye muziki, amewahi kufunguka kuwa alimpa kichapo baba yake wa kambo/baba yake wa kufikia ambae alikuwa akimtunza kwa muda huo.
Kisa cha kumpa kichapo mzee wa watu.. ni kwa sababu alikuwa anampiga sana mama yake Nay wa Mitego kitu ambacho kilikua kinamuumiza sana yeye, na mwisho wa siku akachukua uamuzi wa kumpiga akimtetea mama yake.
  Tukio hilo lilimsukuma Nay wa Mitego kuandika mashairi ya wimbo unaohusu wanawake akiwaambia wanaume wenye tabia kama za baba yake wa kufikia kwamba ‘Mwanamke hapigwi, anatulizwa na mapenzi.’
  “Ule wimbo ulikuwa ni dedication kwa mama yangu mzazi, mama yangu mzazi alikuwa anaishi na baba yangu wa kufikia, yule baba yangu alikuwa mkorofi sana, alikuwa anampiga sana mama bila sababu, kiasi kwamba alisababisha mimi na mama tusielewane kwa sababu mimi nilikua sipendi vile alivyokuwa anamfanyia mama, mi nakumbuka kwa bahati mbaya nilishawahi kumpiga yule mzee and then mama yangu akachukua hatua ambayo mimi sikuitegemea kwa sababu mimi nilikuwa namtetea mama.
  “Mi nikajifunza kwamba mwanamke hatakiwi kupigwa hata siku moja, na ndo maana nikaimba, so ilikuwa dedication kwa mama yangu na wanawake wote Afrika.” Alisema Nay wa Mitego.

MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 05, 2013

DSC 0015 383d6
DSC 0016 21d82

SULEIMAN ANAHITAJI MSAADA WETU AENDE INDIA KUTIBIWA

Wapendwa, Siku ya Leo haikuwa nyepesi kwangu na hata kwa mtoto Suleiman na familia yake, baada ya kupokea ujumbe rasmi kutoka kwa madakatri bingwa wa upasuaji wa Hospitali ya CCBRT kuwa Upasuaji huo HAUTAWEZEKANA kufanyika CCBRT kama tulivyojipa moyo mara ya kwanza.

LAKINI, wamekubali kutusaidia kupata hospitali nzuri nchini India kwa ajili ya kumsafirisha kijana Suleiman. Nguvu zenu zinahitajika sana kipindi hiki kigumu kwa familia hii. Tayari msamaria mwema ametoa tiketi moja ya kumsindikiza Suleiman India. Wapendwa, tushikamane, tunaweza. Hatua zinazofuata:
Kwanza kupata hospitali India.
Kufanya malipo
Kupata barua ya referral na kutafuta passport na visa ya Suleiman na msindikizaji Safari

CCBRT wataturudishia milioni 3 tulizolipa kama gharama za matibabu na tukijumlisha na pesa alizo nazo Imelda tuitakuwa tumebakiwa na shilingi milioni 6.2. Safari ni ndefu lakini msichoke.
Asanteni sana. Mola atuongoze. Amen

PAPII KOCHA, BABU SEYA KAZI IMEKWISHA.

Na Mwandishi Wetu

 MABERE Nyaucho Marando, wakili wa mwanamuziki maarufu nchini, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ amesema amemaliza kazi ya kuwatetea wafungwa hao waliohukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na hatia ya kuwanajisi watoto 12 waliokuwa wakisoma Shule ya Msingi Mashujaa, Sinza jijini Dar es Salaam..........
Babu Seya (wa pili kulia) na Papii Kocha (wa pili kushoto) wakiwa mahakamani kusikiliza rufaa yao.

 Akizungumza na gazeti hili juzi, Marando alisema kazi aliyokusudia kuifanya ameimaliza, sasa anasubiri majaji waliosikiliza alichokisema ili watoe uamuzi wa mwisho lakini pia anamtegemea Mungu.

 “Mimi kazi nimemaliza sasa nawasubiri hao wakubwa (majaji) ili wapime nilichowaambia kwa mujibu wa sheria na kisha watoe uamuzi, lakini pia namtegemea Mungu,” alisema Marando.

SERIKALI YAIRUDISHA DARAJA SIFURI


Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imebatilisha uamuzi wake wa kubadili mfumo wa upangaji wa madaraja ya ufaulu kwa mitihani ya kidato cha nne kama ilivyotolewa awali kwa kurudisha daraja sifuri.

Kutokana na uamuzi huo, sasa daraja la tano lililotangazwa wiki iliyopita kuchukua nafasi ya daraja sifuri sasa limefutwa.

Uamuzi huo umetolewa siku nne baada ya wizara hiyo kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Profesa Sifuni Mchome, kutangaza kuwa serikali imeamua kubadilisha mfumo wa kupanga alama na madaraja ya ufaulu.

Uamuzi wa kushusha alama za ufaulu ulipokewa kwa hisia tofauti na wadau wa elimu nchini ambao walikosoa mfumo huo kwa kueleza kuwa unaipeleka kaburini sekta ya elimu ya Tanzania.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo akizungumza na NIPASHE jana kwa njia ya simu kutoka Dodoma, alisema baada ya kutafakari serikali imeamua kuondoa daraja la tano kama ilivyokuwa imetangaza awali na kurejesha daraja sifuri.

“Kwanza niwaombe radhi Watanzania kwa mkanganyiko huo uliojitokeza ambao ni jambo moja tu limewachanganya, lakini walio wengi wanapongeza mfumo huu wa madaraja, tulichokuja kuharibu ni ‘statement’ ya neno division five,” alisema.

Monday, November 04, 2013

GLOBAL EDUCATION LINK YAZINDUA MIKOPO KWA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU NJE YA NCHI

Mkurugenzi wa Elimu ya juu, Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi, Profesa Sylvia Temu ambaye alikuwa mgeni rasmi aliyemwakilisha Waziri wa Elimu na mafunzo ya Ufundi akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa mpango wa utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma vyuo vya nje ya nchi uliofanyika jana katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, Profesa Magishi Nkwabi Mgasa akiwapongeza kampuni ya Global Education Link kwa kushirikiana na Benki ya Afrika (BOA) kwa kuweza kubuni njia itakayowawezesha wanafunzi wengi waliokuwa wanapenda kwenye kusoma nje ya nchi ila wanakosa pesa. Vile vile aliwaomba wanafunzi kuacha kukurupukia vyuo vya nje bila kutambua kama vinatambulika Tanzania ama lah ili kuwaepushia usumbufu.  Uzinduzi huo ulifanyika jana katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

RAIS KIKWETE NAYE ANAFUATILIWA NA MAREKANI?

kikwete_2e5c8.jpg
NA MWANDISHI WETU
HATUA ya Marekani kudaiwa kufuatilia mawasiliano ya viongozi wa nchi washirika wake wa karibu, sasa ni wazi imeiacha Tanzania katika wingu la shaka, kama viongozi wake nao wanafuatiliwa kwa namna ile ile inayoelezwa na viongozi wa Ulaya. Shaka hiyo inatokana na urafiki wa muda mrefu uliopo kati ya Tanzania na Marekani, ambapo kwa nyakati tofauti, marais watatu wa taifa hilo kubwa duniani wamepata kuzuru nchini.
Kauli tofauti zilizotolewa ndani ya wiki hii na majasusi wa mataifa makubwa duniani, ikiwemo Marekani na Uingereza, wakati wakizungumzia madai ya Marekani kufuatilia mawasiliano ya Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, kwamba nchi zote duniani zinachunguzana, ndiyo ambayo baadhi ya wafuatiliaji wa mambo wanadai kuwa Tanzania bila shaka haiwezi kukwepa kufuatiliwa.


Mbali na hiyo, kauli ambayo imepata kutolewa na mfanyakazi wa zamani wa shirika la NSA, Edward Snowden, kwamba ujasusi huo wa Marekani haufanywi dhidi ya watuhumiwa wa ujasusi na wakazi wa nchi zenye ugomvi na Marekani tu, bali hata marafiki na waitifaki wa karibu kabisa na nchi hiyo, ndiyo ambayo inajenga mazingira ya Tanzania nayo kuwemo kwenye orodha hiyo ya kufuatiliwa.
Marais watatu wa Marekani, kwa nyakati tofauti wamepata kuzuru nchini. Maraisi hao ni pamoja na Bill Clinton, George W. Bush na Barack Obama, ambaye alitembelea nchini mwezi Julai, mwaka huu.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 04, 2013

DSC 0002 de89d
DSC 0003 ae6e5
DSC 0004 db5d9

BOBBY WILLIAMSON KOCHA MPYA SIMBA SC

Bobby_3286b.jpg

Maofisa wa ngazi ya juu wa Simba wameanza mazungumzo na kocha Bobby Williamson wa Gor Mahia ya Kenya ili achukue mikoba ya Abdalla Kibadeni.
SIMBA itaanza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, Januari 26 mwakani dhidi ya Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ikiwa na kocha mpya, Mwanaspoti linaweza kuthibitisha.
Maofisa wa ngazi ya juu wa Simba wameanza mazungumzo na kocha Bobby Williamson wa Gor Mahia ya Kenya ili achukue mikoba ya Abdalla Kibadeni.
Williamson (52), ni straika wa zamani wa West Bromwich Albion na katika mechi 53 aliyoichezea timu hiyo alifunga mabao 11.
Williamson, ambaye ni raia wa Scotland alijiunga na Gor Mahia msimu huu na tayari ameipa ubingwa wa Ligi Kuu Kenya ikiwa ni miaka 18 tangu timu hiyo itwae ubingwa wa Kenya mwaka 1995.

WAPINGA KUAHIRISHWA KESI YA KENYATTA

130409101249-kenyas-president-elect-uhuru-kenyatta-story-top_ec903.jpg
Waathirika wa kesi inayomkabili rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta wameutaka Umoja wa Mataifa kukataa wito wa kutaka kucheleweshwa kwa kesi dhidi ya Rais Kenyatta katika mahakama ya kimataifa ya ICC mjini The Hague, Uholanzi.
Baadhi ya viongozi wa Afrika wameandaa rasimu ya azimio la kuomba kesi inayomkabili Rais Kenyatta iahirishwe kwa mwaka mmoja kwa masilahi ya usalama wa taifa, kufuatia shambulio la kigaidi katika kituo cha kibiashara cha Westgate mjini Nairobi.
Lakini mwanasheria wa waathirika, Fergal Gaynor, amesema kucheleweshwa kwa kesi kutapunguza nafasi ya kupatikana haki kwa waathirika. 
Bwana Kenyatta anakanusha mashitaka yanayomkabili dhidi ya uhalifu wa kibinadamu, kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007

Sunday, November 03, 2013

DIAMOND PLATNUMZ ATIBUA MSAFARA WA RAIS...!! USALAMA WA TAIFA WATAKA KUMKAMATA...!!!

STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Alhamisi iliyopita alijikuta akiutibua msafara wa Rais wa Zanzibar, Dk. Mohamed Shein kufuatia kuondoka kwenye msiba wakati ilitangazwa kiongozi huyo ndiye aliyetakiwa kuanza kuondoka.
 Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond'.
Ishu hiyo iliyotafsiriwa kama jeuri ya staa huyo ilitokea Mbuzini Mjini Magharibi, Zanzibar baada ya kumalizika kwa mazishi ya baba wa Wema Sepetu, aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania Urusi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na Waziri wa Elimu wa zamani katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, marehemu Isaac Abraham Sepetu.  
DIAMOND AINGIA
Awali, wakati waombolezaji wamekaa wakiusubiri mwili wa marehemu ufike, ghafla Diamond aliibuka akisindikizwa na kundi la wapambe mpaka alipokaa.

Diamond akiwa mstari wa mbele wakati wa mazishi ya Balozi Sepetu.
AWEKWA MSTARI WA MBELE
Diamond alipofika aliwekwa mstari wa mbele ambako walikaa ndugu wa karibu na watoto wote wa marehemu. 

  MC ATANGAZA ITIFAKI YA SERIKALI
Mwili ulipowasili, ratiba ya mazishi ikatangazwa na MC ambapo alitaja utaratibu wa mazishi mpaka watu watakaotakiwa kuweka mashada ya maua kaburini, akiwemo Rais Shein. 


Baada ya mazishi, Mwongoza Shughuli ambaye jina halikujulikana aliwaomba watu wote wazingatie itifaki ya usalama wa taifa kwamba ni lazima viongozi wote wa serikali waondoke ndipo waombolezaji wengine watawanyike. “Jamani naomba sana itifaki izingatiwe, asiondoke mtu yeyote kabla ya viongozi wetu wa serikali, akiwemo Rais Shein hawajaondoka,” alisema MC huyo. 
  DIAMOND APUUZA, ANYANYUKA
Baada ya MC huyo kutoa mwongozo, watu wote walitulia wakisubiri kiongozi wa kwanza kuondoka ambaye alikuwa ni Rais Shein kama itifaki ilivyotaka.

HOJA YA KUMNG"OA MAKINDA YAPIGWA KOMBORA

makinda_1af6c.jpg
Mchakato wa kumng'oa madarakani Spika wa Bunge, Anne Makinda(pichani) ambao umeanzishwa na Mbunge wa Nzega, Dk Khamis Kigwangalla (CCM), huenda usifanikiwe kutokana na vikwazo kadhaa vikiwamo kupingwa na baadhi ya wabunge wenye ushawishi mkubwa katika Bunge.  

Wabunge wameanza kumpinga hadharani kuhusu suala hilo ambalo jana mjadala wake uliyateka makundi ya wabunge waliokuwa wakihudhuria vikao vya kamati mbalimbali wakati wakiwa kwenye mapumziko. Katika viwanja vya Bunge jana, gazeti hili liliwashuhudia Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM) na swahiba wake kisiasa, Kangi Lugola ambaye ni Mbunge wa Mwibara (CCM) wakikataa kusaini karatasi waliyopelekewa kuunga mkono kung'olewa kwa Spika.

 Baadaye kwa nyakati tofauti walisema "hoja hiyo haina mashiko" na kwamba hawakutumwa na wapigakura wao kuwania posho bungeni.
Wabunge hao walikuwa wakirejea moja ya hoja za Dk Kigwangalla kwamba Makinda amekiuka kanuni kwa kuidhinisha malipo ya Sh430,000 kama posho kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, tofauti na wajumbe wa kamati nyingine ambao malipo yao ni Sh180,000 kwa siku.
Wengine wanaompinga Kigwangalla ni Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage (CCM) na yule wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR - Mageuzi), ambao pia walisema hawaoni sababu za msingi za kumwondoa Makinda madarakani.  

SHEHENA ZA PEMBE ZA NDOVU ZAKAMATWA DAR....!!!

Siku moja baada ya wabunge kuwataka Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kagasheki kujiuzulu kwa kushindwa kusimamia Operesheni Tokomeza Ujangili, pembe 706 za ndovu zimekamatwa jijini Dar es Salaam.
Pembe hizo 706 ni sawa na tembo 353 waliouawa katika hifadhi za wanyama pori mbalimbali hapa nchini. Tukio hilo lililotokea jana jioni katika Mtaa wa Kifaru, Mikocheni, wilayani Kinondoni, liliongozwa na Waziri Kagasheki ambaye aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Tarish Maimuna.

Waliokamatwa na shehena hiyo ya pembe za ndovu ni raia watatu wa China ambao ni Xu Fujie, Chen Jinzha na Huang Qin wote kutoka mji wa Guandung.

Raia hao wa China wamekuwa wakiishi katika nyumba hiyo kwa miaka mingi wakifanya biashara ya kuingiza nchini vitunguu swaumu kutoka China na kusafirisha nje ya nchi makombe yanayopatikana baharini.

Alipoingia ndani ya nyumba hiyo, Kagasheki ambaye aliambatana na askari polisi na baadhi ya maofisa usalama alishuhudia shehena kubwa ya pembe za ndovu ikiwa imehifadhiwa kwenye viroba vyenye uzito wa kilo 50.

MAMBO YAMWENDEA VIGUMU MASOGANGE.... SADC WAINGILIA HUKUMU YAKE NA KUIPINGA

MAKAMANDA wa vitengo vya kudhibiti madawa ya kulevya kwa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wamemaliza kikao chao jana kujadili mustakabali wa uhalifu ikiwemo hukumu iliyotolewa kwa Mtanzania Agness Gerald ‘Masogange’ aliyekamatwa na malighafi haramu aina ya Ephedrine, Julai 5, 2013 nchini Afrika Kusini kwamba ni ndogo.
Taarifa za ndani kutoka Jeshi la Polisi Tanzania zimeeleza kuwa makamanda wa nchi hizo 15 walikutana jijini Arusha kuanzia Jumatatu iliyopita lengo kubwa likiwa kutokubaliana na adhabu zinazotolewa na baadhi ya nchi wanachama kwa wanaokutwa na hatia ya kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’.
WALICHOJADILI
Kwa mujibu wa chanzo kilicho ndani ambacho kiliomba hifadhi ya jina kwa kuwa si msemaji, makamanda wa nchi hizo walikuwa na kibarua kizito cha kujadili mbinu mbalimbali za kukabiliana na uhalifu pamoja na hukumu inayotolewa kwa watu wanaokutwa na hatia ya kukamatwa na unga.
“Walijadili matukio mengi ya uhalifu likiwemo suala la madawa ya kulevya, wakajadili mbinu za kukomesha biashara hiyo haramu ili waweze kupata suluhisho la kudumu,” kilisema chanzo hicho.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 3, 2013


DSC 0010 e5550
DSC 0011 7d3c1
DSC 0012 731e4

CHELSEA YAFUMULIWA 2-0 NA NEWCASTLE, MAN CITY YAPIGA MTU 7-0 ENGLAND

article-2483669-1924F49800000578-379_634x411_69528.jpg
article-2483669-192508D100000578-811_634x561_0ff39.jpg
Mourinho akimpongeza kocha wa Newcastle baada ya mechi
MABAO ya Yoan Gouffran na Loic Remy yameipa Newcastle ushindi wa 2-0 dhidi ya Chelsea katika Ligi Kuu ya England leo, huku Manchester City ikiifumua Norwich 7-0.
Gouffran alifunga bao lake dakika ya 68 na Remy akafunga dakika ya 89 katika mchezo huo ambao timu ya Jose Mourinho ilikamatwa kila idara.
article-2483669-1924F51B00000578-967_634x471_3689c.jpg
Kikosi cha Chelsea kilikuwa: Cech, Ivanovic, Terry, Luiz, Cole, Lampard/Schurrle dk70, Ramires, Oscar, Mata/Willian dk62, Hazard, Torres/Eto'o dk62Newcastle: (4-4-2): Krul 7; Debuchy 7, Williamson 6, Yanga-Mbiwa 6, Santon 6; Sissoko 8, Cabaye 7, Tiote 6 (Anita 53, 7), Gouffran 7 (Obertan 84); Shola Ameobi 5 (Cisse 62, 6), Remy 7.
Newcastle: Krul, Debuchy, Williamson, Yanga-Mbiwa, Santon, Sissoko, Cabaye, Tiote/Anita dk53, Gouffran/Obertan dk84, Shola Ameobi/Cisse dk62 na Remy.

Saturday, November 02, 2013

MATOKEO YA DARASA LA SABA 2013 YATOKA, HAYA HAPA......!!!

Matokeo ya Darasa la Saba yametangazwa leo na mwaka huu ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 30.72 mwaka jana mbaka asilimia 50.61 mwaka huu kutokana na wanafunzi walio fanya mtihani mwaka huu wa darasa la saba wamefaulu zaidi ukilinganisha na wanafunzi wa mwaka jana.
Kaimu mtendaji wa Baraza la Mtihani Charles Msonda amesema ufauru katika masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya 6.01 na 28.06 ukilinganisha na mwaka 2012 Mwaka huu watainiwa wamefahulu zaidi katika somo la Kiswahilin kwa asilimia 69.06 na somo walilio faulu kwa kiwango kidogo zaidi ni somo la Hisabati wamefaulu kwa asilimia 28.62 Msonda amesema jumla ya watahiniwa 427,606 kati ya 844,938 walio fanya mtihani huo wamepata alama ya 100 kati ya alama ya 250 idadi hiyo nisawa na asilimia 50.61

ANGALIA MATUKIO KATIKA PICHA: MBEYA CITY FC YAIBAMIZA ASHANTI UNITED GOLI MOJA BILA.

Timu ya Ashanti United ikiwa katika picha ya pamoja kabla ya Mpira  kuanza 
 Timu ya Mbeya City Fc ikiwa katika Picha ya Pamoja Kabla ya mpira kuanza 

KIONGOZI WA TALIBAN NCHINI PAKISTAN, AUAWA

131102043401_hakimullah-mehsud_2d5a2.jpg
Kiongozi wa kundi la wapiganaji la Taliban nchini Pakistan, Hakimullah Mehsud, ameuawa kwa kutumia ndege zisizokuwa na rubani, hii ni kwa mujibu wa afisaa mmoja mkuu wa kundi hilo.
Shambulizi hilo lililenga gari alimokuwa anasafiria Mehsud, Kaskazini Magharibi mwa Waziristan.
Watu wanne waliokuwa wanasafiri na Mehsoud wakiwemo walinzi wake wawili waliuawa katika shambulizi hilo.
Marekani pamoja na Pakistan zimewahi kudai siku za nyuma kumuua Mehsoud ingawa madai yao hayakuwa na ukweli.
Serikali ya Pakistan imetoa taarifa kulaani vikali mashambulizi ambayo Marekani inafanya kwa kutumia ndege zisizo na rubani, ikisema kuwa mashambulizi kama hayo yanakiuka uhuru wa taifa hilo.
Shambulizi hilo lililofanywa siku ya Ijumaa, lililenga gari la Mehsud.
Afisaa mmoja mkuu wa ujasusi nchini Marekani, aliambia shirika la habari la Associated Press kuwa Marekani ilipokea taarifa muhimu kuthibitisha kifo cha Mehsoud.
Hata hivyo msemaji wa baraza la usalama wa kitaifa la Marekani, alisema kuwa hawawezi kuthibitisha taarifa hizo lakini ikiwa ni kweli basi ni pigo kubwa sana kwa Taliban.
Hakimullah Mehsud alijulikana sana mwaka 2007 kama kamanda wa mwasisi wa kundi hilo Baitullah Mehsud, alipowakamata wanajeshi 300 wa Pakistani .

MASHABIKI SIMBA WATAKA WACHEZAJI WAKONGWE WARUDISHWE


mashabiki_wa_simba_wakifurahia_ushindii_dc4d7.jpg
MASHABIKI WA SIMBA 
Mashabiki Simba wamepiga kelele na kutala benchi lao la ufundi libadilike na kuwarudisha wachezaji wakongwe.
Zaidi ya mashabiki waliotuma ujumbe mfupi kupitia barua pepe na wale waliopiga simu ya mkononi ya SALEHJEMBE, wamemtaka Kocha Mkuu, Abdallah Kibadeni na wasaidizi wake kufikiria na kugeuza misimamo waliyonayo.
"Kweli Kibadeni anatuangusha, ni kocha mkongwe lakini anaonyesha hana msimamo, ninahisi anaburuzwa na watu wengine maana anatoa uamuzi ambao unaonyesha kuna chuki. Wakongwe warudishwe," alisema Mohammed Kassim.
Juma Mroki, Thomas Mapunda waliojitambulisha wanaishi Dar es Salaam na Songea, walisema wakongwe ndiyo tatizo la timu hiyo.
"Angalia tumeongoza hadi dakika ya 90, lakini tumeshindwa kujilinda. Uzoefu pia ni jambo muhimu, wakongwe wasidhalauriwe eti kwa kuwa tuna vijana."
Baadhi ya wachezaji wakongwe wa Simba ambao wameshushwa kikosi cha pili ni Henry Joseph na Ramadhani Chombo 'Redondo'.
Lakini mshambuliaji mwenye kasi, Haruna Chanongo, naye ameshushwa kikosi cha pili kwa kuwa tu alishindwa kucheza vizuri mechi moja dhidi ya Yanga!
Mashabiki Simba, jana walifanya vurugu baada ya timu yao kushindwa kulinda bao na Kagera wakasawazisha katika dakika za nyongeza.
Walifanya vurugu na kuvunja viti huku baadhi yao wakiumia baada ya askari polisi kupambana nao wakati wakijaribu kuzuia vurugu hizo.
Simba imekuwa ikisonga kwa mwendo wa kusuasua na kusababisha kuendelea kuporomoka na sasa iko katika nafasi ya nne baada ya Yanga walioshika usukani jana, Azam FC na Mbeya City.
Chanzo: salehjembe

JELA MAISHA KWA UBAKAJI

kana_mbakaji_512x288_bbc_nocredit_fc7c2.jpg
Johannes alikiri kumbaka Anene lakini alikanusha madai ya kumuua
Mwanamume mmoja nchini Afrika Kusini aliyepatikana na hatia ya ubakaji na mauaji ya msichana mwenye umri wa miaka 17 amepewa hukumu mbili za maisha jela na mahakama moja viungani mwa mji wa Cape Town.
Viongozi wa mashitaka walitaka mshukiwa Johannes Kana afungwe jela maisha bila dhamana.
Marehemu Anene Booysen alifariki mwezi Februari , masaa kadhaa baada ya kuuawa kinyama katika kesi ambayo imewaghadhabisha wengi.
Afrika Kusini ni nchi mojawapo yenye visa vingi vya ukatili wa kijinsia duniani.
Mwandishi wa BBC Nomsa Maseko aliyefika katika mahakama ya Swellendam, umbali wa kilomita 220 kutoka mji wa Cape Town, anasema kuwa mjombake Kana alishanga kwa kupiga makofi na hata kuangua kicheko jaji alipotoa uamuzi wake.
" Hiki ni kichekesho ," alisema huku akiongeza kuwa mfumo wa sheria hauna haki
Lakini wengi waliohudhuria kesi hiyo walihisi kama haki imetendeka
Bi Booysen alitendewa ukatili na mwili wake kutupwa karibu na nyumba yake Bredasdorp lakini alifariki baadaye hospitalini mjini Cape Town
Wakati huohuo, Rais Jacob Zuma alitaja mauaji hayo kama ya kushtua na ya kinyama.
Ametoa wito kwa majaji kutoa adhabu kali sana kwa wanaofanya vitendo vya uhalifu wa kijinsia.
Wakati wa kesi dhidi ya Kana, madaktari waliomtibu Bi Booysen walisema kuwa majereha aliyoyapata yalikuwa mabaya zaidi kwake kuwahi kuyashuhudia.
Kabla ya kifo chake alisema kuwa karibu wanaume watano au sita walihusika na shambulizi dhidi yake , lakini washukiwa watatu walikamatwa baadae ingawa ni mmoja tu aliyehukumiwa.
Kana alikiri kosa la ubakaji ingawa alikana kuwa alimuua.

Friday, November 01, 2013

YANGA SC YAIPIGA JKT 4-0


3_17e1c.jpg
Ngassa alifunga bao la kwanza kwa shuti kali la umbali wa mita 20, baada ya kufanikiwa kuwatoka mabeki wawili wa JKT Ruvu, wakati bao la pili alifunga kwa kichwa akiunganisha mpira wa kurushwa na beki Mbuyu Twite.
Pamoja na kumaliza dakika 45 za kwanza wakiwa nyuma kwa 2-0, lakini JKT Ruvu ndiyo waliocheza soka ya kuvutia ya pasi za hapa na pale, huku Yanga wakitumia mashambulizi ya haraka kwa mabeki kupeleka mipira pembeni, ambako mawinga wanatia krosi washambuliaji wagombanie goli.
Kipindi cha pili, Yanga SC waliendelea na staili yao kushambulia kutokea pembeni, huku JKT Ruvu wakionekana kuanza kupoteza mwelekeo na kutoa mwanya zaidi wa kushambuliwa.
Beki Oscar Joshua aliipatia Yanga bao la tatu dakika ya pili ya kipindi cha pili, akiunganisha kona maridadi iliyochongwa na kiungo Simon Msuva.

Kona hiyo ilitokana na kazi nzuri ya kipa wa JKT Ruvu, Sadick Mecks aliyepangua shuti kali la kiungo wa Yanga, Frank Domayo.

VIWANGO VIPYA VYA ALAMA ZA UFAULU ELIMU YA SEKONDARI HIVI HAPA.....!!!


a_97eff.jpg
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome akifafanua kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya upangaji wa viwango vya alama, matumizi ya alama endelevu ya mwanafunzi na ufaulu leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Kamishna wa Elimu Profesa Eustella Bhalasesa.
b_3754b.jpg
_ Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Sifuni Mchome (hayupo pichani).
c_5b2ab.jpg
Waandishi wa habari na maafisa wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome(hayupo pichani).
Picha zote na Eliphace Marwa (MAELEZO)
UPANGAJI WA VIWANGO VYA ALAMA, MATUMIZI YA ALAMA ENDELEVU YA MWANAFUNZI NA UFAULU
UTANGULIZI
Wizara imekusanya maoni ya Wadau wa Elimu kuhusu Upangaji wa Viwango vya Alama (Grade Ranges) katika Mitihani ya Kuhitimu Kidato cha Nne na cha Sita pamoja na Matumizi ya Alama za Tathmini Endelevu ya Mwanafunzi (Continuous Assessment ama CA) kwa ajili ya kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi.

MUGABE ANAWZA 'KUTUSIWA' AU KUKOSOLEWA

120927121136_mugabe_un_304x171_reuters_nocredit_35956.jpg
Mahakama ya kikatiba nchini Zimbabwe imebatilisha sheria inayosema kuwa ni uhalifu kumtusi Rais wa nchi.
''Viongozi wa mashitaka hawapaswi kuwa na tamaa sana ya kuwashitaki watu wanaomkosoa Rais Mugabe katika kumbi za ulevi na maeneo mengine ya kijamii,'' iliamua mahakama ya kikatiba.
Angalau watu 80 wameshitakiwa chini ya sheria hiyo katika miaka ya hivi karibuni.
Mnamo mwezi Mei, mwanaharakati Solomon Madzore alikamatwa baada ya kudaiwa kumuita Mugabe 'Punda anayechechemaa.'
Alikanusha kosa la kumtusi Rais.
Chini ya kifungu cha 33 cha sheria ya uhalifu nchini Zimbabwe, mtu anaweza kufungwa jela hadi mwaka mmoja au kutozwa faini ya dola 100 kwa kumtusi Rais.
Sheria hiyo ilipingwa na watu kadha nchini humo akiwemo mkaazi mmoja wa mji wa Bulawayo Kusini mwa nchi, Tendai Danga, aliyekamatwa miaka miwili iliyopita kwa madai ya kumtusi Mugabe wakati alipozozana na polisi ndani ya baa.
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC mjini Harare, Brian Hungwe, majaji tisa waliotoa uamuzi huo, walikubaliana kwa kauli moja kuwa sheria hiyo inahujumu uhuru wa kujieleza na kuifanya vigumu kwa serikali kukata rufaa dhidi ya uamuzi wao.
Hata hivyo, mahakama hiyo ilimpa waziri wa sheria, Emmerson Mnangagwa hadi tarehe 20 Novemba kukata rufaa.
Mwezi Agosti mahakama ilimwachilia huru mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 26 Takura Mufumisi, aliyeshitakiwa kwa kuwa na nia ya kutumia bango la karatasi lenye picha ya Mugabe kama karatasi ya kujipangusia chooni ndani ya baa moja.
Katika kura ya maamuzi iliyofanyika mwezi Machi, wananchi walipitisha katiba mpya ambayo inawapa uhuru zaidi wa kujieleza.
Watu wengi wamepongeza uamuzi wa mahakama wakiamini kuwa sheria ilikuwa imemlinda rais dhidi ya kukosolewa.

MAMA RWAKATARE ATENGWA NA MAKANISA KWASABABU YA KUFUNGISHA NDOA YA MBUNGE ALIYEOLEWA NA KIJANA MDOGO...!!!


MBUNGE wa Viti Maalumu, Mchungaji Getrude Rwakatare (CCM) wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Mikocheni B, jijini Dar es Salaam, ametengwa katika Ushirikiano wa Makanisa baada ya kanisa lake kulalamikiwa kufungisha ndoa inayodaiwa kukiuka taratibu za kikanisa, kisheria na kimaadili, Tanzania Daima Jumatano limejulishwa.Ndoa inayolalamikiwa kufungishwa na kanisa hilo ni ile iliyoibuliwa na gazeti hili wiki iliyopita ambayo inamhusisha Mbunge  wa Viti Maalumu, Rosweeter Kasikila (CCM) mwenye umri wa miaka 60 na kijana Michael Christian wa miaka  26.


Ndoa hiyo ambayo ilifungwa katika kanisa hilo Septemba Mosi mwaka 2011, imebaki kuwa gumzo na kuwaacha hoi baadhi ya mawaziri, wabunge pamoja na majirani wanaoishi jirani na mbunge huyo mjini Bagamoyo, Pwani.
Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili na Haki za Jamii ya makanisa hayo, Mchungaji William Mwamalanga, alisema uamuzi wa kulitenga kanisa la Mama Rwakatare umetokana na kikao cha Kamati ya Maadili iliyokutana jana jijiji Dar es Salaam.

LULU MICHAEL AMWAGA MATUSI YA NGUONI KATIKA MSIBA WA BABA YAKE WEMA SEPETU....!!!


  Elizabeth Michael ‘Lulu’.

MSANII nyota wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amejikuta akiporomosha mitusi mizito ya nguoni kwenye msiba wa baba wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, mzee Isaac Abraham Sepetu hali iliyowafanya baadhi ya waombolezaji kumkodolea macho ya mshangao.Tukio hilo lililotawaliwa na hasira lilijiri Oktoba 28, 2013 kwenye msiba huo uliokuwa ukiombolezwa nyumbani kwa marehemu, Sinza-Mori jijini Dar es Salaam.

KISA NA MKASA
Ilikuwa wakati Lulu akitinga msibani hapo, ghafla alimfuata mmoja wa waandishi wa habari hii na kuanza kumporomoshea matusi hayo kwa kile alichodai kukerwa na habari iliyowahi kuandikwa juu ya kitendo chake cha kula chakula sahani tatu katika hafla moja iliyofanyika hivi karibuni huko Kunduchi Beach Hotel, Dar.

TUJIKUMBUSHE KIDOGO
Katika tukio hilo la awali, Lulu alikuwa mmoja wa waalikwa wa harambee ya kuchangia kansa ya matiti kwa akina mama iliyofanyika kwenye hoteli hiyo.
Wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa ajili ya wachangiaji wote, Lulu alionekana akirudia kuchukua msosi kwa zaidi ya mara tatu (alikula sahani tatu).

TURUDI MSIBANI
Baadhi ya watu waliokuwa msibani hapo walimshangaa Lulu kwa kuporomosha matusi hayo ya nguoni wakati akijua kuwa yeye ni kioo cha jamii na baadhi ya maneno machafu aliyoyatamka hadharani hayaandikiki gazetini.

MSIKILIZE LULU
“Siwapendi nyinyi waandishi hasa wewe (akamtaja jina). ‘I don’t want your f**** story dude, go to hell with you’re f**** shit,” alisikika Lulu akitamka matusi hayo. (hatuwezi kuyatafsiri kwa sababu za kimaadili).

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...