Wednesday, November 06, 2013

UJUMBE MZITO WA LULU KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameliomba Bunge kurekebisha sheria za Magereza katika vikao vyao vinavyoendelea mjini Dodoma.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam juzi, Lulu alisema kutokana na kukaa huko kwa mwaka mmoja, ameona mambo mengi ambayo yanatakiwa kufanyiwa marekebisho.
“Unaweza ukamkuta mfungwa ana miaka zaidi ya 20 lakini hajawahi kufikishwa mahakamani wala kuulizwa chochote kutokana na kitu ambacho kimempeleka hapo, kiukweli hata kama ana makosa haiwezekani kumkalisha miaka yote hiyo pasipo kusikilizwa,” alisema.
Alisema yeye amekaa huko kwa muda mfupi lakini amepata shida sana kuyazoea mazingira hayo, kwani huwezi kuishi kama nyumbani, hivyo ni vizuri ukiwekwa utaratibu mtu anasomewa kesi yake kwa muda gani.
Lulu alilazimika kukaa gerezani kwa muda huo kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa nguli wa filamu nchini, Steven Kanumba, aliyefariki dunia nyumbani kwake Sinza Vatican Aprili 7, mwaka jana

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...