Tuesday, November 05, 2013

SULEIMAN ANAHITAJI MSAADA WETU AENDE INDIA KUTIBIWA

Wapendwa, Siku ya Leo haikuwa nyepesi kwangu na hata kwa mtoto Suleiman na familia yake, baada ya kupokea ujumbe rasmi kutoka kwa madakatri bingwa wa upasuaji wa Hospitali ya CCBRT kuwa Upasuaji huo HAUTAWEZEKANA kufanyika CCBRT kama tulivyojipa moyo mara ya kwanza.

LAKINI, wamekubali kutusaidia kupata hospitali nzuri nchini India kwa ajili ya kumsafirisha kijana Suleiman. Nguvu zenu zinahitajika sana kipindi hiki kigumu kwa familia hii. Tayari msamaria mwema ametoa tiketi moja ya kumsindikiza Suleiman India. Wapendwa, tushikamane, tunaweza. Hatua zinazofuata:
Kwanza kupata hospitali India.
Kufanya malipo
Kupata barua ya referral na kutafuta passport na visa ya Suleiman na msindikizaji Safari

CCBRT wataturudishia milioni 3 tulizolipa kama gharama za matibabu na tukijumlisha na pesa alizo nazo Imelda tuitakuwa tumebakiwa na shilingi milioni 6.2. Safari ni ndefu lakini msichoke.
Asanteni sana. Mola atuongoze. Amen

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...