Monday, October 14, 2013

AU YATAKA ICC IAHIRISHE KESI YA KENYATTA


131013212235_kenyattareuters_043c3.jpg
Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika uliofanyika Ehiopia umetaka mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC) huko The Hague icheleweshe kesi ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, iliyopangwa kuanza kusikilizwa Novemba mwaka huu.
AU pia wamekubaliana azimio linaloeleza kuwa hakuna kiongozi mkuu wa taifa la Afrika aliyeko madarakani atakayefikishwa katika mahakama hiyo.
Wakati viongozi wa Kenya na Sudan wakikabiliwa na kesi huko ICC, viongozi wa nchi za Afrika wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu kuwa mahakama hiyo inafanya upendeleo na kuwaonea kwa makusudi.
AU ilijadili uwezekano wa nchi wanachama kujitoa, lakini wazo hilo halikuungwa mkono kiasi cha kutosha.
Wanasiasa na wanadiplomasia waandamizi akiwemo aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan wamekosoa mpango wa kujitoa kutoka ICC. Tembelea jambotz8.blogspot.com kila siku.
Kucheleweshwa
Viongozi hao wa AU, waliokutana Addis Ababa, walikubaliana kuwawekea kinga ya kutoshitakiwa kiongozi yoyote wa taifa la Afrika.
Pia wameitaka Kenya iandike barua kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataiga kuomba ucheleweshwaji wa kesi katika mahakama ya ICC dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya jinai.

Sunday, October 13, 2013

UFO SARO BADO YUKO KATIKA CHUMBA CHA UPASUAJI MHIMBILI

IMG_0031Pichani chini baadhi ya Wafanyakazi wenzake na Ufo Saro kutoka IPP pamoja waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali wakiwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili ambako Ufo Saro ambaye mpaka sasa, yuko katika chumba cha upasuaji  baada ya kupigwa risasi na mchumba wake Anteri Mushi usiku wa kuamkia leo ambapo pia alimpiga mama mzazi wa Ufo Saro Anastazia Peter Saro miaka 59 aliyefariki hapohapo  na baadae kujipiga risasi mwenyewe na kufa hapohapo, Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo huko Mbezi Luisi 1 2Wafanyakazi hao wakibadilishana mawazo hapa na pale katika hospitali ya Muhimbili leo hii 3 4Picha Kwa Hisani ya Fullshangwe Blog

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 13, 2013

DSC 0092 7ee69
DSC 0093 41bc7

SINTOFAHAMU WAIZARA YA HABARI.....!!!


makala dca7a
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, jana alitoa taarifa kwa umma akieleza bayana kwamba yeye ndiye aliyeliruhusu gazeti hili kuendelea kutolewa kwa njia ya mtandao (online) na Gazeti la Rai kutolewa kila siku.
Makalla alitoa ufafanuzi huo muda mfupi baada ya Idara ya Habari-Maelezo kutoa taarifa kwamba Serikali imesikitishwa na Gazeti la Mwananchi na gazeti dada la Rai, Mtanzania kukiuka masharti ya adhabu walizopewa.
Septemba 27, mwaka huu Serikali iliyafungia Mwananchi kwa siku 14 na Mtanzania siku 90.
Wakati likianza kutumikia adhabu yake, Mwananchi ambalo tayari limemaliza kuitumikia, liliendelea kutoa taarifa kwenye tovuti yake wakati Kampuni ya New Habari (2006) Ltd ambayo inamiliki Mtanzania ilianza kuchapisha kila siku gazeti la Rai ambalo awali lilikuwa likichapishwa kila wiki.
Katika ufafanuzi wake alioutoa
jana Makalla alisema: "Nimelazimika kueleza haya baada ya taarifa mpya ya Idara ya Habari-Maelezo iliyohoji uhalali wa gazeti la Mwananchi kuwa online (mtandaoni) na gazeti la Rai kutoka kila siku, badala ya mara moja kwa wiki (Alhamisi)."

IVORY COAST WAIFUMUA SENEGAL 3-1 NA KUBISHA HODI KOMBE LA DUNIA

WASHAMBULIAJI Didier Drogba, Salomon Kalou na Gervinho wote wamefunga jana Ivory Coast ikiifumua 3-1 Senegal na kuongeza matumaini ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia mwakani.Drogba alifunga kwa penalti dakika ya tano, kabla ya winga wa zamani wa Arsenal, Gervinho kufunga la pili dakika tisa na baadaye kipindi cha pili Salomon Kalou akafunga la tatu mjini Abidjan.
article-2456451-18B3202400000578-136_634x423_49689.jpg
Tembo wauwaji: Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia ushindi wao leo
Sasa Ivory Coast watahitaji sare au kufungwa si zaidi ya wastani wa bao moja katika mchezo wa marudiano moja ili kujikatia tiketi ya Brazil mwakani. Seneal yenyewe itahitaji kushinda 2-0 tu nyumbani, ili kujihakikishia kurejea Fainali za Kombe la Dunia.
article-0-18B2FA6200000578-877_634x446_38bb0.jpg
Didier Drogba ameifungia Ivory Coast leo
article-2456451-18B3209700000578-178_634x453_e3f22.jpg
Salomon Kalou na Drogba walicheza pamoja Chelsea miaka kadhaa
article-2456451-18B3D49200000578-154_634x416_2ec82.jpg
Umefanya vizuri: Gervinho akizungumza na kocha Sabri Lamouchi baada ya mechi
Bao pekee la Senegal lilifungwa na Papiss Cisse dakika tano kabla ya filimbi ya mwisho.

Saturday, October 12, 2013

HUU NDIO UTARATIBU MPYA WA KUINGIA MLIMANI CITY BAADA YA KUTOKEA UVAMIZI WESTGATE

 
 Kijana akikaguliwa kwa umakini baada ya kutiliwa mashaka na walinzi wa Mlimani City leo mchana
 
 Mlinzi wa kike akiwasubilia wananwake watakaotaka kuingia kwenye jengo la mlimani city ili hawakague
Ukaguzi ukiendela
PICHA NA PAMOJAPURE/PAMOJA BLOG

STEWART ADAI SIMBA NA YANGA ZINABEBWA NA TFF


Hall1 1eb67
KOCHA Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amesema kwamba ni kazi ngumu Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kupata bingwa nje ya Simba na Yanga kwa sababu timu hizo zinapendelewa mno na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).



Akizungumza Hall amesema kwamba timu nyingine nje ya Simba na Yanga SC ili kuwa bingwa inabidi ifanye kazi ngumu sana ambayo kwa sasa yeye na timu yake, Azam FC wanajaribu.
Kwanza amesema ratiba ya Ligi Kuu inapopangwa inakuwa katika mazingira mazuri kwa timu hizo na mazingira magumu kwa timu nyingine ambazo zinaonekana zikitendewa haki zinaweza kuzima ubabe wa timu hizo katika soka ya Tanzania.
Stewart alitoa mfano hadi sasa katika mechi za Ligi Kuu ambazo tayari zimechezwa, Simba na Yanga kila moja imecheza mechi mbili tu ugenini, wakati Azam FC imecheza mechi sita ugenini, jambo ambalo amesema huwezi kulikuta katika ligi nyingine yoyote duniani.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI, OKTOBA 12, 2013

DSC 0092 59997
DSC 0093 e41e4

RIPOTI YA UN: YAIANIKA SERIKALI, YADAI WATANZANIA NI WATU WASIO NA FURAHA


saada_35554.jpg
Naibu waziri wa fedha, Saada Salum
Wakati Tanzania ikitajwa kuwa ni miongoni mwa nchi zenye amani na utulivu, imebainika kuwa Watanzania ni miongoni mwa watu wasio na furaha na waliokata tamaa hapa duniani.
Ripoti inayoonyesha orodha ya nchi zenye furaha duniani ya mwaka 2013 (World Happiness Report 2013), imeitaja Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi 10 za mwisho duniani kati ya nchi 156 zilizofanyiwa utafiti huo.
Ripoti hiyo iliyoandaliwa na kundi la wataalamu kutoka Umoja wa Mataifa (UN), kati ya mwaka 2010 na 2012, inaonyesha kuwa Tanzania imeshika nafasi ya 151 ikiburuta mkia pamoja na nchi za Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Benin na Togo.
Upatikanaji wa huduma za jamii, mtazamo wa watu kuhusu rushwa, umri wa kuishi, ukosefu wa kazi, pato la taifa na ukarimu wa watu katika nchi husika, ni baadhi ya vigezo vilivyoangaliwa wakati wa kuandaa taarifa hiyo.
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka alieleza kushtushwa na ripoti hiyo kwa maelezo kwamba ni asilimia 11.7 tu ya Watanzania wasio na ajira na kwamba wale wanaofanya kazi, wanapata huduma zote za msingi, ikiwa ni pamoja na kwenda likizo na mishahara inayolingana na taaluma zao.

GARI LA SERIKALI LAKAMTWA LIKITUMIKA KWENYE UTAPELI

2135728_orig_459dd.jpg
Jeshi la Polisi mkoani Temeke, linamshikilia dereva wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, aliyefahamika kwa jina la Bw. Samwel Mulagalazi, ambaye anadaiwa kushirikiana na watu wawili waliotaka kumtapeli mteja wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO), sh. milioni 60.
Tukio hilo limetokea juzi saa 11 jioni katika kiwanda kilichopo Mbagala, Dar es Salaam (jina tunalo), ambapo matapeli (vishoka), waliojifanya wafanyakazi wa TANESCO, Makao Makuu, Ubungo, walitaka kufanya utapeli huo kwa mmiliki wa kiwanda hicho.
Matapeli hao walimpigia simu mmiliki wa kiwanda hicho (jina tunalo), wakidai kiwanda chake kinaiba umeme hivyo walimtaka atoe sh. milioni 60 asiweze kukatiwa umeme.


Mmiliki huyo akitambua kuwa mita zake hazikuwa na tatizo lolote na hahusiki na wizi huo, aliwasiliana na Meneja wa TANESCO wilayani Temeke, Mhandisi Richard Mallamia na kumweleza vitisho alivyopewa na matapeli hao na pesa waliyotaka kupewa.

Friday, October 11, 2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 11, 2013

DSC 0059 cbb36
DSC 0060 33282DSC 0061 02d88

ICC: MAWAKILI WA KENYATTA WATAKA KESI IFUTWE


uhurukenyatta_b6263.jpg
Mawakili wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, wameitaka mahakama ya kimataifa ya jinai kusimamisha mashtaka ya Rais huyo kabla ya kesi yake kuanza mwezi ujao.
Wanasheria hao wamesema mashahidi wa utetezi wamekuwa wakitishwa, na kwamba wanao ushahidi wa kutosha kuthibitisha ukiukwaji wa taratibu za mahakama hiyo.
Rais Kenyatta na Naibu wake William Ruto, wanatuhumiwa kuchochea wimbi la vurugu za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.
Takriban watu1,200 walifariki na wengine laki sita kuachwa bila makao wakati wa ghasia hizo.
Kesi dhidi ya Kenyatta inatarajiwa kuanza tarehe 12 mwezi Novemba.
Naibu Rais pia yuko mbele ya mahakama hiyo na yeye ndiye afisaa mkuu wa kwanza wa serikali kufikishwa mbele ya mahakama ya ICC.
Mawakili wa Kenyatta waliwasilisha nyaraka za kurasa 38 siku ya Alhamisi kwenye mahakama hiyo wakiitaka kesi hiyo kutupiliwa mbali.
Nyaraka hizo zilisema kuwa upande wa utetezi una ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa mahakama imekua ikiendelea kukiuka taratibu zake.
Pia zilisema kuwa kuna ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa mashahidi wa upande wa mashitaka na mwengine mmoja walihusishwa na njama ya kutaka kuhujumu sheria.
Mawakili wa uetetzi aidha walituhumu upande wa mashitaka kwa kuwasilisha kesi ambayo ni ya kifisadi na sio ya haki dhidi ya Rais Kenyatta.
Upande wa mashitaka sasa unatarajiwa kujibu madai hayo na mahakama ya ICC huenda ikaamuru jopo la kusikilizwa kwa madai hayo kuyathibitisha.

"TUMETOKA KUFUNGONI NA HAMASA KUBWA".......... MWANANCHI

MwananchiKurudiClip_1a8e4.jpg
Hata hivyo, huu hakika sio wakati wa kumtafuta mchawi, kwa maana ya kutaka kujua nani hasa serikalini alitoa amri ya kulifungia gazeti hili kwa sababu ambazo sisi tunaona hazikuwa na chembe ya mashiko. Tulishangazwa kuona amri hiyo ya Serikali ikitolewa wakati mkuu wa nchi, Rais Jakaya Kikwete akiwa nje ya nchi, tena akiwa katika majukumu mazito ambayo dunia nzima ilikuwa ikiyafuatilia kwa shauku na umakini mkubwa.
Kulifungia gazeti wakati huo hatuoni kama ilikuwa kwa masilahi ya taifa kwa sababu hatua hiyo iliichafua taswira ya nchi yetu na bila shaka Rais Kikwete alijikuta katika wakati mgumu kila alipoulizwa kuhusu hatua hiyo iliyochukuliwa na Serikali yake.
Ni habari zipi zilizolipeleka gazeti hili kifungoni? Habari ya kwanza ilikuwa juu ya waraka kuhusu mishahara mipya ya watumishi wa Serikali ambayo tuliithibitisha pasipo kuacha shaka yoyote kutoka katika vyanzo vyetu vya habari vya kuaminika katika mamlaka za juu serikalini.

HOTUBA ZA BABA WA TAIFA SASA KUPATIKANA KIGANJANI

11_d1a97.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiki akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa huduma ya kupata hotuba za Marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika kwenye hotel ya Double Tree jana. Ili kuweza kupata hotuba za maneno na picha za video unatakiwa kutuma neno Hotuba kwenda namba 15678, pia unaweza kupata huduma hiyo kwa kutumia www.simu.tv/nyerere mobile tv. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Push Media Mobile Freddie Manento
22_c78fe.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Push Media Mobile, Freddie Manento (katikati) akifafanua jambo kuhusiana na mpango wa kumuenzi marehemu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kupata hotuba zake mbali mbali kwa njia ya simu ya mkononi. Kushoto ni msaidizi maalum wa mkurugenzi mtendaji wa Taasisi mwalimu Nyerere, Gallus Abedi na kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku.
33_5bf0a.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Push Media Mobile, Freddie Manento (kushoto) na Mkurugenzi wa Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku wakibadilisha mkataba mara baada ya kusainiwa katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya kupata hotuba za Marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika kwenye hotel ya Double Tree. Huduma hiyo inamwezesha mwananchi kupata hotuba mbali mbali mbali za marehemu Baba wa Taifa kwa kutuma neno Hotuba kwenda namba 15678. Pia unaweza kupata huduma hiyo kwa kutumiawww.simu.tv/nyerere mobile tv.

BARTON : FERGUSON ALIKUWA HANA UWEZO WA KUPANGA HATA KONI


joey-barton_2698492b_331ce.jpg
Kiungo mtukutu wa Queens Park Rangers Joey Barton ameibuka tena kwenye vichwa vya vyombo vya habari baada ya kudai kocha wa zamani wa Manchester Utd Sir Alex Ferguso hakuwa na uwezo wa kufundisha,
Barton alidai nchini England mameneja wanathaminiwa sana kuliko makocha.
'Sina maana ya kutomuheshimu Sir Alex Ferguson - alikuwa meneja mkubwa lakini hakuwa na uwezo wa kufundisha,
sidhani kama alikuwa na uwezo wa kupanga hata koni. Kuna tofauti kubwa kati ya kocha na meneja'.
Barton pia amesema hakubaliani na wazo la kuundwa kwa tume ya kutafuta njia bora ya kuendeleza soka nchini England.
Akizungumza katika kilele cha mkutano wa Viongozi wa vilabu (Leaders in Sports ) uliofanyika kwenye uwanja wa Stamford Bridge , alisema: 'Timu ya taifa ya England ni mbovu na haiwezi kufanya vizuri hata kama itafuzu fainali za kombe la dunia mwakani nchini Brazil.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...