Wednesday, July 10, 2013

KAMATI KUU YA CHADEMA YABARIKI FUJO MIKUTANONI .... WAANDAA "RED BRIGADE"

MUHTASARI
Ili kukabiliana na vitendo vya fujo vinavyofanywa na vijana wa CCM dhidi ya wagombea, Wanachama na viongozi wa CHADEMA, Kamati Kuu imeagiza kwamba kitengo cha ulinzi cha Chama “Red Brigade” kiimarishwe zaidi kwa kuhakikisha kuwa vijana wote wa Red Brigade Nchi nzima wanapewa mafunzo maalum ya UKAKAMAVU yatakayoandaliwa katika Makambi maalum katika mikoa yote.
RIPOTI KAMILI
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAAMUZI YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHAMA KILICHOFANYIKA TAREHE 06-07/07/2013 KATIKA HOTEL YA BLUE PEARL, DAR ES SALAAM.

Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo ilikutana katika Kikao cha dharura kuanzia tarehe 06-07/07/2013 katika Hotel ya Blue Pearl Dar es salaam kujadili pamoja na mambo mengine Rasimu ya Katiba mpya na hali ya Siasa nchini.

Kamati kuu imejadili na kuyatolea maamuzi mambo mbalimbali kama ifuatavyo:

1:0. Hali ya Siasa Nchini.

Kamati kuu imepokea taarifa ya hali ya siasa nchini na kuzingatia mambo yafuatayo:

a) Shambulio la Bomu Arusha.

 Kamati Kuu imesikitishwa na kulaani kwa nguvu zote tukio la Bomu Arusha lililosababisha watu wanne kuuwawa na zaidi ya watu 70 wengine kujeruhiwa vibaya.

KASEJA ANAWINDWA KILA KONA, USIKU NA MCHANA



KLABU za APR ya Rwanda na Gor Mahia ya Kenya zipo katika harakarti za kumwania aliyekuwa kipa namba moja wa timu ya Simba, Juma Kaseja, imefahamika.
Habari za uhakika ambazo Sports Lady Blog imezinyaka zinasema viongozi wa timu hizo wameshaanza mazungumzo na Kaseja ili kumsajili kwa msimu ujao katika nchi hizo.
 
Mdau mmoja wa soka ambaye yupo karibu na uongozi wa timu hizo, alidokeza jana kwamba, kwa nyakati viongozi wa timu hizo mbili, wamekuwa kwenye harakati za kumsaka Kaseja, wakiamini bado ni kipa mwenye uwezo mkubwa langoni.
 
Licha ya kutemwa kwenye kikosi cha Simba kwa msimu ujao, Kaseja bado kipa namba moja wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha wake Kim Poulsen, raia wa Denmark.
Habari zaidi zinasema, klabu ya APR iliyofika fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashabiki na Kati-Kagame Cup na kufungwa na Vital’o wiki moja iliyopira nchini Sudan, inapewa nafasi kubwa ya kumpata kipa huyo.
 
Hayo yanatokea huku Kaseja akiwa kwenye kambi ya timu ya Stars inayojiandaa na mechi ya kuwania tiketi ya Fainali za Afrika kwa Nyota wa Ndani –CHAN dhidi ya Uganda itakayopigwa Julai 13, Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
“Ujue baada ya Simba kutangaza kuachana na Kaseja, kuna timu nyingi hasa za nje zimeonesha nia ya kutaka kumsajili lakini mpaka sasa ni APR na Gor Mahia ndio wako makini zaidi na mchakato huo,” kilisema chanzo hicho.

HUYU NDIE MWIGIZAJI WA HOLLYWOOD ALIYEMTUKANA OBAMA NA MKE WAKE

amanda bynes obama ugly tweet

 
 
Anaitwa Amanda Bynes ni mwigizaji maarufu HoolyWood. Wiki chache zilizopita alikua katika vita ya maneno na msanii Rihana kupitia mtandao wa twitter, sasa vita hiyo kaihamishia kwa Raisi wa nchi yake Obama pamoja na mke wake.

Katika tweet aliyoandika jana alisema “Barack Obama and Michelle Obama are Ugly” na mda mchache tu baada ya kuandika hivyo watu walianza kumshambulia kwa kumwambia kua alichofanya si kitu kizuri kabisa. Pia katika kuonyesha kua watu hawamungi mkono wengi wa followers wake walimunfollow.


Hii si mara yake ya kwanza kuwaita watu weusi ugly kwani alishawahi kumuita na Drake jina hilo

MWANAMKE APEWA MIMBA NA MAITI, ALIJIFANYISHA MAPENZI WAKATI ANAMUOGESHA.


Mwanamke mmoja mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti ameushangaza ulimwengu kwa kitendo chake cha Kujilazimishia mapenzi kutoka kwa mwanaume ambaye amekufa hadi kufikia kupata Ujauzito.
Felicity Marmaduke (38), Mkazi wa Lexington Missouri, alikumbwa na mkasa huo baada ya kumtamani marehemu huyo wakati wa kumuosha na ndipo alipoamua kujiweka juu yake na kuanza kufanya naye mapenzi, cha kushangaza ni kwamba maiti hiyo iliweza kutoa mbegu za kiume.

Baada ya wiki mbili, mwanamke huyo alienda kujipima ujauzito baada ya kujihisi tofauti na ndipo alipogundua ya kwamba ameshika mimba.
Ilimbidi atoe taarifa kwa familia husika ambayo ilimfungulia mashataka kwa kitendo chake hata hivyo naye amefungua mashtaka akidai iuzwe moja ya nyumba ya marehemu huyo ili alipwe gharama za matunzo.

MCHUNGAJI AKAMATWA KWA KOSA LA KUUPINGA USHOGA NA USAGAJI.



Tonny Miano ni Mchungaji kutoka nchini mMarekani ambaye alikwenda Nchini Uingereza katika Kufanya Mahubiri Huko. Kilichomkuta kilisababishwa na yeye kusema ya kwamba tabia za kishoga na kisagaji ni Dhambi na hazimvutii Mungu,.


Polisi walipigiwa simu na mwanamke mmoja aliyekuwa eneo la tukio akilalamika ya kwamba hajafurahishwa na maneno anayoongea Tonny, ambaye ni askari mstaafu wa jeshi la polisi nchini Marekani.

Tuesday, July 09, 2013

MBONA MAJANGAAA....!!! AGNESS MASOGANGE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AFRIKA KUSINI

 

HATIMAYE  wale Wanawake wawili walionaswa  na  madawa ya  kulevya  Afrika  kusini wametambuliwa kuwa  ni  mabinti  wa  KITANZANIA ..
Mabinti  hao  wanadaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevya zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania.
Akizungumza na mwandishi wetu  jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.
Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Jerald (MASOGANGE)  ambaye alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24. Wawili hao bado wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.

CHELSEA WAANDAA DAU LA JUU ZAIDI KUMSAJILI ROONEY....!!!



Target: Chelsea are set to launch a bid for Wayne Rooney despite David Moyes saying he is not for saleAnasakwa vibaya sana: Chelsea wameamua kutuma ofa kwa David Moyes ingawa alitangaza kuwa hafanya biashara, lakini wakali hao wa darajani wanamhitaji jembe  Wayne Roonye

Will he stay or will he go? Rooney's future at Manchester United has been debated this summerAtabaki au ataondoka? Maisha ya baadaye ya Rooney katika klabu yake ya  Manchester United bado hayajulikani

New man in charge: David Moyes says he does not want to sell RooneyKocha mpya wa United: David Moyes amesema hamuuzi Rooney kwa sasa

Welcome back, Jose: Frank Lampard and John Terry will be pleased to see the return of Mourinho to Chelsea Karibu tena Jose: Malejendari, Frank Lampard na John Terry wamefurahi kuona ujio wa Mourinho katika klau yao ya Chelsea

WAKATI MZEE MANDELA AKIENDELEA KUPATA MATIBABU FAMILIA YAKE WAZIDI KUTIBUANA



Mandla Mandela aendelea kulikoroga
WAKATI mgogoro kati ya watoto wa Mandela na wajukuu ukizidi kutokota kuhusu uhalali wa uchifu wa Mandla Mandela, yeye amejibu mapigo akisema Mfalme Buyelekhaya Dalindyebo wa kabila la abaThembu ”hana akili timamu”.
Hiyo inatokana na madai yaliyotolewa na mfalme huyo kwamba Mandla hakuwa chifu sahihi wa ukoo wa Madiba. Alidai kwamba hakukuwa na cheti chochote halali kilichotiwa saini wakati mandla alipotawazwa kuwa chifu mwaka 2007 – sherehe ambazo zilisimamiwa na Mandela mwenyewe.
Gazeti la Mail & Guardian wiki iliyopita liliripoti kuwa uchifu wa Mandla ulilalamikiwa kabla ya Mandela kulazwa hospitalini, ikielezwa kama kweli anafaa kuendelea kuwa chofu ikizingatiwa kuwa mama na baba yake walimzaa bila kuoana.
Mgogoro unaoendelea hivi sasa kati ya Manla na shangazio yake, Makaziwe Mandela, na wanafamilia wengine unaonekana kama kichocheo kwa baadhi ya wanafamilia hiyo ambao wangetaka Mandla avuliwe uchifu.

WEMA SEPETU ANASAKWA NA POLISI BAADA YA KUMTUKANA MENEJA WA HOTELI WAKATI YUKO POMBE...!!!



Msanii wa filamu za Bongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu anasakwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, Dar es Salaam kwa tuhuma za kufanya fujo hotelini, kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga makofi meneja wa hoteli hiyo, Godluck Kuyumbu. Songombingo hilo lilijiri saa tano usiku wa Jumatano iliyopita kwenye hoteli hiyo  iliyopo Kawe Beach, jijini Dar. 
Akizungumza na mwandishi wetu , meneja huyo alisema siku ya tukio majira ya saa nane mchana, Wema alifika kwenye mgahawa wa hoteli hiyo akiwa ameongozana na marafiki zake wapatao kumi.


Meneja huyo akaendelea kusema, ilipofika  saa tano usiku, Wema na marafiki zake  walionekana kuzidiwa na kilevi, wakaanza kufanya fujo kwa kupiga kelele, kitendo kilichowakera wateja waliokuwa katika mgahawa huo, wengi wakiwa ni Wazungu ambao waliondoka kutokana na fujo hizo. 


Aliongeza kuwa mmoja wa marafiki wa Wema ambaye ilidaiwa ni mpenzi wake, aliyejulikana kwa jina moja la D, alichukua glasi na kuipasua chini kwa makusudi huku meneja huyo akishuhudia.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Akutana na Waandishi Wa Habari Nakutoa maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.


  
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake.
 Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya wakimsikiliza mkuu wa mkoa Mbeya akiongea na waandishi wa habari.Picha na Habari na Mdau Joseph Mwaisango
--
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya hatimaye yatoa ufafanuzi na kupigilia Msumari maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 10, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

"NGUVU YA UMMA" INAVYOGHARIMU UHAI WA WAMISRI...!!!


 

Miili  ya wafuasi  wa Rais  aliyeondolewa madarakani nchini Misri ikiwa imehifadhiwa
 


 
MAAFISA wa Afya Misri wamesema takriban watu 42 wameuawa kwa kupigwa risasi mjini Cairo nje ya kambi ya kijeshi ambapo wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi walikua wamekusanyika na wanaamini anazuiliwa hapo. Watu wengine 300 wamejeruhiwa.

Kundi la Muslima Brotherhood limewataka raia wa Misri kuwapinga wale linawaita wanaopokonya raia uhuru na demokrasia.

Brotherhood imelaumu jeshi kwa kuwaua raia wake.
Katika kikao na waandishi wa habari, wafuasi hao walimlaani vikali mkuu wa jeshi Abdel Fattah Al-Sisi na kumtaja kama muuaji aliyewashambulia raia wenzake.

Haya yanajiri huku ghasia zikiendelea baada ya kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa rais Mohammed Morsi.

NDEGE YA RAIS WA SOMALIA 'YASHIKA MOTO'

somali f9f1f
Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mahamud
*******
NDEGE iliyokuwa inambeba rais wa Somalia, imelazimika kutua kwa dharura mjini Mogadishu baada ya moja ya mabawa yake kushika moto. (HM)
Msemaji wa Hassan Sheikh Mohamud, alisema kuwa haijulikani kwa nini injini ya ndege ilisita kufanya kazi.
 
Rais Hassan Sheikh Mohamud, alielezea kuwa rais hakujeruhiwa lakini wazima moto walifanya kila hali kuzima moto huo.
Bwana Mohamud alichaguliwa kama rais wa Somalia mwaka jana katika mpango ulioungwa mkono na Umoja wa Mataifa, katika hatua za kumaliza vita vya miaka mingi.
Mwandishi wa BBC Mohamed Mwalimu, alisema kuwa magurugumu ya ndege yaliharibiwa vibaya baada ya tukio hilo.

Rais alikuwa anaelekea katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba, wakati ndege hiyo ilipolazimika kurejea Mogadishu.
Moja ya ripoti zilizotolewa za mwanzo kuhusu tukio hilo, ilitoka kwa akaunti ya Twitter ya kundi la al-Shabab lakini haikusema kama imeshambulia ndege hiyo.

 
Wanajeshi wa Muungano wa Afrika pamoja na wale wa Somalia, wanaounga mkono bwana Mohamud wamewaondoa wapiganaji wa al-Shabab kutoka mji mkuu Mogadishu, mwaka jana ingawa kundi hilo bado hufanya mashambulizi ya mara kwa mara ya kuvizia.
Serikali mpya ni ya kwanza kwa zaidi ya miaka 10 kutambuliwa na serikali ya Marekani na shirika la fedha duniani (IMF). 

Chanzo: bbcswahili

HILI NDILO GHETTO LA DIAMOND THE PLATNUMZ...!!!

Photo by diamondplatnumz
Photo by diamondplatnumz


Monday, July 08, 2013

RAIS WA ZANZIBAR DK. ALI MOHAMED SHEIN AWAASA WAISLAMU NCHINI

 

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein amewataka Waislamu wote nchini kuishi na Watanzania wenzao katika misingi ya kuheshimiana, kuvumiliana na kupendana, kama Uislamu ulivyofundisha.

Dk Shein aliyasema hayo jana katika ufunguzi wa msikiti wa Masjid Taqwa, uliopo Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam, katika hotuba ilyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Mwinyihaji MakameKatika hotuba hiyo ya ufunguzi wa msikiti huo, Dk Shein alisema kuwa ni wajibu kwa Waislamu kufanya kila jitihada katika kuilinda amani na utulivu alioubariki Mwenyezi Mungu hapa Tanzania. 

Alisema kuwa kuna kila sababu kwa Waislamu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba wanaweza kufanya ibada zao katika mkusanyiko mkubwa kama huo wa ufunguzi wa msikiti bila ya hofu, woga wala bughudha ya namna yoyote.Dk Shein alipongeza jitihada zinazochukuliwa na wasimamizi wa msikiti huo katika kuimarisha na kuitunza historia yake tangu ulipoanzishwa mnamo mwaka 1927, ambapo historia hiyo inadhihirisha kuwa msikiti huo ni miongoni mwa misikiti mikongwe katika Jiji la Dar es Salaam.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...