Tuesday, July 09, 2013

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Akutana na Waandishi Wa Habari Nakutoa maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.


  
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake.
 Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya wakimsikiliza mkuu wa mkoa Mbeya akiongea na waandishi wa habari.Picha na Habari na Mdau Joseph Mwaisango
--
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya hatimaye yatoa ufafanuzi na kupigilia Msumari maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.
             
Akitoa maamuzi ya Kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake  amesema Kamati  imeridhika na ushauri uliotolewa na Kamati ya Ushauri iliyofanyika Julai 4, Mwaka huu.

Kandoro amesema lengo la kukutana na kamati ya ulinzi na usalama ni kutokana na kuibuka kwa maneno toka kwa baadhi ya Wananchi ambao wanadai maamuzi yaliyotolewa na Kamati ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa Mpya Mkwajuni Wilayani Chunya hayakuzingatia vigezo vya umbali wa baadhi ya maeneo.

Amesema katika kuliletea ufafanuzi jambo hilo Mkuu huyo wa Mkoa alidai kuwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya Ushauri wakiwemo Wakurugenzi wa Halmashauri na Wenyeviti wao wameitwa ili kutoa maelezo kwenye kamati ya Ulinzi kama endapo mapendekezo yaliyotolewa na RCC hayakuzingatia matakwa ya wananchi.

Ameongeza kuwa baada ya Kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa kuridhika na maelezo ya wajumbe hao imebariki na kuamua kuwa mapendekezo ya Kamati ya Ushauri yabaki vile vile kwa Mkoa mpya kuwa Songwe inayotokana na Mto Songwe uliopita kila Wilaya zinazounda Mkoa huo ambazo ni Momba, Mbozi, Chunya na Ileje.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...