Saturday, June 22, 2013

HATIMAE NDUGU YETU MPENDWA CHARLES HILILA AZIKWA LEO KIJIJINI KWAO



 

 NYUMBA YA MILELE ALIMOLALA MWANDISHI WA HABARI KITUO CHA MATANGAZO CHA CHANELL TEN

Habari Na Steven Kanyeph
Mwili wa aliyekuwa mwandishi wa habari wa chaneli ten Charles hilila umezikwa leo katika makaburi ya nyumbani kwao katika kijiji cha Dumida kata ya Tinde mkoani Shinyanga nakuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji akiwemo mkuu wa mkoa wa shinyanga na viongozi wengine wa kiserikali , vyama vya siasa pamoja na viongozi wa kidini.

Mazishi hayo yametanguliwa na ibada ya misa takatifu iliofanyika katika kanisa la mama mwenye huruma Ngokolo mjini Shinyangsa na baade kufuatiwa na ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwao na kuongozwa na padre Emmanueli Makolo akisaidiana na padri Josephati Mahalu kabla ya maziko.
katika mahubiri padre Mahalu amewaasa wanajamii kudumisha upendo na kuwakumbusha kuwa kifo kipo mahali popote hivyo wanajamii wanapaswa kumrudia Mungu na kutenda matendo mazuri yenye kuleta amani na yanayompendeza Mungu.


Hali kadhalika mkuu wa mkoa wa Shinyanga Alli Nassoro Lufunga ametoa salamu za rambirambi kutoka katika serikali ya mkoa na kuwaomba wanahabari kudumisha upendo zaidi hasa katika umojawao kwani utawasaidia kufanya kazi kwa weledi na kuleta tija zaidi kwa wanajamii.
Marehemu Charles hilila amefariki juni 19 katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa TB ya mifupa uliokuwa unamsumbua .
Aidha marehemu ameacha mjane na watoto watatu ,
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema mbinguni amina

*********************************************************************************


 

MEYA AZIMIA BAADA YA KUPIGWA NA POLISI

Meya wa Mji Mkuu wa Kampala nchini Uganda akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukamatwa kwa tuhumza za kusababisha vurugu.

Kampala, Uganda. Watu wawili wameuawa kwa risasi nchini Uganda juzi, wakiwa katika mkusanyiko kwenye eneo la soko la Kisekka.

Meya wa mji mkuu wa Uganda, Kampala, Erias Lukwago, pia alizirai baada ya kupigwa na polisi hao waliofyatua risasi za mipira kuutawanya umati wa wafuasi wake.

Akiwa kitandani, Meya huyo amesema baada ya kupata kipigo hicho alipoteza fahamu na kukimbizwa hospitalini.

“Bomu ambalo lilinifanya nipoteze fahamu lilirushwa katika gari langu na kuingia ndani,” amesema.


Meya huyo ni mpinzani wa rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni, alieleza kwamba maofisa wa polisi walimpiga kifuani na kuzirarua nguo zake wakimtuhumu kwa kuchochea ghasia. 

NKAMIA AZUA VURUGU TENA BUNGENI SAFARI HII ATAKA KUMPIGA MBUNGE MWENZAKE...!!!

1625 cb219Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM), kwa mara nyingine ameingia katika kashfa nzito akituhumiwa kutaka kumpiga Mbunge wa Viti Maalumu CUF, Moza Abeid ndani ya Ukumbi wa Bunge.

Tukio hilo lilitokea mwanzoni mwa wiki ambapo imeelezwa kuwa Nkamia mbali na kutaka kumpiga mbunge huyo, pia alimtolea matusi mazito ya nguoni (gazeti hili haliwezi kuandika).

Kwa mara ya kwanza mbunge huyo aliingia katika kashfa baada ya kutoa kauli bungeni kuwa hazungumzi na mbwa, bali anazungumza na mwenye mbwa kabla ya kuingia katika mzozo na wahariri na baraza la habari aliposema kuwa Jukwaa la Wahariri na Baraza la Habari ni NGOs za kutafuta fedha.

Uchunguzi wa Mwananchi ambao umethibitishwa na Nkamia mwenyewe umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni kutokana na kuzomewa kwa Nkamia katika kampeni za uchaguzi mdogo Kata ya Dalai Wilaya ya Chemba.

Kwa mujibu wa wabunge mashuhuda ambao waliliona tukio hilo, ilielezwa kuwa Nkamia, ambaye pia ni mwandishi wa habari, alianza kumshushia matusi Moza wakiwa ndani ya Bunge hadi walipotoka nje alimfuata na kutaka kumpiga.

MCHUNGAJI AZAA NA HAUSIGELI WA MIAKA 17 HUKO KIMARA....AVULIWA UCHUNGAJI, MKEWE AOMBA TALAKA...!!!

HAYA ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.

Akizungumza nasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.


MATESO YAANZA
Mwanamke huyo alidai amani katika ndoa yake ilipotea baada ya kujifungua mtoto wa pili (marehemu), mumewe alianza kumtuhumu kuwa alitoka nje ya ndoa na huyo mtoto hakuwa wake.

MIMBA YA PENNY YACHOROPOKA..... PENZI LAKE NA DIAMOND LAKAA PABAYA...!!!

TAARIFA ya ndani zinazodai kwamba, mimba ya mchumba wa Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nassibu Abdul ‘Diamond’, Peniel Mgilwa ‘Penny’ imechoropoka zimevujaKwa mujibu wa chanzo makini kilichojitambulisha kwa jina la wifi (jina kapuni) kwa Penny, ni kwamba mtangazaji huyo wa Runinga ya Channel 10 cha jijini Dar hivi sasa  hana ujauzito tena kama wengi wanavyodhani.
“Penny hana mimba jamani, yupo fiti kabisa na sidhani hata kama anatarajia kushika ujauzito leo wala kesho,” kilisema chanzo hicho.
 
Hata hivyo, wifi huyo alisema kwamba awali kulikuwa na dalili zilizoonesha kwamba Penny alikuwa ni mjamzito kutokana na mtangazaji huyo kutumia vitu vichachu kama vile maembe na mara kwa mara alikuwa akiumwa hadi kufikia kulazwa hospitali.
Inadaiwa kwamba Penny alipotoka hospitali alionekana kuwa fiti zaidi na hakuwa na dalili zozote za kuwa na ujauzito kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Baada ya gazeti hili kupata habari hizo lililimpigia simu Penny ili kuthibitisha madai hayo:
Mwandishi: Mambo vipi, Penny pole sana.
Penny: Pole ya nini sasa?
Mwandishi: Si nimesikia kwamba unaumwa jamani na ukakumbwa na mkasa mwingine?
Penny: Mkasa gani huo unaousema maana mimi niko fiti tu.
Mwandishi: Nilisikia kwamba baada ya kuumwa na kulazwa hopsitali mimba yako ikatoka?
Penny: (Kimya kwa dakika 3) Asante ni mipango ya Mungu.
Mwandishi: Sasa unatarajia lini utapata tena mimba nyingine?
Penny :(Kwachuuuuuu). Simu ilikatwa na hata ilipokuwa ikipigwa tena haikuwa ikipokelewa.

ANGALIA PICHA ZA BOB JUNIOR AKIPEWA KICHAPO LOCATION...!!!


Bob Junior ameshare picha hizi kwenye ukurasa wake wa Facebook na kuandika: Kwa Dizaini hii lazima nirudi kwetu k…Aaaaah Maisha Haya Ya Bongo?,,,,COMING SOON Huu Mzigo…1 Love.


Bob Junior akiwa location kushoot video yake mpya, duuuuuuh...!!! kaaazi kweli kwelii

BOMU LA ARUSHA LAWATESA CCM, POLISI.

 
IGP SAIDI MWEMA. 
KATIBU MKUU MPYA WA CCM ABDULRAHMAN KINANA.

MLIPUKO wa bomu uliotokea wiki iliyopita katika mkutano wa kufunga kampeni za udiwani kwa CHADEMA mkoani Arusha na kuua watu wanne, umeiweka kwenye wakati mgumu serikali ya CCM, Jeshi la Polisi na Bunge.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema juzi bomu lililolipuliwa katika mkutano wa CHADEMA ni la kijeshi na limetengenezwa China na uzoefu unaonesha hutumiwa na wanajeshi kujihami wakiwa katika makabiliano na maadui vitani.

Wakati Pinda akitoa kauli hiyo bungeni, viongozi wa CHADEMA wamelihusisha Jeshi la Polisi na tukio hilo huku wakidai wanao ushahidi unaon
esha askari aliyevalia sare akilirusha kwenye mkutano huo.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kijamii, wamelidokeza Tanzania Daima kuwa kukiri kwa serikali kuwa bomu hilo limetengenezwa China, inapaswa iibane nchi hiyo ieleze iliyemuuzia na alivyoliingiza nchini.

“Kwanini isiundwe tume huru nchini ili nchi ya China iulizwe baada ya kutengeneza bomu hilo ilimuuzia nani? Na kama haikuiuzia serikali, basi ni dhahiri tuiulize China kwanini inafadhili vikundi vya kigaidi nchini kwetu ?.

NASSARI: WAZIRI MKUU MSTAFU EDWARD LOWASSA ANAHUSIKA KUNIPIGA.

 
Mbunge wa Arumeru Mashariki(Chadema) Joshua Nassari akiwa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi), jana, baada ya kuhamishwa kutoka Arusha kwa ajili ya kupata matibabu zaidi baada ya kuumizwa kwenye vurugu za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Makuyuni mkoani Arusha.Picha na Silvan Kiwale.


DAR ES SALAAM.
MBUNGE wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amemtuhumu Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kwamba anahusika na kipigo alichokipata kutokana na chuki aliyonayo kwake.

Aidha amemtuhumu Spika wa Bunge, Anne Makinda kwamba naye ni miongoni mwa watu wanaomchukia pamoja na viongozi wengine wa Bunge, kwa kuwa hakuna kati yao aliyempigia simu au kumtumia ujumbe wa kumjulia hali kutokana na kipigo alichopata ambacho kimemsababishia maumivu makali.

Akizungumza jana akiwa kwenye chumba alicholazwa katika Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa na Ufahamu Muhimbili (Moi), Nassari alidai Lowassa ambaye amewahi kuwa waziri mkuu kabla ya kujiuzulu, amemchukia tangu alipomshinda mkwewe Sioi Sumari, kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika Aprili mwaka jana.

Nassari aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Selian ya jijini Arusha kabla ya kuhamishiwa MOI, alidai kupigwa na kuchaniwa nguo na Green Guard wakati alipokuwa katika jitihada zake za kuhesabu kura kwenye uchaguzi wa udiwani wa Kata ya Makuyuni-Monduli.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNE 22, 2013

Friday, June 21, 2013

Mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari Anendelea Vyema na Matibabu katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam

 Mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari akionesha simu yake ya mkononi iliyokuwa na matukio ya tukio la kufavamiwa kwake.
 Mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari akiwa katika hospitali ya Taifa muhimbili jijini Dar es Salaam jana akipata matibabu baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana wakati wa mkutano wa kampeni za udiwani jijini Arusha.
Mbunge wa Vunjo-TLP, Mh. Agustino Lyatonga Mrema akimjulia hali mbunge wa Arumeru Mashariki-Chadema, Joshua Nassari.

HII NDIO HISTORIA YA MWANDISHI WA HABARI WA CHANNEL TEN ALIYEFARIKI DUNIAI JUZI

Marehemu CHARLES HILILA 

Na Mwandishi Wetu Steven Kanyeph
Mwili wa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha matangazo cha television cha chanel ten mkoani Shinyanga, CHARLES HILILA unatarajiwa kuzikwa kesho katika kijiji cha tinde alikozaliwa.
Mazishi hayo yatatanguliwa na ibada itayofanyika katika kanisa la mama mwenye huruma la ngokolo mjini shinyanga, ibada inayotarajiwa kufanyika saa nne kamili asubuhi ambayo itakwenda sambamba zoezi la kuaga mwili wa marehemu.

Taarifa kutoka familia ya marehemu HILILA zinasema kuwa baada ya ibada ya mazishi msafara utaelekea katika kijiji cha tinde kwaajiri ya mazishi. Marehemu CHARLES HILILA alizaliwa tarehe 15 mwezi wa 9 mwaka 1964 katika kijiji cha tinde mkoani shinyanga na ni mtoto wa tatu kati ya watoto wanne katika familia ya bwana na bibi BARTHOROMEO HILILA wa kijiji cha mishepo-mwamtini wilaya ya shinyanga.

SERIKALI YA MKOA WA SHINYANGA YATOA TAKWIMU YA UFAULU KWA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI

Afisa elimu mkoa wa Shinyanga Bi. Eva M. Lopa
Na Steven Kanyeph
Afisa elimu mkoa wa Shinyanga Bi. Eva M. Lopa ametoa takwimu ya ufaulu kwa elimu ya msingi na sekondari kwa muda wa miaka mitatu kwa mkoa wa shinyanga katika kikao cha taarifa ya elimu kwa mkoa wa Shinyanga kilichofanyika katika ukumbi wa Mkoa uliopo mkoani Shinyanga , siku ya jana.

Akitoa takwimu hizo kwa elimu ya msingi Bi. Lopa amesema kuwa matokeo ya elimu ya msingi yamekuwa ya yakipanda mwaka hadi mwaka , na kwa mwaka 2010 yalikuwa ni asilimia 42.5 wakati mwaka 2009 yalikuwa asilimia 31.9 mwaka 2011 matokeo yalikuwa asilimia 44.2 hivyo kuwepo na ongezeko la asilimia 1.7% kwa mwaka 2009 hadi 2011 wakati mwaka 2012 wanafunzi waliofauru ni asilimia 56.1% sawa na ong ezeko la asilimia 11.9

Afisa elimu huyo ameainisha sababu zilizopelekea ongezeko la ufaulu huo kwa mwaka 2012 kwa elimu ya msingi kwa mkoa wa Shinyanga kuwa ni pamoja na ufuatiliaji wa karibu wa viongozi wa elimu ngazi za wilaya na mkoa , ufuatiliaji wa ufundisha ji, ongezeko la walimu kutoka uwiano wa 1.74 hadi 1.54 na ongezeko la vitabu kwa wanafunzi kutoka uwiano wa f1.6 hadi 1.4

RAIS MSTAAFU WA MAREKANI GEORGE W BUSH KUTUA JIJINI DAR ES SALAAM MWEZI UJAO..!!

 
Rais mstaafu wa Marekani, George W. Bush na mkewe, Laura, wanatarajiwa kuwasili nchini mwezi ujao ambapo watahutubia kongamano litakalojadili wajibu wa wake za marais katika kuinua wanawake duniani.
Taasisi ya George Bush  ndiyo imeandaa kongamano  hilo litakalofanyika Dar es Salaam kuanzia Julai 2 hadi 3.
Taarifa iliyotolewa jana na taasisi hiyo kwa vyombo vya habari, ilisema kongamano hilo, litahudhuriwa pia na mke wa Rais Barack Obama wa Marekani, Michelle na  muasisi wa Taasisi ya Wanawake ya Cherie, Cherie Blair ambaye ni mke wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair. 


 Wake wengine wa marais wa Afrika watakaohudhuria ni Mama Salma Kikwete, Chantal Campaore wa Burkina Faso, Roman Tesfaye wa Ethiopia, Maria da Luz Dai Guebuza (Msumbiji),  Penehupifo Pohamba (Namibia), Sia Nyama Koroma (Sierra Leone), Janet Museveni (Uganda) na Christine Kaseba wa Zambia.
Kongamano hilo litajikita zaidi katika kujadili masuala ya kuwekeza kwa wake, kuimarisha Afrika lakini pia wajibu wa wake za marais  kuhamasisha wanawake katika maeneo ya elimu, afya na kuwakwamua kiuchumi.

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU UDSM APIGWA RISASI YA TUMBO USIKU WA KUAMKIA LEO HUKO YOMBO..!!


Taarifa zilizotufikia katika chumba cha habari zinaeleza kuwa wanafunzi wanne wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo maeneo ya Yombo chuoni hapo.
Wanafunzi hao wanaosemekana kuwa ni wa mwaka wa nne na wa mwisho wa masomo walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo, wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha,  na majambazi kuanza safari yao.

Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.


AUNTY LULU..... "MAZISHI YANGU WATAJAA MASHOGA NA WATOTO TU"

MSANII wa filamu Bongo, Lulu Mathias ‘Aunty Lulu’ amefunguka kuwa siku akifa anaamini mbali na watu wengine mazishi yake yatatawaliwa na mashoga pamoja na watoto
 
 

Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Aunty Lulu alisema kutokana na ukweli kwamba wengi wanaompenda na ambao wamemzoea ni watoto waliokuwa wakimsikiliza kwenye Kipindi cha Watoto Shoo kupitia Radio One na ITV na mashoga ambao awali alikuwa kama mama yao, hao ndiyo watakaojaa kwenye mazishi yake.
Alisema sababu kubwa ya msiba wake kujaa mashoga wengi ni kwa kuwa kabla hajabadili mfumo wa maisha anayoishi sasa, alikuwa akiwalea hivyo siku ya mazishi lazima wakumbuke fadhila.
“Unajua kufa ni kama kulala, naamini siku ya mazishi yangu watakaokuwa wengi ni watoto pamoja na mashoga ambao zamani nilikuwa mama yao, wengine ni waandishi na wasanii mbalimbali wa filamu na muziki,”alisema Aunty Lulu.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...