Friday, June 07, 2013

NGONO ZAANZA KUTAWALA JUMBA LA BIG BROTHER.....VIDEO YA BOLT NA BETTY YANASWA WAKIFANYA MAPENZI LIVE


Mpaka sasa tayari tumeshuhudia couple 4 za housemates katika Big Brother ‘The chase’ , lakini couple ya mu Ethiopia Betty na mu Sierra Leon Bolt ndio ilikuwa ya kwanza kufahamika katika wiki ya kwanza toka mchezo uanze (May 26).


bolt & betty


Couple ya Bolt na Betty ndio ilikuwa ya kwanza pia ku’kiss kama uthibitisho wa ‘love at first sight’. Baada ya hapo maisha ya mjengoni yaliendelea vizuri huku mapenzi ya ‘love birds’ hawa yakizidi kukua kila kukicha japo waliamua kupeleka mambo taratibu.


Lakini wiki hii inaonekana kiu ya toka (May 26) iliwakaba ‘love birds’ hawa na kuamua kuikata kwa kufanya kile wanachofanya wapenzi wanapokuwa faragha (watu wazima naamini mnanielewa) yes , they did it! Bolt iliifunga nut ya Betty usiku wa manane wakati washiriki wenzao wakiwa wamelala!!


Ikiwa ni sehemu ya kujaribu kuyaokoa mapenzi yao, wiki hii baada ya Betty kutwaa ukuu wa Diamond House (HOH) aliweza kupata mamlaka ya kumuokoa mshiriki yeyote anayekuwa ameingia kikaangoni. 
Hivyo aliitumia nafasi hiyo kuliokoa penzi lake kwa kumuokoa Bolt ambaye alikuwa amependekezwa kuingia kikaangoni, na kumchagua Feza Kessy wa Tanzania aingie kikaangoni badala ya kipenzi chake.


video  mbili  za  uchafu wao...


video
video

TANGAZO KWA WAKAZI WA MBEYA

Nafasi za Kazi na Mafunzo

SIFA:


>>> Elimu ya kidato cha nne au zaidi.
>>> Taaluma ya uandishi wa habari ni added advantage.
>>> Uwezo, ufahamu, utundu, uzoefu, na ujuzi katika matumizi ya "Mitandao ya Kijamii" ndio kigezo kikuu.
>>> Umri miaka 18 na kuendelea.
>>> Uchapakazi, kujituma, creativity na ubunifu katika masuala ya mitandao ya kijamii ni vigezo muhimu.
>>> Awe mkazi wa Mbeya Mjini.


NAFASI ZILIZOPO NI NNE KAMA VIGEZO VITAKIDHIWA.

FIKISHA MAOMBI YA KAZI OFISI YA JIGAMBE (MbeyaCity.com) ILIYOPO KATIKA YA SAE NA ILOMBA OPPOSITE/MKABALA NA MASHOKO BAR.

The Boss lady Huddah Monroe na Prezzo Mapenzi Tele, Diva Aamua Kuweka Picha ya Nusu Uchi Kupoteza Soo

Prezzo akiwa na huddah jana muda mchache baada ya lady boss kutua katika  ardhi ya kenya.. ahahahahahah  prezzo kajiachiajeee!!!
Baada ya huddah kuweka picha yake akiwa na prezzo na kuzua gumzo ndani ya mtandao huo wa twirraa, dada yetu akaamua kuweka picha yake ya.....(sijaielewa sijui AVI na hii ahahahha samahani lakini) ili kupotezea soo hilo..
ahahahahah Sasa bado hatuelewi  kama ile LOVE AT THE FIRST SIGHT IMEISHIA WAPI maana presidente anaongea kwa vitendo tu!! #okeee

Source: Zeddylious blog

HUYU NDO MBUNGE ALIYEHUKUMIWA KWENDA JELA MIEZI KUMI, HILI NDO KOSA ALILOFANYA

 

MBUNGE wa Mbarali, Modestus Kilufi (CCM) amehukumiwa kifungo cha miezi 10 baada ya kupatikana na hatia ya kutishia kuua, Mbunge huyo (51) alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Oktoba 10 akidaiwa kutishia kumuua Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ruiwa, Mbarali, Jordan Masweve.


Kabla ya kusoma hukumu hiyo leo Mbunge aliomba Mahakama impunguzie adhabu, kwani ana watoto watano kati yao wawili wanasoma Chuo Kikuu na wananchi wanamtegemea kuwasilisha matatizo yao bungeni.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, Michael Mteite, alisema ameridhika na ushahidi wa upande wa mashitaka ukiongozwa na mawakili wa Serikali, Epimack Mabrouk na Griffin Mwakapeje, pia mawakili wa upande wa mashitaka walimwomba Hakimu Mteite kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa, ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

"Kutokana na maelezo hayo na ushahidi ulioletwa mahakamani, ninakuhukumu kifungo cha miezi 10" alisema Hakimu Mteite.

Mbunge akihojiwa katika chumba cha mahakama alisema unajuwa siku hizi haki inatendeka pale tu iwapo mwanaCCM ametiwa hatiani, lakini kama ni mpinzani ametiwa hatiani utasikia ooh kaonewa au hii ni hukumu kutoka ikulu, hata hivyo alisema atakata rufaa katika hukumu hiyo

SAKATA LA DADA MTANZANIA KUNYONGWA WIZARA YA MAMBO YA NCHI ZA NJE YASEMA..

Dada anaetuhumiwa kukamatwa na madawa ya kulevya.

Akizungumza na Gazeti la Mwananchi jana Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Mkubwa Ali, alikiri kukamatwa kwa watu hao (majina yanahifadhiwa) ambao mmoja ni mkazi wa Ilala na mwingine wa Magomeni jijini Dar es Salaam. “Taarifa tulizonazo zilizo rasmi kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Misri kwa sasa ni kukamatwa kwa Watanzania wawili waliokuwa wakisafirisha heroin kuelekea Bara la Asia na walikamatwa nchini Misri wiki mbili zilizopita.”

“Tumewasiliana na balozi wetu nchini Misri amesema hana taarifa za kuhukumiwa kunyongwa kwa watuhumiwa hao, isipokuwa wameshasomewa shtaka lao la awali. Wapo rumande kwa sasa kwani kesi hiyo imetajwa mara moja tu. Balozi amekiri kushikiliwa kwa watuhumiwa hao wakiwa na dawa zinazoaminiwa ni za kulevya,” alisema.

Alisema watuhumiwa wote wanashikiliwa polisi na wanatarajia kufikishwa mahakamani wakati wowote.

Video inayomwonyesha mmoja akikaguliwa na maofisa wa polisi wa nchini Misri na kukutwa na dawa hizo, ilisambaa siku nne zilizopita katika mitandao mbalimbali ya kijamii.,

TFF KUTOA TAMKO KOMBE LA KAGAME

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema linafanyia kazi hoja ya klabu za Yanga na Simba kutaka kujitoa kwenye michunao ya Kombe la Kagame zikihofia usalama wa Sudan Kusini.
Akizunguza kwa njia ya simu jana jioni, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema baada
ya kuibuka hofu hiyo, wanafanyia kazi jambo
hilo kabla ya kutoa tamko rasmi.
“Tunalifahamu vizuri jambo hilo. Tutakaa na kujadili kwa kina kabla ya kutoa tamko rasmi,” alisema Angetile.
Kauli ya Angetile imekuja siku moja tangu Simba na Yanga zitamke kujitoa kwenye michuano hiyo kama itafanyika Darfur zikhofia hali ya usalama.
Juzi, kwa nyakati tofauti viongozi wa Simba na Yanga, walisema wao wametafakari kwa kina tahadhari ya Serikali kupitia kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, hivyo hawakwenda Darfur.
Viongozi hao walitamka wazi kuliacha jambo hilo mikononi mwa TFF kuamua nini kifanyike baada ya tahadhari ya serikali kuona nini kifanyike.

HUYU NDIYE DADA WA KIZUNGU ANAYEDAIWA KUWA NDIO SHEMEJI WETU KWA NGWEA

Mzungu anayedaiwa kuwa alikuwa demu wa Ngwea aitwaye Misheily akilia kwa uchungu wakati wa kuaga.
Na Gladness Mallya
MAJONZI na vilio vilitawala juzi katika zoezi la kuuaga mwili wa marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ kwenye Viwanja vya Leaders lakini mmoja wa waliotia fora katika kuangua kilio alikuwa dada mmoja mzungu anayedaiwa kuwa alikuwa demu wa Ngwea aitwaye Misheily.Mzungu huyo alionekana akilia kwa uchungu huku akitoa maneno yaliyoashiria kuwa ameumia sana kuondokewa na ‘mtu’ wake huyo ambaye huenda walikuwa na malengo mazuri ya baadaye.

...akiwa na simanzi nzito.
Aidha, kilio alichokuwa akiporomosha binti huyo kiliwafanya watu waliokuwa karibu naye kumsikitikia na kuzidishiwa majonzi kwani ilifika wakati akaishiwa nguvu.
...Akitolewa eneo hilo kwa kusaidiwa na mtu wake wa karibu.
Paparazi wetu alijaribu kumfuata na kumuomba kuzungumzia juu ya kifo cha Ngwea lakini alikataa na kusema asingeweza kufanya hivyo kufuatia majonzi aliyokuwanayo huku akionekana kutoamini kama jamaa yake huyo ametutoka .
 
na global publisher

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 7, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.
.
.

Thursday, June 06, 2013

AJALI MBAYA YATOKEA IFISI MBALIZI LEO MCHANA, YAJERUHI ZAIDI YA ABIRIA 15.

Daladala ambayo ilikuwa inatoka Mbalizi kwenda Songwe  yenye namba za usajili T 635 ALS ikiwa imeharibika vibaya Baada ya Ajali kutokea Eneo la Ifisi Mbalizi Mbeya
Hapa ndipo eneo ambalo Daladala iliingia wakati ilijaribu kulipita Gari lengine akiwa mwendo kasi na kuukutana na Tela la Mafuta
Daladala upande wa nyuma
 Lori aina ya Scania yenye namba ZA usajili T378 AGD likiwa limepaki Baada ya ajali hiyo kutokea

Mabaki ya daladala 

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA MSANII MAREHEMU ALBERT MANGWEA

bb21b674cea911e2918122000a9f4d8a_7

Hapa ndipo Mwili wa Marehemu Albert Mangwea ulipopumzishwa leo Mkoani Morogoro
Baada ya siku kadhaa zilizokuwa na kila aina ya harakati, ugumu na majonzi makubwa, Albert Mangweha aka Ngwair hatimaye leo amezikwa kwenye makaburi ya Kihonda mkoani Morogoro ambako ni nyumbani kwao.
Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili wake kwenye uwanja wa Jamhuri. Umati mkubwa wa wananchi ulijitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Ngwair aliyefariki nchini Afrika Kusini, wiki iliyopita. Wasanii wengi kutoka Dar es Salaam nao wamehudhuria mazishi hayo.

16f11344cea711e2813a22000a1f8f34_7


75e8603ecea511e29ecd22000aaa08de_7

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KUHUSU MABADILIKO KWA BAADHI YA MAKAMANDA

Advera-Senso 

                                   (Msemaji wa jeshi la polisi nchini Advera Senso-SSP)
………………………………………………………………………………
 Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734                                                                                    Makao Makuu ya Polisi,
Fax Na. (022) 2135556                                                                                                           S.L.P. 9141,
Unapojibu tafadhali taja:                                                                                       DAR ES SALAAM.
                                                                                        06 JUNI, 2013
TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI
Inspekta Jenerali wa Polisi, IGP Said Mwema, amefanya mabadiliko ya makamanda na wakuu wa upelelezi katika baadhi ya mikoa hapa nchini.
Katika mabadiliko hayo aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Michael Kamhanda amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhani Mungi ambae alikuwa Makao Makuu ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai.
Aidha, DCP Ally Mlege aliyekuwa Makao Makuu ya Polisi amehamishiwa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwenda kuwa Mkuu wa utawala na raslimali watu.
Vilevile, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela amehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi wa makosa ya jinai  na nafasi yake inachukuliwa na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai mkoa wa Arusha ACP Camilius Wambura. Aidha, ACP Duwan Nyanda aliyekuwa Makao Makuu ya Upelelezi anaenda kuwa Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Arusha.
Uhamisho huo ni wakawaida kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.
Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi (T).

BABA YAKE DIAMOND YUPO HOI ANAUMWA...... DIAMOND HAJAWAHI KANYAGA KUMJULIA HALI...!!

BABA wa msanii Nasibu Abdul ‘Diamond’, Abdul Juma yupo hoi akisumbuliwa na ugonjwa wa miguu.
 

Kwa mujibu wa chanzo makini, Baba Diamond anasumbuliwa na tatizo la miguu kuvimba hali ambayo imemfanya ashindwe kutembea lakini cha kushangaza mwanaye, Diamond hajaenda kumjulia hali.

“Baba Diamond ni mgonjwa kwa muda mrefu sana lakini Diamond hajawahi kuja kumuona hata siku moja,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kuzinyaka habari hizo, waandishi  wetu walifunga safari mpaka nyumbani kwa mzee huyo, Magomeni-Kagera, jijini Dar ambapo alikiri kuugua kwa muda mrefu na kukosa msaada kutoka kwa Diamond.

“Nasumbuliwa na miguu kwa muda mrefu sana na ninatibiwa katika Hospitali ya Saint Monica, Manzese-Darajani. Diamond ana taarifa za kuumwa kwangu lakini hajawahi kuja kuniona.

“Namshukuru mwanangu Queen Doreen kwa kunijali kwa kila kitu,” alisema baba Diamond.

HII NDIO HALI YA KHADIJA KOPA MARA BAADA YA KUPOKEA TAARIFA ZA MSIBA WA MUMEWE KIPENZI HII LEO...!!

 
Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stalla Manyanya akimfariji msanii na taarab na malkia wa mipasho Tanzania,Khadija omar Kopa alipokua kwenye chumba maalum cha kupumzikia wageni kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leoa alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani kitaifa yaliyoaadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana.
 
Baadhi ya viongozi na wananchi wa mkoa wa Rukwa na Mpanda wakimsindikiza kuapanda ndege msanii wa taarab na malkia wa mipasho Tanzania Khadija Omar kopa kwenye uwanja wa ndege wa mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leo alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye Maadhimnisho ya siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyoadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana. 

Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stalla Manyanya kushoto akimfariji msanii na taarab na malkia wa mipasho Tanzania Khadija omar Kopa alipokua kwenye chumba maalum cha kupumzikia wageni kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leoa alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani kitaifa yaliyoaadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana. (Picha na ofisi ya Makamu wa Rais)

UMATI WA WAKAZI WA MOROGORO WALIOJITOKEZA KUUAGA MWILI WA NGWEA.... UWANJA WA JAMHURI WAFURIKA..!!

 Wananchi waliojitoka uwanjani
                                     Huyu nimmoja kati ya walipoteza fahamu uwanjani





zoezi la uuagaji wa mwili ukiendelea
Rafiki wa wa karibu wa marehemu Albert Mangwea aliyekuwa amelazwa nchini Afrika Kusini amerejea Tanzania na yuko njiani akielekea mkoani Morogoro kwaajili ya kushiriki mazishi ya swahiba wake Mangwea jioni ya leo

PICHA MBALIMBALI KWENYE SEND OFF YA FROLA MVUNGI ILIYOFANYIKA JANA

Msanii H.Baba akiwa na bestman wake wakiwa kwenye sendoff ya mke wake mtarajiwa
 

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...