Wednesday, April 17, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUSAMBAA KWA HABARI ZA MISHAHARA YA WALIMU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII



BI KIDUDE AFARIKI DUNIA

.
 
MSANII WA MUZIKI WA TAARABU NCHINI TANZANIA KUTOKA VISIWANI ZANZIBAR FATUMA BINT BARAKA MAARUFU KAMA BIBI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA LEO HUKO VISIWANI ZANZIBAR.
 
BI. KIDUDE AMEFIKWA NA MATUTI HAYO LEO KUTOKANA NA MARADHI YALIYOKUWA YAKIMSUMBUA KWA MUDA MREFU.
 
BI. KIDUDE  AMESHAWAHI KUFANYA KAZI NYINGI IKIWEMO MHONGO WA JANG'OMBE, KIJITI, ALAMINADURA, YA LAITI, AHMADA NA NYINGINE NYINGI.

Mwana Mziki wa Tanzania AY awa Verified on Twitter


Account ya mtandao wa kijamii ya Twitter ya mwanamuziki maarufu Afrika kutoka Tanzania, Ambwene Yesaya (AY) yatambulika rasmi na kuwa mwanamuziki wa kwanza hapa Bongo account yake kutambulika yaani (Verified Account) .

Twitter ambayo hufanya hivyo kwa kukuwekea alama ya tick ya blue mbele ya jina lako ili kukutambulisha kwa marafiki, ndugu, jamaa, mashabiki wako wanaokufuata [followers] kuwa wewe ni mtumiaji halisi wa account hiyo walifanya hivyo kwenye account ya Ambwene ndani ya masaa kadhaa yaliyopita.

Twitter pia hufanya hivi ili kukutofautisha na watumiaji wengine wanaoweza kutumia jina lako katika mtandao huo na wamekuwa wakifanya hivyo kwa watu maarufu katika nyanja mbalimbali.
AY amekuwa mmoja kati ya watanzania wachache ambao account zao zimekuwa hivyo akiwemo mcheza kikapu wa Oklahoma City Thunder(OKC) Hasheem Thabeet [@hasheemthedream], Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete [@jmkikwete] Flaviana Matata [@FlavianaMatata] na Waziri January Makamba

VIGOGO WIZARA YA ARDHI KORTINI KWA UBADHIRIFU

Simoni Lazaro (kushoto) akiwa na mtuhumiwa mwenzake, Gerald Mango.
Watuhumiwa hao wakiwa mahakamani.
Charles Kijuba akikwepa kamera mahakamani.
MAOFISA watatu waandamizi kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Makazi leo wameburuzwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za ufujaji wa pesa za serikali zaidi ya milioni 200. Watuhumiwa hao ni Simon Lazaro ambaye alikuwa ni Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Sera, Gerald Mango, Mkuu wa Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi , na Charles Kijuba, Kaimu Mhasibu Mkuu.
Watuhumiwa hao wamekana mashitaka na mahakama hiyo imesema kuwa dhamana iko wazi

MAGAZETI YA LEO APRILI 17, 2013

.
.

ANGALIA KILICHOJIRI KATIKA BIRTHDAY YA LULU........!!!

MAKAMBA ASHITAKIWA KWA KINANA

WanaCCM wa Ifakara mjini ‘wamemshtaki’ Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuph Makamba kwa Katibu Mkuu wa sasa wa chama hicho, Abdulrahman Kinana kwa ahadi yake aliyoitoa 2008 ya kuwapatia Sh1 milioni ambayo hajaitimiza. 

Mwenyekiti wa CCM wa tawi la Ifakara mjini, Felista Chakachaka alisema kwamba mwaka 2008, Makamba alipotembelea tawi hilo, aliwaahidi kuwapatia
Sh1 milioni kwa ajili ya kazi za tawi hilo lakini hakuitekeleza.

Hata hivyo, Makamba aliyeko Bumbuli mkoani Tanga, alisema jana: “Sawa, mimi nilitoa ahadi hiyo, sikuitekeleza, sasa aliyepo si ndiyo anatoa...kwani ahadi za Mwalimu Nyerere si Mzee Ali Hassan Mwinyi kazitekeleza, sawa na ahadi za Benjamini Mkapa ambazo Rais Jakaya Kikwete anatekeleza.

“Huyu wa sasa aliyepo madarakani ndiye chama, ile ni ahadi ya chama, ulifikiri Makamba n’toe fedha yangu mfukoni, ile ni ahadi ya chama,” alisema Makamba.

Akijibu hoja hiyo, Kinana alisema kwa kuwa Makamba aliahidi kiasi hicho cha fedha akiwa katibu mkuu, basi yeye atatoa fedha hizo. “Katika kipindi cha wiki mbili fedha hizo zitakuwa zimeingia katika akaunti yenu..nitawapatia kama alivyoahidi alisema Kinana.
Mbali na kutembelea tawi hilo, Kinana alifungua mashina ya wakereketwa matano mjini Ifakara.Kinana yuko ziarani mkoani humo kuangalia maendeleo ya chama hicho tawala.

SOURCE::MWANANCHI:

MILA POTOFU ZACHANGIA KUONGEZEKA KWA MAAMBUKIZO YA UGONJWA MALARIA MKOANI MBEYA

......................................................................

Na Esther Macha, Mbeya
LICHA ya Serikali kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya matumizi ya vyandarua hali hiyo bado imekuwa tatizo kutokana jamii zilizo nyingi Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya kuwa na imani potofu kuhusu matumizi ya vyandarua vyenye dawa kuwa hawapati usingizi na wengine kudai ni njia ya uzazi wa mpango.

Hayo yalisemwa jana Bwana afya katika Ofisi ya Wilaya ya Mbarali Bw.Yona Msyani wakati wa mahojiano maalumu na gazeti hili, kuhusiana na elimu ya ugonjwa wa maralia katika viwanja vya hospitali ya Chimala Mission .
 
Alisema kuwa suala la utumiaji wa vyandarua imekuwa changamoto kubwa kwa katuiika utendaji kazi kwa wataalamu wa afya kutokana na wananchi kuwa na imani potofu juu ya matumizi ya vyandarua vyenye dawa.

“Bado tuna changamoto kubwa sana hivyo inatupasa kujipanga na kuelimisha jamii kutambua umuhimu wa matumizi ya vyandarua “alisema.

Hata hivyo alisema kuwa imani hiyo potofu si kwa Wilaya ya mbarali tu kwani hali hiyo ilijitokeza wakati wa kampani ya ugawaji wa vyandarua hivyo mwaka 2010 kwa nchi nzima.
Bw. Msyani alisema kuwa kama wataalamu wa afya bado wanaendelea kutoa elimu ya afya kwa wananchi jinsi ya kujizuia na ugonjwa wa maralia ikiwa ni pamoja na kuondokana na dhana potofu waliyojenga wananchi.

Akizungumzia kuhusu vifo ambavyo vinatokana na ugonjwa maralia ,Bwana afya huyo alisema kuwa maralia I ugonjwa ambao unaongoza kwa vifo hasa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

“Tatizo hili lipo kwa kiasi kikubwa kwa watoto , mwaka 2012 mwezi januari mpaka desemba waliugua watoto 1,635 chini ya umri wa miaka mitano ambapo kati ya hao waliofariki ni 100 kwa mwaka jana kutokana na ugonjwa wa maralia.

Tuesday, April 16, 2013

ANGALIA RIHANA ALIPOFANYA SHEREHE YA UCHI AKIWA BARBADOS SEHEMU ALIYOZALIWA, AIBU....!!





DIAMOND AMTOLEA NJE WEMA NA KUMPAMBANISHA NA PENNY AMREKODI NA KUSAMBAZA CLIP

 
 Clip iliyosambaa inayomuhusisha Wema Diamond na Penny imefika ndani ya blog yako, clip ambayo inaonekana kurecodiwa kwa maksudi na Diamond pale alipopigiwa simu na Wema Sepetu jana usiku. Inasemekana Wema alimpigia simu Diamond usiku, lakini baada ya Diamond kupokea alimtaka kuacha drama na kumsisitizia kuwa sasa hivi anampenda Penny.
maongezi yako hivi 
Diamond: mi sikufanyii drama na wala sitaki drama yoyote, am inlove with penny we unajua hilo right?
Wema: yeah your inlove with Penny and i i ... 
Diamond: sipendi kwasababu sipendezewi kwasababu mwisho wa siku itakuja kutuletea matatizo drama, nakujua kitu kidogo hukawi kukifanya kikubwa mji mzima na nini na nini sitaki.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA SIKU MBILI WA UDHIBITI WA HUDUMA ZA KIUCHUMI BARA LA AFRIKA, JIJINI ARUSHA LEO

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa kimataiafa wa siku mbili wa Udhibiti wa Huduma za Kiuchumi Bara la Afrika, ulioshirikisha mataifa mbalimbali kutoka Bara la Afrika, ulioanza leo Aprili 16, 2013 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizindua Kitabu cha Udhibiti wa Huduma za Kiuchumi Bara la Afrika, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa siku mbili wa Udhibiti wa Huduma za Kiuchumi Bara la Afrika, ulioshirikisha mataifa mbalimbali kutoka Bara la Afrika, ulioanza leo Aprili 16, 2013 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha. Kitabu hicho kimetungwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum) Prof. Mark Mwandosya. Kulia ni Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) ni Mkurugenzi wa Ewura, Haruna Masebu.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakiwa ukumbini wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal wakati akiwahutubia.

HUYU NDIYE MBUNGE ALIYEMWAMBIA SUGU 'SIONGEI NA MBWA NAONGEA NA MWENYE MBWA........!!

Mkutano wa 11 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaendelea huko Dodoma na wabunge wameendelea kujadili bajeti ya ofisi ya waziri Mkuu katika kikao cha 5.
Siku hizi watu wengi wamezoea kusikia malumbano ama vijembe wanavyotoleana
wabunge wetu, licha ya kuwa vinakuwa sehemu ndogo tu na wanaendelea na hoja za kutusaidia watanzania, lakini bunge limekuwa tofauti sana hasa kwa kuzingatia matumizi ya lugha na hata tafsiri ya lugha hizo.

Leo asubuhi mbunge wa jimbo la Kondoa kusini Juma Suleiman Nkamia alimwambia mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (Sugu) kuwa “kumbuka siongei na mbwa naongea na mwenye Mbwa”. Sentensi hii ilitamkwa na mbunge huyo baada ya kusikia sauti ya Sugu akijaribu kukataa kile alichokuwa anachangia bila kufuata utaratibu wa kunyoosha mkono ama kumuomba naibu spika, na ndipo alipomuomba kuwa na heshima kwanza kwa kumtaja kwa jina la ‘Sugu'

PENNY: "NIMEMSAMEHE DIAMOND INGAWA ALINISALITI KWA UWOYA....KWA SASA TUMEYAMALIZA"


Katika muda ambao kila mmoja alikuwa amejaribu kuamini kuwa Diamond Platnumz ameamua kutulia na mpenzi mmoja, mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa, hivi karibuni  staa huyo ameanzisha uhusiano wa kimapenzi na muigizaji wa filamu Irene Uwoya.....
 
Magazeti ya udaku nchini yaliandika habari hiyo ikiwa na picha inazowaoenesha mastaa hao wakichukua chumba kwenye hoteli ambako  walienda kufanya yao.
DIAMOND3
Kufuatia tetesi hizo, mwandishi wetu amezungumza na mpenzi wa sasa wa Diamond, Penny ambaye amesema kwa ufupi kuwa wameshayazungumza na Diamond na wako vizuri kwa sasa lakini akasisitiza kuwa asingependa kuliongelea zaidi suala hilo.

Katia hatua nyingine, Jokate Mwegelo aliyewahi kuwa na uhusiano na Diamond amekanusha  taarifa iliyoandikwa na gazeti moja la udaku kuwa amemcheka Irene kwa kunaswa kwenye himaya ya Diamond.

“Mimi hivyo vitu havinihusu na wanapenda kupata quotes zangu pasipo hitajika. I don’t know why? I don’t why wanatafuta story. That’s their life kiukweli with whatever they choose to do, more power to them,” amesema Jokate.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE APRIL 16, 2013

.
.
.
.

Kutoa Taarifa za Siri Katika Mawasiliano ya Elektroniki ni Kosa la Jinai.

Jana na leo, Serikali imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunzaji wa siri za taarifa za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa huduma za simu za mkononi. Taarifa hizo zimefikia hatua ya kuchapishwa katika vyombo vya habari kwa kutaja bila idhini yao, namba za simu, wahusika wa namba hizo, maongezi na muda wa mawasiliano Kati yao. Jambo hili ni Kosa la Jinai. Mfano; tamko la Chadema lililotolewa na Ndugu Mabare Marando Mjini Dar es Salaam tarehe 14/04/2013.
Serekali inapenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenye makampuni ya Simu, Vyombo vya Habari na wananchi kwa ujumla kuwa, kutoa taarifa za mawasiliano binafsi ya simu baina ya watumiaji wa huduma hiyo, ni uvunjaji wa Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta Na. 3 ya mwaka 2010 na Kanuni za Mawasiliano (Kulinda Wateja) za mwaka 2005.
Kifungu cha 98 ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kinasema;
“Mtu yeyote ambaye ni mfanyakazi wa kampuni yenye leseni ya kutoa huduma za mawasiliano, au mwakilishi wake, ana wajibu wa kutunza siri za mawasiliano binafsi na taarifa zozote za siri za wateja kwa mujibu wa sheria hii”. Aidha, “Mtu yeyote haruhusiwi kutoa taarifa binafsi za mteja yeyote alizopokea au kusikia kwa mujibu wa sheria hii isipokuwa tu mtu huyo ameruhusiwa kwa mujibu wa sheria”

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...