Tuesday, April 16, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA SIKU MBILI WA UDHIBITI WA HUDUMA ZA KIUCHUMI BARA LA AFRIKA, JIJINI ARUSHA LEO

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa kimataiafa wa siku mbili wa Udhibiti wa Huduma za Kiuchumi Bara la Afrika, ulioshirikisha mataifa mbalimbali kutoka Bara la Afrika, ulioanza leo Aprili 16, 2013 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizindua Kitabu cha Udhibiti wa Huduma za Kiuchumi Bara la Afrika, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa siku mbili wa Udhibiti wa Huduma za Kiuchumi Bara la Afrika, ulioshirikisha mataifa mbalimbali kutoka Bara la Afrika, ulioanza leo Aprili 16, 2013 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha. Kitabu hicho kimetungwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum) Prof. Mark Mwandosya. Kulia ni Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) ni Mkurugenzi wa Ewura, Haruna Masebu.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakiwa ukumbini wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal wakati akiwahutubia.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...