Thursday, April 04, 2013

MAUNO YA WOLPER YAWACHENGUA WATU UKUMBINI

  VIUNO alivyokatika  staa maarufu wa filamu, Jacqueline Wolper viliwachengua ile mbaya watu waliohudhuria harusi ya wasanii maarufu wa Bongo Movies, Jimmy Mafufu na Idrissa Makupa ‘Kupa’.Tukio hilo lilitokea hivi karibuni katika Ukumbi wa Urafiki uliopo Ubungo, jijini Dar baada ya  wasanii kwenda mbele ya ukumbi kwa zamu na kuonyesha uhodari wa kuyarudi mangoma ambapo ilipofika zamu ya Wolper, alionekana kuwazidi wenzake kwa utundu wa kucheza.
Baada ya kuonesha vitu adimu ambavyo havikuoneshwa na staa yeyote kati ya waliomtangulia, wageni waalikwa walishangilia na kupiga makofi hadi aliporejea sehemu aliyokaa awali.

RAY ASALIMU AMRI JUU YA FILAMU YAKE INAYO SHUTUMIWA KUUDHALILISHA UKATOLIKI

 
Cover la filamu hiyo ya Sister Marry.
HATIMA ya filamu ya mwigizaji, Vincent Kigosi ‘Ray’, Sister Mary iliyokuwa imezuiwa kwa kudaiwa kudhalilisha ukatoliki, imefahamika kuwa mwigizaji huyo amesalimu amri ya viongozi wa kanisa hilo.Kanisa Katoliki nchini linaloongozwa na Muadhama Polycarp Kadinali Pengo, liliizuia filamu hiyo kwa kile kilichodaiwa kuwa ilikuwa ikionesha udhalilishaji kwa namna ambavyo watawa wamevaa mavazi mafupi.

Baadhi ya vipande vilivyomo katika filamu hiyo.
Akipiga stori na paparazi wetu, Ray amebainisha kuwa baada ya kuambiwa achomoe vipande vingi kwenye filamu hiyo, ameona ni bora kuachana nayo kwani hata akitoa haitaleta maana hivyo atakujairudia upya wakati mwingine. “Asilimia 85 ya filamu niliigizia kanisani na ndivyo walivyosema niviondoe, sina ujanja kwa sasa nimeanza kushuti filamu nyingine kabisa ile labda nije kuirudia upya hapo baadaye,” alisema Ray.

WAJUE WASANII SITA (6) WA BONGO FLEVA WENYE KUHESHIMIKA SANA TANZANIA.

1.LADY JAY DEE
Mwanadada JIDE ama binti machozi ameweza kuongelewa sana kama msanii anayeheshimika sana tanzania kutokana na idadi kubwa ya watu walio hojiwa kumtaja yeye kama ndo mwana muziki mwenye kuheshimika sana tanzania kwa upande wa muziki wa kizazi kipya

2.PROF J
Prof J naye hakuwa nyuma katika kutajwa na idadi kubwa,Prof j kama muhasisi mkubwa wa huu muziki wa kizazi kipya anaheshimika sana kutokana na mchango wake mkubwa katika hii gemu bila ya kuwa na sifa mbaya zinazo weza kumchafulia heshima yake
3.FID, Q

Polisi Wavamia Nyumba Ya Diddy

Diddy

Polisi na Helikopta mbili za polisi walivamia Nyumba ya Diddy iliyopo Los Angelos Marekani Usiku wakuakia Leo . Lakini habari zilizotoka kwenye vyomba vya usalama viliimbia TMZ kuwa tukio hilo lilikuwa la bahati mbaya
Habari zilizotoka polisi ziliwaambia TMZ kuwa Kuna Mtu alipiga simu polisi kuwa ndani nyumba ya Diddy kuna mtu anarusha risasi.
Baadae polisi na wakubwa wengine walipojua kuwa ni mchezo mwingine unaofanyiwa wasani wakubwa marekani waliamukuondoka katika tuukio hilo.

TMZ wanasema kuwa waliambiwa kuwa Tukio hilo lilikuwa limepangiwa kufanyiwa kwa muigizajiSteve Carell ambapo nyumba yake ilikuwa imezungukwa na Polisi wengi kwasababu ilikuwa karibu na nyumba ya Diddy.
Hapa ndio nje kwa Diddy

Inasemekana Diddy sio staa wa kwanza kufanyiwa tukio hilo, kuna baadhi ya mastaa walishawahi kufanyiwa hivyo kama vile nyumbani kwa wazazi wa Miley Cyrus mwaka jana Walifanyiwa kitendo hicho hicho.
Polisi wamesema kuwa matukio hayo yakutishia ya mekuwa ya kudumu na sugu sasa wamesema watamshitaki kwa sheria kali kwa yeyote atakayefanya tena tukio kama hilo.

Mauaji ya Padri: DPP, Polisi wakorogana



Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Zanzibar, Ibrahim Mzee Ibrahim, ametupilia mbali uchunguzi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi uliofanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Maafisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) na kusema mtuhumiwa hana kesi ya kujibu mahakamani.

Padri Mushi ambaye alikuwa Paroko wa Kanisa Katoliki Minara Miwili aliuawa kwa kupigwa risasi Febuari 17, mwaka huu katika eneo la Beitrasi mjini hapa akiwa ndani ya gari alipokuwa akielekea kuongoza misa ya Jumapili katika Kanisa la Mtakatifu Theresia, mjini Zanzibar.
Baada ya mauaji hayo, Rais Jakaya Kikwete alitoa kibali cha kukaribisha maafisa wa FBI kushirikiana na Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa mauaji hayo na Machi 17, mwaka huu Jeshi la Polisi lilimkamata Omar Mussa Makame kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE APRIL 04, 2013

.
.
.
.

Wednesday, April 03, 2013

UWOYA NA NDIKUMANA WARUDIANA...ANGALIA PICHA ZAO MBILI WAKIWA KATIKA POZI LA MAHABA


KUNA maswali tena? Ndoa ya staa kiwango cha juu Bongo, Irene Uwoya na mumewe Hamad Ndikumana 'Kataut' anayeng'ara katika kabumbu akikipiga pande za Rwanda imerejewa na uhai tena..

BREAKING NEWzzzzzzzzzzzzzzz!!!! MPAKA WA TUNDUMA MBEYA WAFUNGWA KWA MUDA POLISI WATUMIA MABOMU

 
kamanda  wa polisi  wa mkoa  wa Mbeya  Diwani Athuman 

Taarifa  kutoka Tunduma mkoani Mbeya zinadai  kuwa hali  si shwari katika eneo hilo kutokana na kuzuka kwa  vurugu kubwa zinazodaiwa kusababisha na masuala ya  kiimani ya nani achinje kati ya mkristo na Muislam . Mwandishi  kutoka Tunduma mkoani Mbeya Moses Ng'wat anaripoti kuwa  vurugu  hizo zimeanza  majira ya saa nne asubuhi  kwa makundi  ya vijana  kuandamana mitaani na kuvutana  kuhusu uamuzi  wa viongozi  wa dini ya kikristo Tunduma  kuandika barua kwa mkuu  wa wilaya  kutaka  kuruhusiwa kuchinja  wakati wa pasaka.

WEMA SEPETU AAMUA KUMUENZI MCHINA WAKE KWA KUJITANDIKA TATTOO ZA KICHINA SHINGONI NA MGONGONI


PINDA AFUNGA MACHIMBO YA MORAMU

 

Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa wamebeba mwili wa mtu aliyepoteza maisha  kutokana na  kuporomoka kwa udongo katika machimbo ya Moramu yaliyopo eneo la Moshono, Arusha. 

 Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana alitangaza kuyafunga rasmi machimbo ya moramu eneo la Moshono, Arusha hadi Serikali itakapoweka utaratibu mzuri wa shughuli mbalimbali za uchimbaji katika eneo hilo.

Hatua hiyo ya Pinda imetokana na ajali ya watu 14 waliopoteza maisha baada ya kufukiwa na kifusi juzi, wakati wengine wawili walijeruhiwa kwenye ajali hiyo iliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na mvua zinazonyesha jijini Arusha.
Pinda alitoa agizo hilo alipotembelea eneo hilo pamoja na kuwajulia hali majeruhi wawili waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mt Meru
CHANZO:MWANANHI.

KAJALA AMLIPA FADHILA WEMA

Siku chache baada ya kuhukumiwa na kuachiwa huru baada ya kulipiwa faini ya sh. Millioni 13 mwanadada wa bongo movie Kajala Masanja kaamua kumlipa fadhira ya kuchora tatoo yenye jina la msanii mwenzake Wema Sepetu ambae ndie aliemlipia kiasi hicho cha fedha na kumfanya kuwa huru tena.










jambotz8.blogspot.com

MAGAZETI YA LEO APRIL 3, 2013

DSC03777DSC03778
DSC03775 

DSC03776

LOWASSA AMTOA KAFARA PINDA

WABUNGE WAUNGANISHA NGUVU KUTAKA KUMSULUBU BUNGENI





RIPOTI ya tume iliyoundwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa mwaka 2006 kuchunguza ujenzi wa maghorofa katika Jiji la Dar es Salaam, imemweka mahala pabaya na inaweza kumtoa kafara, Waziri Mkuu wa sasa, Mizengo Pinda, Tanzania Daima Jumatano limedokezwa.
Pinda anatolewa kafara katika sakata la jengo la ghorofa 16 lililoporomoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam wiki iliyopita na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 40.

Kutokana na janga hilo, Pinda analalamikiwa kukalia ripoti ya Tume ya Lowassa ambayo ilikuja na mapendekezo ya kukabiliana na maghorofa yaliyojengwa chini ya kiwango.

KANGAMOKO WATIA AIBU TENA MKOANI KAGERA HEBU ANGALIA PICHA HIZI




SUMATRA YATANGAZA KUPANDA KWA NAULI ZA MABASI YA MASAFA MAREFU NA DALADALA KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM

IMG_6840Kaimu Mkurugenzi wa SUMATRA Athman Kilima akizungumza na waandishi wa habari leo katika makao makuu ya taasisi hiyo wakati akitangaza kupanda kwa viwango vya nauli ya mabasi ya mikoani na Daladala.
………………………………………………………………..

 Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imekamilisha mchakato na kuridhia viwango vipya vya nauli kwa ajili ya usafiri wa mijini na usafiri wa kwenda mikoani. Viwango hivi vipya vimefikiwa baada ya kufuata taratibu za kisheria na za kiutendaji ambazo SUMATRA kama msimamizi na mdhibiti wa sekta ya usafiri wa barabara inapaswa kuzifuata kabla ya kuridhia viwango hivyo. Viwango vipya vya nauli vitaanza kutumika kuanzia tarehe 12 Aprili, 2013.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...