Thursday, April 04, 2013

WAJUE WASANII SITA (6) WA BONGO FLEVA WENYE KUHESHIMIKA SANA TANZANIA.

1.LADY JAY DEE
Mwanadada JIDE ama binti machozi ameweza kuongelewa sana kama msanii anayeheshimika sana tanzania kutokana na idadi kubwa ya watu walio hojiwa kumtaja yeye kama ndo mwana muziki mwenye kuheshimika sana tanzania kwa upande wa muziki wa kizazi kipya

2.PROF J
Prof J naye hakuwa nyuma katika kutajwa na idadi kubwa,Prof j kama muhasisi mkubwa wa huu muziki wa kizazi kipya anaheshimika sana kutokana na mchango wake mkubwa katika hii gemu bila ya kuwa na sifa mbaya zinazo weza kumchafulia heshima yake
3.FID, Q

Huyu ni msanii aliyezungumziwa kuwa ni mpole sana mkinywa na hufanya kazi zake kwa umakini mkubwa,Ni mtu apendaye kufikiri jambo kwa umakini sana kabla ya kulitenda,Pia kazungumziwa sana na idadi kubwa ya walio hojiwa
4.A.Y
 AY kati ya mchakalikaji mkubwa na mpenda maendeleo katika kazi zake, ni kijana anaye ibeba nembo ya Tanzania katika ngazi ya kimataifa,Kujiheshimu kwake na kuto kuwa na skendo pamoja na kuchakalika kwake kunamfanya aonekane kuwa mtu wa kuigwa kwa vijana wengine.
5.MWANA FA
Binamu ama waweza sema pacha wa A.Y kutokana na kuwa na urafiki wa karibu sana na wa muda mrefu na A.Y.mWANA FA pia katajwa kwa idadi kubwa ya wadau kama mtu anayeheshimika sana nchini hasahasa katika nyanja hii ya muziki wa kizazi kipya.
 6. JUMA NATURE
Juma Nature ama kiroboto, ni mtu asiye penda makuu pia kazungumziwa kama mtu anayependa kuona watu wote wakiwa sawa na  hapendi kuona manyanyaso kwa watu wengine sababu ya kuto kuwa na uwezo.Wamemtaja kama mtu mwenye nyota ya kupendwa sana na watu kwani yaonyesha anaweza akakaa hata miaka kadhaa bila ya kutoa wimbo wowote ila pindi apandapo tu jukwaani watu hufarijika hata aimbapo nyimbo za zamani.
Imefanyiwa utafiti na kuandaliwa na Timu nzima ya www.SHUKRANI THE CHOICE

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...