Thursday, April 04, 2013

Airtel, Samsung wakubaliana kukuza soka la vijana: Airtel Rising Stars Awamu ya tatu kuanza mwishoni mwa mwezi huu

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayofanya kazi pamoja na kampuni ya Samsung zimesaini makubaliano ya kushirikiana kudhamini mashindano makubwa Afrika kwa vijana wa chini ya miaka 17. 

Katika mkataba huo wa mamilioni ya dola, Samsung pia itakuwa mtoaji rasmi wa vifaa vya mawasiliano kwenye mpango huo wa mashindano maarufu kama Airtel Raising Star (ARS) unaoendeshwa na Airtel. 

Airtel inatoa huduma za mawasiliano kwa simu za mkononi kwenye nchi 20 barani Asia na Africa huku Samsung ikiwa ni miongoni mwa makampuni makubwa ya vifaa vya kisasa vya elektoniki. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam leo, Airtel imefanya kazi kwa karibu sana na taasisi za elimu kwenye nchi 17 zinazozungumza Kiingereza na Kifaransa ambapo kwa kupitia mashindano hayo ya soka ya Airtel Rising Stars yamefanikiwa kushirikisha zaidi ya timu 18,000. ambapo vijana wa kike na wa kiume wapatao 400,000 barani Afrika walishiriki katika mashindano hayo ya Airtel Rising Star. 

 Mwaka jana mashindano haya ya Airtel Rising Stars yalionekana kukua kwa asiliamia 65 na kuna kila dalili kwa mwaka huu kukua zaidi,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa na Airtel Makao Makuu. 

Mkakati huo wa kukuza soka barani Afrika unaungwa mkono kwa dhati na klabu kubwa za England; Arsenal FC na Manchester United ukiwa na lengo la kuibua na kukuza vipaji vipya vya vijana wa Kiafrika. “ARS imefikia kuwa chanzo kizuri cha wachezaji wapya wa timu za mataifa mbalimbali huku pia wengine wakijiunga na klabu zinazoshiriki ligi kuu barani humu. Afrika ina vijana wengi zaidi duniani. 

Uwiano wa vijana barani humu ni mkubwa kuliko mabara yote kwani takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 60 ya Waafrika zaidi ya bilioni moja ni vijana,” alisema George Ferreira, Makamu wa Rais wa Samsung Electronics, Africa.
Akizungumzia ushirikiano huo, Andre Beyers, Ofisa Masoko Mkuu wa Airtel Africa alisema: "Ushirikiano huu utapanua wigo wa biashara na kuyawezesha mashindano ya ARS kufikia malengo yake.” 

Msimu ujao wa Airtel Rising Stars ukiwa ni wa tatu tangu kuanzishwa kwake utaanza mwishoni mwa mwezi huu. Moja kati ya matunda ya mashindano haya ya Airtel ni Priscilla Okyere, binti aliyeibuka kutoka ARS na sasa ni nahodha wa timu ya taifa ya wasichana chini ya miaka 17 ya Ghana. Aliiongoza timu hiyo kunyakua medali ya fedha kwenye mashindano ya Dunia ya FIFA Under-17 kwa wanawake mwaka jana huko Azerbaijan.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...