Monday, April 01, 2013

Mgodi wafukia wachimbaji Arusha; zaidi ya watu 18 wanahofiwa kufariki.. Wanajeshi wafanaya uokozi sasa na tayari mtu mmoja ameokolewa hai na wengine watatu wakiwa wameshakufa

ajali (55)
Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema akiwasili eneo la ajali mapema 
ajali (66)



Mwili wa dereva wa lori moja kubwa lenye ujazo wa tani 18 ukiwa umeopolewa na askari jeshi, tayari kupelekwa mochwari ya Hospitali ya Mt Meru. Dereva huyu ametambulika kwa jina moja tu la Alex amefikwa na mauti akiwa ndani ya gari hilo wakati vijana wengine wakiendelea kupakia moram asubuhi ya leo

KAMANDA MPINGA MATATANI

ADAIWA KUAMURU GARI LILILOBEBA MAZAO YA MISITU LIACHIWE.

KAMANDA wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga ameingia kwenye kashfa akidaiwa kuamrisha askari wa kikosi hicho mkoani Singida kuliachia gari lililokamatwa usiku likiwa na shehena ya mazao ya misitu juzi.

Kutokana na tukio hilo, askari mwenye namba D.9523 Koplo Azizi wa kituo kidogo cha polisi Ikungi mkoani Singida ameingia matatani baada ya kulikamata gari hilo lenye namba za usajili T 271 BTR na trela namba T 686 BTX lenye urefu wa futi 40.

SIMULIZI YA ALIYENUSURIKA KIFO KUTOKA GHOROFA YA 15.


Fundi ujenzi, Yusuph Abdallah ambaye amelazwa katika Taasisi ya Mifupa (Moi), ameeleza jinsi alivyonusurika kifo baada ya jengo la ghorofa 16 kuporomoka Ijumaa iliyopita.
 

Rais Kikwete na Mkewe, Mama Salma Kikwete wakimpa pole Yusuph Abdallah katika Hospitali ya Muhimbili walipotembelea majeruhi wa ajali ya kuporomoka jengo la ghorofa 16. Picha na Muhidin Michuzi. 


FUNDI ujenzi, Yusuph Abdallah ambaye amelazwa katika Taasisi ya Mifupa (Moi), ameeleza jinsi alivyonusurika kifo baada ya jengo la ghorofa 16 kuporomoka Ijumaa iliyopita.


Yusuph aliliambia Mwananchi akiwa wodini kwamba kilichomponya ni neema za Mungu kwani kabla jengo hilo kuporomoka yeye alikuwa ghorofa ya 15 kwenye jengo hilo katika Mtaa wa Indira Gandhi akiendelea na ujenzi.

Alieleza kuwa hakuwa anafahamu kinachoendelea, bali aliona ghafla jengo linaaanza kuporomoka, na baada ya hapo hakufahamu zaidi kilichotokea hadi alipojikuta yuko hospitalini.

OBAMA AENDA KANISANI KWA MIGUU NA FAMILIA YAKE SIKU YA PASAKA, TAZAMA PICHA HAPA

Rais Barack Obama akitembea kwa miguu na Familia yake kutoka White House across Pennsylvania Ave.  hadi Lafayette Park. huku akiwa amemshikili mtoto wake wa pili Sasha mkono pamoja, Mkewe Michelle Obama  na binti yao mkubwa Malia kuelekea katika Kanisa la St. John’s Episcopal liliopo Washington, DC ambapo walihudhuria  katika Pasaka  Siku ya Jumapili Machi 31, 2013. ( Official White House Picha na Pete Souza)

Pastor at Obamas Easter Church Service: Captains of the Religious Right Want Blacks in the Back of the Bus, Women Back in the Kitchen
Rais Barack Obama na first lady Michelle Obama walipotembea kutoka White House na binti zao Sasha Obama, wa pili kutoka kushoto, na Malia Obama, kulia, wakitembea kwa miguu kupitia Lafayette Park kwenda  katika Kanisa la St. John’s Episcopal kwa ajili ya Pasaka Siku Jumapili, Machi 31, 2013, Mjini Washington. (AP)

Obama alipokua akitembea Mitaa ya Lafayette Park  hadi  St. John's Episcopal Church Siku ya Jumapili  , March 31, 2013, ndani ya Jiji la Washington. (Picha na Carolyn Kaster)
OBAMAEASTER1N_2_WEB
Obamas akitembea kupitia Lafayette Park kwenda Kanisasani  kwajili ya Pasaka.
OBAMAEASTER1N_4_WEB
Rais wa Marekani Barack Obama na familia yake walipo maliza ibada katika Kanisa la St. John’s Episcopal kwa ajili ya Pasaka Siku Jumapili, Machi 31, 2013, Mjini Washington.

HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 MACHI, 2013


Ndugu Wananchi;
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na kunipa fursa ya kuzungumza nanyi kwa kupitia utaratibu wetu huu mzuri wa kila mwisho wa mwezi.  Leo ninayo mambo matatu ninayopenda kuzungumza nanyi.
Ziara ya Rais wa China Nchini Tanzania
Ndugu wananchi; 
Jambo la kwanza ni ziara ya Mheshimiwa Xi Jinping, Rais wa Jamhuri ya Watu wa China aliyoifanya nchini kwetu kati ya tarehe 24 na 25 Machi, 2013.  Lengo la ziara yake ilikuwa kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya China na Tanzania.  Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wakazi wa Dar es Salaam kwa kumpokea vizuri mgeni wetu na ujumbe wake.  Wameondoka wakiwa na kumbukumbu nzuri ya nchi yetu na watu wake.

MKAPA ASEMA:TUSITANGULIZE UDINI KWENYE KATIBA


Ujumbe wa amani na tahadhari ya umakini kwenye utoaji maoni kwenye Katiba ndiyo vilitawala wakati wa misa za Sikukuu ya Pasaka zilizofanyika sehemu mbalimbali nchini jana na juzi. 
Miongoni mwa waliotoa hotuba wakati wa sikukuu hiyo ni 
pamoja na Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, ambaye alikuwa mkoani Mtwara; na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo aliyekuwa jijini Dar es Salaam. 
Mkapa akataa udini 
Rais mstaafu Mkapa alitumia fursa ya kutoa salamu katika Kanisa Katoliki mjini Masasi kuliasa taifa kujiepusha na utoaji wa maoni ya Katiba kwa misingi ya dini. 
Mkapa alisema katiba ijayo haipaswi kuwa na itikadi za kidini kwa kuwa zinaweza kuliangamiza taifa.

WANAUME BONGO MOVIE HAWANA MAPENZI YA KWELI: SNURA

MKALI wa filamu na muziki Bongo, Snura Mushi amesema anaogopa kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na wasanii wa filamu kwani wengi wao hawana mapenzi ya kweli.
 
Akipiga domo na paparazi wetu, Snura alisema tangu aanze kucheza filamu alijiapiza kuwa kamwe hatajiingiza kwenye mapenzi na waigizaji zaidi ya kushirikiana nao katika kazi ya kuzalisha filamu.
“Mimi siwapendi wanaume wasanii wa filamu, sijawahi kuwa nao labda awe msanii wa Bongo Fleva,” alisema Snura.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 01.04.2013

.
.
.
.
.
.

MAKAHABA RAIA WA RWANDA MATATANI DODOMA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1tiX0ExlorOYy5PlS5BybXxR-RE62-JNK58tvu27-tZ3kOtyvmVN2ONaQvBZkjXobq3njO7egLEHYvTvkYpM6sK3IVK9LvhxlzFp9Msw1t8IgR6jC29Sw0C4juffM53C24B3FetSfhoQ/s1600/changudoa+%281%29.jpg
WANAWAKE watatu raia wa Rwanda wanaosadikiwa kuendesha biashara ya ukahaba mjini Dodoma wamekamatwa na
kupewa siku tatu kuondoka nchini, huku wawili kati yao wakikutwa na vidonge vya kupunguza makali ya virusi ya Ukimwi (ARVs).

Sunday, March 31, 2013

ANGALIA PICHA YA KHANGA MOJA WAFUNIKA USIKU WA IJUMAA KUU NA MASHUJAA BAND

 Rapa wa bendi ya Mashujaa, Saulo John 'Fagason', akirap na kumchezesha mmoja wa wasanii wa kundi la Khanga moja, wakati walipofanya shoo ya pamoja kwenye Ukumbi wa Green Acres, Victoria usiku wa Ijumaa Kuu na kuwapagawisha vilivyo mashabiki wa bendi hiyo.
 Kiongozi wa bendi ya Mashujaa, Chalz Baba (wa pili kushoto) akiwaongoza waimbaji wa bendi hiyo kushambulia jukwaa wakati wa onyesho lililofanyika kwa pamoja na kundi la Khanga Moja, katika ukumbi wa Green Acrers uliopo Victoria jijini Dar es Salaam, usiku wa Ijumaa Kuu.
 Mnenguaji wa kundi la Khanga moja akionyesha umahiri wake wa 'Miuno Miuno, jukwaani
 Wanenguaji wa bendi hiyo ya Mashujaa, wakishambulia jukwaa wakaati wa onyesho hilo.
Mashambulizi yanaendelea jukwaani...
NA SUFIANI MAFOTO

ANGALIA PICHA ZA MTUHUMIWA WA MAUAJI YA PADRI- ZANZIBAR






 Hapo ndio tujue kuwa wenzetu hawabahatishi na hawana siasa kwenye kazi zao proffessional....kazi kweli kweli!!wamehadithiwa tu wamemchora mtu yule yule!!Angalia Mchoro wa Polisi Hapo chini na Ufananishe na mtu Huyu..



Mchoro Uliyotumika Kumpata Muuaji


NA MPEKUZI BLOGSPOT

RAIS KIKWETE ATEMBELEA MAJERUHI WALIOUMIA KATIKA GHOROFA LILILOPOROMOKA DAR ES SALAAM

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakimpa pole Bw. Yusuf Abdallah ambaye ni mmoja wa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25, katika wodi ya Sewa Haji ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam. kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Mhe. Hawa Ghasia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika wodi ya Sewa haji ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam leo Machi 31, 2013 wakimjulia hali na kumpa pole Bw. Selemani Saidi, mmoja wa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25 Kushoto mwenye suti nyeusi ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Raymond Mushi Kulia ni Daktari C.N. Mcharo wa taasisi ya Mifupa ya Moi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika wodi ya Sewa haji ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam leo Machi 31, 2013 wakimjulia hali na kumpa pole kijana Baqir Dhamji, mmoja wa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25. Kulia ni Daktari C.N. Mcharo wa taasisi ya Mifupa ya MOI.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika wodi ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam wakimpa pole kijana Mohamed Ally Dhamji ambaye ni miongoni mwa majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 25.PICHA NA IKULU.

ANGALIA PICHA ZA KANGA MOKO WA KANDA YA ZIWA

Hawa ni kanga moja pia walikuwa ndani wakazi wa mapokezi ya msanii wa mziki DIAMOND kanda ya ziwa.Bila wasiwasi wakicheza kwenywe gari ya .bila kujali walikuwa wanacheza mbele watoto.
haatariiii

LADY JAYDEE ADAI KUWA CLOUDS FM NI WANAFIKI....WANATAKA WAHONGWE ILI WAPIGE NYIMBO ZA WASANII


Lady Jay Dee
East African popular musician Lady Jay Dee ameamua kuwapa modongo Clouds fm kupitia Twitter leo kutokana na wimbo wake mpya uliotoka hivi karibuni Joto hasira kutopigwa katika radio hiyo. Jay dee ameandika kuwa radio ya watu isiyopiga nyimbo za wasanii wa watu ila wasanii wao tu. Angalia tweet za Queen of Bongofleva huyo.

"Radio ya watu isiopiga nyimbo za wasanii wa watu ila za wasanii wao tu, wasiopendwa na watu. #JotoHasira"

"Anaedai kuianzisha bongoflava aliapa kuiua bongo flava. Sasa hata wasioijua Hiphop nao wana beef na Bongo flava! Damn !!"

Jay Dee pia anaonekana kujizatiti na kujiamini kuonyesha kuwa yupo kwa lolote yeye kama Komandoo Binti Machozi aliandika tena "Kill me if u can. Am on Fire, siogopi ng'oooooo Jipangeni, Ni kweli nimelamba sumu, lakini hainidhulu. Nakunywa maziwa daily, I will survive".

"Hee! Kuna wajinga wanadhani nili tweet nikiwa nimelewa, nilimaanisha na msimamo ni huo. Sitasema oooh kuna mtu ka hack ac yangu nooo its me"

" Kuna DJ flani alikuwa akipiga nyimbo nilizoshirikishwa akifika sehemu nilioimba mimi anakata verse yangu nimtaje?? Sa hivi anakat ya Prof J"

Hata hivyo si Jay Dee pekee kuanza kulaumu kwani wapo wanamuziki wengine wanaolaumu nyimbo zao kutokupigwa

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 31.03.2013

.
.
.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...