Saturday, March 30, 2013

Lady Gaga anunua ‘wheelchair’ yenye dhahabu tupu

Siku zote Lady Gaga hupenda kuwa tofauti na kwa kuthibitisha hilo, amenunua baiskeli ya walemavu yenye dhahabu tupu iliyobuniwa na Ken Borochov kwaajili ya brand ya Louis Vuitton ambayo alionekana nayo mitaa ya Chicago jana.
article-2301275-18FEF183000005DC-721_634x868
Hiyo ilikuwa ni zawadi yake mwenyewe kwa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka 27 hiyo jana.
Gaga amekuwa akitumia wheelchair tangu February, baada ya kupata tatizo kwenye hips na hivyo kulazimisha kusitisha ziara yake ya Born This Way Ball na hatimaye kufanyiwa upasuaji.
Pamoja na kuwa mgonjwa, Lady Gaga ameendelea kuipromote perfume yake ya FAME. Pia albam yake ijayo iitwayo ARTPOP, itapatikana kwa awamu mbili miezi kadhaa ijayo.

UWANJA WA NDEGE WA SONGWE KUITWA JK, SUGU ANG'AKA


MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA) amesema haungi mkono pendekezo la Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Mbeya kutaka kuuita Uwanja wa Ndege wa Songwe jina la Rais Jakaya Kikwete. 

Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Mbilinyi maarufu kama Sugu alisema mapendekezo hayo yametolewa na watu wenye kutaka kujipendekeza kwa mkuu wa nchi badala ya kufikiria kuutangaza Mkoa wa Mbeya katika nyanja ya kimataifa. 

Alisema Mbeya ina historia ya kutaka kujitangaza kimataifa na uwanja huo ni fursa pekee ya kufikia malengo hayo aliyoeleza kuwa yanataka kufifishwa na wateule wa rais. 

“Siungi mkono uwanja kuitwa kwa jina la JK, tunataka jina litakaloasisi uhalisia wa Mbeya nasi tufahamike kimataifa, kamati ya ushauri ya mkoa chini ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya mjini, Norman Sigala ilikurupuka kuleta wazo hilo kabla ya kuwasiliana na wabunge,” alisema. 

Alisema hatua hiyo ya Sigala haiwakilishi mawazo ya wananchi bali inawakilisha mawazo ya mtu aliyeteuliwa na kwamba wao wakiwa wawakilishi wa Mkoa wa Mbeya kwa ridhaa ya wananchi hawawezi kukubaliana na suala hilo. 

Kauli ya Sugu iliungwa mkono na wabunge wengine wa Mkoa wa Mbeya, ambapo Mchungaji Lukson Mwanjale wa Mbeya Vijijini (CCM) alisema anasikitishwa na hatua hiyo ya kuliwasilisha wazo hilo bila ya kuwashirikisha wabunge. 

Alisema wakati wa kikao cha kamati ya ushauri wabunge wengi hawakuwepo na taarifa hizo walizisikia baada ya kusoma kwenye vyombo vya habari. 

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo ambaye pia ni mbunge wa Songwe, aliomba apewe muda wa kutaka kujua sababu zilizoibua wazo hilo. 

Wazo la kuuita Uwanja wa Ndege wa Songwe jina la Rais Jakaya Kikwete linazidi kupata upinzani ambapo awali chama cha NCCR-Mageuzi na kile cha PPT Maendeleo kupitia kwa viongozi wa Mkoa wa Mbeya vilipinga wazo hilo. 

:::TANZANIA DAIMA:::

Friday, March 29, 2013

KAULI YA UAMSHO BAADA YA MUUAJI WA PADRI ZANZIBAR KUKAMATWA

Taarifa ya Polisi kwa wanahabari - Anaedaiwa kumuua Padri Mushi akamatwa



Picha za scenes za movie ya mwisho ya Kanumba ‘Love and Power’

31
April 7, 2012 ni siku Steven Kanumba aliyofariki katika kuadhimisha mwaka mmoja tangu kifo chake watanzania kutoka sehemu mbalimbali watakutana kwenye tamasha la bure pale Leaders club kwa lengo la kumuenzi na kuangalia yale aliyofanya katika enzi za uhai wake pamoja na uzinduzi wa filamu yake ya mwisho, Love and Power. Hizi ni baadhi ya picha kwenye filamu hiyo.

41
51
61
vlcsnap-2013-03-24-09h48m30s175
vlcsnap-2013-03-24-09h48m43s56

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 29 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.
.

P FUNK AMCHANA MAKAVU MSANII NAY WA MITEGO

Producer maarufu bongo na mmiliki wa studio za bongo record P funk Majan ametoa makavu kwa watu wanaochonga kuhusu maendeleo yake husasani wale wote ambao wanapiga majungu kuwa mkali huyo amepotezwa na vijana wadogo kwenye soko la mziki bongo.
“Kuna watoto wadogo siku hizi wanakurupuka wanajiona wao baabkubwa juzi kati nikiwa kwenye club moja naskia kiproducer kinachonga kuhusu mimi kenyewe kana sijui nyimbo moja au tatu zimehit mimi nina yimbo zaidi ya 100 ambazo zimehit na hadi akina Mhe Mkapa enzi hizo, wametukubali we utaniambia nini” P funk alifunguka.

Majani amefunguka kuwa kuna watu wanamtafuta chuki ili kumpachika skendo akitolea mfano msanii wa kizazi kipya Ney wa Mitego kuwa haelewi kitendo cha rapper huyo kumtukana kwenye nyimbo yake kulikua na lengo gani kwasababu msanii huyo hamkaribii hata kidogo kwa level zake.

JACK PENTZEL ALONGA KUHUSU KUOLEWA KWAKE

MSANII wa bongo movie 'star 'wa bongo asiyekauka vituko' Jackline Pentzel a.k.a Jack wa Chuzi ameibuka na kuwataka mashabiki wake kuamini ameolewa na hajakurupuka kufanya maamuzi hayo kwani ni jambo ambalo alikuwa akilifikiria kila wakati

Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni Jack alisema kuwa anawataka mashabiki kuamini na kutowasikiliza watu wengine wanaotoa maneno ya uzushi juu yake kuwa maamuzi ya kuolewa ameyapanga na ameolewa na mwanaume wake wa siku nyingi hivyo anaamini anachokifanya ni sahihi kwake


Alisema kuwa watambue mwanaume aliolewa naye si mume wa mtu bali ni mchumba wake wa muda mrefu na walikuwa wakiishi pamoja kbala ya kuoa na ndipo maamuzi ya kufunga ndoa yalipokuja kwa kutotaka kuendelea kufanya uzinifu wakati uwezo wa kufunga ndoa walikuwa wanao


"Mimi nawashangaa kwani kuolewa ni kitu gani cha ajabu mpaka watu wasiamini mimi kufunga ndoa nimeamua kuolewa kwa sababu nampenda mwanaume wangu na nilikuwa naishi naye kwa kalibu hivyo tunajuana vizuri sijakulupuka" alisema Pentzel


Akizungumzia sababu za kutotangaza harusi yake alisema ameamua kutofanya hivyo ili kuepusha maneno na vizuizi vya ndoa yake ambavyo vingeweza kuibuka na kupoteza mawazo ya mumewake huyo


Alisema kuwa hakutaka hali hiyo itokee ndio maana akaamua kufanya iwe siri na ya kushutika ili wambaya wake wakose nafasi ya kufanya jambo lolote baya na kwa sasa baada ya harusi hiyo ndio vikao kwa ajili ya kufanya sherehe hiyo vinapangwa

PICHA ZAIDI YA HALI ILIVYO SASA KWENYE JENGO LA GHOROFA LILILOANGUKA KATIKATI YA JIJI, DAR


Ni moja ya Kifaa pekee kilichokuwepo eneo hilo Trekta, likifukua kifusi ili kuokoa watu wanaodaiwa kufukiwa na kifusi hicho.
Baadhi ya watu waliwahi kufika kujaribu kutoa msaada bila mafanikio hapa wakiwa wamekwama baada ya kukosa vifaa vya kutosha.
Wahindi nao walikuwapo kutoa msaada hapa wakilielekeza Trekta kusogea mahala walipo wao wakihisi kuwa kuna mtu mahala hapo.

BEAKING NEEEEEWZZZZZZZZ!!!!! GHOROFA LIMEANGUKA MITAA YA ILIGANDI K/KOO

Mpaka sasa watu watu 12 wameshapoteza maisha,limedondokea msikiti wa SHIA.
Mpaka sasa eneo la tukio kuna mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na meya,Mmiliki wa jengo hilo bado hajajulikana.Ndani ya jengo hilo kulikuwa na watu wasio pungua 60 wakiendelea na ujenzi.Watu zaidi ya 14mpaka sasa wameshakimbizwa hospitali. Tutaendelea kuwajulisha zaidi.
Chanzo bado hakijajulikana waokoaji wako wanaendelea na shughuli za uhokoaji zinaendelea..
Limeangukia msikiti na ndani kulikuwa na watoto,mpaka sasa watu 10 wameshakimbizwa hospital.Jengo hilo lilikuwa linaendelewa kujengwa lina golofa 16.
              
Picha kutoka K/KOO eneo la tukio. Picha Irene Mwamfupe

UZINDUZI WA TAWI LA YANGA MAREKANI


TUNAPENDA KUWATANGAZIA RASMI MASHABIKI, WADAU NA WAPENZI WOTE WA TIMU YETU YA SOCCER YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB MLIOPO MAREKANI KUWA TUNAZINDUA RASMI TAWI LETU HAPA MAREKANI LITAKALO JULIKANA KAMA YOUNG AFRICANS FAMILY USA. TUNAOMBA UKIPATA TANGAZO HILI MWARIFU NA MWENZIO.

TAREHE: JUMAMOSI 03/30/2013 

MAHALI: KILIMANJARO PASSION RESTAURANT

ADDRESS: 2310 PRICE AVENUE, WHEATON,MD 20902

MUDA:  4:00 PM

KWA MAWASILIANO: 
ALEX KASSUWI : TEL :301 305 9685

YOUNG AFRICANS "DAIMA MBELE NYUMA MWIKO"

SHIRIKISHO LA FILAMU TANZANIA LAMSHUSHIA PONGEZI WEMA SEPETU..


SHIRIKISHO la Filamu Tanzania (TAFF) limempongeza msanii wa kike Wema Sepetu kwa moyo wa upendo aliouonyesha kwa msanii mwenzie Kajala Masanja kwa kumlipia faini ya sh. milioni 13 alizotozwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokana na kupatikana na hatia katika kesi ya utakatishaji fedha iliyokuwa inamkabili mahakamani hapo

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wengine rais wa shirikisho hilo Simon Mwakifwamba alisema kuwa imani na moyo wa upendo aliokuwa nao msanii Wema ndio uliomsukuma kumlipia kiwango hicho cha fedha bila ya kujiuliza mara mbili kitendo hiko kimeonyesha jinsi gani wanavyohitaji kushirikiana katika matatizo.

LEO NI IJUMAA KUU

INAPOFIKA saa tisa alasiri, siku kama ya leo, maarufu kama Ijumaa Kuu, katika nyumba za ibada za Kikristo, kimya hutanda, mishumaa huzimwa na kuashiria kuwa ni siku ya majonzi.

 http://www.topnews.in/usa/files/jesus-crucifixion-full.jpg
Ijumaa Kuu ni siku ambayo Wakristo duniani kote hukumbuka mateso aliyoyapata Yesu baada ya kusulubishwa msalabani yapata zaidi ya miaka elfu mbili iliyopita. Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimeipa thamani siku hii kwa kuitangaza kuwa ya mapunziko.

Siku hii huadhimishwa kwa ibada inayoambatana na kusoma mistari ya Biblia inayoelezea undani wa matukio yaliyosababisha kusulubiwa kwa Yesu Kristo.

FILAMU YA SISTER MARRY KUINGIA SOKONI MUDA WOWOTE.

Ray amesema kuwa filamu yake ya SISTER MARRY iliyozua kasheshe na viongozi wa kidini kutoka kanisa katoliki hivi karibuni haijazuiliwa kabisa bali ameambiwa arekebishe baadhi ya vipande katika filamu hiyo hivyo mashabiki wake wakae mkao wa kula filamu hiyo itaingia sokoni kila kitu kikikamilika. The film stars Vicent Kigosi(Ray), Irene Uwoya, Blandina Chagula(Johari) and Grace Mapunda.

CAG akabidhi Ripoti ya ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2011-2012 kwa Rais Kikwete.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) Bwana Ludovick Utouh akikabidhi Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2011-2012 kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo.(picha na Freddy Maro).

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...