Sunday, March 17, 2013

Dk. Slaa aivuruga CCM


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kauli ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa kwamba kuna baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola wanaripoti kwake, kimesababisha baadhi ya wananchi kukosa imani na vyombo hivyo.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkoa Maalum wa CCM Dar es Salaam baada ya kikao chao kutathimini mambo na matukio mbalimbali yanayolitikisa taifa kwa sasa.
Katika taarifa yao iliyosainiwa na Katibu wa Wilaya ya Dar es Salaam (ya kisiasa - CCM), Daniel Zenda ilisema kuwa Dk. Slaa amekuwa akitoa kauli hizo mara kwa mara tangu wakati wa kampeni za urais mwaka 2010, lakini hajaitwa kuulizwa wala kuchukuliwa hatua.
“Lakini pia kauli ya Dk. Slaa imesababisha wananchi wakose imani na Idara ya Usalama na zaidi kupoteza imani juu ya uwezo wa serikali kuwalinda na kuwahakikishia usalama wa maisha yao, ambapo ni jukumu la kikatiba la serikali,” ilisema taarifa hiyo.

Rais Kikwete apokea Ujumbe maalumu toka kwa Rais wa Botswana.


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Botswana uliowasilishwa na  Waziri wa Mambo ya Nje ya nchi hiyo Mhe Pandu Skelemi Ikulu jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Botswana uliowasilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje ya nchi hiyo Mhe. Pandu Skelemi Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na  Waziri wa Mambo ya Nje wa Botwana Mhe Pandu Skelemi baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa nchi hiyo jana Ikulu jijini Dar es salaam.(PICHA NA IKULU).

Papa Francis akataa vitu vya kifahari

Siku chache baada ya kuchaguliwa kuwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amewashangaza wengi mengi kwa kukataa kuvaa viatu vya kifahari na msimamo wake kuwekwa wazi kuwa hatavumilia makasisi watakaotenda uovu.
 
 Papa Francis 1
Tayari, Papa Francis ameelezwa kuwa kiongozi asiyetaka makuu, mhafidhina na mtu ambaye hataweza kubadili mengi katika kanisa hilo lenye waumini bilioni 1.2 duniani.
Katika siku mbili za uongozi wake, Papa Francis amelithibitisha hilo kwa kutokea hadharani akiwa amevaa viatu rahisi, vyeusi na kuachana na vyekundu vya kifahari vilivyopendelewa na mtangulizi wake, Benedict VXI.
Kutoka Uk 1

Katika uongozi wake, siku zote Papa Benedict, alivaa viatu vyekundu vilivyotengenezwa kwa mkono, jambo ambalo Papa Francis anaonekana kuachana nalo.
Watu walio karibu naye Papa Francis, wanaeleza kuwa kabla ya kuondoka Buenos Aires, Argentina kwenda Rome, Kardinali Jorge Mario Bergoglio, kama alivyojulikana awali, alivaa viatu rahisi vya rangi nyeusi, na kuwafanya marafiki zake, wakiwamo mapadri kutaka kumnunulia viatu vingine vipya.

“Siku ile aliyoondoka mjini Buenos Aires kuelekea Rome kwa ajili ya mkutano wa uchaguzi wa Papa (conclave), marafiki zake walimpa zawadi ya viatu. Yeye, siku zote amekuwa akitokea hadharani akiwa amevaa nguo rahisi, viatu vya kawaida,” walieleza mapadri hao kutoka Amerika Kusini walipozungumza na Kituo cha Redio Vatican.
Mbele ya makardinali 106
Juzi Ijumaa alipokutana na makardinali 106, kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 76, licha ya kuonyesha uso wa furaha na kuwatania aliwaonya makardinali hao kuhusu wajibu wao kama viongozi wa kanisa maeneo mbalimbali duniani akiwataka kutosahau kuwa hawarudi kwenye ujana.


Katika ukumbi wa Sala Clementina, ulioko Vatican Papa Francis pia aliwataka makardinali hao wakiwamo waliomchagua kuwategemea zaidi vijana aliosema ndio nguzo kuu muhimu ya ustawi wa Kanisa Katoliki, huku aliwashauri makardinali kusaka njia sahihi ya kueneza Ukristo pande zote za uso wa dunia katika karne ya 21.
Aidha, alimsifu mtangulizi wake, Papa Benedict kwa uamuzi wa kijasiri wa kustaafu, akieleza kuwa ni uamuzi wa busara, wenye kuonyesha ukomavu na kuwataka wasichoke kuiga matendo mema.
Yaliyomo kitabuni mwake

Kupitia kitabu, On Earth and Heaven (Duniani na Mbinguni) alichokiandika akiwa kardinali, Papa Francis alitoa taswira yake kama mtu mwenye dhamira safi hasa katika masuala ya kusaidia jamii, muumini thabiti anayeamini katika majadiliano baina ya makundi ya imani tofauti.

Msimamo kuhusu makasisi
Papa Francis ameonyesha wazi kuchukizwa na matendo ya makasisi (mapadri) wasio waadilifu, ambao kwa miaka mingi wamelifedhehesha kanisa na kwamba yeye hakubaliani na wanaoficha maovu ya baadhi ya mapadri ukiwamo ulawiti.
“Suala la useja (mapadri kutokuoa) kwamba ndicho chanzo cha ulawiti linaweza kusahaulika,” anaeleza katika kitabu hicho. “Endapo padri ni mlawiti, alikuwa hivyo hata kabla ya ukasisi wake. Lakini, hili linapotokea, lisiangaliwe kwa mtazamo tofauti, lisifichwe. 

Kama kiongozi, hutakiwi kutumia madaraka yako kuangamiza maisha ya mwingine.”
Kuhusu hatua gani atachukua, wakati akiwa Kardinali Bergoglio, alijibu kuwa hawezi kukubaliana na waovu, lakini alipoulizwa kama askofu angechukua hatua gani dhidi ya mapadri wa aina hiyo, alijibu,” Nitamfukuza kazi, kisha kumshtaki, jukumu langu ni kuweka usafi wa kanisa mbele.
“Hili ni suluhisho kwa matukio kama hayo kama jinsi ilivyopendekezwa Marekani; lakini si kuwahamisha wakosaji kutoka parokia moja kwenda nyingine.
“Huu ni upuuzi, kwani hata huko wataendeleza tatizo hilo. Jibu sahihi kwa tatizo hili ni kutowavumilia.”

Katika kitabu hicho, Papa Francis anazungumzia maisha ya utauwa (usafi wa moyo), uadilifu na maovu akiweka wazi msimamo wake usio wa mzaha na kuruhusu mijadala baina ya makundi ya imani tofauti, msimamo ambao unaweza kupingwa na baadhi ya Wakatoliki wenye msimamo mkali.Kwa maneno yake, Papa Francis anaonyesha kuwa mtu mwenye akili, anayefikiri haraka, mjuzi wa mambo, anayechanganya uhafidhina wa kijamii na akiwa mwenye msimamo mkali wala kutokukubali upuuzi kwa mambo asiyoyapenda au kuyakubali.

Kiongozi huyo ameahidi kutumia Jumamosi ya Machi 23 kumtembelea mtangulizi wake, Papa Benedict katika jumba analoishi huko Castel Gandolf, kusini mwa Rome na anaeleza kuwa kanisa limepitia nyakati ngumu. “Kumekuwa na vipindi vingi, majaribu mengi. Kumekuwa na vipindi vigumu, lakini, kanisa limesimama imara.”
Hata hivyo, katika misa yake ya kwanza, Alhamisi, Papa Francis alieleza kuwa kanisa hilo halina budi kwenda na wakati, kukubali mabadiliko.

“Ni dhahiri kuwa katika historia yake, kanisa limebadilika mno, sioni sababu za kwa nini tusikubali mabadiliko na kuwa utamaduni wetu wa sasa,” anaeleza.
Alieleza kuwa mafundisho ya msimu ya Kikatoliki, msimamo kuhusu mashoga, ndoa za jinsia moja, hayawezi kubadilika.
Pia, anaeleza kuwa utoaji mimba ni tatizo la kisayansi zaidi, lakini ambalo haliwezi kukubaliwa na kanisa.
Kuhusu utandawazi, Papa Francis alieleza kwamba hakubaliani nao kwa kuwa mfumo huo hauheshimu tamaduni. “Aina ya utandawazi unaofanya vitu vyote kuwa sawa ni aina ya unyama,” anaeleza akiongeza kwamba tofauti za kitamaduni hazina budi kudumishwa.
“Hatimaye, utandawazi unageuka njia ya kuwatumikisha wengine,” alisema.

BALOZI KAMALA AKUTANA NA WATANZANIA WAISHIO UHOLANZI

IMG_1539Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania waishio Uholanzi (TANE), Bw. Musuto wa Chirangi  (aliyesimama) akizungumza wakati wa kumkaribisha Balozi Kamala.IMG_1548Mwenyekiti wa TANE, Bw. Kweba Bulemo (aliyesimama Kulia), akisema machache kabla ya kumkaribisha Mhe. Balozi.

Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe Atua Shinyanga, tayari kuzindua Kanda ya Ziwa Mashariki

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kakola, mahali ambapo mgodi wa dhahabu wa Buzwagi unapatikana, Emmanuel Bombeda anayetokana na chama hicho, wakati kiongozi huyo mkuu wa CHADEMA alipokuwa akisalimiana na viongozi mbalimbali wa chama hicho, baada ya kuwasili mkoani Shinyanga, kwenye kikao cha Baraza la Uongozi Kanda ya Ziwa Mashariki (Mara, Shinyanga na Simiyu). Mbowe anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara Mjini Shinyanga, kufanya uzinduzi wa kanda hiyo.

Saturday, March 16, 2013

HEBU ANGALIA WASANII TUNAOWAITA KIOO CHA JAMII


Kuna msemo unasema wasanii kioo cha jamii je ni kweli?hili ni kava linalobeba kazi za wasanii kwa hali kama hii bado tunadhubutu kusema wasanii ni kioo cha jamii? Mimi naona waitwe waharibifu wa jamii kwa halii hii. Hapa watoto wanajifunza nini kwa kweli?

MWANA FA AITAKA SERIKALI IRUDISHE MFUMO WA ANALOGIA

faaa

Rapper Hamis Mwinjuma aka Mwana FA ambaye March 13 mwaka huu alisherehekea siku yake ya kuzaliwa, ameiomba serikali kuwafikiria mara mbili mbili wasanii na kuachia mifumo yote miwili ya digitali na analojia kwakuwa mfumo wa digitali unawaumiza.

Akiongea na gazeti la Habari Leo, FA amesema kwa sasa wasanii nchini wanaumizwa na mfumo wa digitali kwakuwa wamekuwa wakitumia fedha nyingi katika kutengeneza video, lakini zinaishia kutazamwa na watu wachache tu wenye ving’amuzi.

“Waachie mifumo yote kwani kila mtu atakuwa na uamuzi wa kufanya, kutokana na ubora wa kazi,” alisema Mwana FA.

Alisisitiza kuwa huenda akasubiri hata miezi miwili na zaidi, kama serikali itakubali kuachia mifumo yote miwili wa digitali na analojia, na kama hawatotaka, basi ataachia hivyo hivyo kwa kuwa hawezi kukaa nayo ndani.

BAADA ya UKIMNYA KWA MDA MREFU HATIMAYE AGNESS MASOGANGE ATUPIA PICHA ZAKE INSTAGRAM.AMEPENDEZAJEE


CHECK OUT ALICHOKISEMA LULU KUHUSU MAREHEMU STEVEN CHARLES KANUMBA.

Leo kutoka akaunti ya Twitter ya  msanii wa filamu(Boongomovie) amefunguka na juu ya aliyekuwa mpenzi wake marehemu Steven Charles Kanumba ambae kifo cha mraehemu kilichosababisha yeye kuingia gerezani  sasa hiki ndicho alicho kiandika kupitia ukurasa wake huo wa mtandao wa kijamiaa Twitter 


BASI LA NDENJELA LAUNGUA MOTO LIKIWA SAFARINI MAENEO YA KIBAHA LEO HII


Basi la Ndenjela likiwa linatoka Dar kuelekea Mbeya limeteketea kwa moto Kibaha Kongowe asubuhi ya leo. Abiria wote wamenusurika janga hilo.MIZIGO IMTEKETEA KATIKA JANGA HILO

MASTAA WAANDAA MKESHA KUMUOMBEA KAJALA

Stori: Sifael Paul
ZIkiwa zimebaki siku 8 tu kabla ya hukumu ya staa wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja kusomwa Machi 25, mwaka huu, inasemekana kuwa baadhi ya mastaa wa filamu na muziki Bongo, wameandaa mkesha wa kumuombea ili hukumu hiyo iende vizuri na aachiwe  huru arudi uraiani.
Kajala anakabiliwa na kesi ya kutakatisha fedha haramu kwa kuuza nyumba iliyokuwa imewekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa kushirikiana na mumewe, Faraji Agustino.
Kwa mujibu wa mwigizaji mmoja maarufu wa kiume, tayari ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) na ujumbe kupitia mitandao ya kijamii umeanza kusambazwa kwa baadhi ya mastaa hao ambao kila mmoja anaonesha kuwa tayari kwa ishu hiyo ya kumuomba Mungu amsaidie Kajala.



Mwigizaji huyo ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, alidadavua kuwa wanachotafuta kwa sasa ni mahali au nyumba ya ibada kwa ajili ya kufunga na kumwombea Kajala kuanzia saa 2:00 usiku hadi asubuhi.
“Mwanzoni ilikuwa ni kuhamasishana tu kumkumbuka Kajala katika sala zetu za kila siku kama ilivyokuwa kwa Lulu (Elizabeth Michael), lakini sasa tumeona ni vema tukakutana kwa pamoja tumlilie Mungu ili hukumu yake imuendee vizuri,” alisema mwigizaji huyo na kuongeza:

“Yah! Kajala anatia huruma sana ndiyo maana kuna wasanii ambao ni watu wa karibu yake, wapo tayari kwa ajili ya mkesha wa maombi kama (Jacqueline) Wolper, Irene Uwoya, Patcho Mwamba, JB (Steven Jacob), Ray (Vincent Kigosi), Richie (Single Mtambalike), Dude (Kulwa Kikumba) na wengine wengi.”

Katika kesi hiyo iliyopo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar, Kajala amesota Segerea kwa takribani mwaka mmoja ambapo sasa hatma yake itajulikana tarehe tajwa hapo juu. 

CHUCHU HANS: NIMEANZA KUIGIZA TANGU NIKIWA MDOGO

Tangu akiwa mdogo alikuwa anaigiza na kufanya umiss wakati alipokuwa shuleni mkoani Tanga. Chuchu who has acted in many films including Lose Control, Hit Back and Tone la Damu. 

 Mshindi huyo wa taji la Miss Tanzania talent in 2005.Kiukweli mimi toka utotoni nilikuwa na kipaji cha u-miss na kuigiza  nimeanza tangia shule Tanga nilikuwa naigiza maigizo na nafanya fashion shows so naamini nilikuwa na talent that's y nilivyoingia miss Tanzania pia niliweza kutwaa taji la Miss Tanzania Talent Tanzania 2005" . Some of  her upcoming films include Mimba by Chekibud, Safari produced by Rich and her own film Raula.

US Hip Hop Rapper Lil Wayne is Recovering After Seizures.

The hip hop star tweets that he is “good” after suffering a reported seizure that led to claims he was in a coma and near death.
Grammy-winning hip hop star Lil Wayne has said he is recovering and has thanked fans for their concern after he suffered a reported seizure.
 One of the Celebrity news website claimed the star was in critical condition in Los Angeles after being admitted to hospital twice this week.
 In a message from his official Twitter account Lil Wayne said: “I’m good everybody. Thx for the prayers and love.”
 The 30-year-old rapper, who has a history of seizures, was first rushed to Cedars Sinai hospital on Tuesday after suffering multiple episodes, it said.
 He left the following day but was re-admitted hours later.
 His spokeswoman Sarah Cunningham said in an email that “Lil Wayne is recovering,” but did not specify what he was suffering from.
In October last year, the star, who won four Grammy awards in 2008 including best rap song and best rap album, reportedly suffered a number of seizures while on his private jet.

Wazimbabwe wanapiga kura ya maoni leo huku wanachama wa upinzani wakidaiwa kushambuliwa.

Wananchi wa Zimbabwe leo wanapiga kura ya maoni kuhusu katiba mpya ambayo itaweka kikomo cha muhula wa urais na kuongeza uhuru wa vyombo vya habari. 
Hata hivyo, wasiwasi umeongezeka baada ya wanachama kadhaa wa chama cha upinzani cha Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai kushambuliwa wakati wakifanya kampeni katika kitongoji cha Mbare kwenye mji mkuu Harare, hapo jana.
Msemaji wa chama hicho cha Movement for Democratic Change-MDC, Douglas Mwonzora, amewashutumu wafuasi wa Rais Robert Mugabe kuhusika na tukio hilo.
Katiba hiyo mpya itadhibiti mamlaka ya Rais Mugabe na kuweka misingi ya kufanyika kwa uchaguzi mwezi Julai, mwaka huu.
Uchaguzi huo utahitimisha makubaliano yaliyokumbwa na matatizo ya kugawana madaraka kati ya Rais Mugabe na Waziri Mkuu Tsvangirai.-DW.

MNYIKA::Tutaandamana kudai maji

MBUNGE wa Ubungo John Mnyika leo ataongoza maandamano ya amani kwenda Wizara ya Maji kupata majibu kuhusu matatizo ya maji, licha ya kuzuiwa na Jeshi la Polisi. 
Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kinondoni, ACP Charles Kenyela amekataza maandamano na mkutano huo kwa madai kuwa eneo la Manzese Bakhresa walilopanga kufanyia mkutano ni maegesho ya magari ya mizigo. 
Akizungumza kwa niaba ya Mnyika, mratibu wa maandamano hayo kutoka ofisi ya mbunge, Gaston Garubindi, alisema kuwa maandalizi yamekamilika na mbunge huyo ataongoza kama ilivyopangwa. 
Garubindi alisema kuwa Kenyela amewadanganya wananchi kwa kueleza kuwa Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe hakuwa na taarifa wakati ofisi ya mbunge ilimwandikia barua yenye kumbukumbu namba OMU/MJ/001/2013 na nakala nyingine kupelekwa kwa viongozi wengine wa wizara hiyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...