Saturday, March 16, 2013

MNYIKA::Tutaandamana kudai maji

MBUNGE wa Ubungo John Mnyika leo ataongoza maandamano ya amani kwenda Wizara ya Maji kupata majibu kuhusu matatizo ya maji, licha ya kuzuiwa na Jeshi la Polisi. 
Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kinondoni, ACP Charles Kenyela amekataza maandamano na mkutano huo kwa madai kuwa eneo la Manzese Bakhresa walilopanga kufanyia mkutano ni maegesho ya magari ya mizigo. 
Akizungumza kwa niaba ya Mnyika, mratibu wa maandamano hayo kutoka ofisi ya mbunge, Gaston Garubindi, alisema kuwa maandalizi yamekamilika na mbunge huyo ataongoza kama ilivyopangwa. 
Garubindi alisema kuwa Kenyela amewadanganya wananchi kwa kueleza kuwa Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe hakuwa na taarifa wakati ofisi ya mbunge ilimwandikia barua yenye kumbukumbu namba OMU/MJ/001/2013 na nakala nyingine kupelekwa kwa viongozi wengine wa wizara hiyo.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...