Taasisi ya Mwalimu Nyerere
imesema kuwa wanaotaka aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, Jaji Joseph Warioba akae kimya kuhusu Katiba Inayopendekezwa
hawana hoja.
Imesema kuwa wanaosema hivyo hasa wale wa chama
tawala (CCM) wanatakiwa kujiuliza kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita
wamefanya nini kuhusu Katiba, ikisisitiza kuwa itaendelea kufanya
midahalo ya kuwaelimisha Watanzania kuhusu mchakato wa Katiba ili
utakapofika wakati wa kura ya maoni waelewe kipi wanatakiwa kukifanya
kwa mustakabali wa taifa.
Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Joseph Butiku
alisema hayo jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam katika mahojiano
maalumu na gazeti hili kuhusu kazi na majukumu ya Taasisi ya Mwalimu
Nyerere tangu ilipoanzishwa hadi sasa. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza
kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz













Mkurugenzi Mstaafu waTaasisi ya Utafiti ya Twaweza, Rakesh Rajan (kulia)
akiwaelezea jambo Mwenyekiti wa Bodi ya Uhariri ya Raia Mwema, Jenerali
Ulimwengu (kushoto) na Mkurugenzi wa Compass Communication Limited,
Maria Sarungi katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa kabla ya taasisi hiyo
kutangaza matoke ya utafiti wao kuhusu Tanzania Kuelekea 2015, jijini
Dar es Salaam juzi.







