Friday, November 14, 2014

MBOWE AMTAKA KIKWETE AVUNJE BARAZA LA MAWAZIRI


Rais Jakaya Kikwete akiteta jambo na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe. Picha na Maktaba 

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amemtaka Rais Jakaya Kikwete kulivunja Baraza la Mawaziri na kuunda jipya kutokana na tuhuma za ufisadi.

Katika taarifa yake aliyoitoa jana kwa vyombo vya habari baada ya mikutano yake katika mikoa ya Magharibi alisema ni lazima hatua hiyo kuchukuliwa ili kukabiliana na mafisadi ambao hakuwataja, vinginevyo alisema Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni anayoiongoza, itaanza maandalizi ya kuwasilisha bungeni, hoja ya kutokuwa na imani naye.

Alisema Serikali imekuwa ikishindwa kuchukua hatua za ufisadi ambazo zinawakabili watendaji wake: “Kambi ya Upinzani Bungeni inamtaka Rais Kikwete kumfukuza kazi Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mawaziri wake na kuunda Serikali mpya.” Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Hivi karibuni, Mbowe alitoa tuhuma nzito kuhusu ufisadi katika ujenzi na bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam akisema kuna ufisadi umefanywa na vigogo wa Serikali wakiwamo baadhi ya mawaziri.

Alisema mradi huo ulitakiwa kugharimu Sh1.2 trilioni lakini vigogo hao wakaongeza kiasi kama hicho na sasa unagharimu Sh2.4 trilioni. Alitaka kuteuliwa kwa taasisi ya kimataifa ya ukaguzi ili kufahamu thamani halisi ya ujenzi wa bomba hilo.

Alisema kutokana na ufisadi huo na mwingine katika Akaunti ya Tegeta Escrow, ni dhahiri kuwa Baraza la Mawaziri limeshindwa kazi ya kumsaidia Rais.

Mbowe amnanga Zitto

Katika mkutano wa juzi mjini Kigoma, Mbowe alimzungumzia aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe akisema alimsaidia kuhakikisha anashinda ubunge wa Kigoma Kaskazini mwaka 2005 lakini akakosa shukrani.

Akihutubia mamia ya wakazi wa Kata ya Kalinzi iliyopo katika Jimbo la Kigoma Kaskazini, Mbowe alisema hamchukii Zitto kama baadhi ya watu wanavyofikiri, bali mbunge huyo alikiuka maadili ya chama hicho akavuliwa uongozi. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

“Nilimshauri Zitto Kabwe akagombee katika Jimbo la Kigoma Kaskazini, lakini akaniambia kwamba hawezi kufanya hivyo kwa sababu hana fedha, nikampa fedha za kutosha, nikampa gari Toyota Hilux la kuzungukia katika jimbo na akawa mbunge.

Alisema gari hilo hajawahi kulirudisha hadi leo na yeye hakumuuliza kwa sababu alimchukulia kama ndugu yake... “Zitto ni kama mdogo wangu, amelala na kula nyumbani kwangu, nyumba yangu ilikuwa kama yake, nashangaa anakosa shukrani.”

Alisema kabla ya kugombea alimlipia nauli kutoka Ujerumani kurudi nchini kwa ajili ya kutafuta nafasi hiyo ya ubunge, hivyo anashangaa mtu wa aina hiyo amchukie kwa lipi.
Mbowe alisema Mkoa wa Kigoma umebahatika kuwa viongozi wa upinzani wenye uwezo lakini wamekuwa wakiwasaliti wananchi wa mkoa huo.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu alisema uchaguzi wa serikali ya vijiji, mitaa na vitongoji kiwe kipimo cha kuing’oa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Aliwataka vijana kufanya uamuzi sahihi kwenye uchaguzi huo kwa kuvichagua vyama vinavyounda Ukawa kwa kuwa CCM imewatelekeza.
Zitto ajibu
Akizungumzia madai ya Mbowe, Zitto alisema ni utoto kwenda kumtangaza kwamba alimsaidia... “Yeye Mbowe anajua nilivyomsaidia pia lakini kwa kuwa nimelelewa kwa maadili mema na wazazi wangu siwezi kumtangaza. Ila muulizeni alikuwa na hali gani baada ya uchaguzi wa mwaka 2005 na nilimsaidia nini?
“Nimeshangazwa na tabia hiyo ya kusimanga tena kunisimanga kwetu, nyumbani kwetu. Hata hivyo, nimepuuza maana kwa vyovyote vile aliongea bila kufikiri.
“Anasema nilitaka kusaliti chama, aseme kwa ushahidi maana kutamka tu hakuna maana kitu hata kidogo.”
Alisema kiongozi mkubwa kama Mbowe anapaswa kujadili masuala ya Taifa na namna ya kutatua changamoto si, kusema watu na kuwasimanga.
“Nimeibadilisha Kigoma na kusimamia ujenzi wa miundombinu ya barabara, madaraja na viwanja vya ndege. Yeye kafanya nini Hai? Nimewezesha wakulima wangu kuwa na hifadhi ya jamii, bima ya afya na kukuza uzalishaji, yeye kafanya nini Hai?
Nimeibua hoja bungeni za maana ikiwamo kubadili sheria kwa manufaa ya nchi. Yeye kafanya nini bungeni tangu aingie, ametoa hoja gani binafsi, ametunga sheria gani binafsi? Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...