Wednesday, February 13, 2013

BENKI YA NMB YATAHADHARISHA WATEJA WAKE

DAR ES SALAAM, Tanzania

MENEJIMENTI ya NMB imewaonya wateja wake na umma kwa ujumla kuwa imegundua kwamba kuna taasisi inayojitambulisha kama Tanzania Loans Society inadai kuwa mshirika wa benki hiyo katika kutoa huduma za kibenki.

Taasisi hiyo imedaiwa kuwa kwa kutumia mtandao wake wa intaneti imekuwa ikijinasibu kutoa mikopo ambayo fedha zake zimeidhinishwa na NMB kupitia kwa mameneja wa matawi.

Aidha, Tanzania Loan Society pia inadaiwa kueleza kwamba fomu za maombi ya mkopo na malipo ya usajili vinaweza kulipwa kwa  kutumia namba ya simu ya mkononi.

Menejimenti ya NMB imezidi kuwatahadharisha wateja wake na umma kwa ujumla kwamba haina ushirika au makubaliano yoyote na taasisi hiyo katika shughuli  zake.

Imeongeza kuwa, NMB hutoa mikopo yake kupitia matawi yake tu, na hakuna  namna yoyote ambayo inaweza kusababisha gharama za  maombi ya mikopo au mikopo kutolewa kupitia simu za mkononi.

Menejimenti hiyo imesisitiza  kuwataka  wateja na umma kwa ujumla kutojihusisha na taasisi  hiyo katika shughuli yoyote inayoihusu Benki ya NMB na kwamba haitahusika kwa namna yoyote  na matatizo yatakayojitokeza

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...