Sunday, November 26, 2017

RAIS MAGUFULI ATOA SIKU SABA KWA VYOMBO VYA UCHUNGUZI KUBAINI MMILIKI WA MAGARI YALIYOTELEKEZWA BANDARINI

Haya ndio maagizo ya Rais John Pombe Magufuli Bandarini leo baada ya kugundua uwepo wa magari zaidi ya 50 yaliyoingizwa nchini kwa kutumia jina la Ofisi ya Rais.

Saturday, November 25, 2017

TAZAMA VIDEO YA WAZIMBABWE WAKIIGIZA JINSI MUGABE ALIVYOLAZIMISHWA KIJIUZULU

Subscriber to our channel on YouTube @jambotz upate video nyingine zaidi.

PROF. LIPUMBA "SIKUTEGEMEA KAMA DR. SLAA ATATEULIWA"

Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amezungumzia uteuzi wa Dk. Wilbroad Slaa kuwa balozi akisema hakutarajia.

Rais John Magufuli juzi alimteua Dk. Slaa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa Chadema kabla ya kukihama chama hicho wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Wakati wa mchakato wa uchaguzi huo, Profesa Lipumba na Dk. Slaa ambao vyama vyao vilikuwa katika umoja uliojulikana Ukawa, walijiondoa baada ya Chadema kumpitisha Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.

Akizungumza na Mwananchi jana, Profesa Lipumba alisema, “Imekuwa kama surprise, sikutegemea kama Dk. Slaa atateuliwa kwa sababu muda mwingi yupo Canada”.

Hata hivyo, Profesa Lipumba alisema hana shaka na uteuzi huo “Narudia, sikutegemea. Ila popote atakapopangiwa kazi Dk. Slaa atafanya kwa sababu najua ni mchapakazi,” alisema.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema Rais Magufuli ana mamlaka kisheria ya kumteua mtu atakayemuona anafaa katika nafasi fulani.

FAMILIA YAPATA UPOFU KATIKA MAZINGIRA TATANISHI

(Picha hii haihusiani na tukio)

Mama mmoja aliyetambulika kwa jila la Doroth Otieno na watoto wake watatu wanaoishi Kisumu nchini Kenya, wamepata upofu wa ghafla bila kujua chanzo chake.

Doroth ambaye ameolewa na mkata miwa nchini Kenya, amesema hali hiyo imeleta matatizo kwenye ndoa yake na familia.

Akisimulia jinsi alivyopata upofu wake huo Doroth amesema mtoto wake wa kwanza nwenye miaka 16 na mwanafunzi wa kidato cha kwanza sekondari ya wasichana ya Nyamonye, alipata upofu ghafla baada ya kuhisi kama macho yake yana mchanga, na kisha kuwa kipofu kabisa, huku watoto wake wawili wa kiume Vicent na Benson nao wakiwa na tatizo hilo hilo.

MUGABE NA MKEWE WASUSIA SHEREHE ZA KUAPISHWA RAIS MPYA

 Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkewe Grace walikosa kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mpya wa nchi hiyo Emmerson Mnangagwa baada ya wananiasa hao kukubaliana kwamba Mugabe anaweza kupumzika.

Sababu kuu ilioteolewa ni kwamba bwana Mugabe alikuwa amechoka.
Mugabe na mkewe Grace hawajaonekana hadharani tangu kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 kujiuzulu kama rais kufuatia shinikizo kutoka kwa jeshi na raia.

Hatua hiyo inajiri baada ya Mugabe na mkewe kufumta kazi rais huyo mpya wakati alipokuwa makamu wa rais kwa madai kwamba alikuwa akipanga njama za kutaka kumuondoa madarakani rais Mugabe.

Saturday, November 18, 2017

WALEMAVU DAR WAANZA KUPATA NEEMA.

Hospitali ya CCBRT imeguswa na kampeni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ya kutafuta miguu bandia kwaajili ya watu wenye uhitaji kwa kuwapatia matibabu wagonjwa 35 waliokatwa miguu kutokana na ugonjwa wa kisukari.
Miguu hiyo ya kisasa ina thamani ya zaidi ya Shilling Million 157 ambapo kati ya wagonjwa 35 waliokuwa wakitembelea magongo kwa muda mrefu baada ya kukatwa miguu, 21 wameshawekewa Miguu Bandia na sasa wanaendelea na shuguli zao baada ya kuwa wazima.

Tuesday, November 14, 2017

TAZAMA VIDEO YA DR. SHIKA AKIREJEA NYUMBANI KWAKE KUTOKA KITUO CHA POLISI ALIPOKUWA AKISHIKILIWA


Dkt. Luis Shika akiwasili nyumbani akitokea Polisi.
Afafanua kwanini hakuweza kulipa 25% iliyokiwa mnadani adai tatizo ni kutokuelewana.

Monday, November 13, 2017

LULU AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MIWILI JELA

Mahakama kuu ya Dar es salaam imemuhukumu muigizaji wa filamu, Elizabeth Michale, maarufu kama 'Lulu', kifungo cha miaka miwili baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba.

Marehemu Steven Kanumba alifariki majira ya saa nane usiku, mnamo mwaka 2012 baada ya kutokea mzozo kati yake na Elizabeth Michael ambaye inaaminika kuwa walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi.
Kanumba, ambaye alijizolea umaarufu mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati na hadi Afrika Magharibi baada ya kuwashirikisha katika filamu zake baadhi ya wasanii maarufu wa kutoka Nigeria akiwemo Mercy Johnson na Noah Ramsey.

Wednesday, November 08, 2017

MCHUNGAJI AWANANGA WANAWAKE WANAOONGEZA MAKALIO NA MAZIWA

Huu ni ushauri wa bure kwa wote wenye tabia ya kubadili uumbaji wa Mwenyezi Mungu. Share ili wenye tabia hiyo wajifunze na kuacha.

Sunday, November 05, 2017

MAAJABU: MCHUNGAJI ATUMIA POMBE KUBATIZA WAUMINI

Mchungaji mmoja huko Afrika Kusini amekuwa akikosolewa vikali baada ya kuanza kubatiza washirika kwa kutumia vilevi ambavyo wanavipenda kitendo ambacho ni kinyume na utaratibu.

Askofu Tsietsi Makiti, (52) ambaye pia  ni Mwanzilishi wa kanisa hilo linalojulikana kama 'Gabola', amesema kuwa ameongozwa na maandiko katika Biblia ambapo Yesu alibadilisha maji kuwa divai.
"Watu wanao kunywa na kubatizwa na bia wana furaha na amani. Hii inamaanisha kuwa wanaishi katika kivuli cha Mungu, "alisema Makiti.

Kanisa hilo lenye jina 'Gabola' jina likimaanisha 'Kunywa' limesema linakubali kuwapokea waumini waliotoka makanisa mengine huku likiweka wazi kwamba idadi ya watu wameongezeka kufikia 500 ndani ya miezi miwili tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo.

Waumini pia wanaruhusiwa kunywa wakati huduma za kanisa zikiendelea. Aidha Askofu huyo ameweka wazi kwamba ana mipango ya kuanzisha matawi ya kanisa lake hilo katika miji mbali mbali.

Saturday, October 28, 2017

TAZAMA PICHA ZA MAFURIKO YALIYOATHIRI MAKAZI YA WATU DAR ES SALAAM

Mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha maeneo mengi pwani ya Tanzania imesababisha mafuriko na uharibifu mkubwa.

Katika eneo la Mji Mpya, Kawe, nyumba zimebomoka na baadhi ya maeneo hayapitiki. Nyumba zaidi ya 20 zimeharibiwa vibaya na mafuriko.

Hizi hapa ni baadhi ya picha za hali ilivyo mtaani humo.

WALIOMUINGIZA MTU MWEUSI KWENYE JENEZA AKIWA HAI WAFUNGWA

Wakulima wawili wa Afrika Kusini waliomlazimisha mtu mweusi kuingia katika jeneza akiwa hai wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela.

Theo Martins na Willem Oosthuizen walihukumiwa mnamo mwezi Agosti kwa jaribio la mauaji na utekaji nyara.

Walimtuhumu Victor Mlotshwa kwa kupita katika ardhi, wakamshambulia na kumlazimisha kuingia katika jeneza na kutishia kumchoma akiwa hai.


Kesi hiyo ilizua hisia nchini Afrika Kusini na kuangazia wasiwasi wa ubaguzi wa rangi katika jamii kadhaa za wakulima.

Friday, October 27, 2017

IDADI YA WALIOPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA MARUDIO NCHINI KENYA UTATA MTUPU

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya Wafula Chebukati amesema wanakadiria kwamba idadi ya waliojitokeza kupiga kura jana kufikia wakati wa kufungwa kwa vituo saa kumi na moja jioni ni asilimia 48.

Akihutubia wanahabari, mwenyekiti huyo amesema vituo 87 kati ya vituo vyote vya kupigia kura vilifunguliwa, ambavyo ni vituo 35,564.

Kati ya vituo hivyo, fomu za matokeo kutoka kwa fomu za matokeo kutoka kwa fomu 27,124 zimepokelewa.

"Vituo 5,389 ambavyo vimetapakaa kote nchini havikufunguliwa. Baadhi vimo katika kaunti nne ambazo nilitangaza awali kwamba uchaguzi umeahirishwa," amesema.

VIDEO: RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

Rais John Magufuli amemteua aliyekuwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, huku aliyekuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Ernest Mangu akiteuliwa kuwa balozi.

Dk. Kashilillah ameteuliwa ikiwa ni takriban wiki tatu kupita tangu alipoondolewa katika wadhifa wa Katibu wa Bunge, nafasi iliyochukuliwa na Stephen Kigaigai.
Rais Magufuli Mei 28,2017 alitengua uteuzi wa IGP Mangu na kumteua Simon Sirro kushika wadhifa huo. Mangu anasubiri kupangiwa kituo cha kazi pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Dk Aziz Mlima.

Monday, October 23, 2017

USHAHIDI ALIOUTOA LULU MAHAKAMANI KUHUSU KIFO CHA KANUMBA

Msanii wa filamu, Elizabeth Michael (22) amejitetea katika kesi ya kuuwa bila kukusudia katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Katika utetezi wake, Lulu amesema anakumbuka siku ya tukio ilikuwa Ijumaa ya April 6, 2012 ambapo aliahidiana na rafiki zake kwamba wangetoka usiku.

Amesema kuwa asubuhi ya siku hiyo alienda kuonana na rafiki zake maeneo ya Mikocheni, ambapo pia alikuwa akiwasiliana na Kanumba.

"Marehemu alikuwa ni msanii mwenzangu lakini pia nilikuwa naye na mahusiano naye ya kimapenzi,".

Lulu alisema kuwa marehemu Kanumba alikuwa hapendi kumuona akitoka, hivyo hadi siku ya tukio hakutaka kumwambia kwamba atatoka na rafiki zake.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...