Saturday, July 18, 2015

TUNAWATAKIA EID MUBARAKA WATU WOTE



Leo ni sikukuu kubwa sana duniani... ina maana kubwa sana kwa waislam na watu wote duniani.

Kwakulijua hili Jambo Tz tunachukua nafasi hii kuwatakia sikukuu njema watanzania wote na dunia kwa ujumla.

OBAMA KUTOTEMBELEA KIJIJI CHA BABA YAKE

Barack Obama

#ObamainKenya ndilo neno linalotawala mitandao ya kijamii nchini Kenya huku rais huyo akitarajiwa kulitembelea taifa hilo.

Hata hivyo wakaazi wa kijiji cha Kogelo ambapo babaake Obama alizaliwa na kulelewa sasa hawatalazimika kufanya maandalizi ya aina yoyote kufuatia ziara hiyo baada ya balozi wa Marekani nchini Kenya Robert Godec kusema kuwa rais huyo hatozuru kijiji cha Kogelo.

''Ana mda mchache sana kwa hivyo basi atakuwa nairobi pekee'', alisema bwana Godec akizungumza na runinga ya KTN.

Bibiye Obama Sarah Obama alikuwa amejiunga na wakaazi wa Kogelo akimtaka Obama kuwatembelea kulingana na ripoti za kituo cha habari cha Capital fm.

Friday, July 17, 2015

MSAIDIZI WA NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA AJIUNGA NA CHADEMA

 Bw. Jumanne Juma Msunga.

MSAIDIZI wa Naibu Katibu Mkuu wa (CCM) Bara, Jumanne Juma Msunga ametangaza rasmi kuhama CCM na kujiunga na CHADEMA, kwa madai kuwa CCM ni chama cha kudhulumu haki za wanachama wake. 

Akitangaza uamuzi wake huo jana mbele ya waandishi wa habari kwenye ofisi za CHADEMA Mkoani Singida, Msunga alisema ameamua kujinga na CHADEMA, huku akidai kuwa CCM haikutenda haki katika mchakato mzima wa kumpata Mgombea wa nafasi ya Urais.

Alisema CCM haina shukrani kwani imejaa dhuluma kwani katika mchakato huo baadhi ya Wagombea walikatwa bila kujieleza mbele ya kamati husika.

WATU ZAIDI YA 40 WAFA KATIKA MLIPUKO NIGERIA

Wapiganaji wa Boko haram

Wafanyakazi wa uwokoaji Nigeria wanasema katika eno la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo katika mji wa Gombe watu arobaini wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya milipuko kutokea kwenye soko katika eneo hilo.

Mlipuko wa kwanza umetokea nje ya kwenye maegesho nje ya duka la viatu, na kufuatiwa na mlipuko mwingine muda mfupi baadae.

Mmoja ya wafanyakazi wa uokoaji miongoni mwa waliouwa ni wanawake na watoto. Mashuhuda wa tukio hilo amesema hali ni mbaya kwenye mitaa ya Gombe.

WANAJESHI WANNE WANAMAJI WAUAWA MAREKANI

Rais wa Marekani Barack Obama

Mtu mwenye silaha amewaua askari wanne wa jeshi la wanamajiwa Marekani katika shambulio lililofanywa kwenye majengo mawili ya jeshi hilo katika mji wa Chattanooga, Tennessee.

Wanajeshi hao wote waliuawa katika jengo moja. Maafisa nchini humo wameyaita mauaji hayo kuwa ni Shambulio la ndani. 

Shirika la Upelelezi la Marekani FBI linalochunguza mauaji hayo, limesema halijajua bado kilichosababisha shambulio hilo.

SIMBA KUCHEZA NA AFC LEOPARDS, SIMBA DAY 2015

Afisa Mtendaji Mkuu wa EAG Group, Imani Kajula akiwa Pamoja na Rais wa Simba Sport Club, Evans Aveva, wakati wa uzinduzi wa Simba Day. 

Dima ya Simba Sports Club ya kuendeleza mabadiliko ndani ya Simba bado inaendelea kushika kasi, Katika kipindi cha miezi mitatu sasa, mmekuwa mashuhuda wa Simba inayolenga kuleta mapinduzi makubwa katika jinsi mpira unavyoendeshwa, kujali wanachama, wapenzi wake na kukuza vyanzo vya mapato.

Akizungumza wakati wa kutangaza rasmi Simba Week 2015 Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema ‘’Kila mwaka timu yetu ya Simba imekuwa na utaratibu wa kuwa na siku maalum kwa ajili ya kufurahi, kuwatambulisha rasmi wachezaji, jezi za timu na kujiandaa kwa msimu mpya, siku hii imekuwa maarufu kama Simba Day.

FIFA KUZIFANYIA MABADILIKO BAADHI YA KANUNI

Makao makuu ya FIFA

Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA lina mpango wa kuzifanyia marekebisho kanuni zake ili kuzibana nchi zinazowania kuandaa Kombe la Dunia, zisitumie mwanya wa misaada ya kifedha kwa nchi nyingine kama rushwa.

Kipengele kile kinachoziruhusu nchi zinazoshindania nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia kusambaza pesa katika nchi nyingine huenda kikafutwa. 

Aidha FIFA inazitaka nchi zote zinazowania nafasi hiyo kuzingatia haki za binadamu na sheria za kazi wakati wote. Hivi sasa nchi zinazotupiwa jicho ni Urusi inayoandaa kombe la dunia mwaka 2018 na Qatar inayoandaa 2022. 

ura za kuamua nchi gani italiandaa Kombe la Dunia la mwaka 2026 zitapigwa mwaka 2017 huko Kuala Lumpur, Malaysia. Nchi zinazoiwania nafasi hiyo ni Marekani,Canada, Mexico na Colombia.

Tuesday, July 14, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 14, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

MICHUANO YA KAGAME KUANZA KUTIMUA VUMBI

Rais wa Rwanda Paul Kagame
Michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati jumamosi wiki hii inaanza kutimua vumbi mjini Dar es Salaam Tanzania huku jumla ya vilabu 13 vikishiriki.

Rais wa Rwanda Paul Kagame anatarajiwa kutoa kiasi cha dola elfu 60 za marekani kama zawadi kwa washindi. Kundi A itajumuisha timu za Yanga yaTanzania, Gor Mahia ya Kenya, Kmkm Zanzibar, Telecom ya Djibout na Khartoum- Sudani Kaskazini.

Kundi B - APR Rwanda, Al Shandy ya Sudan, LLB FC Burundi naHeegan Somalia.
Wakati kundi C - Azam ya Tanzania, Malakia ya Sudan Kusini, Adama ya Ethiopia na KCCA ya Uganda.

Hata hivyo mgawanyo wa zawadi kwa kila mshindi ni kwamba mshindi wa kwanza atajinyakulia dola elfu 30, wa pili dola elfu 20 na wa tatu dola elfu 10. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

Monday, July 13, 2015

NEC YATANGAZA MAJIMBO MAPYA 26 YA UCHAGUZI

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza majimbo mapya ya uchaguzi katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam leo.

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza majimbo 26 mapya ya uchaguzi ambayo yatakuwa na wagombea katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kukata kwa majimbo hayo wamezingatia idadi ya watu pamoja na Jiografia katika majimbo mapya.

Amesema katika upande wa Zanzibar majimbo yamebaki kuwa 50 kama awali hiyo inatokana vigezo vilivyowekwa na tume hiyo.

Majimbo yaliongezwa ni Handeni Mjini, Nanyamba, Makambako, Butiama, Tarime Mjini, Tunduma, Msimbo, Kavu, Geita Mjini, Mafinga Mjini, Ushetu, Nzega Mjini, Kahama Mjini, Kondoa Mjini, Newala Mjini, Bunda Mjini, Mbulu Mjini, Ndanda, Madaba, Mbinga Mjini, Mbagala, Kibamba, Vwawa, Monongo, Mlimba, Pamoja na Uliambulu.

Jaji Lubuva amesema baadhi ya wabunge wamekuwa wakiingia katika Halmashauri mbili hiyo kuweka mipaka katika maeneo ili mbunge aweze kushiriki katika Halmashauri moja tu.

Amesema baadhi majimbo yamebadilishwa majina na kuendelea kuwepo kwa majimbo hayo kisheria.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 13, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

POLISI WANNE WAUAWA KATIKA SHAMBULIO

Mkuu wa polisi Ernest Mangu amethibitisha uvamizi huo
Maafisa wanne wa polisi na raia wawili wameuawa baada ya watu wasiojulikana kuvamia kituo cha polisi mjini Dar es salaam Tanzania.

Shambulizi hilo limetokea katika kituo cha polisi kilichoko Ukonga, viungani mwa jiji kuu la Dar es salaam. Polisi wanasema kuwa wavamizi hao walitekeleza shambulizi hilo la kuvizia usiku wa kuamkia leo.

Waliwafyatulia risasi maafisa wa polisi katika kituo hicho na kuua wanne.
Kwa mujibu na raia wanoishi karibu na kituo hicho,makabiliano ya risasi yalidumu kwa zaidi ya saa moja.
Uchunguzi unaendelea kujua nani aliyetekeleza shambulizi hilo
Mkuu wa polisi Ernest Mangu amethibitisha uvamizi huo akisema askari 4 na raia 3 wameaga dunia. Hadi sasa haijabainika iwapo kuna majeruhi.

Aidha amesema kuwa walipora handaki ya kituo hicho na kuiba bunduki za polisi na idadi ya risasi isiyojulikana. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

KAMBI YA JESHI YAPOROMOKA YAUA 23

Takriban wanajeshi 23 wa Urusi wameuawa karibu na mji wa Omsk ulioko Siberia baada ya jengo la kambi ya kijeshi kuporomoka.

Wanajeshi wengine 19 waliokolewa kutoka kwa vifusi vya jengo hilo.
Mwanajeshi mmoja aliyeokolewa ameileza runinga ya Urusi kwamba wanajeshi walikuwa wamelala wakati wa ajali hiyo.

Picha za televisheni zilionyesha sehemu ya jengo hilo la ghorofa nne likiwa limeharibika kabisa huku wanajeshi wakishirikiana kuondosha vifusi.

Mwandishi wa BBC Moscow amesema inadhaniwa kwamba ukarabati duni uliofanyika mwaka jana ndio uliosababisha kuporomoka kwa jengo hilo. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

MAN CITY YAKUBALI KUMUUZA STERLING KWA LIVERPOOL


Raheem Sterling
Klabu ya Manchester City ya Uingereza imekubaliana na wapinzani wao Liverpool dau la pauni milioni £49 kumsajili mshambulizi Raheem Sterling.
Uhamisho wa mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 20 sasa unategemea makubaliano baina yao na vipimo vya afya. Sterling alikuwa ameomba kundoka Anfield kabla ya klabu hiyo kukataa dau mbili za Man City mwezi Juni.

Mshambulizi huyo atakuwa mchezaji aliyegharimu pesa nyingi zaidi raia wa Uingereza baada yake kukatalia mbali mshahara wa pauni laki moja kwa juma kutoka Liverpool.
Sterling aliyejiunga na Liverpool akiwa na umri wa miaka 15 kutoka QPR mwezi februari mwaka wa 2010 yuko katika kandarasi inayokamilika mwaka wa 2017. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

VAN PERSIE ATUA UTURUKI


Van Persie akipokelewa Uturuki
Mashabiki wa manchester United wengi walijua kuwa Van Persie anaondoka kuelekea Fenabashe lakini kwa mtoto mdogo mwingereza wa miaka minne Louis Diamond hakufahamu kuwa kipenzi chake Robin Van Persie anaondoka mpaka pale alipoambiwa na wazazi wake kwamba mpachika magoli Robin alikuwa tayari kuelekea uturuki. 

Hivi sasa waturuki wameanzisha kampeni ya kuchangishana pesa ili mtoto huyo ambaye video yake imesambaa mitandaoni na kutizamwa na watu wengi aletwe Uturuki kumshuhudia mchezaji huyo. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...