Thursday, April 23, 2015

AJARI ZARUDI TENA, BASI LAUA 10 SHINYANGA

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga.

Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga
SIKU sita tangu ajali ya basi dogo aina ya Toyota Hiace kuua watu 19 mkoani Mbeya, nchi imeendelea kukumbwa na ajali za barabarani. Safari hii watu kumi wamekatishwa uhai, kutokana na ajali ya basi na lori, iliyotokea mkoani Shinyanga jana.


Katika ajali hiyo, watu tisa walikufa papo hapo na mmoja aliaga dunia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga. Abiria 51 walijeruhiwa na wanatibiwa hospitali hapo, wakati tisa, akiwemo dereva wa basi, wako katika hali mbaya.

Ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Ibingo Kata ya Samuye wilayani Shinyanga Vijijini na ilithibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha.

Alisema ajali ilitokea majira ya saa 9:30 alasiri baada ya basi la kampuni ya Unique, lililokuwa linatoka Mwanza kwenda Tabora kugongana na lori la kampuni ya Coca Cola, lililokuwa linatoka Kahama. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ORODHA VYAMA VYA KIJAMII VITAKAVYOFUTWA KUANZA KUTOLEWA

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nch, Isaac Nantanga.
 
WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakati wowote wiki hii itaanza kutoa orodha ya vyama vya kijamii vitakavyofutwa kwa kuanzia na mkoa wa Dar es Salaam.

Imesema vyama hivyo vitafutwa kutokana na kutotekeleza matakwa ya kisheria ya kuwasilisha taarifa za mwaka za ukaguzi wa hesabu za vyama na vile ambavyo havilipi ada ya mwaka kama sheria inavyoelekeza.

Msemaji wa wizara hiyo, Isaac Nantanga alisema hayo jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kufafanua suala la uhakiki wa vyama vya kijamii nchini.

Alisema vyama vitakavyobainika vitafutwa katika Daftari la msajili wa vyama vya kijamii na wala siyo Taasisi zisizo za kiserikali (NGO,s) kwani haihusiki nazo.

“Orodha ya vyama vitakavyofutwa itaanza kutolewa kwa awamu kuanzia wiki hii na kwa kuanzia orodha hiyo itahusu vyama vilivyosajiliwa mkoa wa Dar es Salaam”Alisema 

Alisema kufuatana na orodha iliyopo vyama 10,000 vya kijamii na Taasisi za Dini vimesajiliwa na wizara hiyo na vitakavyofutwa ni vile tu ambavyo haviwasilishi taarifa za kila mwaka za ukaguzi wa hesabu zao na pia kama havilipi ada ya kila mwaka kama sheria inavyotaka.

Juzi, gazeti moja la kila siku liliandika kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mathias Chikawe anaanza kuhakiki NGOs jambo ambalo siyo la kweli kinachofanyika ni kwa taasisi za kijamii. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRILI 23, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01667
DSC01668
DSC01669 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

VOLCANO YALIPUKA CHILE

Mlipuko wa Volcano 
 
Volcano aina ya Calbuco imelipuka kwa muda mfupi huko ikiwa ni mara ya kwanza ndani ya zaidi ya miaka 40. Watu waliokuwa wakiishi maeneo jirani na ulikotokea mlipuko wa Volcano hiyo wamelazimika kuyahama makazi yao.

Picha za televisheni zilionyesha wingu zito na majivu vikipanda hewani umbali kilomita kadhaa angani katika jimbo la Los Lagos kusini mwa Chile.

Mamlaka nchini humo zimetoa tangazo la hali ya hatari kwa wakazi wote ambao wapo umbali wa kilomita la mlipuko wa Volcano hiyo huku safari za ndege kuelekea eneo hilo zikiwa zimeahirishwa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

HALI MBAYA YEMEN...!!!

Wapiganaji wa Houthi nchini Yemen 
 
Shirika la kimataifa la msalaba mwekundu limesema kuwa hali inazidi kuwa mbaya nchini Yemen, huku Mji mkuu Sanaa ukikosa umeme na maji kwa kipindi cha siku tisa zilizopita.

Afisa wa ngazi ya juu wa Shirika hilo nchini humo Robert Mardini amesema ameshuhudia miili kadhaa kwenye mitaa alipotembelea mji wa Aden, na kueleza kuwa changamoto iliyopo ni upelekaji wa huduma za kitabibu.

Awali Saudi Arabia ilisema itaendelea kutumia jeshi kuzuia waasi wa kihudhi kudhibiti Yemen, waasi nao wametaka kumalizwa kwa mashambulizi ya anga dhidi yao na kuanza mazungumzo.
Mpiganaji anayemuunga mkono Rais Abdrabbuh Mansour Hadi amesema ni mapema mno kuanza kuzungumzia makubaliano kati ya pande mbili. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TIMU 4 ZATINGA NUSU FAINALI ULAYA


Javier Hernandez akishangilia goli mbele ya mashabiki wa Real Madrid
Timu nne zimetinga hatua ya nusu fainali katika ligi ya mabingwa barani Ulaya iliyokamilika hapo jana, baada ya Real Madrid ya Hispania na Juventus ya Uitaliano kufanikiwa kuingia nusu fainali.
Timu ya Juventus
Wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani wa Santiago Bernabeu, Madrid walilazimika kusubiri hadi dakika ya 88, walipopata bao lao la pekee lililotiwa kimia Javier Hernandez almaarufu kama Chicharito,na hivyo kuhitimisha safari ya Atletico Madrid.
Katika msimu uliopita, huko Lisbon Ureno, Atletico walitolewa na Real Madrid katika hatua ya fainali.
Nayo Juventus imezima matumaini ya Monaco ya Ufaransa kwa kulinda bao lake lililofungwa katika mechi ya awali na hapo matokeo ikawa sare ya bila kutofungana. Hata hivyo nyota ni njema kwa Spain ambao sasa wanawakilishwa na timu mbili ambazo ni Real Madrid na Barcelona. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Monday, April 20, 2015

CHADEMA: ZITTO NI ADUI YETU NAMBA MOJA...!!!

MNYIKA
Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, John Mnyika

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kuwa adui yake namba moja ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha Alliance for Change and Transparance (ACT-wazalendo), Zitto Kabwe.

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, John Mnyika akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Furahisha Mwanza juzi, alisema Chadema haiko tayari kuikaribisha ACT-Wazalendo ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutokana na kile alichosema ‘ni adui kwao’.

“Mtume Muhamad (S.A.W) alikuwa anazungumzia unafiki ambao una sura mbili na sifa zake, leo (ACT) wanasema wapo upinzani, wanasema msiunge mkono Ukawa halafu mnawakaribisha?

“Nendeni kila mahali waambieni wananchi adui yetu mkuu ni Zitto. Sikilizeni niwaambie Taifa hili kama ni ufisadi tumeshazungumzia sana kuanzia EPA mpaka Richmond. Dk. Slaa (Willbrod) alipoingia bungeni aliyasema haya kwa sasa si mapya. Adui yetu ni Zitto na hatumtaki Ukawa,” alisema Mnyika.

Alisema Chadema haiko tayari kuikaribisha ACT-Wazalendo Ukawa kwa sababu adui kwao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ANGALIA PICHA ZA MAMIA YA WATU WALIOHUDHURIA MKUTANO WA ACT-WAZALENDO MKOANI MWANZA

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, akiwahutubia wakazi wa mji wa Mwanza kwenye viwanja vya Furahisha jijini humo.

 Umati wa watu ukiwa katika mkutano wa ACT-Wazalendo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
(Picha na Said Powa)

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 20, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01536

DSC01535 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

LOWASSA ATHIBITISHA UBORA WA AFYA YAKE

lowassa 1

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowasa akiwa katika matembezi ya kupinga mauaji ya albino.

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowasa, jana alithibitisha kwa vitendo kuwa afya yake iko safi baada ya kutembea umbali wa kilomita tano kwa miguu kwenye matembezi ya kupinga mauaji ya albino nchini.

Kwa muda mrefu, Lowassa ambaye ni mmoja wa makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, amekuwa akidaiwa kuwa na matatizo ya afya na kuwa hawezi kuhimili mikimiki ya kampeni na shughuli nyingine zinazohitaji nguvu.

Lakini matembezi ya jana yaliyoongozwa na Lowassa kuanzia Uwanja wa Taifa wilayani Temeke mpaka viwanja vya TCC Chan’gombe na kutumia dakika 25, yamedhihirisha vinginevyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UCHINA KUWEKEZA MABILIONI PAKISTAN

Bango la kumkaribisha rais Xi nchini Pakistan.
Rais wa China Xi Jinping ameanza ziara ya siku mbili nchini Pakistan hii leo.
Bwana Xi atazindua mpango wa uwekezaji wa kichina wa gharama ya dola bilioni 50 ambao Pakistan ina matumaini kuwa utasuluhisha tatizo lake ya nishati.

Mpango huo unaofahamika kama barabara ya uchumi ya China na Pakistan ni pamoja na barabara , reli na mabomba ya jumla ya umbali wa kilomita 3000 kutoka mji wa bandari wa Gwadar nchini Pakistan hadi mji wa ulio mashariki mwa China wa Kashgar.

Waandishi wa habari wanasema kuwa lengo la China ni kuongeza ushawishi wake wa kiuchumi kwa Pakistan ili kulegeza ule wa Marekani na India. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SULUHU YATAKIWA KUHUSU WAHAMIAJI

Boti ya Italia iliyokuwa katika Operesheni ya kuokoa wahamiaji ikiwa imebeba wahamiaji walikuwa wakisafiri kwenda Ulaya.
 
Waziri mkuu wa Italia Matteo Renzi ametoa wito wa kufanyika kikao cha dharura cha viongozi wa umoja wa ulaya kujadili swala la wahamiaji wanaoangamia kwenye bahari ya Meditarenean wakijaribu kuingia ulaya. Inafuatia ajali ya hivi punde ambao karibu watu 700 wanahofiwa kufa maji baada ya boti kuzama baharini kaskazini mwa Libya, kilomita 200 kutoka kisiwa cha Lampedusa, nchini Italia.

Manusura 28 wa janga la hivi punde kwenye bahari ya Meditaranean walitarajiwa kufikishwa kisiwani Sicily alfajiri ya Jumatatu. Hadi kufikia usiku, ni miili 24 iliyokuwa imeopolewa, na maafisa wa usalama kwenye pwani ya Italia, wakaipeleka kisiwani Malta.

Ni vigumu kuhakikisha idadi ya watu walioanza safari kwenye boti hiyo kutoka pwani ya Libya. Lakini walionusurika wanasema walikuwa kati ya watu 500 na 700 kabla ya kupinduka kilomita mia mbili kutoka Lampedusa, kwenye maji ya Libya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA

IMG_4798

Rnk
Team MP W D L GF GA +/- Pts

1
Young Africans 21 14 4 3 39 12 27 46

2
Azam 22 11 9 2 29 15 14 42

3
Simba SC 22 9 8 5 27 17 10 35

4
Kagera Sugar 23 8 7 8 22 22 0 31

5
Ruvu Shooting 23 7 8 8 16 21 -5 29

6
Mtibwa Sugar 23 6 10 7 22 23 -1 28

7
Mbeya City 23 6 10 7 19 21 -2 28

8
Mgambo JKT 22 8 4 10 18 21 -3 28

9
Stand United 22 7 7 8 19 24 -5 28

10
Coastal Union 23 6 9 8 16 23 -7 27

11
JKT Ruvu 23 6 7 10 17 23 -6 25

12
Ndanda 23 6 7 10 18 26 -8 25

13
Polisi Morogoro 23 5 9 9 15 22 -7 24

14
Tanzania Prisons 23 3 13 7 15 22 -7 22
 Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

LOOO...!!! SIMBA NOMA "INA WAGANGA WENGI WA KIENYEJI KULIKO WATAALAMU WA BENCHI LA UFUNDI"

IMG_9433
Simba waligoma kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo walipocheza na Mbeya City jumamosi iliyopita uwanja wa Sokoine

MTANDAO wa SHAFFIH DAUDA kwa muda mrefu sasa umekuwa ukifanya tafiti na kufuatilia mwenendo wa klabu ya Simba katika mechi za ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu.
Mwishoni mwa juma lililopita, Simba ilifungwa magoli 2-0 na Mbeya City fc katika uwanja wa Sokoine, Mbeya na kuifanya klabu hiyo kongwe nchini kuendelea kukaa nafasi ya tatu kwa pointi 35 walizokusanya baada ya kushuka dimbani mara 22.
Machi 18 mwaka huu walifungwa magoli 2-0 na Mgambo JKT katika uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga, lakini wakashinda 2-1 ugenini dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga na ilikuwa aprili 6 mwaka huu (jumatatu ya pasaka).
Katika mechi hizo tatu, mtandao huu ulikuwa unachunguza mwenendo wa Simba na namna wanavyoiandaa timu kwa ajili ya mechi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MBWANA AWATAKA MASHABIKI WA PRISONS KUISAPOTI HADI MWISHO

makata-march6-2015
Mbwana Makata, kocha mkuu wa Tanzania Prisons.
 
MBWANA Makata, kocha mwenye uzoefu wa kufundisha timu za majeshi safari hii amepewa jukumu la kuibakisha Tanzania Prisons ligi kuu Tanzania bara msimu ujao.

Makata, kocha wa zamani wa JKT Ruvu na JKT Oljoro jana ameiongoza Prisons kupata sare nyumbani ya goli 1-1 dhidi ya Wakata miwa wa Mtibwa Sugar katika mechi ya ligi kuu iliyopigwa uwanja wa CCM Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya.

Baada ya sare hiyo, Makata amesema: “Mechi ilikuwa ni muhimu kwetu kuweza kupata matokeo ya ushindi, lakini mechi ilikuwa ngumu na tumeweza kutapa sare ya goli 1-1. Kikubwa niwapongeze vijana wangu kwasababu ratiba kwetu ilibana wiki hii, tulicheza jumatano, tukawa safarini na kucheza tena leo (jana), muda wa maandalizi haukuwepo."

"Cha msingi niwaombe wakazi wa Mbeya, mashabiki wa Prisons waisapoti timu yao, tupambane mpaka dakika za mwisho tuone nini kitatokea” Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...