Friday, November 21, 2014

POLISI WABAKAJI WAONGEZEWA ADHABU

 Baadhi ya wanawake ndio walilalamika kuwa adhabu waliyopewa polisi hao ilikuwa ndogo sana 
 
Polisi wawili nchini Tunisia walioshitakiwa kwa kumbaka mwanamke ndani ya gari la polisi, wameongezewa adhabu katika kesi iliyowashtua wengi.
Maafisa hao walifungwa jela mwezi Machi huku kukiwa na malalamiko kwamba adhabu hiyo haitoshi.
Hukumu hiyo, iliongezwa hadi miaka 15 Alhamisi baada ya rufaa kuwasilishwa mahakamani na mwathiriwa wa kitendo hicho cha unyama Meriem Ben Mohamed.
Wakili wake alitaja hatua ya mahakama kuwoangeza adhabu watuhumiwa kama jambo zuri, na pia kusifu ambavyo kesi za ubakaji zinashughulikiwa nchini Tunisia.
Aliambia shirika la habari la AFP, kwamba ameridhishwa na adhabu hiyo.
"lakini bado haitoshi, kwa maoni yangu kwa tendo la kukera kama hilo,'' aliongeza kusema wakili huyo.
Meriem Ben Mohamed alishambuliwa mwaka 2012 na maafisa wa polisi waliosimamisha gari lake alimokuwa na mpenzi wake mjini Tunis. Alikuwa na umri wa miaka 27.
Polisi wa kupambana na vurugu nchini Tunisia
Watuhumiwa walikanusha mashitaka wakisema kuwa waliwapata wawili hao wakiwa wanashirki tendo la ndoa ndani ya gari lao.
Maafisa wa polisi walijaribu kuwashitaki Meriam na mpenzi wake kwa kosa la kukosa maadili lakini maandamano yalifanywa kupinga hatua kama hiyo huku wengi wakiwatetea wawili hao.
Ilisababisha Rais wa Tunisia kumsamehe Meriam na mpenzi wake.
Afisaa mwingine wa tatu aliyejaribu kuwatoza hongo wawili hao, atatumikia kifungo cha miaka miwili alichokuwa amepewa.
Ripoti iliyotolewa na mtaalamu wa kisaikolojia ilisema kuwa yote yaliyotokea yalimsababisha Meriam kusongwa na mawazo.
Kesi hii inatokea wakati ambapo kumekuwa na shinikizo kali kwa serikali kuzingatia haki za wanawake kufuatia kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa Rais Zine al-Abidine Ben Ali.

Na BBC

MKANYAGANO HATARI WAWAUA 11 ZIMBABWE

Watu 11 wamefariki katika mkanyagano nchini Zimbabwe baada ya ibada ya kidini kufnayika katika uwanja wa soka.
Polisi wanasema kuwa watu wanne walifariki katika uwanja huo ulio mjini Kwekwe wakati wengine saba wakifariki hospitalini.
Mkanyagano huo ulitokea wakati maelfu ya waumini wakikimbilia kuondoka uwanjani humo baada ya ibada iliyoongozwa na mhubiri wa kipentekoste Walter Magaya.
Mhubiri huyo anadai kuwaponya watu kwa kufanya miujiza.
Baadhi ya walioshuhudia mkanyagano huo wanatuhumu polisi kwa kufunga baadhi ya milngo ya kuondokea uwanjani humo, huku watu wakiondoka kupitia mlango mmoja tu.
Hata hivyo polisi wanakana kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya.
Bwana Mugaya ambaye ni mkuu wa kanisa la 'Prophetic Healing and Deliverance' aliambia vyombo vya habari kuwa alipopata habari ya kutokea vifo hivyo alihuzunika sana. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RONALDO AOSHA VYOMBO BAADA YA KUSHINDWA

Ronaldo aosha vyombo baada ya kushindwa katika karata na mchezaji wa Tenisi Rafa Nadal 

Aliyekuwa mchezaji wa timu ya Brazil Ronaldo alilazimika kuosha vyombo baada ya kushindwa katika mchezo wa karata na mchezaji wa tennisi Rafa Nadal,
na kumfanya mchezaji huyo wa tenisi kupokea dola 50,000 za hazina yake ya kutoa msaada huku Ronaldo akiosha vyombo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 alikabiliana vilivyo na mwana tenisi huyo kutoka uhispania katika mechi kati ya wawili hao katika meza ya pokerstar, Casino ya Hippodrome mjini London ambapo Nadal alishinda fedha hizo.
Duru ziliarifu kwamba kiini cha nyota hao wawili kukutana katika chumba kimoja ni chakula kilichoandaliwa katika hafla hiyo.
Hatahivyo kitu kilichowafurahisha wengi kulingana na wageni ni hatua ya Ronaldo kukubali kushindwa na kupewa kazi ya kuviosha vyombo vya Nadal alivyotumia kula. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ADEBAYOR ADAI MAMAAKE NI MCHAWI


Mchezaji huyu wa kilabu ya Totenham amedai kuwa mamaake amekuwa akitumia uchawi kujaribu kumuharibia kazi yake. 
 
Mshambuliaji wa kilabu ya Totenham nchini Uingereza Emmanuel Adebayor amekosana na mamaake kwa madai kwamba anatumia uchawi kumharibia kazi yake.
Duru zimearifu kuwa mama huyo tayari ameondoka katika nyumba ya familia huku dadaake Adebayor akiambia radio moja ya mjini Accra kwamba Adebayor ndiye aliyemfukuza.
Lakini mchezaji huyo wa zamani wa kilabu ya Arsenal anadai kwamba mamaake aliondoka mwenyewe na kwamba hawana mawasiliano yoyote kati yao kwa kuwa amekuwa akitumia uchawi kutaka kumuharibia kazi yake.

Adebayo aliwahi kuchezea Arsenal
'' Ninawezaje kuzungumza na mama ambaye yeye na dadaangu wamekuwa wakijaribu kuniroga''aliwauliza maripota.Mchezo wa Adebayor katika kilabu ya Tottenham umeathirika katika kipindi cha miezi kadhaa iliopita huku Tottenham ikidaiwa kujaribu kumuuza kwa mkopo mchezaji huyo katika dirisha la uhamisho mnamo mwezi January kufuatia kushuka kwa mchezo wake.

Thursday, November 20, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS NOVEMBA 20, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

OBAMA KUTANGAZA MABADILIKO YA UHAMIAJI

Rais Barack Obama
Ikulu ya Marekani imesema Rais Obama atatumia muda ambao watazamaji wa televisheni nchini humo wanaangalia zaidi matangazo siku ya Alhamisi kutangaza mabadiliko makubwa ya mfumo wa uhamiaji wa nchi hiyo.
Inatarajiwa kuwa Rais Obama atasema kuwa atatumia madaraka yake aliyopewa kikatiba kuzuia wahamiaji wapatao milioni tano kurejeshwa makwao na badala yake wapatiwe vibali vya kufanya kazi nchini humo.
Rais Obama amesema hayo katika video iliyotumwa katika ukurasa wa facebook kabla ya hotuba yake.Tangu kuingia madaraka Obama amekuwa akipigania baadhi ya mabadiliko ikiwemo huduma ya utoaji wa huduma za afya kwa mfumo wa bima ya afya. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BINTI AJINASUA NA NDOA YA MWANAMGAMBO

Raia wengi kutoka Ulaya wamejiunga na kundi la wapiganaji wa Islamic State nchini Syria 

Mwanamke mmoja raia wa Uholanzi amewasili nchini Uturuki baada ya safari iliyojaa hatari nchini Syria kwa ajili ya kumchukua binti yake aliyekua mjini Raqqa, mji unaokaliwa na waasi wa Islamic State.
Monique alikwenda Uturuki mara ya kwanza baada ya binti yake aitwae Aicha kusafiri kwenda Syria kuoana na mmoja wa wanamgambo wa kundi hilo mwenye asili ya Uholanzi na Uturuki.
Mamia ya Wanamgambo wenye asili ya Ulaya wamekua wakienda Syria kupigana ndani ya kundi la IS.
Aicha ,19 ni miongoni mwa Wasichana ambao walisafiri kujiunga na IS.Raia wawili wa Austria wenye umri wa miaka 15 na 17 walikwenda Syria Mwezi Aprili na mmoja wao aliripotiwa kuuawa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BIANCHI KUENDELEA NA MATIBABU UFARANSA

 Jules Bianchi dereva wa F1 wa timu ya Marussia aliyepata ajali katika mashindano ya Japanese Grand Prix Oktoba,5, 2014 
 
Dereva wa magari ya langa langa ya Formula 1 Jules Bianchi ametoka katika hali ya kuwa mgonjwa mahututi na sasa anapua bila msaada wa mashine, wamesema wazazi wake katika taarifa yao.
Dereva huyo wa timu ya Marussia mwenye umri wa miaka 25, alijeruhiwa kichwani alipoligonga gari la kuvuta magari katika michuano ya Japanese Grand Prix Oktoba 5,2014.
Dereva huyo raia wa Ufaransa amehamishwa kutoka hospitali ya mjini Yokkaichi nchini Japan na kupelekwa katika hospitali ya Nice nchini Ufaransa kwa uchunguzi zaidi. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

FAINALI ZA CAF 2015: TIMU 15 ZAFUZU


Timu ya Algeria wakishangilia ushindi wa timu yao kufuzu kucheza fainali za Caf 2015 nchini Equatorial Guinea 
 
Matumaini ya eneo la Afrika Mashariki kuwa na timu angalau moja katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika nchini Equatorial Guinea mwaka 2015, yameyeyuka baada ya mwakilishi pekee wa eneo hilo timu ya Uganda kucharazwa na Guinea
mabao 2-0 katika mchezo wa kundi E uliofanyika mjini Casablanca, Morocco, Jumatano.


Timu ya Nigeria mabingwa watetezi hawatashiriki fainali za Caf 2015 baada ya kutolewa katika makundi
Uganda iliyokuwa na pointi 7 kama Guinea ilitakiwa kushinda mchezo huo. Ghana inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 11. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MADAI YA RUSHWA QUATAR: NAJIHISI KUONEWA

Sepp Blatter, rais wa FIFA akiitangaza Qatar kuwa mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2022
Mfichua siri kuhusu tuhuma za rushwa kutolewa na Qatar ili kuiwezesha nchi hiyo kushinda nafasi ya kuandaa Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2022 ameiambia BBC kuwa anaishi kwa hofu kutokana na hatua yake hiyo.
Mwaka 2011, Phaedra al-Majid alidai kuwa maafisa wa Qatar walijitolea kuwalipa maafisa watatu wa vyama vya soka barani Afrika kiasi cha dola milioni moja na nusu ili kuiunga mkono Qatar kuwa mwenyeji wa michuano hiyo mikubwa duniani.
Baadaye Bi Phaedra al-Majid aliondoa tuhuma hizo, lakini sasa anasema alilazimishwa kubadili kauli yake. Anasema ameingia katika hali ya uendawazimu ya "kujiona anaonewa kila wakati, hofu na vitisho" (na kwamba atajiona mkosaji maisha yake yote.) 
Kamati ya Qatar ya uandaaji wa Fainali za Kombe la Dunia imesema ushahidi wa Phaedra al-Majid ulitiliwa mashaka na timu ya uchunguzi ya FIFA, na kwamba tuhuma zote zilichunguzwa na kutupiliwa mbali. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, November 19, 2014

WAPINZANI WAMSULUBU MWAKYEMBE BUNGENI


Dk Harrison Mwakyembe

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, jana ilimsulubu Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ikieleza kuwa wizara yake iliingia mkataba wa mradi wa treni za kisasa kutoka Stesheni ya Dar es Salaam hadi Pugu kupitia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) bila kufuata taratibu.
Kambi hiyo ililieleza Bunge kuwa mkataba huo ulisainiwa baina ya mmiliki wa Kampuni ya M/s Shumoja, Robert Shumake na Shirika la Reli Tanzania huku Waziri Mwakyembe akishuhudia.
Msemaji Mkuu wa kambi hiyo, Ofisi ya Waziri Mkuu,  Uwekezaji na Uwezeshaji, Pauline Gekul alitoa madai hayo wakati akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu muswada wa marekebisho ya Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP). Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NABII: "URAIS 2015 BALAA!... JK ASINGEWAHI KUPASULIWA, NCHI INGECHAFUKA"

NABII wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi Bendera amesema uchaguzi mkuu ujao utakuwa balaa kubwa kufuatia maono anayoyaona wakati akishiriki ibada katika nyakati mbalimbali, Risasi Jumatano linakupa mkanda kamili.

Nbii wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi Bendera.
Akizungumza wakati wa ibada kanisani kwake na baadaye na waandishi wetu Novemba 16 mwaka huu, Nabii Yaspi alisema kuna mgongano mkubwa miongoni mwa watu wanaotajwa kugombea urais, ili kumrithi rais Jakaya Kikwete ambaye alimwelezea kama kiongozi anayemuona kiroho kila mara.


“Nilimuona katika maono yangu kama mtu aliye kwenye majaribu makubwa kiroho, nikaandaa maombi hapa kanisani na tukamuombea kwa muda wa nusu saa na tunashukuru Mungu hali yake inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume nchini Marekani. Bado namuona akiwa na maumivu kuanzia sehemu za kiuno, uti wa mgongo na shingoni mwake.

Mhe. Edward Lowasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MOTO WATEKETEZA SOKO LA BIDHAA ZA UTAMADUNI JIJINI ARUSHA


Baadhi ya Mabaki ya bidhaa zilizoteketea kwa moto katika SOKO la bidhaa za utamaduni lijulikanalo kwa jina la MT.MERU CURIOS& CRAFTS MARKET usiku wa kuamkia leo. 

Bango la Soko hilo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UJERUMANI YAIUA HISPANIA 1-0

Mario Gotze, who scored Germany's winning goal at the World Cup final, is put under pressure by Cesar Azpiliciueta and Sergio Busquets 
Mario Gotze akiwapita Cesar Azpiliciueta wa Sergio Busquets wa Hispania katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa mjini Vigo. Ujerumani ilishinda 1-0, bao pekee la Toni Kroos dakika ya mwisho.
Gotze is grounded under the challenge of Spain defender Sergio Ramos as the rain beings to fall in Vigo on Tuesday evening
Gotze akienda chini baada ya kukwatuliwa na beki wa Hispania, Sergio Ramos. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...