Saturday, October 04, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WABUNGE KUANDAMANA NA KENYATTA ICC


Rais Uhuru Kenyatta akiwasili katika mahakama ya kimataifa ya ICC

Idadi kubwa ya wabunge nchini Kenya wanajiandaa kuandamana na Rais Uhuru Kenyatta katika mahakama ya kimataifa ya ICC,Uholanzi ambako anatarajiwa kuhudhuria kikao maalum kuhusiana na kesi inayomkabili katika mahakama hiyo.
Kenyatta ametakiwa kufika mbele ya mahakama hiyo tarehe nane mwezi huu huku kiongozi wa mashitaka Fatou Bensouda akilalamika kuwa Kenya imekataa kushirikiana na mahakama hiyo kuhusiana na ushahidi dhidi ya Kenyatta.
Mapema wiki hii, mahakama hiyo ya ICC ilitupilia mbali ombi la Rais Kenyatta, la kutaka kikao hicho cha Octoba 8 kuhairishwa au aruhusiwe kutumia video. Majaji wa Mahakama hiyo walimuagiza Uhuru kufika binafsi mbele yao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TOFAUTI YA DINI YAVUNJA NDOA INDIA

Ndoa ya kihindi
Maafisa wa polisi katikati mwa India wamefutilia mbali harusi kati ya mwanamume mkristo na mwanamke wa kihindu baada ya shinikizo kutoka kwa makundi ya kihindu yenye mrengo wa kulia.
Wanandoa hao wawili kutoka Madhya Pradesh walitoroshana na kuoana katika sherehe ya kihindu bila ruhusa ya familia ya msichana.
Baada ya makundi hayo ya Kihindu kupinga hatua hiyo na kutishia kushambulia majengo ya serikali,maafisa wa polisi katika eneo hilo waliwasaka wapenzi hao na kuwalazimisha kuachana.
Waandishi wanasema kuwa hatua hiyo ya makundi ya kihindu imekuwa ya kawaida katika jimbo hilo katika siku za hivi karibuni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MESSI AKUTWA NA KESI YA KUKWEPA KULIPA KODI

messi
Nyota wa Barcelona Lionel Messi anakabiliwa na kesi ya kukwepa kodi,majaji nchini Hispania wamethibitisha tuhuma hizo.
Ikumbukwe Messi alikuwa akikabiliwa na tuhuma za ukwepaji kulipa kodi kwa muda sasa.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, October 03, 2014

KURA MBILI ZAPITISHA RASIMU YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA

http://jambotz8.blogspot.com/

Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Deo Sanga akisakata muziki katikati ya Ukumbi wa Bunge hilo baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kura zilizopigwa kupitisha Rasimu ya Mwisho ya Katiba inayopendekezwa mjini Dodoma jana.


Dodoma/Dar. Licha ya upinzani kutoka makundi kadhaa ya wananchi, Bunge la Katiba jana lilihitimisha kazi yake kwa kupitisha Katiba inayopendekezwa baada ya kupata theluthi mbili za wajumbe wa kila upande wa Muungano.

Matokeo hayo yaliyohitimisha mchakato huo, yalifanikishwa kwa tofauti ya kura mbili za wajumbe katika baadhi ya ibara na nyingine kwa kura moja tu, ikimaanisha kuwa iwapo kura hizo mbili zingekosekana hadithi ingekuwa tofauti.

 Kutangazwa kwa matokeo hayo kuliwafanya wajumbe walioshiriki mchakato hadi hatua ya mwisho baada ya wenzao wa kundi la Ukawa kususia, kulipuka kwa furaha, nyimbo, tambo, vijembe na vigelegele huku wakijimwaga ukumbini kusakata dansi.

Akitangaza matokeo hayo, Naibu Katibu wa Bunge hilo, Dk Thomas Kashililah alisema hali ya upigaji kura ilikuwa ni nzuri na kila kura za kila upande zilitosheleza na kutoa uhalali wa Katiba inayopendekezwa kupelekwa kwa wananchi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PINDA: "KATIBA IPATIKANE KABLA YA RAIS MPYA"


Bunge Maalumu la Katiba, kabla ya kuahirishwa kwake 

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema atafurahi kuona mchakato mzima wa Katiba ukikamilika kabla rais mpya hajapatikana katika Uchaguzi Mkuu ujao, pendekezo ambalo ni kinyume na makubaliano baina ya Rais Jakaya Kikwete na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kuwa upigaji wa kura ya maoni ufanyike baada ya Uchaguzi Mkuu 2015.

Akizungumza Bungeni baada ya kupewa nafasi na Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta kutoa shukrani, Pinda alipendekeza kura ya maoni ipigwe sambamba na Rais ili kiongozi ajaye afanye kazi ya kutekeleza matakwa ya Katiba hiyo.

Alisema rais ajaye anaweza kuwa na ajenda zake, hivyo ni muhimu kumaliza kazi yote na kumkabidhi Katiba ambayo imekamilika ili aitekeleze.

“Nampongeza sana mwenyekiti kwa kufanya kazi nzuri ya kuhakikisha Katiba inayopendekezwa inapatikana kwa wakati na kwa kuzingatia maoni ya wananchi,” alisema Waziri Mkuu Pinda.

Alichojifunza

Pinda alieleza kuwa katika mchakato huo wa Mabadiliko ya Katiba, amejifunza mambo makuu manne, kubwa likiwa ni kutii sauti ya wengi, kwani ni sauti ya Mungu. Alisema wingi wao bungeni ni kiashiria cha uwepo wa sauti ya Mungu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAFUNZI 40 MEXICO WAPOTEA

http://jambotz8.blogspot.com/
Mamia ya wanafunzi nchini Mexico katika jimbo la Guerrero wameandamana katika mji mkuu wa jimbo la Chilpancingo kulalamikia kutoweka kwa zaidi ya wanafunzi wenzao arobaini wiki iliyyopita.
Wanafunzi hao wanasemekana kuwa mwisho walionekana kusombwa katika magari ya polisi kufuatia maandamano walioshiriki wakilalamikia ubaguzi katika ajira ya walimu wa maeneo ya vijijini.
Polisi walifyatua rissasi kwenye basi na kwa waandamaji na kuua watu sita na wengine 17 kujeruhiwa.
Maafisa ishirini na wawili wa polisi wanashikiliwa na kwa kutuhuma za kufyatua risasi.
Ndugu ya waliouawa wanaosaidiwa na polisi waliingia mlango kwa mlango katika eneo la Iguala wakiwa wameshikilia picha za wapendwa wao na kutafuta eneo ambalo miili ya ndugu zao ilipofichwa. Serikali ya jimbo hilo imetoa dola 75,000 kwa yeyote atakayetoa taarifa kueleza wanafunzi hao walipo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WANAFUNZI WA HONG KONG KUKUTANA NA SERAKALI

http://jambotz8.blogspot.com/
 
Viongozi wa wanafunzi huko Hong Kong wamekubali kukutana na upande wa serikali kujadili malalamiko yao siku tano baada ya maandamano makubwa ya kupigania demokrasia.
Hiyo inafuatia mwaliko kutoka kwa mkuu wa utawala wa Hong Kong CY Leung. Alitoa taarifa hiyo muda mfupi kabla ya kumalizika kwa muda wa mwisho uliowekwa na wanafunzi hao waliotishia kuvamia majengo ya serikali iwapo mkuu huyo hatajiuzulu.
Muda wa mwisho uliowekwa na wanafunzi hao umemalizika salama.
Bwana Leung amesema atabakia madarakani na kuwaonya waandamanaji kuwa watapata matatizo iwapo watavamia majengo ya serikali.
Kumekuwa na makabiliano makali katika eneo la majengo ya serikali ambapo waandamanaji wamekuwa wakiendelea kudai uchaguzi wa haki mwaka 2017. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MIAKA 15 YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA BABA WA TAIFA MWL. J. K. NYERERE

Kutoka kushoto ni Marehemu Habib Halala, Mzee Paul Soizgwa, JK Nyerere, Brig. Hashim Mbita, Mzee Benjamin Mkapa, siku kumi kabla ya JK kustaafu uraisi 1985.  Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, October 02, 2014

HAWA NDIO WAKE WA MARAIS WA AFRIKA WANAOTIKISA...!!!

 
Ana Paula Dos Santos.
alizaliwa1964, ni mke wa Rais wa Angola, Jose Eduardo Dos Santos, Paula ni mwanamitindo wa zamani, anasifika kwa uzuri na kujua kuvaa.
Mama Salma Kikwete.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, alizaliwa 1963, anatajwa kuwa katika orodha ya wake wazuri wa marais wa Afrika, anasifika kwa mavazi yake ya kitenge.
Margaret Wanjiku Kenyatta.
Ni mke wa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, anatajwa kuwa na tabasamu zuri ingawa nywele zake zenye rangi ya kijivu ni kivutio kikubwa. Kazaliwa Mwaka 1963.
 
Hinda Deby Itno.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TAARIFA TOKA BUNGE LA KATIBA DHIDI YA MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR


Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman akisindikizwa kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge Maalum leo mjini Dodoma na Askari Polisi.
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman (mwenye Kaunda suti ya kijivu) akisindikizwa kutoka nje ya viwanja vya Bunge Maalum la Katiba leo mjini Dodoma na Askari Polisi mara baada ya kushutumiwa na baadhi ya Wajumbe wa Zanzibar. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NAFASI ZA AJIRA WIZARA YA MAMBO YA NDANI {UHAMIAJI}

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi anatangaza nafasi za kazi zifuatazo katika Idara ya Uhamiaji kwa Raia wote wa Tanzania wenye sifa. 

1. KOPLO WA UHAMIAJI Nafasi 114 - (Nafasi 100 kwa ajili ya Tanzania 
Bara na Zanzibar na nafasi 14 maalum kwa ajili ya Zanzibar tu) 
A. SIFA ZA MWOMBAJI: 
(i) Awe Raia wa Tanzania mwenye umri kuanzia miaka 25 hadi 30. 
(ii) Awe amehitimu kidato cha sita na kufaulu masomo ya Kiingereza, Kiswahili, Historia, Jiografia, Kifaransa, Hisabati ambapo masomo mawili kati ya hayo yawe katika kiwango cha “Principal”. 
(iii) Awe pia na mojawapo ya sifa zifuatazo:
• Cheti cha Sheria; 
• Cheti cha Kompyuta; 
• Cheti cha Ufundi (FTC) kwenye fani ya umeme na mitambo 
(iv) Waombaji wenye ujuzi wa mojawapo ya lugha zifuatazo (Kifaransa, Kichina, Kijerumani, Kiarabu au Kihispania) watafikiriwa kwanza. 
(v) Aidha, Mwombaji aliyepitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa atapewa kipaumbele. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA CHAMA CHA ACT-TANZANIA KUHUSU ZITTO KABWE

 Zitto Kabwe
--
ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPERANCY. 
--
Ndugu wanahabari kumekuwa na utaratibu wa habari zinazoupotosha umma wa watanzania kuhusu chama chetu cha ACT-Tanzania.

Katika gazeti la mwanahabari toleo na 117 la tarehe 29/09/2014 katika ukurasa wake wa mbele iliandikwa "MKAKATI WA KUKIPA NGUVU CHAMA CHA KIPYA CHA ZITTO KABWE WAVUJA".

Act-Tanzania tunaeleza kuwa ni chama cha watanzania wote kisichokuwa na mmilki wake na tunaunganishwa na misingi kumi ya chama pamoja na Itikadi yetu ya Demokrasia jamii.

Act-Tanzania tunatambua uwezo na mchango wa kisiasa na ujenzi wa demokrasia ya vyama vyingi nchini uliotolewa na Mheshimiwa Zitto Kabwe mbunge wa Kigoma Kaskazini.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KAJALA AMSHTAKI MAMA WEMA...!!!

KIMENUKA! Habari ya mjini kwa sasa ni bethidei ya Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu kutimiza miaka 26 tangu kuzaliwa, lakini ndani ya tukio hilo, mengine yameibuka!

Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Kajala Masanja.
Miongoni mwa yaliyoibuka kwenye sherehe hiyo iliyofanyika Jumapili iliyopita nyumbani kwa Wema, Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar es Salaam ni madai ya mama Wema, Mariam Sepetu kudaiwa kupewa nafasi ya kutoa ‘neno la hekima’ lakini akaitumia kumvurumishia mitusi aliyekuwa shosti wa Wema, Kajala Masanja.
KUNASWA KWA SAUTI NA PICHA
Baada ya sherehe hiyo, Jumatatu na Jumanne, mitandao mingi ya kijamii ilitumbukiza video yenye sauti ikimuonesha mama Wema akimrushia matusi Kajala kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na kukorofishana kwa mwanaye na Kajala aliyewahi kumfadhili mahakamani kwa kumlipia faini ya shilingi milioni 13 asiende jela kwa kesi ya kuuza nyumba iliyokuwa na zuio la kisheria.
 
Wema Sepetu akiwa na mama yake.
KAJALA AAMUA ZITO
Katika kufuatilia sakata hilo, Amani lilinyetishiwa kwamba Kajala baada ya kushindwa kuvumilia, ameamua kumshitaki mahakamani mama Wema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

GARDNER ATAKA JIDE AELEZE UKWELI JUU YA NDOA YAO


Habari ya mjini katika ulimwengu wa mastaa Bongo ni kitendo cha mtangazaji mwenye jina kubwa wa Kipindi cha Maskani cha Redio Times FM, Gardner G Habash ‘Kepteini’ kutaka mwanamuziki Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ ndiye aeleze ukweli juu ya ndoa yao.
 
Mtangazaji wa Redio Times FM, Gardner G Habash ‘Kepteini’
Akizungumza kwenye Kipindi cha Mkasi kinachorushwa hewani kupitia Televisheni ya EATV chini ya ‘hosti’ wake, Salama Jabir, Jumanne iliyopita, Gardner alikataa kuzungumzia ndoa yake inayodaiwa kuvunjika.
Pamoja na mambo mengine ambayo aliyajibu kwa ufasaha, Gardner alipoulizwa juu ya habari zinazozungumzwa mtaani kuhusu kuvunjika uhusiano wake na Jide au Lady Jaydee, aligoma kulizungumzia kwa kigezo kwamba kipindi hicho kilimhusu yeye tu.
 
Mwanamuziki wa Bongo fleva kitambo, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’
Mtangazaji huyo alikwenda mbele zaidi kwa kumwambia Salama kwamba amwite Jaydee kwenye kipindi hicho ili alielezee jambo hilo kwa undani.Gardner na Jaydee ambao walifunga ndoa mwaka 2005, wamekuwa wakidaiwa kuwa hawapo pamoja tena huku majukumu ya mtangazaji huyo ambaye alikuwa meneja wa mwanamuziki huyo yakielea.
Kupitia kipindi chake cha Diary of Lady Jaydee kilichokuwa kikisimamiwa na Gardner ambacho sasa kinaongozwa na ndugu wa msanii huyo aitwaye Wakazi, Jumapili iliyopita Jide alionekana kwenye harusi ya ndugu yake aitwaye Lameck Mbibo ‘Dabo’ ambaye pia ni msanii wa Dance Hall akiwa mpweke bila mumewe kama ilivyozoeleka. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na GPL

RAILA ODINGA ATANDIKWA BAKORA HADHARANI...!!!

Mzee Mdzombo anasemekana kutokuwa timamu kiakili
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amemsamehe mzee aliyempiga bakora katika mkutano wa hadhara wa kisiasa katika jimbo la Kwale Pwani ya Kenya,
Mwanamume huyo, Lengo Mdzombo, anayefanya kibarua katika shamba moja Kwale, alikamatwa Jumanne na kufikishwa mahakamani.
Alishitakiwa kwa kosa la kumshambulia kiongozi huyo pamoja na gavana wa Kwale.
Hali ya taharuki ilitanda katika mkutano wa hadhara Jumatatu wiki hii baada ya Mdzombo kwenda ukumbini na kuanza kumtandika bakora kiongozi wa upinzani Raila Odinga pamoja na wanasiasa wengine.
Raila alikuwa amejiunga na kikundi cha wanawake waliokuwa wanacheza densi ya kitamaduni kuwatumbuiza wageni, pamoja na gavana wa jimbo la Kwale Pwani ya Kenya Salim Mvuruya katika mkutanmo wa kisiasa.
Raila alikuwa ameambatana na viongozi wengine, wakiwemo, Seneta Juma Boy, Hassan Omar, Agnes Zani, James Orengo, Johnstone Muthama na wengineo.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga
Mzee huyo alimpiga bakora Odinga ambaye ni waziri mkuu wa zamani kabla ya kumgeukia gavana wa jimbo hilo na kumchapa mara mbili. Hata hivyo mwanamume huyo alishindwa nguvu na walinzi wa Raila Odinga.
Polisi walithibitisha kuwa walimkamata mwanamume huyo na kumwachilia baada ya kugundua kuwa alikuwa na matatizo ya kiakili.
Haijulikani kwa nini mwanamume huyo alimshambulia Raila ila baadhi wanasema ni kwa sababu alighadhabishwa pale waziri mkuu alipocheza densi na mwanamke aliyesemekana kuwa mke wake ambaye alikuwa katika kikundi cha wanawake waliokuwa wanawatumbuiza wageni waheshimiwa.
Viongozi waliofika walilazimika kusitisha densi hiyo kabla ya mwanamume huyo kushindwa nguvu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

ARSENAL YAUA 4-1, WELBECK APIGA HAT-TRICK


Mshambuliaji Danny Welbeck akishangilia baada ya kupiga 'hat-trick'.

Alexis Sanchez akiifungia Arsenal bao la tatu dhidi ya Galatasaray.

Welbeck akitupia bao la nne. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ametimiza miaka 18 akiwa meneja wa klabu hiyo leo.
KLABU ya Arsenal imetoa kichapo cha mabao 4-1 dhidi ya Galatasaray kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyopigwa Uwanja wa Emirates jijini London usiku huu.
Mshambuliaji Danny Welbeck ametupia kambani mabao matatu 'hat-trick' huku bao la nne likiwekwa kimianai na Alexis Sanchez. Katika mtanange huo, kipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny alizawadiwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi mshambuliaji wa Galatasaray, Burak Yilmaz.
Ushindi wa leo wa Arsenal umeongeza furaha kwa Meneja wa timu hiyo, Arsene Wenger aliyetimiza miaka 18 akiwa kocha wa klabu hiyo leo.
VIKOSI: 
Arsenal: Szczesny, Chambers, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Flamini, Cazorla, Ozil (Wilshere 77), Sanchez (Ospina 62), Oxlade-Chamberlain (Rosicky 68), Welbeck.
Waliokuwa benchi: Coquelin, Bellerin, Campbell, Podolski.
Galatasaray: Muslera, Chedjou, Felipe Melo, Semih Kaya, Veysel (Bulut 68), Yekta (Altintop 46), Dzemaili, Telles, Sneijder, Pandev (Bruma 68), Burak Yılmaz.
Waliokuwa benchi: Bolat, Balta, Adin, Camdal. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS OKTOBA 02, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKUU WA USALAMA MAREKANI JIUZULU

Julia Pierson mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Marekani
Mkuu wa Idara ya Usalama nchini Marekani, aliyekuwa na jukumu la kumlinda Rais Barack Obama, amejiuzulu kufuatia matukio yenye kuhatarisha usalama wa taifa yaliyotokea.
Mkuu huyo wa usalama Julia Pierson alikabidhi barua ya kujiuzulu kwa Waziri wa Usalama wa Ndani, Jumatano.
Siku moja kabla, alikabiliana na maswali ya wajumbe wenye hasira kutoka Baraza la Congress juu ya udhaifu mkubwa wa usalama wa Ikulu ya Marekani
Habari za tukio lingine likimhusisha mtu mwenye silaha kuruhusiwa kuingia katika lifti moja na Bwana Obama kulizidisha kutolewa wito wa kumtaka mkuu wa usalama kujiuzulu.
"Leo, Julia Pierson, mkurugenzi wa usalama wa taifa wa Marekani, amenikabidhi barua ya kujiuzulu, na nimeikubali," Waziri wa Usalama wa Taifa Jeh Johnson aliandika katika taarifa.
"Nampongeza kwa utumishi wake wa miaka 30 katika idara ya usalama na taifa." Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

CHINA YAONYA MGOGORO WA HONG KONG

 Waandamanaji Hong Kong
Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi ametoa onyo kali dhidi ya maandamano "yasiyo halali" Hong Kong.
Akiwa katika ziara nchini Marekani, Bwana Wang pia alionya kuwa suala la Hong Kong linahusu "mambo ya ndani" ya China
Waziri mwenzake wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry, ameitaka Hong Kong kujizuia na matumizi ya nguvu wakati wa kushughulikia maandamano hayo.
Mapema, waandamanaji wanafunzi waliokasirishwa na China kuwateua wagombea wa uchaguzi wa mwaka 2017 waliapa kuendelea na maandamano iwapo kiongozi wa Hong kong, CY Leung hatajiuzulu.
Wamesema waandamanaji wataanza kukalia majengo ya serikali kama Bwana Leung hatajiuzulu ifikapo Alhamisi.
Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi na John Kerry wa Marekani
Waandamanaji walikusanyika usiku kucha nje ya ofisi ya Bwana Leung, huku polisi 200 wakiwa katika eneo hilo.
Bwana Wang, afisa mwandamizi wa China wa ngazi ya juu akizungumzia waziwazi suala hili, alisema: "Masuala ya Hong Kong ni masuala ya ndani ya China. Nchi zote lazima ziheshimu uhuru wa China kujiamulia mambo yake yenyewe. Kwa nchi yoyote, kwa jamii yoyote, hakuna atakayeruhusu vitendo vilivyo kinyume cha sheria vinavyokuika utulivu wa umma."
Hata hivyo, alisema: "Tunaamini kuwa Utawala maalum wa serikali ya jimbo la Hong Kong ina uwezo wa kushughulikia hali hii kwa mujibu wa sheria."
Bwana Kerry amesema Marekani inaunga mkono madhila ya jumla huko Hong Kong, akisema: "Tuna matumaini makubwa kwamba mamlaka ya Hong Kong itajizuia kutumia nguvu na kuheshimu haki ya waandamanaji kueleza mawazo yao kwa amani." Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Wednesday, October 01, 2014

BUNGE LA KATIBA: WALIOPIGA KURA YA HAPANA WATISHIWA MAISHA


Wahudumu  wa Bunge Maalumu la Katiba wakiwa wamebeba masanduku ya kura za wajumbe waliopiga kura za siri kwa Sura ya 11 hadi 19 ya Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, mjini Dodoma jana.

Baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba waliopiga kura za hapana wamelazimika kuondoka Dodoma na kurudi Zanzibar kwa madai ya vitisho walivyopata kutoka kwa wenzao.

Mmoja wa wajumbe hao, Salma Said alisema jana jioni kuwa yeye na wajumbe wenzake wamekataa kuitikia wito wa Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta kwenye Kamati ya Mashauriano ili kuhojiwa kuhusu kura hiyo na kutokana na vitisho wanavyopata kutoka kwa wajumbe wenzao wameamua kuondoka Dodoma.

Vitisho hivyo vimeripotiwa muda mfupi baada ya Sitta kuunda Kamati ya Mashauriano ya watu tisa inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti, Samia Suluhu Hassan kushughulikia kura hizo zilizopigwa na wajumbe saba zinazoweka njiapanda uwezekano wa kupatikana akidi ya kupitisha Katiba inayopendekezwa.

Wajumbe waliopiga kura za wazi za hapana kwa ibara zote ni Adil Mohamed Adil, Dk Alley Soud Nassor, Fatma Mohamed Hassan, Jamila Ameir Saleh, Salma Hamoud Said, Mwanaidi Othman Twahir na Ali Omary Juma. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WALIODHURIKA KWA TOGWA SONGEA WAFIKIA 340...!!!


 

Idadi ya watu waliolazwa hospitalini kwa kunywa togwa inayosadikiwa kuwa na sumu katika Kijiji cha Litapwasi, Kata ya Mpitimbi mkoani Ruvuma imeongezeka kutoka 270 hadi 340.

Tukio hilo lilitokea Jumapili baada ya watu kushiriki sherehe ya Kipaimara ambako walikula, kunywa pombe na togwa na baadaye wale waliokunywa togwa walianza kuumwa matumbo, kuhara na kutapika.

Hadi jana, watu 102 walikuwa bado wamelazwa katika Zahanati ya Lyangweni, Hospitali ya St. Joseph Peramiho na Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma.

Tayari watu watano wanashikiliwa na Polisi kwa upelelezi kuhusiana na tukio hilo, akiwamo Baba Mzazi wa mtoto Dickson aliyepata kipaimara, Enes Nungu (47). Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 01, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKE WA MUGABE KUSHITAKIWA...!!!

Grace Mugabe kulia
Muungano wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Zimbabwe al maarufu Zinasu, umesema kwamba unawasilisha kesi mahakamani hii leo kutafuta ufafanuzi zaidi wa namna mkewe rais Grace Mugabe alivyopata shahada ya udaktari wa falsafa.
Mwanafunzi mmoja mwanaharakati amesema kuwa ni muhimu kwa taifa hilo kuhifadhi hadhi yake ya elimu.
Baadhi ya watu wamehoji kasi aliyosomea shahada hiyo huku wengine wakidai ni njama za kumuandaa kwa urithi wa kiti cha rais baada ya rais Mugabe.
Gazeti moja linalomilikiwa na serikali , the Herald limechapisha kuwa Bi Grace Mugabe alipata shahada hiyo kwa utafiti wake juu ya mabadiliko ya mfumo wa kijamii na miundo ya familia. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

DRC: WAPIGANAJI WA ZAMANI WAFA NJAA

Wapiganaji hao wa zamani wamekuwa wakila chakula kutoka kwa mashamba ya wakulima
Shirika moja la kimataifa la kutetea haki za binadamu linasema kuwa zaidi ya watu mia moja wamefariki kutokana na njaa pamoja na maradhi katika kambi moja ya kijeshi katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Shirika hilo Human Rights Watch, limesema kuwa watu hao ambao walikuwa wapiganaji wa zamani na wake zao pamoja na watoto walihamishwa katika kambi nyingine iliyotengwa Kaskazini mwa DRC.
Ilikuwa baada ya wao kujisalimisha kutoka kwa kundi la wapiganaji Mashariki ya nchi.
Walipokea chakula kidogo na huduma ya afya baadhi wakiponea kifo kwa kuiba chakula kutoka kwa mashamba ya wakulima.
Serikali ya DRC inasema kuwa inachunguza ripoti hiyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UCL: MATOKEO YA CHELSEA VS SPORTING LISBON

IMG_7653.PNG
Usiku wa jana watu wawili waliowahi kuwa vipenzi vya nchi ya Ureno – Jose Mourinho na Nemanja Matic walirejea nchini humo katika jiji la Lisbon lakini safari hii wakiwa kama wapinzani.
Huku Mourinho akionekana kuchukua ‘attention’ yote ya vyombo vya habari ndani ya jiji Lisbon, Nemanja Matic alikuwa kasahaulika.
Lakini katika dakika ya 34, mchezaji huyo wa zamani wa Benfica aliifungia goli pekee Chelsea katika mchezo huo.
Matic alifunga goli hilo kwa kichwa baada ya kuachwa bila kukabwa vizuri na mabeki wa Sporting Lisbon.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United Luis Nani alikuwa akiitumikia Sporting jana na hakuwa kwenye kiwango kizuri katika kipindi cha kwanza – kipindi cha pili alijitahidi lakini akashindwa kubadili matokeo ya mwisho dhidi ya vijana wa Jose Mourinho.
Takwimu na timu zilizopangwa
Sporting (4-3-3): Patricio 7; Cedric 6, Mauricio 5.5 (Oliveira 63, 6), Sarr 5, J.Silva 5; Mario 6, Carvalho 6, A.Silva 6 (Montero 81); Carrillo 6.5 (Capel 81), Slimani 6, Nani 6.
Subs not used: Marcelo, Jefferson, Martins, Rosell.
Bookings: Carvalho, Mario, Cedric, Mauricio
Manager: Marco Silva
Chelsea (4-2-3-1): Courtois 6; Ivanovic 6, Cahill 6, Terry 6, Luis 6.5; Matic 8, Fabregas 7; Schurrle 5 (Willian 57, 6), Oscar 7.5 (Mikel 71, 6), Hazard 7 (Salah 84); Costa 6.
Subs not used: Cech, Zouma, Azpilicueta, Remy.
Bookings: Ivanovic, Hazard, Luis Filipe, Fabregas
Manager: Jose Mourinho.

UCL: MATOKEO YA MAN CITY VS AS ROMA

IMG_7652.PNG
Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza klabu ya Manchester City imeendelea kutopata matokeo chanya katika michuano ya ligi ya mabingwa wa ulaya kwa mara ya pili mfululizo msimu huu.
Wakicheza kwenye uwanja wao wa Etihad dhidi ya AS Roma ya Serie A, Sergio Aguero aliipatia timu yake goli katika dakika ya 4 kupitia mkwaju wa penati.
Lakini dakika 19 baadae Francisco Totti ‘Mfalme wa Roma’ akaifungia goli la kusawazisha Roma na kuandika historia ya mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kufunga goli kwenye michuano ya ulaya.
Man City sasa inakuwa imeshindwa kupata matokeo chanya katika mechi 2 za kwanza cha UCL – wiki mbili zilizopita walifungwa na Bayern Munich.
Timu zilipangwa hivi
Manchester City: Hart 7; Zabaleta 6.5, Kompany 6, Demichelis 5.5, Clichy 6; Navas 5 (Milner 46, 6), Toure 5.5, Fernandinho 6, Silva 7; Aguero 6.5 (Jovetic 84), Dzeko 6 (Lampard 57)
Subs (not used): Caballero, Sagna, Kolarov, Mangala
Goals: Aguero (Pen, 4)
Booked: Zabaleta
Roma: Skorupski 6; Maicon 6 (Torosidis, 89), Manolas 6, Yanga-Mbiwa 6.5, Cole 6; Pjanic 7.5, Nainggolan 6.5, Keita 6.5; Florenzi 5.5 (Holebas 83), Totti 7 (Iturbe 72, 6), Gervinho 7.
Subs (not used): Curci, Ljajic, Destro, Paredes
Goals: Totti (23)
Booked: Maicon, Nainggolan
Referee: Bjorn Kuipers (Holland) 7
Star man: Miralem Pjanic
Attendance: 37,509

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...