Idadi
kubwa ya wabunge nchini Kenya wanajiandaa kuandamana na Rais Uhuru
Kenyatta katika mahakama ya kimataifa ya ICC,Uholanzi ambako anatarajiwa
kuhudhuria kikao maalum kuhusiana na kesi inayomkabili katika mahakama
hiyo.
Kenyatta ametakiwa kufika mbele ya mahakama hiyo tarehe nane
mwezi huu huku kiongozi wa mashitaka Fatou Bensouda akilalamika kuwa
Kenya imekataa kushirikiana na mahakama hiyo kuhusiana na ushahidi dhidi
ya Kenyatta.Mapema wiki hii, mahakama hiyo ya ICC ilitupilia mbali ombi la Rais Kenyatta, la kutaka kikao hicho cha Octoba 8 kuhairishwa au aruhusiwe kutumia video. Majaji wa Mahakama hiyo walimuagiza Uhuru kufika binafsi mbele yao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz